Ofisi ya DPP nalo jipu?

dm2000inter

Member
Oct 27, 2010
29
10
Mwaka 2012 ofisi ya DPP ili enter nolle prosequi katika kesi ya mauaji inayowakabili matajiri wanne wa Jijini Mwanza wakiongozwa na John Joseph Kisoka maarufu kwa jina la "Magazeti" baada ya kesi hiyo kukosa nguvu kwa vile matajiri hao ambao ndio key suspect walikuwa hawajakamatwa.

Baada ya kesi matajiri hao wakarejea nchini na kuendelea na biashara zao kama kawaida. Ndugu wa marehemu wakalalamika ofisi mbalimbali za umma wakitaka polisi wawakamate watuhumiwa hao bila mafanikio. Badala yake, original file la uchunguzi likiwa na maelezo ya mashahidi likaibwa kimafya katika ofisi ya RCO Kilimanjaro ili kesi hiyo isifufuliwe.

Mwaka jana Ndugu wa marehemu baada ya kuhangaika sqna wakamwandikia barua Rais Kikwete aingilie kati lakini hadi anaondoka madarakani hata kuwajibu ndugu wa marehemu hakuwajibu. Ndugu wakamwandikia barua Rais JPM mara tu alipoingia madarakani. Haikupita wiki DCI Diwani Athman akaunda kikosi kazi kikiongozwa na ACP Charles Kenyela akisaidiwa na SSP Ralph Meela kuanzisha uchunguzi wa suala hilo upya.

Kikosi hicho kilifanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kupata ushahidi mzito dhidi ya matajiri hao. Kikubwa, walifanikiwa kupata original report ya postmoterm baada ya ile iliyokuwepo awali katika jalada lililoibwa kuwa imegushiwa. DCI akapeleka jalada hilo kwa DPP tangu Januari 20 mwaka huu hadi leo hajatoa maamuzi ya watuhumiwa kufikishwa kortini. Badala yake anaibua visingizio kibao akihoji mbona eti baadhi ya mashahidi ni wapya.

DPP anasahau kuwa ni ofisi hiyo hiyo iliyoiondoa kesi hiyo kwa Nolle Prosequi mwaka 2012 leo wanaletewa ushahidi wanaanza kushikwa na kigugumizi. Kigugumizi hiki kimeibua maswali mengi hasa baada ya kuwepo kwa minong'ono ya kutengwa sh100,000,000 ili kesi hiyo imalizikie ofisi ya DPP.

Kwa yanayoendelea, hata kama rupia haijawapitia baadhi ya wasaidizi wake lakini kigugumizi hiki kinaweza kuifanya jamii iamini kuna agenda ya siri na jalada hilo.

DPP anapaswa kusoma alama za nyakati baada ya kauli ile ya Rais JPM wakati wa Law Day alipoinyooshea kidole ofisi hiyo. Kauli ya Rais inaashiria kuna jambo katika utendaji wa ofisi hiyo. Chombo pekee cha utoaji haki ni mahakama, ofisi hiyo isigeuke kuwa kikwazo cha wananchi kuheshimu utawala wa sheria.

Rais JPM na Waziri Mwakyembe wanatakiwa wachukue hatua kurejesha imani ya watanza katika utendaji wa ofisi hii ya umma.
 

Attachments

  • 20160216_072328-1.jpg
    20160216_072328-1.jpg
    392.2 KB · Views: 30
DPP ni kila kitu. Ukimtuliza tu, kesi haiingii mahakamani. Ngoja tuone huyu wa sasa kama haogopi kutumbuliwa.
 
Mkuu hiyo issue imetokea Mwanza au Kilimanjaro? Au wafanyabiashara wanafanyia kazi zao jijini Mwanza?
 
Hawa matajiri wanaishi na kufanya biashara Jijini Mwanza lakini ni wenyeji wa kijiji cha Kindi Kibosho wilaya ya Moshi Vijijini na mauaji yalifanyika nyumbani kwa matajiri hao kijijini Kindi Kibosho.

Ndugu wa marehemu pamoja na wanakijiji walijitahidi sana kumwokoa marehemu na wenzake watatu ambao wako hai lkn walishindwa maana kila walipojaribu kusogelea nyumba walitawanywa kwa risasi na huyo magazeti. Walipiga simu polisi hawakuwahi kupata msaada ila walikuja baadae walipopigiwa simu na huyo magazeti kwamba wakachukue maiti.

Ndugu walipofika Mawenzi walikuta mwili wa ndugu yao umewekewa label kuwa "ameuawa na wananchi wenye hasira kali". Lakini ukweli ni kuwa wote walitekwa nyara Moshi mjini na kupelekwa huko kijijini kuteswa umbali wa kilometa 15-20. Kama waliwashuku kwa kosa lolote lile (kama basi ingekuwa ndio kiini) kwanini waruke kituo kikuu cha polisi Moshi na vituo jirani vyote hadi wawapeleke nyumbani kwao?

Hivi kila mtu akimshuku au akiwa na uadui na mtu akapewa fursa ya kujichukulia sheria mkononi nchi itatawalika? Hao ndugu nao wakiamua kulipiza kisasi ofisi ya DPP si ndio itawajibika kubeba lawama kwa kushindwa kupeleleka suala hilo mahakamani ili lihukumiwe kwa haki?
 
Wapendwa,

Nimesoma post hii lakini bado naamini DPP haweza kufanya kosa kubwa hivyo la kiufundi na kuizima kesi hiyo wakati ni moja ya kesi zenye public interest hasa kwa wakazi wa Kindi Kibosho walioshuhudia mauaji haya. Nafahamu inawezekana dhamira ya DPP ni njema lakini jalada la mauaji kukaa kwake siku 28 huku watuhumiwa wakisota mahabusu kwa zaidi ya siku 40 lazima izue maswali hasa ikizingatiwa kuwa ofisi ya DCI iliyofanya uchunguzi huu inasema ushahidi uliokusanywa ni water tight. Busara pekee kwa kesi ya aina hii ni kwa DPP kujisafisha na kupeleka kesi mahakamani. Bahati nzuri naifahamu vizuri sana hii kesi na tayari baadhi ya maofisa wa polisi wanaotuhumiwa kwa namna moja ama nyingine kupotea kwa jalada hili wamechukuliwa hatu za kinidhamu ama kwa kuondolewa kitengo cha CID au kuhamishiwa mkoa mwingine. DPP ni chombo kinachopaswa kutohisiwa kwa namna yoyote na ukiukwaji wa maadili. Inavyoonekana ndugu pamoja na jamii imeanza kupata mashaka. Njia pekee ya kujiondoa katika huu mtego ni kupeleka kesi mahakamani ambacho ndicho chombo cha kikatiba cha utoaji haki. Huko Jaji ataamua kwa haki na naamini pande zote zitaridhika. Wala DPP asisubiri ndugu wakarudi tena kwa Rais kulalamika. Italeta picha mbaya.
 
DPP sio jipu bali ni tambazi na reference yangu wala haitokani na hicho kisa chako! Kuna siku baada ya kumuona Hosea kila siku anaitaja ofisi ya DPP nikalazimika kutafuta mamlaka ya DPP! Nilishituka kuona DPP alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuifanya Tanzania kuwa mahali salama dhidi ya ufisadi! Kwa bahati mbaya, mamlaka yale alishindwa kabisa kuyatumia; sijui kutokana na maagizi ya waliompa kazi, maslahi binafsi au ni uzembe tu kazini!

Labda kwavile anafahamu Magufuli ni mfuatiliaji tofauti na JK, huenda hatimae mamlaka ya DPP yakaonekana, kinyume chake, ndo yale yale!
 
l
Mwaka 2012 ofisi ya DPP ili enter nolle prosequi katika kesi ya mauaji inayowakabili matajiri wanne wa Jijini Mwanza wakiongozwa na John Joseph Kisoka maarufu kwa jina la "Magazeti" baada ya kesi hiyo kukosa nguvu kwa vile matajiri hao ambao ndio key suspect walikuwa hawajakamatwa.

Baada ya kesi matajiri hao wakarejea nchini na kuendelea na biashara zao kama kawaida. Ndugu wa marehemu wakalalamika ofisi mbalimbali za umma wakitaka polisi wawakamate watuhumiwa hao bila mafanikio. Badala yake, original file la uchunguzi likiwa na maelezo ya mashahidi likaibwa kimafya katika ofisi ya RCO Kilimanjaro ili kesi hiyo isifufuliwe.

Mwaka jana Ndugu wa marehemu baada ya kuhangaika sqna wakamwandikia barua Rais Kikwete aingilie kati lakini hadi anaondoka madarakani hata kuwajibu ndugu wa marehemu hakuwajibu. Ndugu wakamwandikia barua Rais JPM mara tu alipoingia madarakani. Haikupita wiki DCI Diwani Athman akaunda kikosi kazi kikiongozwa na ACP Charles Kenyela akisaidiwa na SSP Ralph Meela kuanzisha uchunguzi wa suala hilo upya.

Kikosi hicho kilifanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kupata ushahidi mzito dhidi ya matajiri hao. Kikubwa, walifanikiwa kupata original report ya postmoterm baada ya ile iliyokuwepo awali katika jalada lililoibwa kuwa imegushiwa. DCI akapeleka jalada hilo kwa DPP tangu Januari 20 mwaka huu hadi leo hajatoa maamuzi ya watuhumiwa kufikishwa kortini. Badala yake anaibua visingizio kibao akihoji mbona eti baadhi ya mashahidi ni wapya.

DPP anasahau kuwa ni ofisi hiyo hiyo iliyoiondoa kesi hiyo kwa Nolle Prosequi mwaka 2012 leo wanaletewa ushahidi wanaanza kushikwa na kigugumizi. Kigugumizi hiki kimeibua maswali mengi hasa baada ya kuwepo kwa minong'ono ya kutengwa sh100,000,000 ili kesi hiyo imalizikie ofisi ya DPP.

Kwa yanayoendelea, hata kama rupia haijawapitia baadhi ya wasaidizi wake lakini kigugumizi hiki kinaweza kuifanya jamii iamini kuna agenda ya siri na jalada hilo.

DPP anapaswa kusoma alama za nyakati baada ya kauli ile ya Rais JPM wakati wa Law Day alipoinyooshea kidole ofisi hiyo. Kauli ya Rais inaashiria kuna jambo katika utendaji wa ofisi hiyo. Chombo pekee cha utoaji haki ni mahakama, ofisi hiyo isigeuke kuwa kikwazo cha wananchi kuheshimu utawala wa sheria.

Rais JPM na Waziri Mwakyembe wanatakiwa wachukue hatua kurejesha imani ya watanza katika utendaji wa ofisi hii ya umma.
dpp ni uozo A to Z. kesi nyingi zinafutwa kwenye mazingira ya shaka. mfano kuna ile kesi ya idd simba baada ya kuonekana ana kesi ya kujibu kesi ikafutwa na dpp.
 
Back
Top Bottom