Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Hivi sasa mkoani Ruvuma hususani manispaa ya Songea kumetokea wimbi kubwa la majambazi wanaoua wananchi.Mpaka hivi sasa ninapoandika thread hii watu 9 wameshapoteza maisha yao.Chanzo kikubwa cha mauaji haya hivi sasa ni kuwa huko msumbiji kuna mganga anayewapa utajiri wachimba madini.Hivyo anayehitaji utajiri huo analazimika kupeleka viungo vya binadamu hususani vyeti zake.Na mwanadamu anayesemekana ana bahati zaidi ni mwanamke.Hivyo watu ambao wameshachinjwa katika manaispaa hii wanakutwa wameshanyofolewa uchi na ulimi.
Hivi sasa mji wa songea upo katika hofu.Wananchi wamelalamikia hali hii na kumpelekea kamanda Michael Kamuhanda,lakini majibu yake yamekuwa kwamba watu wanakufa au kuchinjwa sababu kubwa ni mapaenzi na hadi sasa wameuawa watu 2 tu jambo ambalo ni uwongo.Juzi jioni sheikh amechinjwa akiwa anatokea msikitini.Je huyu naYE NI WIVU WA KIMAPENZI?Leo ninavyoamka lazima tena tupate habari mpya ya kuchinjwa watu.
Wananchi wa kata ya Lizaboni juzi waliandama baada ya kauli ya RPC kuwa hakuna mauaji.Wakafika kwa Said Mwambung mkuu wa mkoa huu.Majibu yake yakawa naye anasikia mauaji hayo lakini hajapewa taarifa kamili.Hapa RPC Kamuhanda tunamshuku ana maslahi binafsi na mauaji haya.
Sambamba na hilo Radio Jogoo iliyopo hapa Songea nayo tutaandamana ifungiwe kusema uongo kuwa hakuna jambo kama hilo mkoani hapa.Kamuhanda ametukera zaidi kwa kushindwa kutoa ulinzi wa polisi.Hakuna msako wowote uliofanyika kuwasaka watu hawa.Na inasemekana watu wanaofanya vitu hivi wanatokea msumbiji amabako dili hilo lilikoanzia.Watanzania wenzetu tuungeni mkono tumwondooe kamanda huyu.
Hivi sasa mji wa songea upo katika hofu.Wananchi wamelalamikia hali hii na kumpelekea kamanda Michael Kamuhanda,lakini majibu yake yamekuwa kwamba watu wanakufa au kuchinjwa sababu kubwa ni mapaenzi na hadi sasa wameuawa watu 2 tu jambo ambalo ni uwongo.Juzi jioni sheikh amechinjwa akiwa anatokea msikitini.Je huyu naYE NI WIVU WA KIMAPENZI?Leo ninavyoamka lazima tena tupate habari mpya ya kuchinjwa watu.
Wananchi wa kata ya Lizaboni juzi waliandama baada ya kauli ya RPC kuwa hakuna mauaji.Wakafika kwa Said Mwambung mkuu wa mkoa huu.Majibu yake yakawa naye anasikia mauaji hayo lakini hajapewa taarifa kamili.Hapa RPC Kamuhanda tunamshuku ana maslahi binafsi na mauaji haya.
Sambamba na hilo Radio Jogoo iliyopo hapa Songea nayo tutaandamana ifungiwe kusema uongo kuwa hakuna jambo kama hilo mkoani hapa.Kamuhanda ametukera zaidi kwa kushindwa kutoa ulinzi wa polisi.Hakuna msako wowote uliofanyika kuwasaka watu hawa.Na inasemekana watu wanaofanya vitu hivi wanatokea msumbiji amabako dili hilo lilikoanzia.Watanzania wenzetu tuungeni mkono tumwondooe kamanda huyu.