Ombi maalumu kwa makamu wa Rais - Shein

MwK, is it the right time?? Well, we need something done fast but ina maana Muungwana ameweka kadi zote mezani na hana la zaidi???????

I believe he is more brilliant than already observed......

Au mimi ndio nina daydream wakuu?
 
MwK, is it the right time?? Well, we need something done fast but ina maana Muungwana ameweka kadi zote mezani na hana la zaidi???????

I believe he is more brilliant than already observed......

Au mimi ndio nina daydream wakuu?

Yaani unahitaji kuamka haraka sana. Hizi safari za Kikwete anazofanya sasa hivi kuzunguka dunia nzima ni part ya strategy.

Amka unuse kahawa mwenzangu!
 
Dada yangu naona umo katika kuumiza kichwa kutaka kuinusuru mama Tz na matumaini yako kwa Mungwana ni zero, lakini nina shaka na ombi lako kwani kama Shein ni matunda ya CCM basi na yey hiyo kazi haiwezi kwani nionavyo mimi ni kuwa tatizo sio mtu tu bali "system" yote imeoza, CCM ni genge fulani lililojichimbia kwenye madaraka na wote wana ugonjwa mmoja wa kutaka kuifisidi nchi hii. Mimi nafikiri kazi ya mikasi ndio anaimdu vyema, tutafute mwengine wa kumumkabidhi barua hii.
 
Ingawa nakubali kwamba Kikwete amekuwa mbwa choka asiye meno (ashakum si matusi, ni lugha ya rangi tu) au kama bibie alivyogonga umombo "incapacitated", nafahamu pia kuwa Shein hawezi kufanya lolote jipya.

Shein amekuwa sehemu ya ufisadi tangu enzi ya Mkapa, hata kama hataweza kuhusishwa moja kwa moja na ufisadi tukumbuke Shein amekubali kuufumbia macho na pia amekubali kuchaguliwa kwa fedha za wizi CCM ilizoiba BOT.

Kwa kifupi Shein, kama Kikwete,Mkapa, Chenge,Balali na ma goons wengine wengi wa CCM, hana "moral high ground" ya kuweza kufanya vitu kama vita dhidi ya rushwa kwani yeye mwenyewe ananuka rushwa kama nilivyoainisha hapo juu.

Tunahitaji radical changes, sio cosmetic change.
 
Mheshimiwa sana Dk Shein,

Naomba nichukue nafasi hii kwanza kwa kukupongeza kwa kazi nzuri sana unayofanya ya kufungua majengo, vituo, maduka ya nyama na biashara mpya katika nchi. Samahani kidogo kwa kuiita hii kazi yako kwa jina la kazi ya mikasi. Pamoja na haya, natoa wito maalumu kwako na kwa ofisi yako kulinusuru taifa letu tukufu la Tanzania.

Ninakumbusha jambo unalolielewa vyema kabisa kuwa kikatiba wewe una ruhusa ya kufanya kazi ya uraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania pale mambo fulani fulani yanapojitokeza. Moja ya mambo hayo ni pale rais wa nchi anapokosa uwezo wa kutenda kazi zake kikamilifu (incapacitated). Najua wataalamu wa sheria na lugha watatumia tafsiri mbalimbali kuelezea hili neno incapacitated lakini kwa mtizamo wangu na watanzania wengi, Rais Kikwete kwa sasa anafit kabisa definition hii ya kukosa uwezo wa kutenda kazi zake kwa ukamilifu.

Ninakuandikia hili huku nikikumbuka maneno ya mtanzania mmoja aliyewashauri watanzania kwenda kunywa chai na Kikwete kama walipenda sura yake au tabasamu lake. Kazi ya uraisi ni kubwa kuliko Kikwete alivyofikiria na inawezekana ameshindwa tu kusema hili wazi. Kwa vile mkuu wako wa kazi sasa ameshindwa kazi yake na anapeleka taifa la Tanzania kubaya, ni jukumu lako kutimiza kiapo ulichoapa kuwa utachukua kazi ya urais na kufanya kazi yako kwa maadili pindi itakapothibitika kuwa raisi hana uwezo tena wa kufanya hivyo.

Chonde chonde Mheshiwa Shein, nchi yote inakuangalia wewe kufanya the right thing kipindi hiki cha mpito ambacho wanaccm wakifikiria nani wampitishe katika uchaguzi mkuu 2010. Tafadhali sana ikomboe nchi hii kwa kuchukua madaraka ya nchi toka kwa Kikwete na kuzuia zahama inayolikabili taifa la watanzania. Kumbuka kuwa watanzania wengi wamechoshwa na wizi huu unaondelea usiku na mchana wakati nchi ikiuzwa kwa wageni kama njugu.

Ahsante sana na ubarikiwe kwa uamuzi huu unaotakiwa kuufanya haraka sana.

Asante

Mwafrika wa Kike,

Kwa kuchombeza naona umeshindikana. JK akisoma hii atatamani amwone huyu bibie. Uliyosema yote ni kweli tupu, kwasasa ni kama nchi haina rais.

Maana ya urais ni kuwa tayari kuchukua maamuzi makubwa na mazito kwa faida ya taifa, yeye anachofanya ni kufurahisha marafiki zake tu.

Hivi rais mzima unazunguka na mwizi Chenge, kweli hapo kuna neema?
 
Mwafrika wa Kike,

Hivi rais mzima unazunguka na mwizi Chenge, kweli hapo kuna neema?

Unajua wakati mwingine huwa nikisoma post za MWK huwa nacheka sana, hata sijui huwa anafikiria nini!? Hii kali sana, hope FMES ata-print ampelekee JK hotelini kwake huko US.

Sasa mimi sishangai JK kumbeba Chenge kwenye safaru zake. Ninachoshangaa kila siku ni kitendo chake cha kumteua Chenge kwenye baraza lake. Kinachonitisha zaidi ni kitendo chake cha kumteua mara ya pili hata baada ya kupata nafasi ya kuvunja baraza. Kwa vyovyote vile JK anamjua Chenge na ufisadi wake vizuri zaidi kuliko sisi wote hapa JF na hata kushinda hilo gazeti la the Guardian. Kwa hiyo hapa hakuna njia ingine ya kulifafanua hili zaidi ya kwamba JK anabariki hivi vitendo vichafu ama kwa kupenda au kwa kukosa nguvu zozote za kushughulikia. In short, I'm really sorry to say this but I am increasingly becoming worried if our president is truly in control of the government he is running (or at least supposed to be running). Huwezi kuniambia wewe unachukia rushwa au ufisadi then at the same time unawateua watu kuingia kwenye serikali yako ambao wanajulikana hata kwa mtoto wa Darasa la saba kwamba ni mafisadi. This is just too much, it is beyond comprehension. Ndio maana wakati mwingine namuelewa rafiki yangu moja anayenilaumu kila siku kwa kuhangaika kufuatlia haya mambo.

I mean every minute a blunder is happening is this government; and yet kuna watu wanataka tuendelee kuamini kwamba CCM wana uwezo kuliko vyama vya upinzani, please give me a break, stop confusing our people!
 
Kitila:
Perhaps, the rhetorical question to ask is: What is it that the opposition parties are going to do about it, if they are that capable as you assert?

Yaani pamoja na misukosuko yote hii nchini na ndani ya CCM, hata msisimko katika upinzani hakuna? Na hii ni mwaka mmoja tu na nusu kufikia kwenye uchaguzi mwingine, 2010!
 
Kitila:
Perhaps, the rhetorical question to ask is: What is it that the opposition parties are going to do about it, if they are that capable as you assert?

Yaani pamoja na misukosuko yote hii nchini na ndani ya CCM, hata msisimko katika upinzani hakuna? Na hii ni mwaka mmoja tu na nusu kufikia kwenye uchaguzi mwingine, 2010!

Kalamu,

Precisely why would you relegate that question to rhetoric?

Is the entire political process in Tanzania thus Abunuwasi-like?
 
Kitila:

Yaani pamoja na misukosuko yote hii nchini na ndani ya CCM, hata msisimko katika upinzani hakuna? Na hii ni mwaka mmoja tu na nusu kufikia kwenye uchaguzi mwingine, 2010!


Lakini usisahau ndugu yangu kuwa misukosuko yote hii ilianzishwa na wapinzania tarehe 15 Septemba 2007, unless kumbukumbu zetu zina matatizo.

So far, kwa maoni yangu upinzani Tanzania wamefanya kazi ambazo hata wao hawakutakiwa kufanya. kwa mfano, katika nchi nyingine duniani, zinazoendelea na zisizoendelea, kazi ya kufunuo maovu yanayofanywa na serikali hufanywa na civil society organisations pamoja na media. Lakini kwa Tanzania kazi hii inafanywa na wapinzani kutokana na ukweli kwamba civil society zetu ndio hizo tena nyingi zipo coopted na haohao akina Rostam.

Kazi kubwa ya upinzani ni kuwaonyesha wananchi uhusiano uliopo kati ya shida zao na blunder za serikali na kuwapa policy mbadala za kujibu hayo matatizo-hili wapinzani wamelifanya na wanaendelea kulifanya. Sasa sidhani kama ni sawa kuendelea kuwakandamiza tu wapinzani as if nothing is being done.

Tuwe wawazi tuseme kwamba wengi wetu CCM imetudumaza na kutufumbaisha akili kiasi kwamba hatuamini kama tunaweza kuishi bila yenyewe. Hata huko Zimbabwe, pamoja na mabaya yote wanayofanyiwa na ZANU PF na Mugabe,wapo wananchi wa kutosha kabisa, wakiwemo wasomi, ambao hawaamini kwamba wanaweza kuishi bila ZANU PF au Mugabe. Chiluba alifanya kazi ya ziada kuwashawishi wazambia kwamba maisha yao yangeweza kuwepo bila UNIP ya mzee Kaunda. Kwa hiyo mimi wakati mwingine silaumu sana maana najua it is a result of many years of systematic and organised indocritination.

Sasa kama tunasema wapinzani hawafanya kazi, haya civil society ndio hizo, wasomi wetu nao tumewaponda, tunasema wananchi wamelala, sasa nauliza nani basi ambaye Tanzania zimo? Au ndio tuseme sisi watanzania wote hamnazo-na tukubaliane na FMES kwamba viongozi wetu ni reflection yetu sisi wananchi!
 
VP ndio maana kaamua kuwa na kazi ya mikasi maana hakubaliki kwenye system yupo kama boya tu pale, nafikiri sometimes ata comment zake hawazitilii maanani, huyu mzee pamoja na kuwa na Che nkapa sijasikia skendo yake sijui inawezekana hawako pamoja kwenye serikali yao.
 
MWK, hilo neno incapacitated hapo nadhani litaleta mgogoro hapa...kuwa na maana inayokubalika, na ambayo kwayo JK anaweza kufit ili kuhalalisha makamu wa rais 'kuchukua nchi'.

Nadhani wataalam wa sheria wangetupa hasa ni mazingira gani tunaweza kusema kuwa rais amekuwa incapacitated?

Mie hapa namuunga kiuno MWK Kuhusu hilo neno Incapacitated. Naamini hii definition inamfaa sana JK maana nchi inajiendea ovyovyo. Mwenye Uwezo wa kuchota anachota, aliyewahi kuchota ana baki kuendelea kulipwa mishahara inayotokana na kodi zetu e.g Chenge, Mgonja, Rutabanzibwa na wengineo. Dowans inaendelea kulamba hela every month. Na rais yupo anaangalia haya.
Yaani ile kumrudisha Chenge kwenye baraza la Mawaziri ilikuwa ni dhahiri kuwa taasisi mojawapo (Maybe Usalama wa Taifa) au afisa mojawapo (maybe JK) alikuwa incapacitated due to to the fact that hakuna hata mmoja aliyeona huo uchafu. Tumesoma kuwa TAKUKURU na SFO walianza huu uchunguzi miaka kadhaa iliyopita, sasa kwa nini mtuhumiwa arudi tena kwenye dhamana kwa wananchi wakati anachunguzwa??????????????? Yes The Prezidaa anaweza akawa incapacitated MAWAZONI NA KIFIKRA na si lazima awe kwenye COMA physically. Yuko kwenye COMA kimawazo, kifikra na kiutendaji.
MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA.
 
yaani mnavyo- discuss kuhusu huyu vasco da gama mimi nataka hata kulia,yaani jamaa kakalia kutembea tembea tu huku nyumba yake inawaka moto,watanzania walikosea sana kumchagua huyu jamaa kuwa raisi, na uhakika kabisa haya mambo yangetokea na raisi ni salim ahmed salim hawa viongozi fisadi wangeishia jela, lakini huyu check-bob wetu anaangalia tu jinsi mawaziri na viongozi wengine wanavyshindana kuiba, JK BURE KABISA.
 
yaani mnavyo- discuss kuhusu huyu vasco da gama mimi nataka hata kulia,yaani jamaa kakalia kutembea tembea tu huku nyumba yake inawaka moto,watanzania walikosea sana kumchagua huyu jamaa kuwa raisi, na uhakika kabisa haya mambo yangetokea na raisi ni salim ahmed salim hawa viongozi fisadi wangeishia jela, lakini huyu check-bob wetu anaangalia tu jinsi mawaziri na viongozi wengine wanavyshindana kuiba, JK BURE KABISA.

Mafisadi wasingeruhusu mtu kama SAS agombee urahisi kwa kuwa walikuwa wanajua kuwa hawatapona ndo maana wakamtangulizia kashifa ya Hizbu.
 
Mheshimiwa sana Dk Shein,

Naomba nichukue nafasi hii kwanza kwa kukupongeza kwa kazi nzuri sana unayofanya ya kufungua majengo, vituo, maduka ya nyama na biashara mpya katika nchi. Samahani kidogo kwa kuiita hii kazi yako kwa jina la kazi ya mikasi. Pamoja na haya, natoa wito maalumu kwako na kwa ofisi yako kulinusuru taifa letu tukufu la Tanzania.

Ninakumbusha jambo unalolielewa vyema kabisa kuwa kikatiba wewe una ruhusa ya kufanya kazi ya uraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania pale mambo fulani fulani yanapojitokeza. Moja ya mambo hayo ni pale rais wa nchi anapokosa uwezo wa kutenda kazi zake kikamilifu (incapacitated). Najua wataalamu wa sheria na lugha watatumia tafsiri mbalimbali kuelezea hili neno incapacitated lakini kwa mtizamo wangu na watanzania wengi, Rais Kikwete kwa sasa anafit kabisa definition hii ya kukosa uwezo wa kutenda kazi zake kwa ukamilifu.

Ninakuandikia hili huku nikikumbuka maneno ya mtanzania mmoja aliyewashauri watanzania kwenda kunywa chai na Kikwete kama walipenda sura yake au tabasamu lake. Kazi ya uraisi ni kubwa kuliko Kikwete alivyofikiria na inawezekana ameshindwa tu kusema hili wazi. Kwa vile mkuu wako wa kazi sasa ameshindwa kazi yake na anapeleka taifa la Tanzania kubaya, ni jukumu lako kutimiza kiapo ulichoapa kuwa utachukua kazi ya urais na kufanya kazi yako kwa maadili pindi itakapothibitika kuwa raisi hana uwezo tena wa kufanya hivyo.

Chonde chonde Mheshiwa Shein, nchi yote inakuangalia wewe kufanya the right thing kipindi hiki cha mpito ambacho wanaccm wakifikiria nani wampitishe katika uchaguzi mkuu 2010. Tafadhali sana ikomboe nchi hii kwa kuchukua madaraka ya nchi toka kwa Kikwete na kuzuia zahama inayolikabili taifa la watanzania. Kumbuka kuwa watanzania wengi wamechoshwa na wizi huu unaondelea usiku na mchana wakati nchi ikiuzwa kwa wageni kama njugu.

Ahsante sana na ubarikiwe kwa uamuzi huu unaotakiwa kuufanya haraka sana.

Asante

Mheshimiwa Shein,

Taifa la watanzania bado linakusubiria ufanye uamuzi huu haraka ili kulinusuru na sunami la matatizo yanayoletwa na uongozi wa Kikwete.
 
Back
Top Bottom