Njombe: Bashungwa ambana Mkandarasi ACIV, atoa wiki 3 mitambo na watalaam kufika ‘site’

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
f16ade73-7bd1-4c9a-8f73-e24fa3791784.jpeg
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ametoa wiki tatu kwa Mkandarasi wa kampuni ya China National Aero-Technology International Engineering Corporation (AVIC) anayetekeleza ujenzi wa barabara ya Isyonje - Kitondo - Makete sehemu ya Kitulo - Iniho (km36.3) kwa kiwango cha lami kufikisha vifaa, mitambo na wataalamu wote katika eneo la mradi ili kazi ifanyike kwa haraka.

Waziri Bashungwa ametoa agizo hilo Januari 22, 2024 Wilayani Makete Mkoani Njombe katika ziara ya kikazi na kukagua utekelezaji wa mradi huo ambao upo nyuma kwa mujibu wa mkataba.

“Natoa wiki tatu kuanzia sasa vifaa na mitambo yote inayohitajika pamoja na wataalaam wa usimamizi wa mradi wawe hapa, hawa Wananchi hawawezi kusubiri wataalamu wapo likizo China wakati sisi shida yetu ni barabara,” amesema Bashungwa.
4fc72dc6-63cf-428f-8c0c-b10e617aa395.jpeg
Aidha, Bashungwa ameahidi kuendelea kushughulika na Wakandarasi ambao wanasuasua katika utekelezaji wa miradi na wanaofanya kazi kinyume na mikataba

“Tunaposaini mikataba, nataka mikataba isimamiwe, namuagiza Mtendaji Mkuu wa TANROADS kusimamia kitengo kinachoshughulikia mikataba na kama wameshindwa kufanya kazi basi fukuzeni wote”, amesisitiza Bashungwa.
7bc95072-cdf8-4ed0-9a52-39c6f17960c2.jpeg

53784834-4c87-4c59-a079-a6441f510fca.jpeg
Kadhalika Bashungwa ameutaka Wakala wa Barabara (TANROADS) kumsimamia Mkandarasi huyo kwa karibu na kuhakikisha anafanya kazi usiku na mchana.

Ameeleza kuwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta Bilioni 82 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo kutokana na umuhimu wa wananchi wa Wilaya ya Makete na Mkoa wa Njombe katika kuleta maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi.

Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa amepokea maombi ya kuunganisha Wilaya ya Makete na Busokelo mkoani Mbeya na tayari usanifu unakwenda kuanza kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe.

Naye, Mbunge wa Makete, Festo Sanga ameiomba Serikali kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwani ni kiungo muhimu kiuchumi kati ya mkoa wa Njombe na Mbeya.

Akitoa taarifa ya mradi, Kaimu Mkurugenzi wa Miradi kutoka TANROADS, Mhandisi Jephason Nko, ameeleza kuwa mradi huo mpaka sasa umefikia asilimia 4.2 ambapo unasimamiwa na Kitengo cha TECU kutoka wakala huo huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Julai 2026.
 
Kwa hiyo Nchi hii Wakandarasi ni Wachina pekee? Wamerundikiwa miradi na yote inasua sua.

Cheap is expensive
 
Mnawapa kazi wachina huku Wakandarasi wenu wakiwa hawana kazi hao Wachina wanatoa rushwa kubwa kupata hizo kazi baadae mkiwafukuza wanashika ndege aisee mimi huwa sielewi iweje kampuni inayojitambua muwe mnaifatilia fatilia kama watoto wa shule acheni kupokea rushwa za Wachina ili mpate kampuni sahihi...
Mbona ile Kampuni iliyojenga bara bara ya Iringa, Sumbawanga na Shinyanga sikuwahi kusikia hizi Movie zenu mpaka wanakabidhi mradi...
 
Mnawapa kazi wachina huku Wakandarasi wenu wakiwa hawana kazi hao Wachina wanatoa rushwa kubwa kupata hizo kazi baadae mkiwafukuza wanashika ndege aisee mimi huwa sielewi iweje kampuni inayojitambua muwe mnaifatilia fatilia kama watoto wa shule acheni kupokea rushwa za Wachina ili mpate kampuni sahihi...
Mbona ile Kampuni iliyojenga bara bara ya Iringa, Sumbawanga na Shinyanga sikuwahi kusikia hizi Movie zenu mpaka wanakabidhi mradi...
Narudia tena Jiwe ndio aliharibu Nchi hii Kwa kulazimisha gharama za kutungwa Yale Yale ya expansion joint.

Wachina wanatoa Rushwa na wanaweka bei za chini za ujenzi harafu miradi inasua sua.

Juzi kule Tabora mkandarasi analalamika kwamba gharama za mradi zimekuwa chini tofauti na uhalisia wa vifaa sokoni na huyo huyo Mchina ndio aliweka hiyo bei.

Hao Wakandarasi unowasemea walikuwa ni Wazungu ambao Huwa hawababaishi wanaweka bei ya ku cover all risks.
 
Narudia tena Jiwe ndio aliharibu Nchi hii Kwa kulazimisha gharama za kutungwa Yale Yale ya expansion joint.

Wachina wanatoa Rushwa na wanaweka bei za chini za ujenzi harafu miradi inasua sua.

Juzi kule Tabora mkandarasi analalamika kwamba gharama za mradi zimekuwa chini tofauti na uhalisia wa vifaa sokoni na huyo huyo Mchina ndio aliweka hiyo bei.
Kuna bara bara ya Dodoma/Moro wamejenga mtoni kila mwaka utasikia bara bara imefungwa wabongo kiboko...lakini toka nilipoona ofisi za mwendokasi zipo mtoni wakati miaka yote tunaona Jangwani ni sehemu ya maji harafu wahuni wakaenda kujenga pale na kufungua kwa mbwembwe sishangai yanayotokea popote pale...ukiona mchina anafatiliwa jua alipewa mradi juu kwa juu tu..
 
Kuna bara bara ya Dodoma/Moro wamejenga mtoni kila mwaka utasikia bara bara imefungwa wabongo kiboko...lakini toka nilipoona ofisi za mwendokasi zipo mtoni wakati miaka yote tunaona Jangwani ni sehemu ya maji harafu wahuni wakaenda kujenga pale na kufungua kwa mbwembwe sishangai yanayotokea popote pale...ukiona mchina anafatiliwa jua alipewa mradi juu kwa juu tu..
Kimsingi uwezo wa TanRoads ni WA kutilia mashaka makubwa sana yaani ni tatizo.

Inatakiwa Serikali iajiri Wakuu wa Vitengo kutoka Nje ya Nchi kuanzia Kwa CEO labda Kuna mabadiliko yatakuja.

TanRoads ni hovyo sana.
 
Bashungwa hiyo Wizara huiwezi kabisa huo ndio ukweli ukiamgalia hata response yako kwenye matatizo ni taratibu sana
Na wewe toa ujinga wako hapa,Bila Bashungwa hiyo Wizara ilishajifia.

Kwanza Rais amfukuze yule Naibu wake alikuwa mtendaji wa TanRoads na hawawezi kabisa kuwasukuma kisa wamekuwa wote kwenye kula ten percent
 
Back
Top Bottom