Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,720
Ni kawaida kwa marais wa Kiafrika kupewa udaktari wa heshima japo ni nadra kwa marais wa nchi za magharibi. ingawa rais Barak Obama anaweza kuvunja rekodi ya kuzipokea lakini asijiite dokta hata mara moja.
Je, ni kwanini? Je ni ile hali ya kutaka sifa, kutojiamini, kupenda ujiko bila kuusotea au je tutajuaje kama wahusika wananunua shahada husika? Je anapopewa shahada ya heshima rais ni mali yake au mali ya nchi?
Je, ilikuwaje mfano, Jakaya Kikwete akajiita daktari wakati hata master's hana? Je na Samia naye atakuwa limbukeni kama Kikwete aridhike na kuitwa daktari wakati hana hata shahada moja inayotambulika aliyoipata kihalali? Je ilikuwaje wasomi bobezi kama Nyerere na Mkapa hawakutumia shahada nyingi za heshima za uzamivu walizopewa? Naomba kutoa hoja.
Je, ni kwanini? Je ni ile hali ya kutaka sifa, kutojiamini, kupenda ujiko bila kuusotea au je tutajuaje kama wahusika wananunua shahada husika? Je anapopewa shahada ya heshima rais ni mali yake au mali ya nchi?
Je, ilikuwaje mfano, Jakaya Kikwete akajiita daktari wakati hata master's hana? Je na Samia naye atakuwa limbukeni kama Kikwete aridhike na kuitwa daktari wakati hana hata shahada moja inayotambulika aliyoipata kihalali? Je ilikuwaje wasomi bobezi kama Nyerere na Mkapa hawakutumia shahada nyingi za heshima za uzamivu walizopewa? Naomba kutoa hoja.