Pharmacy council

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,634
7,005
Napendekeza uwepo utaratibu wa kutoa mitihani kila mwaka kabla ya kutoa leseni kwa wafamasia ngazi zote sababu ni kuwa;Wengi hawajisomei na wanaonekana kuwa incompetent sana wanapokuwa kazini.Wengine wanajisahau na kuwa walevi kila siku.Lengo la kufanya hivi ni kuhakikisha ufanisi wa wafamasia wote wenye leseni.

Pili,wekeni utaratibu wa kuwa na orodha ya watu wa kada ya ufamasia wasiofanya kazi ya ufamasia eidha kwa kukosa ajira ama kutokuwa na interest.Sababu ni kuwa kuna wahitimu wa kozi za nacte wanahangaika kutafuta kazi huku ukweli kazi wanazostahili kuzifanya zinafanywa na watu wasio na elimu hata kidogo ya afya.Mifano ipo mingi na hata leo ukitaka kujua pita katika pharmacy nyingi utashangaa.Naamini mnajua labda mnafumbia macho tu.

Imarisheni mijadala ya kifani kupitia mitandao na majarida mbali mbali,ongezeni network na wafamasia wa nje kama wanavyofanya wauguzi,kuna mengi sana ya kubadilishana uzoefu lakini pia tafiti na machapisho mbali mbali.Naona wazee wa zamani walijitahidi sana kufanya hivyo.Leo hata wafamasia wetu hawana mahali pa ku practice utengenezaji wa vitu kama iv fluids,dawa za macho nk.Tumsaidie Rais kuifanya nchi hii ya viwanda

Mwisho kaimuni madaraka kwa mamlaka za halmashauri ikiwa ni pamoja na wenyeviti wa mitaa kuhakikisha watu wasio na sifa hawauzi dawa kwani kuna matatizo makubwa sana katika suala hili japo linafumbiwa macho
 
Hili ni moja ya majipu makubwa kupundukia Tanzania nzima. Kisheria, Pharmacy moja hufunguliwa kwa kutumia cheti cha mtu mmoja kwa maana ndiyo mwenye utaalam wa kuhudumia pharmacy husika.

Lakini wengi wetu tunaelewa kwamba cheti kimoja hutumika kufungua pharmacy kadhaa. Sijui mwenye cheti hujigawa vipi kuhudumia sehemu zote kwa wakati mmoja.

La pili, kuna vyeti vingi fake mitaani vimetumika kufungua pharmacy nzima. Maana yake ni kwamba maduka mengi ya dawa yanasimamiwa na watu wasio na uwezo na hatari zake ziko wazi.

Ni moja ya mambo ambayo Magufuli hajayaona. Inabidi Waziri wa Afya ajiongeze asingoje amri ya Magufuli kulifanyia kazi hili. Uhakiki wa vyeti kwa kila duka ni muhimu kupita maelezo. Utapeli kwenye fani hii una madhara ya moja kwa moja kwenye afya za wananchi.
 
Hili ni moja ya majipu makubwa kupundukia Tanzania nzima. Kisheria, Pharmacy moja hufunguliwa kwa kutumia cheti cha mtu mmoja kwa maana ndiyo mwenye utaalam wa kuhudumia pharmacy husika.

Lakini wengi wetu tunaelewa kwamba cheti kimoja hutumika kufungua pharmacy kadhaa. Sijui mwenye cheti hujigawa vipi kuhudumia sehemu zote kwa wakati mmoja.

La pili, kuna vyeti vingi fake mitaani vimetumika kufungua pharmacy nzima. Maana yake ni kwamba maduka mengi ya dawa yanasimamiwa na watu wasio na uwezo na hatari zake ziko wazi.

Ni moja ya mambo ambayo Magufuli hajayaona. Inabidi Waziri wa Afya ajiongeze asingoje amri ya Magufuli kulifanyia kazi hili. Uhakiki wa vyeti kwa kila duka ni muhimu kupita maelezo. Utapeli kwenye fani hii una madhara ya moja kwa moja kwenye afya za wananchi.

Mkuu, kuhusu hilo swala, sheria zilishatungwa yapata miaka mitatu sasa. Hiyo ilikuwa zamani. Siku hizi hairuhusiwi tena.
 
Napendekeza uwepo utaratibu wa kutoa mitihani kila mwaka kabla ya kutoa leseni kwa wafamasia ngazi zote sababu ni kuwa;Wengi hawajisomei na wanaonekana kuwa incompetent sana wanapokuwa kazini.Wengine wanajisahau na kuwa walevi kila siku.Lengo la kufanya hivi ni kuhakikisha ufanisi wa wafamasia wote wenye leseni.

Pili,wekeni utaratibu wa kuwa na orodha ya watu wa kada ya ufamasia wasiofanya kazi ya ufamasia eidha kwa kukosa ajira ama kutokuwa na interest.Sababu ni kuwa kuna wahitimu wa kozi za nacte wanahangaika kutafuta kazi huku ukweli kazi wanazostahili kuzifanya zinafanywa na watu wasio na elimu hata kidogo ya afya.BMifano ipo mingi na hata leo ukitaka kujua pita katika pharmacy nyingi utashangaa.Naamini mnajua labda mnafumbia macho tu.

Imarisheni mijadala ya kifani kupitia mitandao na majarida mbali mbali,ongezeni network na wafamasia wa nje kama wanavyofanya wauguzi,kuna mengi sana ya kubadilishana uzoefu lakini pia tafiti na machapisho mbali mbali.Naona wazee wa zamani walijitahidi sana kufanya hivyo.Leo hata wafamasia wetu hawana mahali pa ku practice utengenezaji wa vitu kama iv fluids,dawa za macho nk.Tumsaidie Rais kuifanya nchi hii ya viwanda

Mwisho kaimuni madaraka kwa mamlaka za halmashauri ikiwa ni pamoja na wenyeviti wa mitaa kuhakikisha watu wasio na sifa hawauzi dawa kwani kuna matatizo makubwa sana katika suala hili japo linafumbiwa macho

Profession ya famasia mkuu si kila mtu yoyote mwenye ujuzi au aliyesomea profession yoyote ile (mfano hao wahitimu wa NACTE) anaweza ku practice. Sikubaliani na hiyo hoja yako kwani kufanya hivyo ni sawa na kutaka kuwaangamiza watanzania.
Ngoja nikupe mfano
Uwepo wa kada kama drug dispenser ambayo ni kada ya famasi inayotambulika kisheria ambapo mhusika husomea kwa kipindi cha miezi mitatu na anapohitimu mafunzo yake hutunukiwa cheti kinachomruhusu kuuza dawa kwenye maduka dawa, mfano maduka ya dawa baridi niseme tu bila kumumunya maneno kuwa hili ni JIPU kubwa sana.
Haya makosa makubwa sanakuwahi kutokea katika fani hii ya famasi ambayo yaliyofanywa na serikali ya awamu ya nne kupitia baraza lake la wafamsia nchini.
Haiwezekani leo hii mtu akasomea madawa ya binadamu tena (ambayo ni sumu endapo yatatolewa au kutumika vibaya na yanayoweza kupelekea kuhatarisha afya ya mtumiaji) kwa miezi mitatu. Miezi mitatu!! ..Hii ni hatari sana kwa wagonjwa na watanzania kwa ujumla kwani kuuza dawa si sawa na biashara nyingine yoyote ile. Hii kitu inapaswa kurekebishwa mara moja.
 
Mkuu, kuhusu hilo swala, sheria zilishatungwa yapata miaka mitatu sasa. Hiyo ilikuwa zamani. Siku hizi hairuhusiwi tena.
Mkuu, kama kawaida ya Bongo, sheria zipo lakini hazifuatwi. Wakiamua kufanya zoezi hilo, nina uhakika wapata wengi tu. Njia ni rahisi sana. Kila mwenye pharmacy atoe cheti kilichotumika kuifungua. Uhakiki wa vyeti ufuate kwa speed ya mwendokasi. Utashangaa nusu ya pharmacy zitafungwa!
 
Yani wafamasia wafanye mtihani kila mwaka kisa kuna wanaolewa?? Uko serious kweli?? Why only pharmacist wafanye exams??? Au una chuki binafsi na pharmacist. Ulitakiwa u declare interest
 
Hili ni moja ya majipu makubwa kupundukia Tanzania nzima. Kisheria, Pharmacy moja hufunguliwa kwa kutumia cheti cha mtu mmoja kwa maana ndiyo mwenye utaalam wa kuhudumia pharmacy husika.

Lakini wengi wetu tunaelewa kwamba cheti kimoja hutumika kufungua pharmacy kadhaa. Sijui mwenye cheti hujigawa vipi kuhudumia sehemu zote kwa wakati mmoja.

La pili, kuna vyeti vingi fake mitaani vimetumika kufungua pharmacy nzima. Maana yake ni kwamba maduka mengi ya dawa yanasimamiwa na watu wasio na uwezo na hatari zake ziko wazi.

Ni moja ya mambo ambayo Magufuli hajayaona. Inabidi Waziri wa Afya ajiongeze asingoje amri ya Magufuli kulifanyia kazi hili. Uhakiki wa vyeti kwa kila duka ni muhimu kupita maelezo. Utapeli kwenye fani hii una madhara ya moja kwa moja kwenye afya za wananchi.
Ni kweli waziri wa Afya asisubiri Mh Magufuli aagize ndipo atekeleze.Mimi nashangaa ni kwa nini hawa mawaziri wanakuwa wazito sana wakati mambo muhimu ya kufanya yako wazi na ni mengi
 
Yani wafamasia wafanye mtihani kila mwaka kisa kuna wanaolewa?? Uko serious kweli?? Why only pharmacist wafanye exams??? Au una chuki binafsi na pharmacist. Ulitakiwa u declare interest
Una hofu gani mkuu?Mtihani si adhabu ni sawa na mazoezi kwa mcheza mpira ama bondia.Huwezi kufanya vizuri bila kufanya mazoezi ama match za kujipima uwezo
 
Hili ni moja ya majipu makubwa kupundukia Tanzania nzima. Kisheria, Pharmacy moja hufunguliwa kwa kutumia cheti cha mtu mmoja kwa maana ndiyo mwenye utaalam wa kuhudumia pharmacy husika.

Lakini wengi wetu tunaelewa kwamba cheti kimoja hutumika kufungua pharmacy kadhaa. Sijui mwenye cheti hujigawa vipi kuhudumia sehemu zote kwa wakati mmoja.

La pili, kuna vyeti vingi fake mitaani vimetumika kufungua pharmacy nzima. Maana yake ni kwamba maduka mengi ya dawa yanasimamiwa na watu wasio na uwezo na hatari zake ziko wazi.

Ni moja ya mambo ambayo Magufuli hajayaona. Inabidi Waziri wa Afya ajiongeze asingoje amri ya Magufuli kulifanyia kazi hili. Uhakiki wa vyeti kwa kila duka ni muhimu kupita maelezo. Utapeli kwenye fani hii una madhara ya moja kwa moja kwenye afya za wananchi.
mkuu unaposema tunaelewa cheti kimoja hutumika kufungua pharmacy kadhaa sijui kama una uhakika na unachosema,labda kama unashindwa kutofautisha pharmacy(ambazo ndizo zinahitaji cheti cha mfamasia) na medical stores (ambazo cheti cha mfamasia hakihusiki bali ni cheti cha pharmaceutical technician).kwenye kipengele hiki pharmacy council wako makini sana,fanya utafiti mkuu.
katika profession hii ya pharmacy, degree holder anajulikana kama pharmacist na akishasajiliwa na council anaitwa registered pharmacist,diploma holder anajulikana kama pharmaceutical technician na akisajiliwa na council anaitwa enrolled pharmaceutical technician na certificate holder anajulikana kama pharmaceutical assistant na akisajiliwa na council anaitwa enlisted pharmaceutical assistant.kufungua pharmacy ni cheti cha registered pharmacist na cheti kimoja hakifungui pharmacy zaidi ya moja.
 
mkuu unaposema tunaelewa cheti kimoja hutumika kufungua pharmacy kadhaa sijui kama una uhakika na unachosema,labda kama unashindwa kutofautisha pharmacy(ambazo ndizo zinahitaji cheti cha mfamasia) na medical stores (ambazo cheti cha mfamasia hakihusiki bali ni cheti cha pharmaceutical technician).kwenye kipengele hiki pharmacy council wako makini sana,fanya utafiti mkuu.
katika profession hii ya pharmacy, degree holder anajulikana kama pharmacist na akishasajiliwa na council anaitwa registered pharmacist,diploma holder anajulikana kama pharmaceutical technician na akisajiliwa na council anaitwa enrolled pharmaceutical technician na certificate holder anajulikana kama pharmaceutical assistant na akisajiliwa na council anaitwa enlisted pharmaceutical assistant.kufungua pharmacy ni cheti cha registered pharmacist na cheti kimoja hakifungui pharmacy zaidi ya moja.
Mkuu, nashukuru kwa ufafanuzi mzuri sana. Nadhani utakubaliana nami Bongo sheria au kanuni ni kitu kimoja na utekelezaji ni kitu kingine. Hivi vitu vipo Mkuu. Hatuwezi kuweka mifano hapa. Usisahau tulishafika mahali kila kitu Bongo kiliwezekana hata kama sheria haisemi hivyo. Watu wamefoji sana vyeti vya kila aina vikiwemo vya wafamasia!
 
Mkuu, nashukuru kwa ufafanuzi mzuri sana. Nadhani utakubaliana nami Bongo sheria au kanuni ni kitu kimoja na utekelezaji ni kitu kingine. Hivi vitu vipo Mkuu. Hatuwezi kuweka mifano hapa. Usisahau tulishafika mahali kila kitu Bongo kiliwezekana hata kama sheria haisemi hivyo. Watu wamefoji sana vyeti vya kila aina vikiwemo vya wafamasia!
inawezekana kuna case mojamoja lakini PC wako makini sana. hizi pharmacy hurenew usajili kila mwaka na hapo huitaji cheti cha mfamasia na mkataba. ni ngumu sana kufanya manuva.
 
Back
Top Bottom