PhD mbili za Nchimbi Emmanuel ni halali? High level ya uchakachuaji Tanzania

Kwanza nashangazwa na vigezo vya vipimo vyako.....Nchimbi hawezi kuongea kiingereza...umejuaje hujasema na wewe umekuwa TOEFL siku hizi.Unasema ameandikiwa,lakini unajua kuna viva voce hapa ambayo mwanafunzi anakaa mbele ya panel inayohusisha walimu toka vyuo mbalimbali na kujidefend ili apate?alikuilipa wewe umfanyie?.....mwenzio anasema kuwa Msemakweli alimuumbua ndio akaenda shule tena...huu ni uongo msemakweli katoa kitabu chake mwaka 2009 na nchimbi kaanza phd yake mwaka 2006.alimuogopaje bila kitabu kuwepo.....chuki mbaya sana magufuli alipopata phd wote mlipongeza now kwa kuwa ni nchimbi unaibuka....imetoka hio u can't reverse kamanda

Hata mimi nakuunga mkono kwenye red hapo juu.

Mtu akiandikiwa PHD kazi itakuwa kwenye "viva" maana atalia na kusaga meno! Kama kapita Viva basi ni bora aheshimiwe kama msomi badala ya kummbeza.
 
Mtoa hoja ana mtazamo wa jumla sana inaonekana tatizo ninnchimbi kuwa mwanasiasa,mbona magufuli aliweza kumaliza Phd na tukashangilia na kumsifia?kama Nchimbi ameweza kubalance majukumu na kukamilisha Thesis yake anastahili kupongezwa na sio kubezwa tatizo wa Tz wengi kutwa kucha porojo tu na umbea watu wanapiga shule wakihitimu mnasena shahada feke present basi yako real tuione kama mfano,we talk much than what we act wake TZ
well said! Angetunukiwa mtu wa cdm hapa hayo Yasingesemwa angepongezwa sana.
 
Naweza kuwa na mashaka kidogo kwa ile PhD ya kwanza, nafikiri ndio maaana hata yeye alikaa kimya, lakini hii ya pili ndio yenyewe. Ni vizuri kumpongeza huyu kijana anayejibidisha kusoma, na vijana wengine muige mfano huo badala ya kukaa na kulalamika. Jaribuni vile vile kutafuta fact, ziko hata online ya jinsi mtu anavyoweza kupata PhD. Nyingi sana zinavyoenda, hususani sayansi jamii ambazo huitaji kuwa kwenye maabara muda wote, ukiisha maliza course work, ambayo ni masomo takribani yote ya masters kwenye shule nyingi, basi unakuwa huru kuzunguka kukusanya data, kuzinyia kazi mpaka utakapokuwa tayari kuita jopo la wazamivu kwenye idara hiyo kutetea uzamivu wako. Ndio wapo wanasiasa ndani ya CCM ambao ni wajinga kabisa, lakini sio wanasiasa wote wa CCM ni wajinga.
 
Kuna watu humu wanafikiri PhD ni sunday school au ka tuition fulani. Kupata PhD sio lelemama wandugu. Nchimbi anastahili pongeza kituo. acheni majungu yanayotokana na ufinyu wa fikra. Na kama unaleta mambo ya itikadi kwenye Phd ya Nchimbi wewe una tatizo
 
Alidanganya wapi kima wewe,alikuwa nayo na bado anayo tatizo alikuwa kwenye college ambayo haitambuliwi tanzania.....hata phd za udsm hazitambuliwi na oxford na ndio kawaida,sasa hata useme nini amepata tayari na ameregister nyingine cape town university.haahahaha
Sasa matusi yanakujaje mkuu? We ni nani kwa Nchimbi mbona unakuja na jazba sana ktk kujibu hutuma? Manake povu linakutoka mdomoni kumtetea kwa jazba na matusi why? Hata kama we ni mwosha mbwa wake but uje polepole na ubishane kwa hoja na facts na siyo mijitusi...lol
 
wakuu wa kazi, juzi mzumbe walikaririwa na vyombo vya habari wakimtunuka nchimbi phd. Ieleweke kuwa kwa muda mrefu huyu jamaa amekuwa akiitwa doctor kumbe hana phd. Kama hali imefikia hivi hatuoni kuwa Tanzania tumefika kubaya? Mtu anajiita dr wakati he doesnt have such qualification. Na hata kama mzumbe wamempa hii phd tuambiwe amesoma saa ngapi?

hiyo thesis imefanywa na nani kwa sababu ndi ngumu sana kubalance between masomo na siasa, especially being a minister. I am doubting universities zetu hizi, zinachangia kuzalisha wasomi feki. The top most three in fake phd are UDOM, UDSM and MZUMBE. Hii ni embarassment kwa jamii ya wasomi kutoa degree zisizofanyiwa kazi.

Hatuwezi kufika huko tunakotaka kama hali yetu ndiyo hii. maana tumefikia upumbavu wa hali ya juu kwa kujidanganya kuwa tuna wasomi kumbe sifa haziendani na kisomo cha mtu. Huu ni ufisadi wa aina ya pekee. Wanasiasa wanaweza kupata phd ki rahais hivi!
Jamaa wewe ni muongo wa kutupwa! Acha majungu akili yako ikue!!
Nchimbi kasimamiwa na watu wenye utaalamu, na kweli kachapa kazi kwelikweli! na anastahili kuipata hiyo PhD! Bravo Dr Nchimbi!!
 
Sio ya pili amaregister ya tatu captown iniversity.....tumtakie kheri
akimaliza zote tatu tutampa
nafasi ya kusaini mikataba ya hovyo hovyo, kama vile kutoa dhahabu na sie kupewa vyandarua ! Yeye atoe uranium kwa condm !
 
mwanzo wa kuwa na madoctor fake ndio mwanzo wakupata viongozi feki , tutaishi kifeki feki, kuimport vitu TBS inapitisha bidhaa feki, madawa feki, nguo feki, viatu feki, sasa na elimu ishakuwa feki maana Academy nyingi wanaiba mitiani wanashindisha watoto fake, ndio maana hata ma-mama home wanatuzalia vitoto feki maana hatuko makini tunaishi ki-feki zaid.
 
Hivi watu mmekosa kazi kila siku ni kuropoka tu, UDOM hawajatoa phd hata moja we umeanza kuita feki, UDSM haya twambie ufeki wao uko wapi? Na wewe umepata wapi uwezo wa kutambua phd feki na genuin?
Vijana mbona mmejiingiza kwenye majungu ambayo hayatawasaidia? Nchimbi wewe huwezi kushindana nae phd kashapewa unapoteza muda wako na ela yako kuandika pumba humu.
Vijana chapeni kazi acha majungu

Kati ya waropokaji nahisi ww ndo unaongoza,fanya utafiti kabla ya kuongea,udom wametoa phd mwaka huu ni mmojawapo aliyepata phd ni Mohamed seif Khatib,Doctor of philosopy in kiswahili literature!
 
wakuu wa kazi, juzi mzumbe walikaririwa na vyombo vya habari wakimtunuka nchimbi phd. Ieleweke kuwa kwa muda mrefu huyu jamaa amekuwa akiitwa doctor kumbe hana phd. Kama hali imefikia hivi hatuoni kuwa Tanzania tumefika kubaya? Mtu anajiita dr wakati he doesnt have such qualification. Na hata kama mzumbe wamempa hii phd tuambiwe amesoma saa ngapi?

hiyo thesis imefanywa na nani kwa sababu ndi ngumu sana kubalance between masomo na siasa, especially being a minister. I am doubting universities zetu hizi, zinachangia kuzalisha wasomi feki. The top most three in fake phd are UDOM, UDSM and MZUMBE. Hii ni embarassment kwa jamii ya wasomi kutoa degree zisizofanyiwa kazi.

Hatuwezi kufika huko tunakotaka kama hali yetu ndiyo hii. maana tumefikia upumbavu wa hali ya juu kwa kujidanganya kuwa tuna wasomi kumbe sifa haziendani na kisomo cha mtu. Huu ni ufisadi wa aina ya pekee. Wanasiasa wanaweza kupata phd ki rahais hivi!

hapo kwa red n bolded: mkuu hebu zifuate akili zako ulikoziacha, maana hujui unaloliongelea. Huenda hata hujui idadi ya waliopata PhD za ukweli pale UDOM tangu kilipoanzishwa. Bora uzitafute akili zako ulikoziacha
 
Kati ya waropokaji nahisi ww ndo unaongoza,fanya utafiti kabla ya kuongea,udom wametoa phd mwaka huu ni mmojawapo aliyepata phd ni Mohamed seif Khatib,Doctor of philosopy in kiswahili literature!
Uwezo wa seif khatib kwenye kiswahili uko juu sana kuliko unavyodhania ni kati ya washahiri wa mwanzo kuvunja kanuni ya kimapokeo ya Mizania na bado dhima ya mashahiri ikabaki vilevile
 
Waliohudhuria vivavove yake wanasema hajajibu swali hata moja kwa ufasaha. Na imedhirika kwamba hata kuandika yawezekana hakuandika yeye maana alishindwa kujua kilicho ndani ya hiyo kazi
 
Nitajikita zaidi kwenye namna elimu aliyonayo "anavoitumia" zaidi kuliko kama anastahili kuwa na elimu hiyo au la. Kati ya watu waliowahi kuaibisha kiasi nikajisikia aibu kubwa ni Dr. Nchimbi. Wakati huo akiwa Naibu waziri wa Ulinzi aifanya ziara katika moja ya nchi ambazo Tanzania inapeleka majeshi. Wenyeji ambao ni moja ya taifa la Ulaya magahribi walijiandaa sana wakidhani jamaa yukp fresh kwa mambo ya wizara hiyo. Katika hali ya mshangao, performance ya jamaa ilionekana kama ni ya kitalii zaidi. Ni Dr. wa kwanza kwa upande wangu kuonekana kuna disconnect kati ya kiwango cha elimu yake na matumizi yake.

Hata wanaopinga yeye kupewa doctorate ni kwa msingi kuwa haoneshi ktk chochote kuwa yuko hivo. Kwa kifupi, elimu yake haisaidii wala kuongeza thamani katika mambo mengi. Hebu tuwaangalie wengine wenzake, Dr. Shukuru Kawambwa, Dr. Juma Kapuya, Dr. Juma Ngasongwa, Prof. Maghembe. Hivi hawa wamesaidia matatizo ya nchi hii?? Unaweza uona disconnect iliyopo na utendaji wao?
 
Mwamtetea nasikia anataka uraisi nae mteteeni akipata atawapeleka na nyie ikuluu phd fekiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii tu hiyo !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Qualification za makaratasi haimaanishi weledi.
Watanzania ACHENI kujaza makaratasi kwenye mafaili na kuta zenu.
Jazeni weledi kwenye utendaji wenu ili hizo elimu zenu mnazojidai nazo zilete maana.
Mpaka sasa ivi sijaelewa kwanini kila mtu anataka kupata PHD.Mwanasiasa PHD ya nini?
PHD ni nzuri kwa academicians, Researchers, nk.Aidha angalieni wenzenu wanaofanya Siasa na huku wana PHD kama akina Obama hawajitutumui kujiita "Dr".Acheni izo bana!
 
Magufuli never proclaimed himself as a Phd holder before he was awarded the Phd. Huyu b.w.e.g.e alidanganya watu kwamba ana Phd kumbe muongo mkubwa kabisa.


Someni na nyie mpate za kwenu acheni kujadili mambo ya watu. Mbona kuna madokta wengi tu mtaani hamsemi? Au kwa sababu mna bifu na Nchimbi? Angalieni mambo yenu!
 
Back
Top Bottom