Soma vizuri ulichoandika alafu unisaidie kukadiria ulipo wewe maana mimi nimeshindwa.
Wapinzani wako ndani ya CCM,wakipanga mikakati na kufanyiana timing na figisu wao kwa wao.Naanza kuelewa Sasa, huwenda ni kweli kwamba Watanzania ni watu wa hovyo na ambao hawawezi Kila kitu na hawawezi Kuibadirisha nchi Yao kutoka Hali mbaya ya umasikini na kuwa nchi yenye neema na uchumi mkubwa
Tumeshindwa kuendesha bandari zetu wenyewe, mbuga zetu tunawapa wageni, Bado tutawapa pia SGR, Tanesco na Hata Ikulu ikiwezekana ili wageni wakae hapo, hii ni kwa sababu moja tu ambayo ni, Majungu na wivu wa kijinga!
Wenzetu wa nchi zinazoendelea, Kila kukicha wanazalisha mawazo mapya ya kipi wafanye ili kitokee kikubwa zaidi,
Hii ni tofauti kabisa na nchi yetu, watu wamejaa wivu na ujinga mwingi, wapo tayari kushinda mitandaoni kumjadili mtu na kumnanga na Bado kusiwe na matokeo yoyote
Ni ajabu kama nchi isimame kisa Paul Makonda ameaminiwa na Rais kupewa ukuu wa mkoa
Umasikini wa Watanzania unatokana na ujinga wa wanaoitwa watetezi wa wananchi kwa maana kwamba wao ni mbadara wa wanaotupeleka chaka na kutufanya tuwe na MAISHA magumu!
Ikiwa mambo haya ni kweli ni yamekuwa agenda kwa wapinzani, basi tunaupinzani wa hovyo na usio na malengo yoyote na nchi yetu
Okay! Tufanye Makonda ameondolewa kwenye nafasi hiyo, wewe unapata faida Gani kama mpinzani, Makonda amekuwa nje ya mfumo wa serikali Karibu miaka miwili unusu hivi, wapinzani, kwa kipindi hiko mmebadirisha nini na kipi kimeshindikana kufanywa na nyinyi baada ya Makonda kupewa nafasi aliyopo?
Tukumbushane tu kwamba, Jambo linaloamriwa na MUNGU mwenyewe kama ambavyo mmeamini Mbowe kuwepo hapo kama M/kiti wa chama chetu CHADEMA kwamba ni Mungu alimpa, ndivyo anaweza kufanya kwa Makonda na kwa mwingine
Suala la dhambi mnayoiona kwa macho yenu kwa Makonda, mkumbuke pia Iko dhambi pia ambayo hamjawahi kuiona kwa mliowaamini kuwa wao ni malaika, lakini jicho la Mungu linajua na kwa wote hawasitahili kuwepo kama mnavyomwombea Makonda
Fanyeni kazi acheni Majungu na wivu wa kijinga!
Makonda chapa kazi usisikilize kelele za chura
Niwakumbushe hivi!
Iwapo Mungu amekuwa upande wa Makonda, mtaomba mno Dua zenu na hazitafanya lolote dhidi yake