mkuu We subiri zifikishwe kwa mkemia wa serikali ili kuthibitishwa kama kweli ni za Ndovu. Usishangae kusikia baadae taarifa ikitoka kuwa ni za Ng'ombe,hapo ndiyo utajua kuwa Mafisadi wapo kazini !.Kwahiyo ungezihifadhi kwanza hizo hongera zako.
Sidhani kama polisi wanastahili kupongezwa kwa hili... walitakiwa kuhakikisha hao tembo hawauawiPembe nyingi tu zipatazo 214 zimekamatwa na Polisi wa Mkoa wa kinondoni maeneo ya kimara usiku wa kuamkia leo.hongera kwao askari wa doria pamoja na kamanda wa polisi mkoa wa kinondoni.
Pembe nyingi tu zipatazo 214 zimekamatwa na Polisi wa Mkoa wa kinondoni maeneo ya kimara usiku wa kuamkia leo.hongera kwao askari wa doria pamoja na kamanda wa polisi mkoa wa kinondoni.
Ni pembe 214 au vipande 214 maana kama ni pembe 214 ni kuwa tembo 107 wameuwawa kwani tembo m 1 ana pembe 2 tu. Hata hivyo vyovyote vile tembo hao hawakustahili kuuwawa kama nchi ingekuwa makini ktk kulinda maliasili zetu.