Mohammad Waziri
Member
- Jul 4, 2011
- 14
- 6
Je kama Mungu akikujalia uzima na afya tele Novemba 2015 atakapo apishwa raisi mpya utajisikiaje? Je uta huzunika JK kuondoka? Je utafurahia yoyote yule kuingia ikulu ilimradi tu JK anaondoka? Au je una matumaini mengine ambayo ungependa kuona yatumie?
Binafsi mimi nitafurahi sana serikali mpya itakavyo ingia madarakani. Najua bado sijui nani atakuepo madarakani ila naamini Watanzania kwa sasa wamechoshwa vya kutosha kiasi kwamba wao wanataka kuona tu sura zikibadilika.
Japo natambua kila serikali ina mazuri yake na mabaya yake ina awamu hii kiujumla imeshindwa kufanya chochote cha maana na sioni mabadiliko yoyote muhimu yatakayo tokea ndani ya hii miaka minne. Kibaya zaidi ni kwamba hakuna raisi aliyeingia madarakani akibeba matumaini makubwa zaidi kama alivyo beba JK 2005. Hakuna kitu kibaya kama matumaini kuwa juu sana na matokeo kuwa chini sana.
Ila nataka tu kumpongeza JK. Umefanikiwa kutimiza ndoto yako. Umeshaingia kwenye vitabu vya historia kama raisi wa nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mafanikio yako kama raisi yana anzia hapo na kwa bahati mbaya yanaishia hapo hapo.
Binafsi mimi nitafurahi sana serikali mpya itakavyo ingia madarakani. Najua bado sijui nani atakuepo madarakani ila naamini Watanzania kwa sasa wamechoshwa vya kutosha kiasi kwamba wao wanataka kuona tu sura zikibadilika.
Japo natambua kila serikali ina mazuri yake na mabaya yake ina awamu hii kiujumla imeshindwa kufanya chochote cha maana na sioni mabadiliko yoyote muhimu yatakayo tokea ndani ya hii miaka minne. Kibaya zaidi ni kwamba hakuna raisi aliyeingia madarakani akibeba matumaini makubwa zaidi kama alivyo beba JK 2005. Hakuna kitu kibaya kama matumaini kuwa juu sana na matokeo kuwa chini sana.
Ila nataka tu kumpongeza JK. Umefanikiwa kutimiza ndoto yako. Umeshaingia kwenye vitabu vya historia kama raisi wa nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mafanikio yako kama raisi yana anzia hapo na kwa bahati mbaya yanaishia hapo hapo.