BabyGal
Senior Member
- Jun 30, 2011
- 165
- 62
Hii ndio thread yangu ya kwanza inayohitaji michango kwahiyo naomba nianze kwa kuwasalimia wote.
Salama aleykum kwa ndugu zangu waisilamu na Bwana Yesu asifiwe kwa ndugu zangu wakristo.
Siku hizi nyumba ndogo zimekua zaidi ya fasheni ambayo wengi hawataki iwapite. Wakina baba wanazidi kuzijenga na kina mama wanazidi kulia nazo.Mimi sina upande kwenye hili swala kwasababu mara nyingi wakina mama wenyewe ndio wanaosababisha hivyo wakina baba wengi wanalazimika kua nazo kujipatia amani na furaha ya moyo.Na utandawazi huu mtu unakuta yuko bize na tv,computer au magazeti yake ya udaku hata hana muda wa kumuuliza mume siku yake iliendaje.Wakati wa kulala bize na simu hata kumpa mumewe busu la kumtakia usiku mwema hatoi.Baridi inapiga badala ya kumkumbatia mume mama yuko bize kuchat na mashoga zake au kuchangia matatizo ya ndoa za wenzake mtandaoni wakati yake inapoteza muelekeo.
Mume hata atamani vipi kuongea anashindwa kukwambia ukweli kwasababu wewe sio msikilizaji.Mwisho wa siku inabidi akatafute yale anayokosa kwako kwingine.We unakua umempa ndoa jina tu ila matendo yote na raha alizostahili kutoka kwako anapata kwingine.Mkigundua mna wasaidizi ndo viroho vinaanza kupaa na machozi yanawatoka.Sasa badala ya kuweka simu zenu chini muanze kurekebisha nyumba mnaanza tena kulia mitandaoni na kwa marafiki ili muambiwe shoga mumeo hajatulia. wewe ujione hujakosa.Na ndio maana mara nyingi hua hamuelezei tabia zenu zilizopelekea wenzenu kuwatenda bali mnakimbilia tu kuelezea yeye alivyoanza kubadilika.Wakati aliyetangulia ni wewe.
Mi nnachojaribu kusema ni kwamba sisi wanawake ndio creators wa situation kama hizi.Wengine mtabisha kwamba kuna wanaume hawatulii mara hawathamini wanayofanyiwa sasa mbona huko kwenye nyumba ndogo hua wanakua na adabu?!Unajua kwanini?!Kwasababu anajua anaheshimiwa tofauti na nyumbani ambapo kazi zote zinazomhusu mume mama kamwachia housegirl na majukumu yake ya ndani zaidi amesahau au hata kuyapuuza.
Nawashaurini kama mama umehusika kwa namna moja au nyingine kumbadili mumeo mpaka akatafuta pakujipumzisha na kero zako au hata kua mlevi acha kulaumu ,kubali makosa na ujitahidi kurekebisha mambo.
Mwanamke jiwezeshe!Pamoja tunaweza!
Salama aleykum kwa ndugu zangu waisilamu na Bwana Yesu asifiwe kwa ndugu zangu wakristo.
Siku hizi nyumba ndogo zimekua zaidi ya fasheni ambayo wengi hawataki iwapite. Wakina baba wanazidi kuzijenga na kina mama wanazidi kulia nazo.Mimi sina upande kwenye hili swala kwasababu mara nyingi wakina mama wenyewe ndio wanaosababisha hivyo wakina baba wengi wanalazimika kua nazo kujipatia amani na furaha ya moyo.Na utandawazi huu mtu unakuta yuko bize na tv,computer au magazeti yake ya udaku hata hana muda wa kumuuliza mume siku yake iliendaje.Wakati wa kulala bize na simu hata kumpa mumewe busu la kumtakia usiku mwema hatoi.Baridi inapiga badala ya kumkumbatia mume mama yuko bize kuchat na mashoga zake au kuchangia matatizo ya ndoa za wenzake mtandaoni wakati yake inapoteza muelekeo.
Mume hata atamani vipi kuongea anashindwa kukwambia ukweli kwasababu wewe sio msikilizaji.Mwisho wa siku inabidi akatafute yale anayokosa kwako kwingine.We unakua umempa ndoa jina tu ila matendo yote na raha alizostahili kutoka kwako anapata kwingine.Mkigundua mna wasaidizi ndo viroho vinaanza kupaa na machozi yanawatoka.Sasa badala ya kuweka simu zenu chini muanze kurekebisha nyumba mnaanza tena kulia mitandaoni na kwa marafiki ili muambiwe shoga mumeo hajatulia. wewe ujione hujakosa.Na ndio maana mara nyingi hua hamuelezei tabia zenu zilizopelekea wenzenu kuwatenda bali mnakimbilia tu kuelezea yeye alivyoanza kubadilika.Wakati aliyetangulia ni wewe.
Mi nnachojaribu kusema ni kwamba sisi wanawake ndio creators wa situation kama hizi.Wengine mtabisha kwamba kuna wanaume hawatulii mara hawathamini wanayofanyiwa sasa mbona huko kwenye nyumba ndogo hua wanakua na adabu?!Unajua kwanini?!Kwasababu anajua anaheshimiwa tofauti na nyumbani ambapo kazi zote zinazomhusu mume mama kamwachia housegirl na majukumu yake ya ndani zaidi amesahau au hata kuyapuuza.
Nawashaurini kama mama umehusika kwa namna moja au nyingine kumbadili mumeo mpaka akatafuta pakujipumzisha na kero zako au hata kua mlevi acha kulaumu ,kubali makosa na ujitahidi kurekebisha mambo.
Mwanamke jiwezeshe!Pamoja tunaweza!