mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 16,102
- 36,063
Nilianza kumuona miaka ile na kipindi chake cha Kitimoto.
Nikaja kukutane nae UDSM akisoma LLB na mimi nikisoma kozi ngumu kuliko zote pale chuoni, namkumbuka akinesanesa na pikipiki lake viunga ya UDSM au Mabibo Hostel nilipokuwa naishi.
Mwaka 2005 Au 2006 NIlikuwa napata lunch Hill Park, tukajikuta tuko meza moja, ila kwa vile alikuwa star sikumshobokea, Kama ilivyo desturi yangu ya kuwakaushia mastaa so hanijui, simjui.
Kwa bahati mbaya wote tulidisco chuo,Mimi nilidisco sababu ya ugumu wa masomo ila mwenzangu nasikia ilikuwa ni figisu figisu tu za prof mmoja sio sababu ya uwezo mdogo.
Baada ya kudisco nikakimbia nchi tena kwa mara ya pili. Sikuwahi kumuona tena zaidi ya kumsoma JF na mimi siangalii TV sijui yuko TV gani siku hizi.
Kupitia JF Nimekuwa nikifuatilia maandishi yake, nara kadhaa, niseme tu maandishi yake yana unabii ndani yake, orodha ni ndefu sana nikiweka hapa hapatoshi, vitu vingine huchukua miaka hata mitano kutokea, hakuna mwana JF anayemfikia kwa hilo.
Kama hana pepo wa utambuzi basi ana roho mtakatifu. Nafahamu yeye ni mkatoliki Mzuri ila afungue tu kanisa atapata wafuasi. Nafahamu pia anapenda siasa, madhabahuni pia ni sehemu sahihi ya kupiga siasa kama akina Mama Rwakatale, Kakobe, Gwajima, Pengo, Mtikila, Sheikh Ponda, Alhad Musa wote hao wanapiga siasa kwenye mimbari.
Atumie hilo pepo la utambuzi au roho mtakatifu aliyenae kuwafikia wengi.
Maana kila utawala unamsukumia kambo utadhani hana kitu kichwani na kwa umri wake sitegemei kuona akipata teuzi,
Ni ushauri tu.
Nikaja kukutane nae UDSM akisoma LLB na mimi nikisoma kozi ngumu kuliko zote pale chuoni, namkumbuka akinesanesa na pikipiki lake viunga ya UDSM au Mabibo Hostel nilipokuwa naishi.
Mwaka 2005 Au 2006 NIlikuwa napata lunch Hill Park, tukajikuta tuko meza moja, ila kwa vile alikuwa star sikumshobokea, Kama ilivyo desturi yangu ya kuwakaushia mastaa so hanijui, simjui.
Kwa bahati mbaya wote tulidisco chuo,Mimi nilidisco sababu ya ugumu wa masomo ila mwenzangu nasikia ilikuwa ni figisu figisu tu za prof mmoja sio sababu ya uwezo mdogo.
Baada ya kudisco nikakimbia nchi tena kwa mara ya pili. Sikuwahi kumuona tena zaidi ya kumsoma JF na mimi siangalii TV sijui yuko TV gani siku hizi.
Kupitia JF Nimekuwa nikifuatilia maandishi yake, nara kadhaa, niseme tu maandishi yake yana unabii ndani yake, orodha ni ndefu sana nikiweka hapa hapatoshi, vitu vingine huchukua miaka hata mitano kutokea, hakuna mwana JF anayemfikia kwa hilo.
Kama hana pepo wa utambuzi basi ana roho mtakatifu. Nafahamu yeye ni mkatoliki Mzuri ila afungue tu kanisa atapata wafuasi. Nafahamu pia anapenda siasa, madhabahuni pia ni sehemu sahihi ya kupiga siasa kama akina Mama Rwakatale, Kakobe, Gwajima, Pengo, Mtikila, Sheikh Ponda, Alhad Musa wote hao wanapiga siasa kwenye mimbari.
Atumie hilo pepo la utambuzi au roho mtakatifu aliyenae kuwafikia wengi.
Maana kila utawala unamsukumia kambo utadhani hana kitu kichwani na kwa umri wake sitegemei kuona akipata teuzi,
Ni ushauri tu.