FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,792
- 5,375
Asante mkuu,
lakini mimi nilikuwa nazungumzia kuanzia mstari wa kwanza unapoanzia
ilianza hivi,
Nilihisi kuna mtu amesimama karibu na kochi nililokuwa nimejilaza. Ni ile hisia ambapo bila kuangalia nyuma unahisi kuna mtu anakunyemelea au kuna mtu anakuangalia na unapogeuka unakuta ni kweli. Nilikuwa nimejilaza chali kwenye kochi kubwa la rangi nyeusi huku Radhiya akiwa bado amekaa juu yangu. Shanga zake zikiwa zinaninginia na kugusa kiuno changu. Kiunoni mwake alikuwa amejifunga kanga tu, tulikuwa tumeloa jasho, miili imechoka huku usingizi ukitupitia taratibu. Ilikuwa ni mara ya pili ndani ya saa moja tulifanya mapenzi ya nguvu.
Hisia hiyo ya mtu kuwa karibu ilinishtua mimi na kabla sijafanya lolote Radhiya naye alishtuka pia. Tulipofumbua macho yetu tulipigwa na butwaa la mwaka. Mke wangu Husna, alikuwa amesimama pembeni ya kochi tulilokuwa tumejilaza. Mkononi alikuwa ameshika kisu kikubwa chenye ncha kali kilichokuwa kinameremeta. Alikuwa amekunja uso wake, huku machozi yakimtoka na midomo ikimtetemeka. Kabla sijapata nafasi ya kusema Radhiya alijiondoa kwa nguvu na kuruka pembeni huku akishikilia kanga iliyokuwa ikimninginia. Hakufanya ajizi alinyakuwa mkoba wake uliokuwa mezani na funguo za gari lake na kukimbilia mlangoni huku akijaribu kujisitiri na kanga yake. Alitoweka
Hapa inaonyesha msaliti wa ndoa ndio alianza kusimulia kisa na mwanamama akamalizia mkasa.