Operesheni Sangara pamoja na vuguvugu la mabadiliko iliyoingia katika Jimbo la Ulanga Mashariki linaloongozwa na aliyekuwa waziri wa afya Dk Haji Mponda kabla ya kutemwa kwenye baraza la sasa imegundua mambo mengi ya uonevu kwa Wananchi wa Ulanga. Baadhi ya mambo ambayo yaliyotolewa kama kero na wananchi ni haya yafuatayo:-
Leo Operesheni inafanyika katika Kata 8 za Jimbo la Ulanga Magharibi na sasa Makamanda ndio wameingia Mahenge. Kesho itakuwa ni kata 4 za Ulanga Mashariki na 4 za Ulanga Magharibi
- Katika kata ya Usangule na Mtimbila akina mama wanaojifungua hupaswa kulipia Tsh 15,000/= kwa kila mtoto wa kiume anayezaliwa na Tsh 20,000/= kwa kila mtoto wa kike anayezaliwa.
- Wananchi wanalazimishwa kujiunga na jeshi la mgambo na wale wanaokataa hukamatwa na kulazamishwa kulipa faini ya Tsh 20,000/= bila ya risiti
- Baadhi ya wafugaji wa Kisukuma walipigwa faini ya Tsh 1,000,000/= kila mmoja bila ya risiti kwa tuhuma za ng'ombe wao kuharibu mazingira wakati wakiwa wanalima.
- Mkuu wa Wilaya na OCD wameweka kituo cha kukusanya ushuru wa mazao kwa wakulima wa Tsh 3700/= kwa kila gunia la mpunga ambapo hupitia makusanyo kila weekend.
- Kuna tuhuma za askari kuwapiga wananchi hadi kuwaua
Leo Operesheni inafanyika katika Kata 8 za Jimbo la Ulanga Magharibi na sasa Makamanda ndio wameingia Mahenge. Kesho itakuwa ni kata 4 za Ulanga Mashariki na 4 za Ulanga Magharibi