PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,725
Ndugu Wana-JF,
Huenda nikaenda kwenye lugha yenye extremes kwenye hii thread, maana tayari adrenalin level yangu ishapandishwa na watu wa Ofisi tajwa hapo juu.
Ofisi ya NSSF hapa Arusha ina matatizo yaliyobobea.
Kwanza unapoingia tu hapa ENISISIEFU utadhani umefika msibani, maana kwa kawaida watu waliofiwa utawajua tu kwa sura zao!..Ni nyuso za huzuni tupu. Nilifanikiwa kuwepo katika Ofisi hiyo kwa Lisaa limoja, lakini sikufanikiwa kuona CHEKO la mteja yeyote...ni kila mtu anaeleza anavyoteseka!
Baada ya kujiunga kwenye foleni nilisikia mama mmoja akiongea kwa hasira.."Basi mtupe kazi za kufanya hapa, maana tunashinda hapa miezi, toka asubuhi mpaka jioni na hakuna kinachoendelea"!
Ukianzia counter ya mapokezi unakutana na mama mmoja ambaye nadhani ni kutokana na kauli zake ndo aliwekwa pale...Amevaa sura ya Mbuzi, na anaongea kwa kero ajabu.
Ukutani wamebandika makaratasi yanayoeleza uzuri wa huduma zao, ambapo when you go to reality, all the shit is a white elephant, Kimaasai tunasema "Meti-Onyo!
Ukitoka hapo unakutana na vibao vyenye vyeo vizuri ajabu..eti "SENIOR BENEFITS OFFICERS"...sijui "TECHNICAL naninani huko"...etc.
Lakini jaribu kuwafuata hao Oficcers, unakumbana na kero za kutisha huko.
Mafaili yametupwa chini ovyo na mengine yamefungwa kamba za kudu utasema mitumba!..sijui ni utaratibu gani wa filing wanaoutumia pale, maana hata mtoto wa miaka 17 aliyesoma Office Practise pale KIMAHAMA Centre hatakuwa careless vile!
Mbaya zaidi ulizia faili lako, watahangaika kulitafuta hadi unasahau shida iliyokupeleka, na unaanza kuwaonea huruma tena!...In short there is not a single filing system or order in use there.
Kila ukienda wanakuwa hawajui kabisa faili liko wapi.Wanaishia kulikosa kabisa, na kukuandikia tarehe ya kurudi tena kwenye kikaratasi, ambapo hawarekodi popote hiyo tarehe, na utakaporudi unaanza na square-one!..too boring!
Unakuta wanazunguka tuu, toka mlango huu kwenda mwingine, wanagongana tu makoridoni, wanaangalia saa na muda, na kubip watu kwa simu...kweli mwenye hasira asisogee zile ofisi, atapata kesi buure!
Meneja wa Tawi hili bwana Mwakatobe nadhani hajachukua initiative yoyote kuangalia dhiki wanayopata wateja pale. Anawasikiliza wale wanaopata access ya kuingia Ofisini kwake tu!
Suggestion box lililopo hapo ofisini limepigwa vumbi ajabu, nadhani lina miaka kadha halijafunguliwa na mtu!
Inasikitisha sana kwa watu wasomi kama hawa kufanya huduma za stone-age-era kwa wateja miaka hii ya competition, wakati wamekaa na makompyuta makubwa mezani, na nje kwenye yadi wamepaki magari ya hela mingi ajabu!
Kama wakubwa wenu watapita hapa JF, nawaomba wagharamie kidogo tu kuleta mkufunzi wa Mada rahisi ya Customer Care hapo ofisini, huenda hawa watu watabadilika, japo kwa kiasi cha chini kabisa...huh!
Nawasilisha, at least hasira zimenishuka baada ya kuweka hazarani...!
Huenda nikaenda kwenye lugha yenye extremes kwenye hii thread, maana tayari adrenalin level yangu ishapandishwa na watu wa Ofisi tajwa hapo juu.
Ofisi ya NSSF hapa Arusha ina matatizo yaliyobobea.
Kwanza unapoingia tu hapa ENISISIEFU utadhani umefika msibani, maana kwa kawaida watu waliofiwa utawajua tu kwa sura zao!..Ni nyuso za huzuni tupu. Nilifanikiwa kuwepo katika Ofisi hiyo kwa Lisaa limoja, lakini sikufanikiwa kuona CHEKO la mteja yeyote...ni kila mtu anaeleza anavyoteseka!
Baada ya kujiunga kwenye foleni nilisikia mama mmoja akiongea kwa hasira.."Basi mtupe kazi za kufanya hapa, maana tunashinda hapa miezi, toka asubuhi mpaka jioni na hakuna kinachoendelea"!
Ukianzia counter ya mapokezi unakutana na mama mmoja ambaye nadhani ni kutokana na kauli zake ndo aliwekwa pale...Amevaa sura ya Mbuzi, na anaongea kwa kero ajabu.
Ukutani wamebandika makaratasi yanayoeleza uzuri wa huduma zao, ambapo when you go to reality, all the shit is a white elephant, Kimaasai tunasema "Meti-Onyo!
Ukitoka hapo unakutana na vibao vyenye vyeo vizuri ajabu..eti "SENIOR BENEFITS OFFICERS"...sijui "TECHNICAL naninani huko"...etc.
Lakini jaribu kuwafuata hao Oficcers, unakumbana na kero za kutisha huko.
Mafaili yametupwa chini ovyo na mengine yamefungwa kamba za kudu utasema mitumba!..sijui ni utaratibu gani wa filing wanaoutumia pale, maana hata mtoto wa miaka 17 aliyesoma Office Practise pale KIMAHAMA Centre hatakuwa careless vile!
Mbaya zaidi ulizia faili lako, watahangaika kulitafuta hadi unasahau shida iliyokupeleka, na unaanza kuwaonea huruma tena!...In short there is not a single filing system or order in use there.
Kila ukienda wanakuwa hawajui kabisa faili liko wapi.Wanaishia kulikosa kabisa, na kukuandikia tarehe ya kurudi tena kwenye kikaratasi, ambapo hawarekodi popote hiyo tarehe, na utakaporudi unaanza na square-one!..too boring!
Unakuta wanazunguka tuu, toka mlango huu kwenda mwingine, wanagongana tu makoridoni, wanaangalia saa na muda, na kubip watu kwa simu...kweli mwenye hasira asisogee zile ofisi, atapata kesi buure!
Meneja wa Tawi hili bwana Mwakatobe nadhani hajachukua initiative yoyote kuangalia dhiki wanayopata wateja pale. Anawasikiliza wale wanaopata access ya kuingia Ofisini kwake tu!
Suggestion box lililopo hapo ofisini limepigwa vumbi ajabu, nadhani lina miaka kadha halijafunguliwa na mtu!
Inasikitisha sana kwa watu wasomi kama hawa kufanya huduma za stone-age-era kwa wateja miaka hii ya competition, wakati wamekaa na makompyuta makubwa mezani, na nje kwenye yadi wamepaki magari ya hela mingi ajabu!
Kama wakubwa wenu watapita hapa JF, nawaomba wagharamie kidogo tu kuleta mkufunzi wa Mada rahisi ya Customer Care hapo ofisini, huenda hawa watu watabadilika, japo kwa kiasi cha chini kabisa...huh!
Nawasilisha, at least hasira zimenishuka baada ya kuweka hazarani...!