Orville Lynn Majors: Je alikuwa ni Malaika wa kifo……!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
majors2.jpg
bilde.jpg
imagesCA72HPXD.jpg
Orville Lynn Majors

imagesCAIF4LXO.jpg
Wahanga waOrville Lynn Majors

Kila mgonjwa aliyewahi kukutana na muuguzi Orville Lynn Majors, alimuona kama nesi mpole na mwenye upendo wa hali ya juu na anayejua kuwahudumia wagonjwa kwa uadilifu mkubwa. Lakini katika hali kushangaza ikawa kila mgonjwa anaehudumiwa na muuguzi huyu katika Hospitali ya wilaya ya Vermillion iliyopo katika jimbo la Indiana akawa anakufa katika mazingira ya kutatanisha.

Mpaka kufikia mwaka 1995 takwimu za idadi ya vifo vilivyokuwa vikitokea katika Hospitali hiyo iliyokuwa na idadi ya vitanda 60 tu vya kulaza wagonjwa ilikuwa ni ya kutisha na hata wafanyakazi wa hospitali hiyo walipoulizwa hawakuwa na majibu ya kuridhisha. Mnamo March 7 1995 uongozi wa hospitali ya Vermillion ulikuwa na wakati mgumu wa kujibu tuhuma hizo kwani kulikuwa na uwezekano wa hospitali hiyo kushitakiwa kwa uzembe wa kusababisha idadi kubwa ya vifo katika hospitali hiyo ambapo watu walihisi kwamba huenda kuna mchezo mchafu unaochezwa na baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo ambao unahitaji kufanyiwa uchunguzi wa kipolisi.

Uongozi wa hospitali hiyo ulitoa ripoti yao kwa askari wa upelelezi ambao ulikuwa ukionyesha kwamba vifo vilivyokuwa vikitokea kwenye chumba maalum cha wagonjwa mahututi vilikuwa vimeongezeka ghafla kutoka wastani wa asilimia 20 kwa mwaka hadi asilimia zaidi ya asilimia100, kwani watu wapatao 147 walikuwa wamepoteza maisha katika chumba hicho kuanzia mwaka 1993. Polisi walianza kuangalia rekodi za utendaji kazi wa kila mfanyakazi wa hospitali hiyo.

Karibu ripoti zote za watu waliopoteza maisha katika hospitali hiyo jina la Orville Lynn Majors lilitajwa kama muuguzi aliyekuwa zamu katika chumba cha wagonjwa mahututi wakati kifo kinatokea. Polisi pia waligundua kwamba vifo hivyo vya mfululizo vilianza wiki chache tangu Orville aanze kazi katika hospitali hiyo. Kwa mujibu wa rekodi zilizopatikana katika hospitali hiyo ilionyesha kuwa Orville alikuwa zamu wakati vifo vya wagonjwa 130 kati ya vifo 147 vilivyotokea katika hospitali hiyo.

Ripoti hiyo ilikuwa ni tofauti na muonekano na tabia aliyokuwa nayo, kwani alikuwa akijulikana na uongozi wa hospitali hiyo pamoja na wagonjwa waliowahi kutumia hospitali hiyo kama muuguzi mwenye kujituma na mwenye upendo kwa wagonjwa. Baada Polisi kutilia mashaka utendaji wake, mnamo March 9 1995 ilibidi uongozi wa hospitali hiyo umsimamishe kazi ili polisi wapate fursa ya kufanya upelelezi wao kwa ufanisi.

Kwa mshangao wafanyakazi wengi wa hospitali hiyo hawakuamini kama Orville angeweza kuwa mtu wa kwanza kutuhumiwa kwa kusababisha vifo vya wagonjwa katika hospitali ile. Hata hivyo kitendo cha Orville kusimamishwa kilikuja kuibua makosa mengi ambayo aliyafanya bila ya kujulikana wakati akiwa kazini.

Katika uchunguzi uliofanywa hospitalini pale ilikuja kugundulika kuwa Orvile alikuwa akifanya kazi za kitabibu kwa wagonjwa wakati alikuwa hana ujuzi nazo, pia ilikuja kugundulika kuwa alikuwa akiwachoma wagonjwa sindano ambazo kitaalamu huchomwa na mtu maalum aliyesomea ujuzi huo. Kutokana na kugundulika kwa makosa hayo mnamo April 1995 Orville alifukuzwa kazi rasmi.

Msemaji wa Bodi ya wauguzi ya Jimbo la Indiana Gerorge Patton Jr. alimzungumzia Orville kama mtu hatari kwa wagonjwa. Kitendo cha Orville kusimamishwa kazi kilikuwa kimeitikisa taaluma ya uuguzi. lakini polisi walikuwa na mtihani mwingine kwani pamoja na kuamini kwamba Orville alihusika na mauaji ya wagonjwa zaidi ya 100 lakini walikuwa na wakati mgumu wa kupata ushahidi wa kumtia hatiani.

Katika ushahidi uliokusanywa katika ripoti ya vifo vingi vya ghafla vilivyotokea katika hospitali hiyo ulionyesha kwamba vilitokana na moyo kushindwa kufanya kazi ghafla au matatizo yatokanayo na mfumo wa kupumua. Wataalam walidai kwamba kama Orville atakuwa ndiye muuaji, basi atakuwa amewauwa kwa kuwachoma sindano yenye kemikali ya Potashiam Kloraid (Potassium Chloride).

Je ni kitu gani kilichosababisha kuwepo na ugumu kuthibitisha madai hayo?

Kwa kawaida sindano yenye kemikali ya Potashiamu Kloraidi hutumika kwa kuwauwa watu walihukumiwa kunyongwa nchini Marekani, ambapo kwa upande wa Orville kulikuwa hakuna ushahidi wa kuthibitisha madai hayo. Wapelelezi wa Polisi walitumia miezi 15 kutafuta ushahidi wa kumfungulia mashitaka Orville lakini bado walikwama kupata ushahidi madhubuti.

Ingawa walikuwa wamepata hizo kemikali za potashiamu kloraidi nyumbani kwake lakini huo haukuwa ushahidi wa kuthibitisha madai yao. Pamoja na polisi wa upelelezi kuchukuwa miaka 3 katika upelelezi wao dhidi ya Orville ambao uliwagharimu walipa kodi wa jimbo la Indiana kiasi cha dola milioni moja na nusu lakini bado ushahidi wa kumtia Orville hatiani ulikuwa ni wa kimazingira zaidi.

Kwani wapelelezi wa polisi waliamini kwamba, ikiwa ni kweli Orville alihusika na mauaji ya wagonjwa zaidi ya 130 katika kipindi cha miezi 32 aliyofanya kazi katika hospital hiyo, basi ni wazi kuwa hakuacha ushahidi wowote nyuma yake zaidi ya takwimu tu.

Hata hivyo bado polisi walikuwa na tegemeo jingine la ushahidi kutoka kwa mtaalamu kutoka jimbo la Washington ambao waliongozwa na mwanasayansi aliyejulikana kwa jina la Steven Lamm.
Katika uchunguzi wao ambao uligharimu kiasi cha dola laki tatu, wataalamu hao walikiri kwamba kwanza kuna ukweli wa kimazingira wa kumuhusisha Orville na vifo vya wagonjwa 130 kati ya wagonjwa 147 waliopoteza maisha katika Hospitali hiyo, ambavyo vyote vilitokea Orville akiwa kazini.

Katika ripoti yao ilionyesha kwamba wagonjwa wote waliopoteza maisha katika Hospitali wakati Orville akiwa kazini walikuwa wakifa kila baada ya masaa 23 na dakika 1, isipokuwa mgonjwa mmoja ambae alifariki baada ya masaa 551 na dakika 6, ambapo Orville hakuwepo kazini. Mmoja wa wauguzi wanaofanya kazi katika hospitali hiyo alidai kwamba hali ilikuwa mbaya sana kutokana na kushuhudia vifo vya wagonjwa kila Orville awapo kazini.

Muuguzi huyo alikiri kwamba kuna wakati walikuwa wakicheza kamari kwa kuwekeana dau juu ya mgonjwa gani atakufa pindi Orville atakapokuwa kazini, na mara zote mshindi alikuwa akipatikana na kujizolea kitita cha fedha. Pamoja na ushahidi huo ambao ulielemea zaidi kwenye minong'ono na maneno ya mitaani, lakini bado wapelelezi walikuwa na wakati mgumu wa kujenga ushahidi madhubuti wa kumtia Orville hatiani.

Waliopoteza wapendwa wao wahusishwa na upelelezi...!

Ili kupata ushahidi huo ilibidi wapelelezi wa polisi watumie muda mwingi kuwaita watu ambao ndugu zao walipoteza maisha katika hospitali hiyo na wanao ushahidi kwamba kwa njia moja au nyingine Orville alihusika. Mtu wa kwanza kujitokeza alikuwa ni kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Russell Firestone au kwa jina la utani aliitwa "Rusty".

Kijana huyu alimpoteza baba yake aliyekuwa na umri wa miaka 74 wakati huo. Kijana huyo akitoa ushahidi wake mbele ya wapelelezi wa Polisi, Rusty alisema kwamba baba yake alilazwa katika hospitali hiyo mnamo December 12, 1994, kwa wiki kadhaa baada ya kusumbuliwa na tatizo la kuzimia ghafla. Kijana huyo aliendelea kuwaeleza Polisi kwamba baba yake alipewa ruhusa kabla ya kulazwa tena siku sita baadae katika hospitali hiyo hiyo.

Baada ya kupata tarifa kuwa baba yake amelazwa tena, Rusty alikwenda kumuona na alipofika hospitalini hapo alimkuta Orville na muuguzi mwingine wakiwa pembeni ya kitanda cha baba yake, alipowakaribia alimsikia yule muuguzi akisema kwa sauti "mwanae huyo anakuja" Alipofika karibu na kitanda alichokuwa amelala baba yake alimuona baba yake akipepesa macho na mara ghafla akaacha kupepesa macho na kubaki kimya kama vile mtu aliyekata roho. Alipowauliza kwamba baba yake amepata tatizo gani, walimjibu kuwa hajui, hata hivyo Orville alitoa mashine yake ya kupimia mapigo ya moyo na kumpima baba yake, lakini kulikuwa hakuna dalili za mtu kuwa hai. Baadae Orville alichukuwa box lake alilokuwa nalo na kuchukuwa sindano kisha akaijaza dawa asiyoifahamu na kumchoma baba yake na kutoweka.

Rusty alimuuliza yule muuguzi kama ile sindano ilikuwa ni ya dawa gani lakini hakupewa jibu na badala yake yule muuguzi aliendelea na shughuli zake. Baadae Orville alirejea na hapo ndipo yule muuguzi alipomuuliza kwamba Rusty anataka kufahamu kama ile sindano ilikuwa ni ya nini?
Kwa maneno yake mwenyewe Orville alimjibu kwa mkato "baba yako amekwisha fariki, je kuna mtu unahitaji kumuita?" kisha wote wawili wakatoweka na kumuacha pale peke yake. Mtu mwingine liyetoa ushahidi wake alikuwa akijulikana kwa jina la Robert Doran.

Akiongea na wapelelezi wa Polisi, Robert alisema kwamba anakumbuka baba yao John Andrew Doran aliyekuwa na umri wa miaka 76 wakati huo, alilazwa katika Hospital hiyo mnamo October 1994. Akisimulia zaidi Robert alisema kwamba baba yao alianza kupoteza uzito ghafla na kuwa dhaifu kulikoambatana na kizunguzungu, hivyo walipoona hali ya baba yao imebadilika ghafla vile yeye na mkewe aliyemtaja kwa jina la Marjorie waliamua kumpeleka katika katika hospitali ya wilaya ya Vermillion kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Walipofika Hospitalini hapo baba yao alilazwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi. Siku iliyofuata walirejea pale Hospitalini ili kufuatilia vipimo vya baba yao, lakini walipofika walikuta baba yao amehamishiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi. Robert alibainisha kwamba hapo ndio kwa mara ya kwanza alipomuona Orville.

Kwa maneno yake mwenyewe Robert alisema "Huyu kijana mwenye mwili mkubwa(Akimaanisha Orville kwa sababu alikuwa ni mnene) alifika pale tulipo na kutusalimia na kisha alijitambulisha kwetu"

Huku akimnukuu Orville Robert alisema, "Jina langu naitwa Orville Lynn Majors, mimi ndie nitakayekuwa muuguzi wa baba yenu leo, si mlikuwa mkihitaji muuguzi Mahiri?" kwa jinsi alivyokuwa akizungumza alionekana kuwa ni muuguzi mzuri anayeifahamu kazi yake na ambaye aliguswa na ugonjwa wa baba yetu, aliendelea kubainisha Robert.

Baadae majira ya mchana Robert alikiri kumuona Orville akimchoma baba yao sindano ambayo wote hawakuifahamu na baada ya sindano hiyo baba yao alionekana kupua kwa shida na kuonekana kama vile anataka kupoteza fahamu.Akiwa amesimama pembeni Orville alikuwa akimpiga piga begani baba yao huku akimwambia "subiri kidogo nakuandalia dawa nyingine"

Baadae baba yao alifariki kwa kile kilichoelezwa na daktari kwamba amefariki kwa ugonjwa wa shambulio la moyo (Heart Attack). Robert aliendelea kuwaeleza wapelelezi wa Polisi kwamba baada ya
habari za hospitali hiyo kutuhumiwa kusababisha vifo vya watu wengi kutoka katika vyombo vya habari, yeye na mkewe Marjorie Doran waligundua kwamba huenda na wao walishuhudia mauaji ya baba yao akiuwawa na Orville mbele ya macho yao. Kwa maneno yake mwenyewe Robert alisema " Tulijiona wote tuwajinga kwa kukaa kimya baada ya tukio lile ambalo lilifanyika mbele ya macho yao"

Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 1997, bado jopo la wapelelezi walijua dhahiri kwamba isingekuwa rahisi kwao kupata ushahidi wa kina wa kumtia hatiani Orville Lynn Majors.

Mtuhumiwa Kizimbani......!

Hata hivyo kesi ya Orville ilianza kusikilizwa rasmi mnamo December 30 1997 katika mahakama ya wilaya ya Clay. Huku akionekana kutokuwa na wasiwasi, Orville alikuwa ametulia wakati Jaji wa mahakama hiyo aliyejlikana kwa jina la Ernest Yelton alimsomea mashitaka ambayo ni ya kuhusika na mauaji ya watu sita, ambapo akipatikana na hatia adhabu yake itakuwa ni kifungo cha miaka isiyopungua 65.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo wakili wa Orville aliyejulikana kwa jina Marshall Pinkus, alikanusha mashtaka yote yaliyosomwa, kwa niaba ya mteja wake.
Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya Orville kusomewa mashitaka, wakili huyo aliwaambia waandishi wa habari kwamba mteja wake amestushwa sana na mashtaka yale.

Wakili yule aliendelea kusema,

"nadhani kuwa baada ya miaka mitatu mingine huenda mtu mwingine akafunguliwa mashtaka yanayofanana na haya kwa sababu vifo vyote vilivyotokea katika Hospitali ya wilaya ya Vermillion kwa jinsi ninavyofahamu vilikuwa ni vifo vya kawaida kabisa. Siamini kabisa kama kuna mtu alihusika na vifo hivyo."

Akiendelea kufafanua kauli yake wakili yule alisema kwamba kilichotokea ni kuwa kulikuwa na wagonjwa ambao wengi walikuwa wazee ambao walifikishwa katika hospitali hiyo kwa matibabu na kama inavyojulikana kuwa mji wa Vermillion ni mji wa pili kwa ongezeko la watu katika jimbo la Indiana hivyo hospitali hiyo ilishuhudia ongezeko hilo la wagonjwa wengi wazee huku kukiwa hakuna maandalizi yoyote ya kuongeza wataalamu. Wakili huyo aliendelea kubainisha kwamba kimsingi Hospitali ya Vermillion haina wataalam wa kutosha ambao wangekwenda sambamba na ongezeko hilo la wagonjwa ambao hasa wengi walikuwa ni wazee, ambapo kama wangekuwepo vifo hivyo visingetokea.

Naye mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo aliyejulikana kwa jina la Mark Greenwall akionekana kujiamini aliwaambia waandishi wa habari kuwa anayo kesi nzito dhidi ya Orville na kesi hiyo inategemea zaidi ushahidi kutoka kwenye jopo lake la wapelelezi wakishirikiana na wataalamu wa kitabibu ambao ndio waliopewa jukumu la kuchunguza vifo 160 vilivyotokea katika hospitali hiyo kati ya mwaka 1993 na mwaka 1995, ambapo asilimia 50 ya vifo hivyo vilionekana kutokea katika mazingira ya kutatanisha.

Akizungumzia kitendo cha Orville kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya watu 6 tu badala ya watu 160 ambao ndio aliokuwa akituhumiwa kuwauwa awali, Greenwall alisema kwamba kitendo cha Orville kufunguliwa mashtaka ya watu sita tu hakimaanishi kuwa kulikuwa na vifo vya watu sita tu, bali walichukuwa kesi za watu sita ambazo walikuwa na uhakika wa kupata ushahidi wa kutosha ambao ungemtia Orville hatiani bila ya kutia shaka yoyote. Baada ya Orville kusomewa mashtaka, nje ya mahakama ile ambayo ilifurika umati wa watu ambao walikuwa wakiifuatilia kesi ile ambayo ilivuta hisia za watu wengi, miongoni mwao wapo waliokuwa wakimtetea Orville.

Akizungumza nje ya mahakama mdogo wake na Orville aitwae Debbie McClelland alisema kuwa kaka yake hana hatia kwa sababu hakuhusika na mauaji ya yale. Kwa maneno yake mwenyewe Debbie alisema "tangu uchunguzi wa kesi hii uanze na mpaka kufikia sasa hivi ambapo kesi ipo mahakamani wazazi wetu wamekuwa na wakati mgumu sana na hii imevuruga kwa kiasi kikubwa maisha yao lakini mungu anatupa nguvu na kuendelea na maisha yetu kama kawaida, japokuwa tunatiwa moyo na majirani zetu lakini hali si ya kuridhisha pale nyumbani"

Naye mwanamke mwingine aliyejulikana kwa jina la Ida Harris ambaye aliwahi kuwa muhudumu wa wazazi wa Orville pale nyumbani kwao wakati fulani alisema kuwa kwa jinsi anavyomfahamu Orville haamini kwamba alihusika na mauaji yale, na anaona kabisa kwamba hawamtendei haki. Kesi ile ambayo iliahirishwa kwa zaidi ya mwaka mmoja hadi mwaka 1999, ilipangwa kuhamishiwa katika mji mwingine uitwao Brazil ambao upo maili kadhaa kutoka katika mji wa Vermillion kusini mwa mji mwingine wa Terre Haute, na hii ilitokana na kwamba mji huo ndipo idadi ya watu waliopoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Vermillion County ni kubwa.

Mashahidi wapatao 79 walijitokeza kutoa ushahidi wao ambapo wengi walikiri kumuona Orville akiwachoma sindano ambazo zilipelekea vifo vya wapendwa wao, ambapo kimsingi alikuwa haruhusiwi kuwachoma wagonjwa sindano hizo. Mnamo October 17, 1999 Orville alipatikana na hatia ya kuhusika na mauaji ya watu sita na hivyo kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani, bila uwezekano wa kifungo cha nje (Parole).
 
Ni Ijumaa nyingine tena, kama kawaida leo nimekuja na kesi hii iliyotokea kule nchini Marekani mwishoni mwa miaka 1990. Kesi hii imenivutia sana na ndio sababu ya kuiweka hapa ili wote tupate kujifunza, naamini mtakapoisoma kwa makini na kutafakari kwa kina kuna jambo ambalo kwa kweli jamii yetu inabidi ijifunze hasa kufuatilia matibabu ya wagonjwa wetu. Kuna uzembe mwingi sana katika baadhi ya hospitali zetu hapa nchini, lakini je, kuna takwimu zinazochukuliwa mara kwa mara ili kujua ni mwaka gani kumekuwa na vifo vingi ukilinganisha na miaka mingine, na pia kutafuta sababu ya vifo hivyo. Hapa sizungumzii vifo vya magonjwa ya milipuko, la hasha, nazungumzia vifo vinayotokana na maradhi mbalimbali, yakiwemo yale yanayotibika na yale yasiyotibika. Nachelea kusema kwamba, iwapo atatokea muuguzi kama Orville Lynn Majors hapa nchini, huenda tukazika maajuza wengi kupindukia na wala watu wasijue kinachoendelea.

Kuna haja ya kuchukuwa tahadhari, haya mamabo yapo sana.
 
Mtambuzi sijui kama umeikata sana kesi hii naona kama kuna mapungufu ya kiupelelezi, haijaonekana sababu ya mauaji ya vikongwe hawa ina maana ilikuwa ni kwa ajili ya dau la kamali tu?

Uzembe wa ufatiliaji matibabu ya wagonjwa wetu unaanzia kwa ndugu wa mgonjwa mpaka kwa wauguzi wetu ukiongeza na upungufu ya nyezo kwa madaktari wetu.
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi sijui kama umeikata sana kesi hii naona kama kuna mapungufu ya kiupelelezi, haijaonekana sababu ya mauaji ya vikongwe hawa ina maana ilikuwa ni kwa ajili ya dau la kamali tu?

Uzembe wa ufatiliaji matibabu ya wagonjwa wetu unaanzia kwa ndugu wa mgonjwa mpaka kwa wauguzi wetu ukiongeza na upungufu ya nyezo kwa madaktari wetu.
taijike ni kweli kabisa sababu ya vifo hapa kwetu haiwezi kuwa muuguzi au daktari ,,,,hapa bongo maisha yenyewe tu na mazingira yetu ni sababu tosha ya vifo.
 
Ni Ijumaa nyingine tena, kama kawaida leo nimekuja na kesi hii iliyotokea kule nchini Marekani mwishoni mwa miaka 1990. Kesi hii imenivutia sana na ndio sababu ya kuiweka hapa ili wote tupate kujifunza, naamini mtakapoisoma kwa makini na kutafakari kwa kina kuna jambo ambalo kwa kweli jamii yetu inabidi ijifunze hasa kufuatilia matibabu ya wagonjwa wetu. Kuna uzembe mwingi sana katika baadhi ya hospitali zetu hapa nchini, lakini je, kuna takwimu zinazochukuliwa mara kwa mara ili kujua ni mwaka gani kumekuwa na vifo vingi ukilinganisha na miaka mingine, na pia kutafuta sababu ya vifo hivyo. Hapa sizungumzii vifo vya magonjwa ya milipuko, la hasha, nazungumzia vifo vinayotokana na maradhi mbalimbali, yakiwemo yale yanayotibika na yale yasiyotibika. Nachelea kusema kwamba, iwapo atatokea muuguzi kama Orville Lynn Majors hapa nchini, huenda tukazika maajuza wengi kupindukia na wala watu wasijue kinachoendelea.

Kuna haja ya kuchukuwa tahadhari, haya mamabo yapo sana.

ukisikia kuna watu na viatu, maana yake halisi ndiyo hii au ukisikia kuna binadamu amevaa ngozi ya kondoo wakati ndani yake ni mbwa mwitu mkali, ujue ndo kama hivi! Nimepata funzo la haraka kuwa pia si kila anayeonekana mwema machoni, ni mwema pia mpaka rohoni! Mambo aliyoyafanya huyo muuguzi, hayakuwa ya kibinaadamu kabisa!

Mbali na hilo, naungana na wewe Mtambuzi kuwa kuna vifo vingi visivyo na sababu ambavyo hutokea kwenye hosp zetu (Muhi2, Mwananyamala, amana nk) lakini hatujajijengea utaratibu wa kufuatilia vyanzo na sababu za vifo kama wenzetu. Kupitia makala hizi, nafikiri ni muhimu mtu mmoja mmoja kuanza kuchukua hatua kwa kufuatilia kwa nafasi yake jambo lolote lile ambalo anaona linatendwa kinyume na taratibu. Kwa utaratibu huo, tunaweza kujikuta na sisi tunafikia hatua ya kuwa makini na mambo yanayohusu afya zetu na maisha yetu kwa ujumla.

Thanks Mtambuzi kwa uzi huu.

HP
 
Angels of Death....
Hawa wako wengi kuna yule wa UK Dr Shipman, huyu aliua zaidi ya wagonjwa 260, Charles Cullen yeye aliconfess kuua 35 lakini wanaweza fikia 40 nimekuwa nikivutiwa kufuatilia kesi za hawa Doctors na Nurses wanaogeuka wauaji inatisha pale mtu unayeamini kuwa anaweza kuokoa maisha yako anapogeuka na kuyatoa.
Mtambuzi umeongelea kesi ya hapa kwetu, mimi naamini tunaishi kwenye society iliyofumbwa mengi kutokana na kutokuwa na kiwango cha intelligence waliyokuwa nayo wenzetu, we let so many things fly by....i seriously wonder how many serial killers, rapists, murderers, gangstars...you name it... are lurking our streets
 
Last edited by a moderator:
Thanks Gustavo,
Kwakweli umenifanya nikumbuke jambo lililowahi kunihuzunisha duniani sana kwa ajili ya mambo ya hawa watabibu wetu.

Jamani nani atukamatie na hawa wa huku kwetu? Yaani ni mauaji mfurulizo ukifuatilia.

Madr uchwara kibao, manesi ndio usiseme red cross leo kesho anakudunga sindano.

Kuna dada alipewa chroquine na dr mmoja kaja dr mwingine akamtundikaquinin na dada akapotea duniani hii si murder kabisa!
Lakini ndugu hawakufanya lolote jamii ikabaki kulalamika tu.

Kuna mambo mengi yanatokea katika hosipitali zetu hapa, sema takwim ndogo na ubinafsi wa wa TZ basi mtu likimpata ni lake si la jamii no follow up katika matukio kutoka kwa jamii kwa ujumla wake .

\So sad jamani
 
Angels of Death....
Hawa wako wengi kuna yule wa UK Dr Shipman, huyu aliua zaidi ya wagonjwa 260, Charles Cullen yeye aliconfess kuua 35 lakini wanaweza fikia 40 nimekuwa nikivutiwa kufuatilia kesi za hawa Doctors na Nurses wanaogeuka wauaji inatisha pale mtu unayeamini kuwa anaweza kuokoa maisha yako anapogeuka na kuyatoa.
Mtambuzi umeongelea kesi ya hapa kwetu, mimi naamini tunaishi kwenye society iliyofumbwa mengi kutokana na kutokuwa na kiwango cha intelligence waliyokuwa nayo wenzetu, we let so many things fly by....i seriously wonder how many serial killers, rapists, murderers, gangstars...you name it... are lurking our streets
Elizabeth Dominic, ahsante kwa maoni yako mazuri.
Hizo kesi za akina Dr Shipman na Charles Cullen nimezisoma zote lakini nilivutiwa zaidi na hii ya Orville Lynn Majors na ndio nikaamua kuiweka hapa. Zipo kesi nyingi zinazofanana na hizi, na nyingine hazijapatiwa ufumbuzi hadi leo.
Kama nilivyosema awali ni kweli kwamba inatakiwa iundwe bodi ya kuchunguza mienendo ya hospitali zetu na pia kuwe na utaratibu wa kila hospitali kutoa takwimu za vifo vinavyotokea katika hospitali hizo kila mwezi ili kuepuka kesi zinazofanana na hii.
 
Last edited by a moderator:
Elizabeth Dominic, ahsante kwa maoni yako mazuri.
Hizo kesi za akina Dr Shipman na Charles Cullen nimezisoma zote lakini nilivutiwa zaidi na hii ya Orville Lynn Majors na ndio nikaamua kuiweka hapa. Zipo kesi nyingi zinazofanana na hizi, na nyingine hazijapatiwa ufumbuzi hadi leo.
Kama nilivyosema awali ni kweli kwamba inatakiwa iundwe bodi ya kuchunguza mienendo ya hospitali zetu na pia kuwe na utaratibu wa kila hospitali kutoa takwimu za vifo vinavyotokea katika hospitali hizo kila mwezi ili kuepuka kesi zinazofanana na hii.

Uko sawa, imefikia wakati kufanywa zoezi hili, nadhani haitaji utaalamu sana au resources nyingi sana kujua watu wangapi wanafariki na ni kwasababu zipi, uzembe umeainishwa hapo juu na NATA lakini kuna mengi nadhani kuna kesi zingine utakutana na nurse katili hata dokta na atafanya vitu kwa dhamira hasa ya kuua na mara itachukuliwa ni uzembe bila uchunguzi wa kina na usikute ana mlolongo wa kesi kama hizo......ni masuala ya kuzingatia kwakweli. Hongera na asante Mtambuzi kwa kuleta mikasa hii, ninajifunza hasa
 
Last edited by a moderator:
Kwa hapa Tanzania, mikasa kama hii ni mingi sana, na kama kutakuwa na chombo cha kufuatilia basi wataalamu wengi sana hasa madaktari na wauguzi hata wafamasia watafungwa. kuna vifo vingi tu vinavyotokea kwa sababu ya uzembe. Changamoto ni kuwa: 1.wananchi hawajui haki zao 2. uhaba wa wataalamu wa afya wenye sifa, maana ukienda zahanati za serikali huko vijijini medical attendant anayefanya kazi za usafi muhimbili ndio daktari na mfamasia, anazalisha, anatibu na anatoa dawa huyo huyo, sasa ukifiwa na kumshitaki, utamfunga tu, lakini tatizo ni rasilimali watu.3. mfumo wa afya wa nchi za wenzetu uko mbali kuliko sisi, maana mfano kama mgonjwa amekufa kwa sababu ya overdose ya dawa, ili upate kuangalia kiwango cha dawa au sumu hiyo, maabara ni mbili tu nchini, muhimbili upande wa chuo na kwa mkemia mkuu, na itachukua muda. Wagonjwa wengi sana wanakufa hapa nchini kwa sababu ya poor management (misdiagnosis)
Uko sawa, imefikia wakati kufanywa zoezi hili, nadhani haitaji utaalamu sana au resources nyingi sana kujua watu wangapi wanafariki na ni kwasababu zipi, uzembe umeainishwa hapo juu na NATA lakini kuna mengi nadhani kuna kesi zingine utakutana na nurse katili hata dokta na atafanya vitu kwa dhamira hasa ya kuua na mara itachukuliwa ni uzembe bila uchunguzi wa kina na usikute ana mlolongo wa kesi kama hizo......ni masuala ya kuzingatia kwakweli. Hongera na asante Mtambuzi kwa kuleta mikasa hii, ninajifunza hasa
 
Hii kweli ni fundisho kwa wauguzi wetu wenye roho kama huyo muuguzi.

Sidhani kama uchunguzi ulifanywa kwa kina kubaini kwa nini alikuwa akiwaua wagonjwa wake.
 
Hii kweli ni fundisho kwa wauguzi wetu wenye roho kama huyo muuguzi.

Sidhani kama uchunguzi ulifanywa kwa kina kubaini kwa nini alikuwa akiwaua wagonjwa wake.

Huwezi jua yeye anadai wagonjwa wengi waliofika katika wodi ile walikuwa ni wazee labda alikuwa na campaign ya punguza wazee.lol!

Anahatari sana huyo, labda walikuwa wanaona taabu kuhudumia wagonjwa mahututi na ndipo akaamua kuwa anawapangua mmoja baada ya mmoja ili asiwe na kazi kubwa ya kuwahudumia.

Kwa kweli nikitendawili ukijiuliza ni kwa nini afaye kitendo cha kikatili kama hicho?
Maisrael kama yeye wapo wengi TZ. Inabdi jamii izinduke na kuanza kufuatilia kwa kina matibabu na huduma zinazotolewa kwa wagonjwa wao.
 
Ni Ijumaa nyingine tena,
kama kawaida leo nimekuja na kesi hii iliyotokea kule nchini Marekani
mwishoni mwa miaka 1990. Kesi hii imenivutia sana na ndio sababu ya
kuiweka hapa ili wote tupate kujifunza, naamini mtakapoisoma kwa makini
na kutafakari kwa kina kuna jambo ambalo kwa kweli jamii yetu inabidi
ijifunze hasa kufuatilia matibabu ya wagonjwa wetu. Kuna uzembe mwingi
sana katika baadhi ya hospitali zetu hapa nchini, lakini je, kuna
takwimu zinazochukuliwa mara kwa mara ili kujua ni mwaka gani kumekuwa
na vifo vingi ukilinganisha na miaka mingine, na pia kutafuta sababu ya
vifo hivyo. Hapa sizungumzii vifo vya magonjwa ya milipuko, la hasha,
nazungumzia vifo vinayotokana na maradhi mbalimbali, yakiwemo yale
yanayotibika na yale yasiyotibika. Nachelea kusema kwamba, iwapo
atatokea muuguzi kama Orville Lynn Majors hapa nchini, huenda tukazika
maajuza wengi kupindukia na wala watu wasijue kinachoendelea.

Kuna haja ya kuchukuwa tahadhari, haya mamabo yapo sana.

dah! nilimiss juzi na jana,nimepta nafasi ya kuisoma leo,pamoja sana mkuu mtambuzi,je jamaa alikula mvua ngap? na jee nini sababu ya kufanya hayo mauaji?
 
dah! nilimiss juzi na jana,nimepta nafasi ya kuisoma leo,pamoja sana mkuu mtambuzi,je jamaa alikula mvua ngap? na jee nini sababu ya kufanya hayo mauaji?
Scofied Orville alihukumiwa kifungo cha maisha jela bila uwezekano wa Parole.
 
Last edited by a moderator:
Huwezi jua yeye anadai wagonjwa wengi waliofika katika wodi ile walikuwa ni wazee labda alikuwa na campaign ya punguza wazee.lol!

Anahatari sana huyo, labda walikuwa wanaona taabu kuhudumia wagonjwa mahututi na ndipo akaamua kuwa anawapangua mmoja baada ya mmoja ili asiwe na kazi kubwa ya kuwahudumia.

Kwa kweli nikitendawili ukijiuliza ni kwa nini afaye kitendo cha kikatili kama hicho?
Maisrael kama yeye wapo wengi TZ. Inabdi jamii izinduke na kuanza kufuatilia kwa kina matibabu na huduma zinazotolewa kwa wagonjwa wao.
NATA Kesi hii iliegemea zaidi ushahidi wa kimazingira na ilikuwa ni vigumu kujua motive ya muuaji.
hata hivyo ushahidi mzito uliotolewa pale mahakamani dhidi ya Orville ulimtia hatiani pasi na shaka yoyote. (He was convicted without reasonable doubt)
 
Last edited by a moderator:
Kwa hapa Tanzania, mikasa kama hii ni mingi sana, na kama kutakuwa na chombo cha kufuatilia basi wataalamu wengi sana hasa madaktari na wauguzi hata wafamasia watafungwa. kuna vifo vingi tu vinavyotokea kwa sababu ya uzembe. Changamoto ni kuwa: 1.wananchi hawajui haki zao 2. uhaba wa wataalamu wa afya wenye sifa, maana ukienda zahanati za serikali huko vijijini medical attendant anayefanya kazi za usafi muhimbili ndio daktari na mfamasia, anazalisha, anatibu na anatoa dawa huyo huyo, sasa ukifiwa na kumshitaki, utamfunga tu, lakini tatizo ni rasilimali watu.3. mfumo wa afya wa nchi za wenzetu uko mbali kuliko sisi, maana mfano kama mgonjwa amekufa kwa sababu ya overdose ya dawa, ili upate kuangalia kiwango cha dawa au sumu hiyo, maabara ni mbili tu nchini, muhimbili upande wa chuo na kwa mkemia mkuu, na itachukua muda. Wagonjwa wengi sana wanakufa hapa nchini kwa sababu ya poor management (misdiagnosis)
msafi nakubaliana na wewe kuhusiana na nchi yetu kuwa na upungufu mkubwa wa wataalamu wa kitabibu, lakini sidhani kama ni vyema kukubali tu kirahisi watu waendelee kupoteza maisha kwa uzembe wa wataalamu hao wasiozingatia ukomo wa kiwango chao cha utaalamu.
Kila mtaalamu ana limitation zake kwa hiyo mtu kukurupuka na kufanya kazi ambayo hana utaalamu nayo eti kwa sababu tu alikuwa na nia nzuri ya kumtibu mgonjwa, hilo haliwezi kukubalika, siku hizi sayansi na teknolojia imekua sana kuna mitandao ya mawasiliano ambayo inaweza kurahisisha mawasiliano kati ya wataalamu wetu hawa na kubadilishana uzoefu.

Ni mpaka pale mtu anakapokuwa convicted kwa makosa ya aina hiyo ndipo wataalamu wachache wasiofuata maadili ya kazi zao watakaposhtuka na kujua kwamba ipo sheria na inafanya kazi......
lakini tukinyamaza kimya itakuwa ni business as usual.............

Kuna uzembe mwingi sana katika hospitali za binafsi, hapo ndipo kilipo kichaka cha wataalamu hawa feki wanaodhulumu roho za watanzania masikini....
watu wanaona kabisa kwamba hawana utaalamu wa kumtibu mgonjwa, lakini watamuweka hapo ili kuongeza mapato yao, na mgonjwa akionekana kuzidiwa kabisa, ndipo hutoa ruhusa apelekwe kwenye hospitali ya rufaa wakati huo ishakuwa too late, mgonjwa anafariki, tamaa ya fedha walio nayo wamiliki hawa wa hospitali binafsi inasababisha umauti wa mgonjwa huyu.

Ipo sheria na inafanya kazi, watanzania inabidi sasa tuamke hata kama itakuchukua miaka kumi, lakini lazima huyo daktari au mmiliki wa hospitali wa- face consequences
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom