Elections 2010 Pendekezo Jepesi: Wagombea Urais wakutane kabla hatujaenda shimoni!

Edwin Mtei said:
Mzee Mwanakijiji,

Nakushuru kwa pendekezo lako linaloonyesha ukomavu wa siasa zako, uzalendo, mapenzi na huruma kwa nchi yetu na watu wake. Ni jambo muhimu sana kwamba kiongozi aliyeko madarakani sasa, yaani Rais Kikwete aongoze katika tamko hilo. Hata kama, kwa sababu yoyote ile, hatafuata ushauri huu, ingefaa Dk. Willibrod Slaa na Profesa Ibrahim Lipumba wakatoa tamko linalozingatia ushauri huu.


Edwin Mtei. (Mwenyekiti Mstaafu na Muasisi wa CHADEMA)

Mzee Mtei,

..kwanza shikamoo.

..naomba nitofautiane kidogo ktk haya mapendekezo yako.

..katika harakati hizi za uchaguzi JK ana hadhi sawa kabisa na ile ya Prof.Lipumba na Dr.Slaa.

..vyama vya upinzani mtakuwa mnajiangusha wenyewe mkianza kumchukulia JK kama yeye ni kiongozi, na wagombea wenu ni waongozwa, ktk suala zima la kushughulikia tatizo lilijitokeza mbele yetu.

..kinachotakiwa kufanyika ni hawa wagombea kukutanishwa chini ya usimamizi wa watu wenye busara na wanaoheshimika na jamii ya wa-Tanzania. katika mkutano huo woote watambuliwe kwamba wana hadhi sawa, yaani ni wagombea wa kiti cha Uraisi wa Jamhuri.
 
Tatizo huwa tatizo kama hujajua kiini cha tatizo, ila huwa si tatizo kama unajua kiini cha tatizo. Hakuna mtu anaependa ugomvi, ila huwa inapotokea tofauti ya aina yoyote kati ya mchokozi na aliechokozwa ndo ugomvi hutokea....Ila kama mchokozi huwa hakubali kama yeye ni mchokozi kwa sababu tu ya ubabe wake, yeye ndiyo kashika mpini then huwa hakuna mnyonge wa milele............

Kwa aina ya ugomvi huu hali ipo tofauti koz hatuongelei maisha ya mtu mmoja ila ya watu wengi (watanzania) wasio na hatia ndiyo watakaoumia..then ni vema kati ya mafahali wawili mmoja akawa mnyonge ili wote wakawa zizi moja......
 
Mzee Mtei,

..kwanza shikamoo.

..naomba nitofautiane kidogo ktk haya mapendekezo yako.

..katika harakati hizi za uchaguzi JK ana hadhi sawa kabisa na ile ya Prof.Lipumba na Dr.Slaa.

..vyama vya upinzani mtakuwa mnajiangusha wenyewe mkianza kumchukulia JK kama yeye ni kiongozi, na wagombea wenu ni waongozwa, ktk suala zima la kushughulikia tatizo lilijitokeza mbele yetu.

..kinachotakiwa kufanyika ni hawa wagombea kukutanishwa chini ya usimamizi wa watu wenye busara na wanaoheshimika na jamii ya wa-Tanzania. katika mkutano huo woote watambuliwe kwamba wana hadhi sawa, yaani ni wagombea wa kiti cha Uraisi wa Jamhuri.
Mkuu JK....si kweli wagombea wana hadhi sawa mbele za macho ya hao mafanatic wao!Kikwete yeye bado ni rais halali wa Tanzania na sauti yake certainly ina nguvu zaidi pale inapokuja kwenye kutoa kauli za kusitisha uvunjaji wa amani...Pia yeye kama mwenyekiti wa chama kilichopo madarakani,ni lazima akemee vitendo vya baadhi ya wanachama wake....Kama anataka wananchi wengine waelewe kuwa anasapoti hao green guards etc,then akae kimya kama unavyotaka afanye....Lakini yeye kama rais,bado wananchi wanasubiri kusikia kauli kutoka kwake....Kauli ya kulaani umwagaji damu unaofanywa na wafuasi wake...Tuache utopian thinking.....Ikija kwenye kampeni tunaweza ku assume kuwa wagombea hao wana nafasi sawa,lakini kimaamuzi hawako sawa,mwenyekiti wa ccm bado anasimamia dola nk.....Hivyo ana uwezo zaidi wa kudeal na issue more practically,na kwa hilo kauli yake pia ni a must.
 
Mwelekeo wa hali ya uchaguzi unasikitisha kidogo. Matukio ya vurugu za hapa na pale unanifanya nitamani kuwa wagombea wa Urais wa kianzia na Kikwete wakutane ili kulipa taifa picha ya umoja katika tofauti. Watoe kauli ya pamoja ya kuwakata wanachama wao na mashabiki kutotumia nguvu na wale wenye vikundi vya ulinzi wawatulize makada wao. Vinginevyo, tujiandae kulipa gharama kubwa zaidi. Wafanye mapema

MMJ,
Hili ni wazo zuri sana, kwa yeyote mwenye mapenzi ya kweli na Tanzania atakubaliana na wazo hili. Lakini uwezekano wa kufanyika kitu kama hicho ni mdogo sana tokana na ukweli unavyojionesha. Watanzania walio wengi wamechoka na CCM hivyo wanataka mabadiliko ya kweli yatakayo wapeleka katika maendeleo ya pamoja kama watanzania kwa kuzingatia uzalendo, usawa, uwazi na uwajibikaji. Watawala na watu wachache ambao wanafaidika na keki ya taifa hawako tayari kuona mabadiliko yanatokea ndani ya Tanzania. Hofu yao inatokana na ukweli kwamba wanajua walichofanya ni madudu na wanaweza kupelekwa mahakamani. Hivyo wanafanya kila wawezalo kubaki madarakani ikiwa ni pamoja na kuruhusu hizi fujo zifanyike ama kutuma wafanya fujo wafanye fujo hizi. Kwa ufupi fujo hizi zinafanywa na vijana wa CCM ambao wametumwa na CCM, kwa faida ya CCM, hivyo si rahisi CCM kuwaambia vijana wao waache kufanya fujo hizi.

Tunakoelekea ni kubaya na njia pekee ya kukwepa kulipeleka taifa huko ni CCM kukubali matokeo na hali halisi kwamba watanzania walio wengi wameichoka CCM.
 
jmushi1,

..siyo vizuri kujitengenezea mazingira ambapo JK ataonekana fahari, na wagombea wenzake ndama, ktk kipindi hiki cha uchaguzi.

..hawa wagombea wakutanishwe na wajadiliane kama wagombea. tuepuke mazingira ambapo Raisi anakutana na wagombea uraisi.
 
Mwelekeo wa hali ya uchaguzi unasikitisha kidogo. Matukio ya vurugu za hapa na pale unanifanya nitamani kuwa wagombea wa Urais wa kianzia na Kikwete wakutane ili kulipa taifa picha ya umoja katika tofauti. Watoe kauli ya pamoja ya kuwakata wanachama wao na mashabiki kutotumia nguvu na wale wenye vikundi vya ulinzi wawatulize makada wao. Vinginevyo, tujiandae kulipa gharama kubwa zaidi. Wafanye mapema
Mzee Mwanakijiji, asante kwa ushauri huu, ni ushauri wa busara unaohitaji wenye busara za kihivyo kuufuata, very unfortunately, rais wetu, Mheshimiwa sana, Jakaya Mrisho Kikwete, sio mtu mwenye busara kihivyo. Please correct me if I'm wrong, hivi kama rais wako sio mtu mwenye busara, jee kusema rais Kikwete hana busara za kihivyo itakuwa ni kumkosea adabu?. Naamini sio, haswa kama nitathibitisha kutokuwa na busara kwake kwa
baadhi ya kauli zake, zilizohitaji kiwango cha busara za wastani tuu ambazo nazo hanazo.

Jinsi alivyoshugulikia lile tishio la mgomo wa wafanyakazi kwa lugha ya vitisho, kebehi, dharau, bezo, mapuuza, kiburi na jeuri isiyo kifani ndio kipimo cha busara za JK. Kama anaikimbia midahalo tuu ya kuonyesha uwezo wake mbele ya washindani wake, leo atakuwa na audacity ya kukutani na washindani wake kuitakia mema nchi hii?!. Mwenzio
anawaza utawapa mtaji wa kisiasa.

Naamini kuna wenye busara wengi tuu CCM na serikali ambao huwa wanamshauri rais wetu nini cha kufanya/sema wakati gani, lakini anawapuuza, kwa kifupi rais wetu hashauriki, he is too proud to bow down to the people for the sake of this nation. Hizo picha mnazoziona mpaka anakaa kwenye mavumbi ni pure pretence, pride inaonekana wazi kwenye paji la uso wake, ana bend down ili aonekane down to earth kuombea kura!.

Tatizo jingine kubwa la rais wetu huyu JK linalofanya kutokubali kuutekeleza ushauri kama huu ni dharau na mapuuza almost kwenye kila kitu, he is never serious on serious maters na kikubwa zaidi hana hata chembe ya aibu when he does mistakes as if yeye ni malaika.

Wakati wa ule mkutano wa CPA wa Arusha, JK alikuwa aufungue saa 3:00 asubuhi, mheshimiwa sana alifika saa 5:17!, just imagine kuwangojesha wageni wote hao tena wa kimataifa kwa muda wote huo, tena afadhali yetu sisi waswahili, wazungu wale waligeuka wekundu. Haya hatimaye alifika na kuufungua, for whataver the reasons zilizopelekea kuchelewa, he had an obligation just to say sorry na kutoa sababu yoyote, un avoidable circumstances zilizomfanya achelewe, he said nothing!, alifika akaufungua as if nothing happened na hiyo saa 5 ndio ilikuwa schedule yake. Wastaarabu huwa wanasema japo sorry to keep you waiting, yeye wala!, huyu ndio leo akae na wenzie kwa pamoja wahubiri amani?!, not this JK, na baada ya uchaguzi sikilizieni hayo mabezo yatakayofuatia.

JK ni rais wetu, heshima yake kama rais iko pale pale, lakini kueleza madhaifu yake, isichukuliwe kama ni kuvunjia heshima kwa wenye busara, huku ni kumjenga.
 
jmushi1,

..siyo vizuri kujitengenezea mazingira ambapo JK ataonekana fahari, na wagombea wenzake ndama, ktk kipindi hiki cha uchaguzi.

..hawa wagombea wakutanishwe na wajadiliane kama wagombea. tuepuke mazingira ambapo Raisi anakutana na wagombea uraisi.
Mkuu nakubaliana na wewe,lakini mind it that the bucks still stops with him!
Inapokuja kwenye practical issues,dimension ya kuzihandle ni lazima piwe iwe practical....Kwafano vurugu na umwagaji damu vikitokea zaidi God forbid,all this will be counted as "They happen under his watch" Na ni wazi kuwa yeye ndiye atakayekuwa accountable kwasababu awamu yake bado haijaisha.
Pili sidhani kama atajengewa ufahari wakati wanaoanzisha fujo ni kikundi tu cha baadhi ya wanachama wa chama chake....Kama ingekuwa ni wanachama wa chadema ndiyo waanzishaji wa vurugu,halafu yeye akaambiwa awatulize,then hiyo point yako ya ufahari itakuwa valid.
Kukutanishwa na kujadili ni sawa,lakini pia ni lazima na yeye atoe kauli ya kulaani vitendo hivyo!
 
jmushi1,

..siyo vizuri kujitengenezea mazingira ambapo JK ataonekana fahari, na wagombea wenzake ndama, ktk kipindi hiki cha uchaguzi.

..hawa wagombea wakutanishwe na wajadiliane kama wagombea. tuepuke mazingira ambapo Raisi anakutana na wagombea uraisi.

nafikirii wote tunabidi tukubaliane kwamba jk ni amniri jeshi mkuu, ndio aliye teu nec, jajimkuu, nk hivyo kama kiongozi mkuu wa njii yetu kwa sasa anatakiwa aongoze kwa vitendo aachane na nkewe, na watoto wake ingawa kila moja wetu angependa mtoto wake awe kinara, hata mwinyi au nyerere alipenda hivyo, lakini haikuwa hivyo.
 
Dr Slaa alishatoa tamko. Amewataka Wafuasi wake sio tu wasianzishe fujo ila hata wasilipize kisasi. Nijuavyo ni kwamba tamko kuhusu fujo ambalo hadi sasa Rais Kiwete amelitoa ni lile la wakati akifunga mafunzo ya kikundi cha Green Guards kule Singachini. Aliwaambia serikali ni yao na hakuna mtu anayeweza kuwafanya chochote.

Kubadilisha chama tawala sio lelemama. Pale ambapo watawala ni waungwana, kama ilivyokuwa kwa Kaunda, wamebadilisha bila umwagaji damu. Ila kwetu CCM imetayarisha wapiganaji. Ni wa nini kama sio wa kumwaga damu?

JK anaweza kuwaamuru hao Intaramwe wake (Green Guards) wasifanye fujo? Kwani wameanzishwa kwa kusudio lingine?

But do not lose hope. History is guided by the hand of God.
 
Hii inaonyesh jinsi nchi huii isivyokuwa na uongozi. Nina wasiwasi sana iwapo hata Kikwete anatambua kuwa taifa la Tanzania ni kubwa kuliko familia yake. Kila wakati nimekuwa nahisi kuwa kwa mheshimiwa Kiwete, familia yake ni ya muhimu zaidi ya taifa katika madaraka na wajibu alio nao. Kumkutanisha yeye na mtu anayetaka kupiokonya familia yake hyo madaraka inaweza kuwa ni kitendo kichungu sana kwake. Atakachofurahia ni kitendo chochote kinachopunguza idadi ya wafuasi wa mpinzani wake kadri iwezekanavyo kwa njia yoyote ile hata kama ni kubomoa taifa kusudi aweze kushinda tena.
 
mwelekeo wa hali ya uchaguzi unasikitisha kidogo. Matukio ya vurugu za hapa na pale unanifanya nitamani kuwa wagombea wa urais wa kianzia na kikwete wakutane ili kulipa taifa picha ya umoja katika tofauti. Watoe kauli ya pamoja ya kuwakata wanachama wao na mashabiki kutotumia nguvu na wale wenye vikundi vya ulinzi wawatulize makada wao. Vinginevyo, tujiandae kulipa gharama kubwa zaidi. Wafanye mapema

january makamba unafikiri atamuandikia jakaya kipi cha kuongea? Labda "wote wanaopigwa mapanga na ccm wanajitakia"
 
Kuna tofauti kati ya viongozi na wafuasi.. katika wiki hizi mbili tutaweza kupambanua tofauti ya makundi hayo mawili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom