Darren2019
JF-Expert Member
- Nov 23, 2019
- 1,112
- 2,379
Viongozi wenzangu,
Nawasalimu Kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ufuatiliaji unaofanyika shuleni na OR TAMISEMI Umebaini mambo mengi ikiwa ni pamoja na:
1. Baadhi ya walimu ktk Shule za Sekondari wameanza kufundisha maudhui ya masomo mbalimbali wakati Wanafunzi hawajawezeshwa kuwa na umahiri wa stadi za lugha ya kiingereza kama ilivyobainishwa kwenye baseline student book na teachers guide ya Taasisi ya elimu; pamoja na Mkakati wetu wa kuboresha ufundishaji wa English orientation course kipengele cha 3.3.3.1.
2. Imebainika pia Wanafunzi hawawezi kuandika Short stories angalau kwa kurasa mbili. Aidha, imebainika wanafunzi hawajaweza kufanya na kumudu midahalo ya kiingereza kwa ngazi yao.
3. Baadhi ya Shule zilizotembelewa zinaonekana kufuata utaratibu waliozoea kila mwaka wa kuanza kufundisha maudhui ya masomo hata kama wanafunzi hawaelewi kinachofundishwa ( business au usual).
4. Shule nyingi katika mikoa iliyotembelewa hazikuwa na barua za maelekezo ya kuzingatia katika ufundishaji wa kiingereza kidato cha kwanza ( kwa sekondari) na darasa la tatu ( kwa shule za msingi) kama ilivyoelekezwa awali. Hivyo, baadhi ya viongozi wa shule wametumia kigezo hicho kuwa hawakuwa na maelekezo kutoka kwenu ya maandishi; ndiyo maana wameendeleza utaratibu waliozoea.
5. Kufuatia hali halisi hiyo, nawaelekeza kuhakikisha kuwa:
(a) Wanafunzi wa kidato cha kwanza wanamudu umahiri wa lugha ya kiingereza ikiwa ni pamoja na uwezo wa kuwasiliana, kujadiliana na kuandika kwa lugha ya kiingereza angalau kurasa mbili kabla ya kuanza ufundishaji wa maudhui ya masomo.
(b) ufundishaji wa english Darasa ya Tatu kuimarishwa kama ilivyoelekezwa awali ili kujenga msingi imara wa lugha hii.
(c) Waelekezeni Wakuu wa Shule/walimu wakuu kuzingatia maelekezo haya ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua wale wote wanaokiuka kwa kuendeleza utaratibu waliozoea kufanya usioleta tija.
6. Endapo tutabaini uwepo wa kiongozi yeyote ambaye anashindwa kusimamia utekelezaji wa maelekezo haya kwenye Shule zilizo kwenye eneo lake kama inavyoonekana Sasa kwenye baadhi ya shule tutalazimika kumchukulia hatua.
7. Dhamira ya kutembelea shule kwa kila kiongozi wa ngazi za mkoa, Halmashauri na Kata ililenga kuwawezesha ninyi viongozi kujua kinachofanyika kwenye shule zote na kuchukua hatua stahiki ili kuleta tija ya elimu inayotarajiwa kwa kila mwanafunzi mmoja mmoja. Zingatieni kwa dhati dhamira hiyo.
Nawatakia utekelezaji mwema.
NAIBU KM
DR.CHARLES MSONDE
Nawasalimu Kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ufuatiliaji unaofanyika shuleni na OR TAMISEMI Umebaini mambo mengi ikiwa ni pamoja na:
1. Baadhi ya walimu ktk Shule za Sekondari wameanza kufundisha maudhui ya masomo mbalimbali wakati Wanafunzi hawajawezeshwa kuwa na umahiri wa stadi za lugha ya kiingereza kama ilivyobainishwa kwenye baseline student book na teachers guide ya Taasisi ya elimu; pamoja na Mkakati wetu wa kuboresha ufundishaji wa English orientation course kipengele cha 3.3.3.1.
2. Imebainika pia Wanafunzi hawawezi kuandika Short stories angalau kwa kurasa mbili. Aidha, imebainika wanafunzi hawajaweza kufanya na kumudu midahalo ya kiingereza kwa ngazi yao.
3. Baadhi ya Shule zilizotembelewa zinaonekana kufuata utaratibu waliozoea kila mwaka wa kuanza kufundisha maudhui ya masomo hata kama wanafunzi hawaelewi kinachofundishwa ( business au usual).
4. Shule nyingi katika mikoa iliyotembelewa hazikuwa na barua za maelekezo ya kuzingatia katika ufundishaji wa kiingereza kidato cha kwanza ( kwa sekondari) na darasa la tatu ( kwa shule za msingi) kama ilivyoelekezwa awali. Hivyo, baadhi ya viongozi wa shule wametumia kigezo hicho kuwa hawakuwa na maelekezo kutoka kwenu ya maandishi; ndiyo maana wameendeleza utaratibu waliozoea.
5. Kufuatia hali halisi hiyo, nawaelekeza kuhakikisha kuwa:
(a) Wanafunzi wa kidato cha kwanza wanamudu umahiri wa lugha ya kiingereza ikiwa ni pamoja na uwezo wa kuwasiliana, kujadiliana na kuandika kwa lugha ya kiingereza angalau kurasa mbili kabla ya kuanza ufundishaji wa maudhui ya masomo.
(b) ufundishaji wa english Darasa ya Tatu kuimarishwa kama ilivyoelekezwa awali ili kujenga msingi imara wa lugha hii.
(c) Waelekezeni Wakuu wa Shule/walimu wakuu kuzingatia maelekezo haya ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua wale wote wanaokiuka kwa kuendeleza utaratibu waliozoea kufanya usioleta tija.
6. Endapo tutabaini uwepo wa kiongozi yeyote ambaye anashindwa kusimamia utekelezaji wa maelekezo haya kwenye Shule zilizo kwenye eneo lake kama inavyoonekana Sasa kwenye baadhi ya shule tutalazimika kumchukulia hatua.
7. Dhamira ya kutembelea shule kwa kila kiongozi wa ngazi za mkoa, Halmashauri na Kata ililenga kuwawezesha ninyi viongozi kujua kinachofanyika kwenye shule zote na kuchukua hatua stahiki ili kuleta tija ya elimu inayotarajiwa kwa kila mwanafunzi mmoja mmoja. Zingatieni kwa dhati dhamira hiyo.
Nawatakia utekelezaji mwema.
NAIBU KM
DR.CHARLES MSONDE