Obama alalamikia wi-fi White House

Primier

Member
Dec 16, 2015
86
14
150318023912_white_house_640x360_bbc.jpg

Image caption Huduma ya wi-fi si ya kutegemewa sana White House
Rais wa Marekani Barack Obama amelalamika kuhusu huduma ya wi-fi katika ikulu ya White House alipokuwa akihojiwa kwenye runinga.


“Kuna maeneo mengi sana hayana wi-fi,” Rais Obama amefichua akihojiwa kabla ya mchuano wa Super Bowl katika runinga ya CBS.

“Huwa inatatiza sana,” ameongeza mkewe Michelle, ambaye amesema mabinti wao Malian a Sasha huudhishwa sana na hilo.


Kwa kawaida, Bw Obama amekuwa akifanya mahojiano ya runinga kabla ya mechi hiyo kuu zaidi katika soka Marekani.

160208052349_obama_wife_sasha_and_malia_obama_624x351_ap.jpg
Image copyright AP
Rais Obama ameongeza kwamba amekuwa akijaribu kuimarisha huduma hiyo “kwa ajili ya jamaa wapya watakaoingia (White House)”.

Bw Obama aliandamana na mkewe kwenye mahojiano hayo kwa mara ya kwanza.
 
Back
Top Bottom