Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,244
- 113,628
Nafuatilia msiba wa Rais Ali Hassan Mwinyi.
Watu wengi wamemzungumzia. Mengi yamesemwa juu yake.
Lakini moja ambalo nimeliona limekosekana ni ule utambulisho wa Dkt.!
Katika maisha yake yote ya uongozi, Rais Mwinyi hakuwahi kupewa shahada ya udaktari wa heshima kama ilivyokuwa kwa aliyemtangulia na waliokuja nyuma yake?
Sijawahi kuona wala kusikia popote pale Rais Mwinyi akitambulishwa kama Dkt. Ali Hassan Mwinyi.
Hiyo ni kwa nini? Hakupewa hiyo shahada ya heshima? Alipewa hiyo shahada ya heshima lakini kwa vile hakuwa mpenda makuu, hakuona umuhimu wa kuutanguliza huo utambulisho na hivyo kuwafanya watu wengine nao kutokumtambulisha kwa huo utambulisho?
Au hatambulishwi hivyo kwa sababu watu walio wengi hawajui kama alipewa hiyo shahada ya heshima?
Najua marais Nyerere na Mkapa walikuwa na hizo shahada za heshima lakini ilikuwa ni nadra sana kusikia au kuona Dkt. Julius Nyerere au Dkt. Benjamin Mkapa.
Ila kuanzia Kikwete kuja mpaka hivi sasa, kila mtu ni Dkt. so and so……
Watu wengi wamemzungumzia. Mengi yamesemwa juu yake.
Lakini moja ambalo nimeliona limekosekana ni ule utambulisho wa Dkt.!
Katika maisha yake yote ya uongozi, Rais Mwinyi hakuwahi kupewa shahada ya udaktari wa heshima kama ilivyokuwa kwa aliyemtangulia na waliokuja nyuma yake?
Sijawahi kuona wala kusikia popote pale Rais Mwinyi akitambulishwa kama Dkt. Ali Hassan Mwinyi.
Hiyo ni kwa nini? Hakupewa hiyo shahada ya heshima? Alipewa hiyo shahada ya heshima lakini kwa vile hakuwa mpenda makuu, hakuona umuhimu wa kuutanguliza huo utambulisho na hivyo kuwafanya watu wengine nao kutokumtambulisha kwa huo utambulisho?
Au hatambulishwi hivyo kwa sababu watu walio wengi hawajui kama alipewa hiyo shahada ya heshima?
Najua marais Nyerere na Mkapa walikuwa na hizo shahada za heshima lakini ilikuwa ni nadra sana kusikia au kuona Dkt. Julius Nyerere au Dkt. Benjamin Mkapa.
Ila kuanzia Kikwete kuja mpaka hivi sasa, kila mtu ni Dkt. so and so……