Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,513
- 113,641
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, imeteketea kabisa kwa moto, jana usiku wa manane, na asubuhi hii, pamebakia kuta tupu na bango linaloonyesha hapa ndipo zilipokuwepo ofisi hizo!.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa Taarifa ya Habari ya TBC asubuhi ya leo, ambapo mwandishi wa TBC, alionyesha moto huo, hatua kwa hatua na jinsi mji wa Dodoma wenye hadhi ya mji mkuu kivuli wa Tanzania, isivyo kuwa na huduma za uhakiza za zima moto.
Huku akishuhudia kwa macho yake mwenyewe, Mkuu wa Dodoma, Dr. James Nsekela, na Kamanda Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Zelote Stephen, walikosa cha kusema, bali kushudia tuu jinsi moto huo ulivyokuwa ukiiteketeza ofisi hizo, huku magari ya zimamoto yamepaki pembeni kutokana na kuzidiwa uwezo na moto huo.
Dr. Nsekela, amesema ni mapema mno kuja chanzo cha moto huo, wakati Zelote Stephen alisema, sina la kusema zaidi ya unachokishuhudia hapa!.
Hata hivyo, wakazi wa Dodoma, walijitolea kuokoa baadhi ya magari, kwa kuyaburuta kwa nguvu, toka eneo la hatari, huku magari hayo yakiwa yamefungwa, mengine waliyabeba na kuyasogeza.
Tukio hili ni la kusikitisha sana, lakini pia huu, ndio uwezo wa serikali yetu, kupitia jeshi lake la zimamoto, katika kukabiliana na majanga ya moto.
Jengo la Nasaco jijini Dar es Salaam lilipoteketea kwa moto, ule mwaka 1996, nilishuhudia kwa macho yangu tukio hilo lililotokea mchana kweupe, na liliteketea likaishia licha ya zima moto za jiji, Mamlaka ya Bandari na Uwanja wa Ndege kujitahidi kuudhibiti, zilishindikana kufuatia kutokuwepo nchini, zimamoto zenye uwezo wa kuzima moto ghorofa ndefu. Huu wa Dodoma, umetokea usiku, na ofisi hizo, sio za ghorofa.
Leo wananchi wa Dodoma, hawataamini macho yao watakaposhuhudhia uwanja wa wazi wa ghafa wenye majivu meusi na kuta nyeusi zisizo na paa, uliochukua nafasi ya zilipokuwepo ofisi hizo, na butwaa kubwa zaidi, itawakumba watumishi wa ofisi hizo, watakaoripoti ofisini asubuhi hii, kukuta hakuna ofisi.
Pia pole ziwaendee wafanyakazi wenzangu na mimi, ambao tunajiaminisha ofisini ndipo mahala salama zaidi pa kuweka nyaraka nyeti za binafsi, hata yale mafungu makubwa ya migao, ambayo huwezi kuiweka benki kwa kuogopa maswali, sambamba huwezi kuziweka nyumbani kwa kuhofia kudhibitiwa matumizi yake, huziweka kwenye droo za ofisi, achilia zile safe za petty cash!.
Poleni wakazi wa Dodoma na vitongoji vyake.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa Taarifa ya Habari ya TBC asubuhi ya leo, ambapo mwandishi wa TBC, alionyesha moto huo, hatua kwa hatua na jinsi mji wa Dodoma wenye hadhi ya mji mkuu kivuli wa Tanzania, isivyo kuwa na huduma za uhakiza za zima moto.
Huku akishuhudia kwa macho yake mwenyewe, Mkuu wa Dodoma, Dr. James Nsekela, na Kamanda Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Zelote Stephen, walikosa cha kusema, bali kushudia tuu jinsi moto huo ulivyokuwa ukiiteketeza ofisi hizo, huku magari ya zimamoto yamepaki pembeni kutokana na kuzidiwa uwezo na moto huo.
Dr. Nsekela, amesema ni mapema mno kuja chanzo cha moto huo, wakati Zelote Stephen alisema, sina la kusema zaidi ya unachokishuhudia hapa!.
Hata hivyo, wakazi wa Dodoma, walijitolea kuokoa baadhi ya magari, kwa kuyaburuta kwa nguvu, toka eneo la hatari, huku magari hayo yakiwa yamefungwa, mengine waliyabeba na kuyasogeza.
Tukio hili ni la kusikitisha sana, lakini pia huu, ndio uwezo wa serikali yetu, kupitia jeshi lake la zimamoto, katika kukabiliana na majanga ya moto.
Jengo la Nasaco jijini Dar es Salaam lilipoteketea kwa moto, ule mwaka 1996, nilishuhudia kwa macho yangu tukio hilo lililotokea mchana kweupe, na liliteketea likaishia licha ya zima moto za jiji, Mamlaka ya Bandari na Uwanja wa Ndege kujitahidi kuudhibiti, zilishindikana kufuatia kutokuwepo nchini, zimamoto zenye uwezo wa kuzima moto ghorofa ndefu. Huu wa Dodoma, umetokea usiku, na ofisi hizo, sio za ghorofa.
Leo wananchi wa Dodoma, hawataamini macho yao watakaposhuhudhia uwanja wa wazi wa ghafa wenye majivu meusi na kuta nyeusi zisizo na paa, uliochukua nafasi ya zilipokuwepo ofisi hizo, na butwaa kubwa zaidi, itawakumba watumishi wa ofisi hizo, watakaoripoti ofisini asubuhi hii, kukuta hakuna ofisi.
Pia pole ziwaendee wafanyakazi wenzangu na mimi, ambao tunajiaminisha ofisini ndipo mahala salama zaidi pa kuweka nyaraka nyeti za binafsi, hata yale mafungu makubwa ya migao, ambayo huwezi kuiweka benki kwa kuogopa maswali, sambamba huwezi kuziweka nyumbani kwa kuhofia kudhibitiwa matumizi yake, huziweka kwenye droo za ofisi, achilia zile safe za petty cash!.
Poleni wakazi wa Dodoma na vitongoji vyake.