Panya road azinduka akiwa Mortuary

Dar es Salaam. Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Lumo wilayani Temeke, Isack Ernest alionja mauti baada ya kupigwa na wananchi kiasi cha kufikiriwa kwamba amekufa, akapelekwa chumba cha maiti ambako alizinduka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto alisema jana kwamba kijana huyo alipigwa hadi kupoteza fahamu na alipofikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke aliwekwa kwenye chumba cha maiti pamoja na kijana mwingine aliyeuawa katika tukio hilo.

“Mwanafunzi huyo hali akiwa amelazwa pamoja na maiti nyingine zinazosubiri kuwekwa katika majokofu, alitikisika kutokana na baridi ya chumba cha maiti, wahudumu wakamwona na kumtoa, wakamvalisha nguo za maiti nyingine, akarudishwa hospitalini kwa ajili ya huduma,” alifafanua Kamanda Muroto.


Alipigwa kwa kosa gani
 
Mbona nilisikia kuwa wafanyakazi wa mochwari wakisha pokea maiti halafu ikaonekana kuwa bado ni mzima jambo la kwanza ni kuhakikisha wana kumaliza kabisa huko huko mochwari kwa sababu ikionekana ni mzima kesi inaenda kwa daktari alie kuhudumia na hospital yote kwa ujumla kumbe sio kweli.!maana kama huyo jamaa wamemuopoa mochwari ndani kabisa au waliona so kulikuwa na watu wengi wengi wakaogopa kufanya kazi yao nini?
 
Huu mchezo mwisho wake lini ?? maana naiona Tz ya matukio madogo madogo ili kusaulisha watu mambo ya msingi na maana.
 
Je ni miongoni mwa wale Taifa Jipya??
Kama 'NDIO', poleni waalimu wa shule za upili.
 
Kwa hali hii napata wasiwasi na wahudum/madaktari wa hospitality zetu,naomba wachunguzwe zaidi kwenye taluma zao kama wanavigezo vya kuwa katika nafasi hizo(MAJIPU)
 
Na askari anasema kabisa bila uoga,inakuwaje mtu kupelekwa sehemu ya kuhifadhia maiti bila kuhakikishiwa na Dr.kama amekufa? Na watu wa haki za binadamu wapo tu,ndo maana waliambiwa nao ni wapiga dili na siasa tu km wengine wote.Na ile kesi ya singida naona imepotezewa inauma sana jamani.
 
Back
Top Bottom