Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Hapo uko sawa, lkn kumbuka tunaongelea Kanisa Katoliki ambalo Mkuu wake ni Papa, ukitoka nje ya Kanisa Katoliki unaweza kumkwepa Papa lkn siyo ndani, na pia Kanisa Roma lina wafuasi 1.23 billion Duniani kati Binadamu Billioi 7, na hawa wote 1.24 billion Mkuu wao ni Papa!
Bado PAPA si Mungu
 
Mwanahabari Huru

Askofu Pengo unafiki sio sehemu yetu wakatoliki, sikutaka kuandika chochote kuhusiana na wewe, mimi nimebatizwa katika RC nimekuwa muumini mkubwa, nimesoma shule ya Upadri St Mary's Seminary, ninaijua Rc.

Nimesikitishwa sana na kauli zako za kipuuzi, zilizo jaa unafiki, tumekusikia sana ukijipambanua kuwa wewe si muumini wa mabadiliko, tuambie upande wako ni UPI.

Askofu wangu Pengo umemjibu Askofu Niwemugizi alie jitokeza hadhalani na kusema watanzania wanataka katiba mpya, umefufuka ulikotoka na kumshambulia Askofu kuwa katiba au maneno ya Askofu sio msimamo wa RC lakini hakusema kuwa ni msimamo wa RC. Lakini unajua Askofu Niwemugizi si msemaji wa Rc, maana yake alisema kama Mawazo yake kikatiba, na wewe unamjua msemaji wa RC ulitaka kutafuta uhalali wa kujibu mashambulizi la watawala, of target.

Naona umetoka kwa kasi sana kujibu shambulizi hill!,! Lakini hutoki hadhalani kuonya matukio ya kuuwawa kwa watanzania na kutupwa kwenye maji wakiwa wamefungwa mikono Nyuma, wanaopigwa Risasi kama kina tundu Lissu, kuonya viongozi wanao toa maneno ya kibaguzi na kikabila, huwezi kuonya kufokea au kushauri, kazi yako imekuwa ni kujibu mashambulizi kwa wanao ikosoa serikali,

Au unavyeti feki? Unamiliki Mali zisizo halali? Kiongozi wa kiroho unashindwa kujua nini wajibu wako? Sio mala ya kwanza kupingwa na maaskofu wenzio akiwepo Gwajima na kupelekana mahakamani ambapo Askofu Gwajima alikushinda kesi.

Viongozi wa dini simamieni haki na sio unafiki kujipendekeza kama mnataka ubunge, au teuzi za kina mama Lwakatale sawa, Hata mkitaka usemaji wa CCM nafasi za kina polepole.

Swali la Kizushi: WATU WASIOJULIKANA WANATOKEA RWANDA TUMUOMBE TUNDU LISSU

Tafadhari sana heshima kwa viongozi wetu wa kanisa ichukue mkondo wake. Acha uongo wewe sio mkatoliki wakotoliki atuna desturi ya kuwadhalilisha viongozi wetu kwenye mitandao na kama kweli wewe ni mkatoliki auelewi dogma za kanisa katoliki---wakatoliki tunaheshimu mamlaka zilizowekwa na Mungu.

Hata kama aukubaliani na alichosema Kardinali Pengo au askofu yeyote au Padri au mkuu yeyote wa kanisa ingekua busara ukaliwasilisha kwa wahusika na sio hapa mitandaoni , ulichofanya sio sahihi kabisa umeishia kuwapa watu wasiojua imani yetu sababu ya kutubeza na kuwadhalilisha viongozi wetu. Utakaposoma hii message kama wewe ni mkatoliki kweli NENDA UKAUNGAME NA USIRUDIE TENA.
 
Hakuna kitu unajua, ikitaka kuulewa Ukatoli, angalia mfumo wa Tanzania au Monarchy kamaUingereza ndiyo utaelewa, Papa ni Kiongozi wa Kisiasa, Roma ni Dola, kuna Bunge, Mahakama na Serikali ambazo zote ziko chini ya Papa na maamuzi yake anachaguza aidha ashirikishe Serikali (Bunge, Mahakama na Serikali) au aamue mwenyewe, ndiyo maana Tanzania kuna Ubalozi wa Vatikani, unafikiri Balozi wa Vatikani Tanzania anamuwakilisha nani?!

Ndiyo maana Ulaya kulikuwa na Mapinduzi yaliyoanzishwa na Martin Luther (Martin Luther original na siyo yule msanii wa USA) ambaye ndiye muanzilishi wa Uprotestani/Ulutheri Duniani, kufanikisha hilo kulitokea Vita kubwa Duniani ambayo ilijulikana kama thirty years war ambapo Mamilioni ya Watu walipoteza maisha, na Vita ilikuwa ni Kidini/Kisiasa ambapo Ukatoliki vs Ulutheri!
We ndio kipusa kabisa hujui kanisa sasa hivi linaongozwaje
 
Ni swala la mtazamo tu, kwako ni kauli ya ukakasi kwa wengine ni kauli ya Mungu kwani Kardinali ni mtumishi wa Mungu ambaye ameteuliwa na Mungu kuwa Kardinali wa Kanisa Katoliki hivyo sauti yake ni sauti ya Mungu kwa wafuasi wa Kanisa Katoliki!
We Embu omba mtu akupige makofi uamke maana umelishwa matango pori sana ya dini.
 
Pengo kashafikia ukingoni, msimuamini sana na anachokisema yeye sio msimamo wa kanisa bali ni mawazo yake binafsi
 
Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
Kwa hiyo unataka kutuaminisha pengo ana akili kuliko ninyi wakatoriki wote TZ. Ama kweli walei ni walei Tu.
 
Wewe unalijua Kanisa Katoliki kuliko Kardinali Pengo ambaye anakaa meza moja na Papa? Pengo ana kiti chake Roma kwenye Meza moja na Papa, Pengo anaweza kuongea na Papa kwa Simu, wewe takataka unaweza kumpigia nani Simu hata akapokea?
Angekuwa na kiti mbinguni pembeni mwa Mungu ingekuwa sawa, Roma kama Dar tu sema yenyewe imejengwa kwa ustadi
 
Neno Kanisani kubwa, lkn kama ni Kanisa Katoliki, Mkuu wake ni Papa, na ndiye Mkuu wa nchi ya Vatikani!
Madaraka ya Papa yako vatican tu huku kwingine akitaka kitu anaomba na wakiona inafaa watamkubali wakiona haifai wanakataa
 
Unadhani ile TUHUMA YA ESCROW inamuachaje salama? Wala simlaumu mwacheni Mhashamu ajiweke katika mazingira salama kwa maana haijui saa wala siku.
 
Huwa hampendi kuambiwa ukweli.....
Mbna hamkumkosoa GWAJIMA kipindi kile yupo upande wenu....
Askofu PENGO yupo sahihi maana kaona mtu sahihi
Kama ambavyo Mbowe anavyosifia mazuri ya MAGUFULI....mbna hausemi ana kiharibu chadema?
Kwani hapo Pengo kasifia nini, nani na kwa vipi. Hovyo kabisa
 
Wakatorik wengi ni wanafiki! Wao mapadr wao wameshiriki kula na kufuja pesa za rushwa lakini hawasemi chochote! At warudishe! Tangu dunia inaumbwa wakatorik wanakuwa na maono tu raisi akiwa muislam ndo utasikia mara walaka, mara nn. Akiwa raisi mkatoriki kama MAGUFULI hata aseme na kufanya upuuzi gani wao wanaunga mkono tuuu.
 
Hapo uko sawa, lkn kumbuka tunaongelea Kanisa Katoliki ambalo Mkuu wake ni Papa, ukitoka nje ya Kanisa Katoliki unaweza kumkwepa Papa lkn siyo ndani, na pia Kanisa Roma lina wafuasi 1.23 billion Duniani kati Binadamu Billioi 7, na hawa wote 1.24 billion Mkuu wao ni Papa!
Tunachohitaji ni usafi...
Hivi kwanini Galileo aliuawa? Na aliyemuua ni nani? Je kuuawa kwake kuliubadili ukweli?
 
Mwanahabari Huru

Askofu Pengo unafiki sio sehemu yetu wakatoliki, sikutaka kuandika chochote kuhusiana na wewe, mimi nimebatizwa katika RC nimekuwa muumini mkubwa, nimesoma shule ya Upadri St Mary's Seminary, ninaijua Rc.

Nimesikitishwa sana na kauli zako za kipuuzi, zilizo jaa unafiki, tumekusikia sana ukijipambanua kuwa wewe si muumini wa mabadiliko, tuambie upande wako ni UPI.

Askofu wangu Pengo umemjibu Askofu Niwemugizi alie jitokeza hadhalani na kusema watanzania wanataka katiba mpya, umefufuka ulikotoka na kumshambulia Askofu kuwa katiba au maneno ya Askofu sio msimamo wa RC lakini hakusema kuwa ni msimamo wa RC. Lakini unajua Askofu Niwemugizi si msemaji wa Rc, maana yake alisema kama Mawazo yake kikatiba, na wewe unamjua msemaji wa RC ulitaka kutafuta uhalali wa kujibu mashambulizi la watawala, of target.

Naona umetoka kwa kasi sana kujibu shambulizi hill!,! Lakini hutoki hadhalani kuonya matukio ya kuuwawa kwa watanzania na kutupwa kwenye maji wakiwa wamefungwa mikono Nyuma, wanaopigwa Risasi kama kina tundu Lissu, kuonya viongozi wanao toa maneno ya kibaguzi na kikabila, huwezi kuonya kufokea au kushauri, kazi yako imekuwa ni kujibu mashambulizi kwa wanao ikosoa serikali,

Au unavyeti feki? Unamiliki Mali zisizo halali? Kiongozi wa kiroho unashindwa kujua nini wajibu wako? Sio mala ya kwanza kupingwa na maaskofu wenzio akiwepo Gwajima na kupelekana mahakamani ambapo Askofu Gwajima alikushinda kesi.

Viongozi wa dini simamieni haki na sio unafiki kujipendekeza kama mnataka ubunge, au teuzi za kina mama Lwakatale sawa, Hata mkitaka usemaji wa Ccm nafasi za kina polepole.

Swali la Kizushi: WATU WASIOJULIKANA WANATOKEA RWANDA TUMUOMBE TUNDU LISSU
Mkuu umenena na sina cha kuongeza.niliandika hapa kama pengo amekuwa kibaraka wa serikali na comment yangu ikaondolewa.Ahsante sana kwa mtililiko huu.
 
Soma uzi wa mkuu barafu kuhusu kanisa na Utawala utaelewa, Tangu zamani kanisa Katoliki limetumika kufanya dhuluma sana, Mpaka leo kanisa limejaa unafiki na uchafu, Wakatoliki wamegeuzwa watu wa ndio tu, Hata askofu akibaka husema ndio tuzidi kumuheshimu, Wakatoliki wamekuwa watu wa kuwayawaya tu, Kanisa limegeuzwa miliki ya askofu na mapandri, Waumini kazi yao ni kutii amri na miongozo ya kanisa, Unaweza cheka sana ukiuliza unaambiwa mapokeo wapi imeandikwa utasikia Papa gani sijui au mtaguso gani sijui, Biblia wameweka kapuni

Sikia wwe askofu hata abake haibadilishi ukatoriki kwani sisi hatutazami matendo yake we ulishawahi ona trafic mla rushwa anaihalalisha rushwa? Matendo yake sio dhamana kwetu bali maneno yake yanayoleta uhusiano na mungu ndiyo matakwa yetu

Katika mtaguso wa pili wa vatican 1962-1964 inaelezwa waziwazi mapungufu ya kiongozi wa kanisa hayamnyimi yule anaemsikiliza katika yale yaliyo yahaki kufika mbinguni so hata abake yeye bado kuhani kwamaana ya mafuta yaliyo tia alama isiyo futika isipokuwa dhambi ni zakwake yeye
 
Wakatorik wengi ni wanafiki! Wao mapadr wao wameshiriki kula na kufuja pesa za rushwa lakini hawasemi chochote! At warudishe! Tangu dunia inaumbwa wakatorik wanakuwa na maono tu raisi akiwa muislam ndo utasikia mara walaka, mara nn. Akiwa raisi mkatoriki kama MAGUFULI hata aseme na kufanya upuuzi gani wao wanaunga mkono tuuu.
,HII NDIO LIST YA VIGOGO WALIOPATA MGAO WA FEDHA ZA ESCROW,TAKUKURU YADAI KUZIRUDISHA HAKUMSAFISHI MTU - MTILAH BLOG

Tukitoka hapo na tuutafute utukufu na utakatifu!
Hivi katika hayo Baba Mhashamu anayeongea na Papa pasi kupepesa alipata kuyakemea hayo?
Ikiwa alikaa kimya kwanini sasa anasema? kwanini sasa anatetewa?
KWELI WAZALENDO WANAJENGA NCHI!!!
 
Madaraka ya Papa yako vatican tu huku kwingine akitaka kitu anaomba na wakiona inafaa watamkubali wakiona haifai wanakataa


Siyo kweli, yeye ni Mkuu wa Wakatoliki bilioni 1.23 Duniani, hivyo Wakatoliki wa Tanzania wanamuwakilisha kama vile Raisi wa JMTZ anavyowawakilisha Watanzania, na haijalishi kama unampenda au haumpendi Magufuli, lkn maadamu unaishi JMTZ ni Raisi wako hilo halikwepeki!
 
Sikia wwe askofu hata abake haibadilishi ukatoriki kwani sisi hatutazami matendo yake we ulishawahi ona trafic mla rushwa anaihalalisha rushwa? Matendo yake sio dhamana kwetu bali maneno yake yanayoleta uhusiano na mungu ndiyo matakwa yetu
Katika mtaguso wa pili wa vatican 1962-1964 inaelezwa waziwazi mapungufu ya kiongozi wa kanisa hayamnyimi yule anaemsikiliza katika yale yaliyo yahaki kufika mbinguni so hata abake yeye bado kuhani kwamaana ya mafuta yaliyo tia alama isiyo futika isipokuwa dhambi ni zakwake yeye
HATARI SANA! Hata akiwazini wake na watoto wa waumini wake!!! Hata akila sadaka na kulihujumu kanisa!!! Hata... hata... hata...
Acheni tuijenge nchi
 
Back
Top Bottom