Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
Watu wamepoteza maisha na makazi yao kuharibika! Sababu kubwa ni Uzembe siwezi elewa mabomu kulipuka kila wakati na raisi kutoa majibu mepesi. Mbona nchi nyingi zina silaha za kijeshi lakini hatusikii milipuko ya kuuwa raia zake. Lazima tuwajibishane ili hali kama hii isitokee tena. Kwa uwezo wa amiri jeshi mkuu hapa atakurupuka na kuunda tume nyingine Kuchunguza mabomu ya Gongo la Mboto. Kwa taarifa za kiintelijensia zilizonifikia kuna idadi kubwa ya Askari imepoteza maisha katika harakati za kuokoa madhara zaidi kwa wanainchi walio karibu na kambi hiyo ya kijeshi.
Nashauri badala ya kumlipa Lowasa na Rostam kupitia Dowans pesa hizo zitumike kulipa fidia na kurudisha maisha katika hali ya kawaida kwa waathirika wa milipuko hii ya Ngongo la Mboto. Hakuna sababu ya kukopesha wabunge Mil 90 wanunue magari ya kifahari wakati kuna wanainchi wanataabika.
Bila shaka busara itatumika na waziri wa Ulinzi atawajibika kwa kujistaafu kwa manufaa ya taifa na kurudisha imani kidogo kwa serikali.
Nashauri badala ya kumlipa Lowasa na Rostam kupitia Dowans pesa hizo zitumike kulipa fidia na kurudisha maisha katika hali ya kawaida kwa waathirika wa milipuko hii ya Ngongo la Mboto. Hakuna sababu ya kukopesha wabunge Mil 90 wanunue magari ya kifahari wakati kuna wanainchi wanataabika.
Bila shaka busara itatumika na waziri wa Ulinzi atawajibika kwa kujistaafu kwa manufaa ya taifa na kurudisha imani kidogo kwa serikali.