Pendekezo:Iitishwe kura rasmi ya maoni juu ya utendaji wa rais na serikali yake!

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,023
144,381
Utaratibu wa kutumia kura ya maoni ili kufanya uamuzi wa jambo lenye maslahi kwa taifa sasa hauna budi kutumika kuamua kama tuna haja ya kuendelea kuwa na serikali hii ya awamu ya nne.Kwa jinsi mambo yanavyokwenda hapa nchini na muda uliobaki ni hatari sana kuendekea kuvumilia watu walioshindwa kuwajibika.Ni bora tukachukua tahadhari mapema kuliko kuchelewa au kutokuchukua tahadhari kabisa.

Iwapo katika kura hiyo ya maoni asilimia zaidi ya 80% wakiunga mkono pendekezo la kuitaka serikali ikae pembeni basi serikali iwajibike.Sisi ndio waajiri na sisi ndio tunapaswa kufukuza.

Bunge ndio limepewa mamlaka kikatib kupiga kura ya kutokuwa na imani na serikali lakini nani ana imani na bunge letu kwa jambo kama hili?Tuendelee kuangamia tukisubiri bunge kibogoyo na lisilojua wajibu wake?

Na ikiwezekana utaratibu huu uwe wa kikatiba , kila raisi awe anapigiwa kura ya maoni katikati ya kipindi chake cha utawala au hata pale inapobidi ili kuleta uwajibikaji na si kufanya nafasi ya uraisi kama ni cheo cha kifalme.Mtu kashindwa basi aondoke sio nchi inayumba naye anayumba nayo huko amengangania usukani.Huu ni uendawazimu!
 
Utaratibu wa kutumia kura ya maoni ili kufanya uamuzi wa jambo lenye maslahi kwa taifa sasa hauna budi kutumika kuamua kama tuna haja ya kuendelea kuwa na serikali hii ya awamu ya nne.Kwa jinsi mambo yanavyokwenda hapa nchini na muda ukiobaki ni hatari sana kuendekea kuvumilia watu walioshindwa kuwajibika.Ni bora tukachukua tahadhari mapema kuliko kuchelewa au kutokuchukua tahadhari yoyote.

Iwapo katika kura hiyo ya maoni asilimia zaidi ya 80% wakiunga mkono pendekezo la kuitaka serikali ikae pembeni basi serikali iwajibike.Sisindio waajiri na sisi ndio tunapaswa kufukuza.

Bunge ndio limepewa mamlaka kikatib kupiga kura ya kutokuwa na imani na serikali lakini nani ana imani na bunge letu kwa jambo kama hili?Tuendelee kuangamia tukisubi bunge kibogoyo na lisilojua wajibu wake?

Na ikiwezekana utaratibu huu uwe wa kikatiba kila raisi awe anapigiwa kura ya maoni katikati ta kipindi chake cha utawala au hata inapobidi ili kuleta uwajibikaji na si kufanya nafasi ya uraisi kama ni cheo cha kifalme.Mtu kashindwa basi aondoke sio nchi inayumba naye anayumba nayo huko amengangania usukani.Huu ni uendawazimu!

Wazo lako ni vigumu kufanikiwa japo umuhimu ni mkubwa.Katiba yetu ni kweli haijatoa njia mbadala ya namna ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais nje ya bunge lakini imefafanua kuwa umma ndo wenye mamlaka ya kuweka na kuondoa dola madarakani.Hivyo njia pekee ni umma kuamka na kuandamana kama ilivyokuwa misri.
 
Kuna umuhimu wa kuingiza kipengele kama hicho kwenye katiba mpya.Nafasi ya uraisi nchii hii ni zaidi ya ufalme!
 
Back
Top Bottom