Njoo tuongee na January Makamba: Asema nyumba ya mama Lwakatare inasubiri maamuzi ya mahakama kubomolewa

Mheshimiwa wanyama pori wanathaminiwa sana na kutengewa sehemu ya hifadhi.
Je ni lini mtawatengea wafugaji mapori ili wawe na sehemu maalumu ya malisho?
Na kwani mnaamini ng'ombe ni adui wa mazingira na Nyati na Nyumbu ni rafiki wa mazingira
 
Mjini Morogoro wananchi wanazidi kuvamia hifadhi za Uluguru na Mindu katika milima inayozunguka mji huu na kuhatarisha vyanzo vya maji na kukata miti kwa shughuli za kilimo na makazi. Je, Wizara ina mikakati ipi katika kuokoa hifadhi hizi na imeshaanza kuchukua hatua zipi?
 
Maelezo tangulizi. Mh.waziri alitangaza kuvunja governing board ya NEMC na kuwasimamisha wahusika. Punde Board hiyo ilirudishwa na waliosimamishwa kurejeshwa ofisini.
Maswali. 1. Je,mh waziri ulikurupuka kuchukua hatua hizo dhidi ya NEMC?
2. Unajisikiaje kuendelea kufanya kazi na watu haohao ambao ulishawahukumu na baadae kurudishwa? Una moral authority ya kuwakemea pale watakapovurunda au utamwachia aliyewarejesha ashughulike nao?
 
Wizara yake itoe tamko kuhusu uwepo wa hivi "viwanda" vya kuchoma tofali katikati ya makazi ya watu.

24/7 Moshi umetawala kwenye makazi ya watu na huu moshi wa pumba zikichomwa in limited supply of O2 ni shida kweli.

Vipi kuhusu kodi ya bidhaa zitokazo na ziendazo Zanzibar? Amefika wapi na mazungumzo yake na TRA?
 
Imepita miaka mingi nyumba ya mama Lwakatare haijabomolewa pamoja na NEMC kutoa notisi ya kuvunja nyumba kwa sababu za kimazingira ambapo inadaiwa ujenzi wake unazuia mto Numbwi na uko jirani na Mikoko, wizara imefikia wapi? Hawaoni kwamba watu waliobomolewa wanajisikia vibaya pamoja kuwa walikuwa na zuio la mahakama kama mama Lwakatare?
Natamani hili swali liwe ndo la kwanza kuulizwa
 
Kwanza naanza na kumpongeza waziri wa mazingira january makamba..na maswali kadhaa ambayo bado sijaelewa na ningependa kujua zaidi.

swali:

1. tunajua mazingira ni watu na watu ni mazingira, je hatua gani za utu na ubinadamu zimefuatwa kwa wale walio fukuzwa katika hifadhi na mazingira atarishi ili wasije kuharibu sehemu nyingine zenye mazingira mazuri na uoto wa asili.?

2. ukweli ni kwamba mazingira bila usafi huwezi kuwa na mazingira bora na hifadhi za kuvutia, je gharama wanazo tozwa wananchi katika sehemu mbalimbali apa nchi kwa ajili ya usafi wao binafsi zina wanufaishaa katika nini.? na hizi tozo za usafi huoni kuwa ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira kwa sababu hali tete mjini watu hawana fedha.?

yote ya yote.. waziri wa mazingira upo vizuri una sikiliza watu,ila mawazo yapo mengii sijajua kama wizara yako itaweza fuataa maana tunaona watu wengine wana haribu mazingira na wanaachiwa but wengine mpaka wanafungwaa, fanyeni kazi kwa moyo na si kwa maono tu.
 
unajua katika maisha watu hawajifunzi kuigaaaa...mada apo juu ni njoo tuongee na january makamba...sasa kila mtu anayo maswali yake kama huelewi ulizaaa papasi usiogope,hajaigwaa mtu na upopoma upo katka mawazo yako una weza kubadilisha mawazo but tabia ya ujinga uwezi kuibadili kama wewe ni mshambaa..acha upapasi
 
Unaota wewe. Hilo jengo halitakaa liguswe maana hata Magufuli kamteua huyo mama kwa moyo safi kuwa Mbunge viti maalumu.. Kuna watu na viwatu!
Na pia huyo mama ni "mpiga kura wake"
 

Kwa ushirikiano wa karibu na JamiiForums, tunatarajia kuanza kwa kipindi kipya kiitwacho 'Njoo Tuongee' ambacho kitahusisha mjadala na Mawaziri kutoka Serikalini kuhusiana na masuala ya wananchi.

Kwa muda wa wiki 7, Mawaziri mbalimbali watawekwa 'Kitimoto' LIVE kupitia Star TV ili kujibu maswali kutoka kwa wanaowaongoza.

Kipindi cha kwanza kitaanza kurushwa kesho (Ijumaa O3, 2017), SAA 12:30 JIONI na Waziri tutakayeanza naye atakuwa ni Mheshimiwa January Makamba ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira.

Lengo kuu la kipindi hiki ni kuwapa nafasi wananchi kujua wanachokifanya Mawaziri na kuwauliza ni wapi wanakwama katika kutatua changamoto mbalimbali.

Sasa kupitia JamiiForums, unaweza kuuliza maswali au kutoa maoni ambayo baadhi yao yatakayopata nafasi, yatakusanywa na kuwasilishwa kunakohusika kisha kuulizwa moja kwa moja kwa mgeni wa siku hiyo.

Je, una swali, maoni, jambo lolote unataka kuliwasilisha kwa Ndg. January Makamba?

Karibu sana..
Ameshindwa kuondoa mifuko ya plasiki Sasa tunashuhudia madaraja yakibomoka kutokana na uchafu wa maplastiki.
 
thanks kwa mtoa uzi huu ;ningependa kumuuliza mh.Waziri nchi yetu imejiandaa vipi kutumia nishati rafiki kwa mazingira,maana nishati ya mafuta imedhihirika inaathiri sana mazingira;nishati rafiki ni pamoja na solar energy,nishati ya upepo,na nyukilia kama tuna uwezo wa kujenga na kuwa na uwezo wa kuitunza;nishati itakanayo na maji;na swali la pili je waziri yupo tayari kuweka hadharani ripoti ya ujenzi wa HEP pale kwenye hifadhi ya wanyama pale selous,kuhusiana na mazingira na athari ambayo wanyama wataathirika kutokana na ujenzi huo.
 
Kupitia wizara ya muungano na mazngira ya mheshimiwa makamba wanazungumziaje kero kuhusu makanisa yanayoendesha ibada zao katikati mji

Mnawasaidiaje wananchi Kwani imekuwa ni kero kubwa kwa wakazi wanaoishi jirani na makanisa hayo
 
Kwa vile ukame unatukabili sana nchi yetu, na kasi ya ukataji kuni sasa hivi inaongezeka sababu ya uwingi wa watu na wengi wananchi hawana uwezo wa kununua rasilimali yetu ya gesi... ukiangalia vilevile tuna nguvu kazi nyingi zinapotea na zinatia hasara. Ningependekeza hawa wafungwa kwa nini wasiweze kwenda kupanda miti hasa sehemu zenye ukame? Kuna miti hata miarobaini inahimiri sana ukame. Au tuna hawa vijana wanao jitolea wa JKT nao wanaweza kusaidia ktk swala hilo.
 
Back
Top Bottom