Njia nyembamba (Simulizi mpya by SteveMollel)

*Njia nyembamba -- 15*



*Mtunzi: SteveMollel*











Baada ya muda mchache Kone alikuwa nyumbani kwake. Mikono na nguo yake vilikuwa vina mabaki ya damu. Alionana na kusalimia na mlinzi kisha akaingia ndani upesi. Ilimchukua dakika tano tu kumaliza kilichomuingiza ndani, akatoka. Alikuwa amevalia nguo safi, mkononi akibebelea funguo ya gari na bunduki ndogo.

Aliwasha gari baada ya kumuachia mlinzi maagizo kadhaa, kwamba hataonekana kwa muda, ila lazima atarudi. Kwa muda wote huo ambao hatakuwapo, basi atazame nyumba maana anamwamini.

Aliondoa gari lake mpaka sheli alipojaza mafuta kujaza kibubu cha gari. Alipotoka hapo akaenda kwenye kiotomotela, akatoa pesa za kumtosha. Sasa akawa tayari kufanya kazi yake mujarabu. Kazi aliyopata kuitandaza kichwani.

Sasa huu ulikuwa ni muda wake kuonyesha na kuyatumia mafunzo yake ya jeshi, na hata karate aliyowahi kuyapata huko nyuma. Maisha yake yalichezewa vya kutosha na sasa moyo wake ulisema basi.

Alijikuta anakunja lips zake. Macho yake yalikuwa njiani lakini akili haikuonekana pale. Macho yake yalikuwa mekundu na machungu. Mishipa ya damu ilijichora kwenye mikono yake kana kwamba barabara. Damu ilikuwa inazunguka mwilini kumpatia joto. Mwili wake ulipokea mapokeo toka ubongoni juu ya shughuli iliyo mbele yake.

“Mungu atanisamehe,” alijikuta anasema mwenyewe. Alikuwa sasa anakaribia jengo mbadala la Raisi. Alipaki gari lake mbali kidogo na jengo hilo kabla hajakaa humo kusoma eneo lake la tukio. Alihitaji dakika tatu tu kutimiza kazi yake hiyo.

Kulikuwa tulivu sana. Mbele ya geti kulikuwapo na wanaume wawili aliowaona wamebebelea bunduki. Walikuwa wamevalia sare za jeshi, warefu. Kwa ukimya uliokuwepo na umakini wake aliweza kusikia hatua zao wakiwa wanatembea kwenda huku na huko.

Kone alivesha mdomo wa bunduki yake kiwamba cha kumezea sauti, kiwamba hiki alikitoa kwenye kadroo kadogo ndani ya gari, kisha akaichomeka bunduki yake nyuma ya kiuno na kushuka garini kujongea jengo lengwa. Alipopiga hatua kadhaa tu, tayari walinzi wale, wanajeshi, wakawa wameshamrushia macho. Kuwaondoa mashaka, alitengua mwendo wake kuigiza mlevi.

Hapo akahitaji tena kama dakika moja na nusu kukaribia mahali alipoweza kufanya jambo. Kama angeendelea kusogea zaidi, ni wazi walinzi wale wangemfuata ama kumtia kwenye rada za ushambuliaji. Haraka mno alichomoa bunduki yake akawafyatua walinzi. Ajabu ni kwamba wote aliwalenga eneo moja, karibia na shina la shingo. Wakadondoka chini na kuwa kimya.

Alisogea mpaka getini akajaribu kuufungua mlango mdogo, ulikuwa wazi. Aliingia ndani kwa haraka, akaufuata mlango wa kuingia ndani ya jengo. Huo ulikuwa umefungwa. Aliuvunja kwa kuupiga teke. Sauti hiyo ikamshtua Raisi aliyekuwa amelala kitandani, kandokando na Bi Fatma.

Alijaribu kutumisha masikio yake kama atasikia jambo, hakuambulia kitu. Aliamka akavuta droo ya kitanda na kutoa silaha, bunduki ndogo, kisha akafuata mlango wa chumba na kuufungua. Alishika korido akienenda katika njia ya tahadhari. Alipaza sauti yake kuuliza:

“Nani? – kuna mtu ndani?” Hakukuwa na majibu. Ghafla alisikia sauti ya kitu cha glasi kuvunjika, moyo ukapiga fundo. Alisimamisha bunduki yake akiangaza. Alisogeza miguu yake taratibu kwenda sebuleni. Alifika pasipo kuona kitu. Aliita walinzi wake, hakuna aliyeitika.

Walinzi wote walikuwa wapo chini wakivuja damu – wa nje na ndani. Kama Raisi angetoka ndani ya sebule kwenda nje, mlangoni tu angekutana na mwili wa mlinzi wa ndani ambaye aliuawa punde tu baada ya Kone kuuvunja mlango. Na basi kama angelimalizia kutoka getini, angeliiona mingine.

Haya yalikuwa makazi ya siri ya Raisi. Si bure ni kama sehemu yake ya kufanyia maovu. Hakutaka kabisa sehemu hii ijulikane na hivyo ndio maana sehemu hiyo ulinzi wake ulikuwa kawaida sana, pia Raisi kutumia kwake magari ya kawaida kuingilia na kutokea ndani ya jengo hili, yote haya yalikuwa jitihada tu za kufanya eneo hilo lisitiliwe shaka.

Sasa leo mambo haya yalikuwa yanamgeukia.

Akili yake pevu ilimfanya ajione yupo hatarini na hawezi tena kujificha humo ndani kama kweli anahitaji uhai. Macho yakiwa yamemtoka, moyo unakita, alikimbia kurudi chumbani mwake apate kupiga simu ya msaada haraka. Alifungua mlango akazama ndani, macho kwa macho akakutana na Kone!

Mifupa yake ya magoti ililia kah-kah! Baridi kali lilimpitia kwanzia kichwani mpaka kwenye ncha ya vidole vya miguu upesi.

Mdomo wa bunduki ya Kone ulikuwa unamtazama. Sura ya Kone haikuwa na masikhara hata kidogo. Pembeni ya mwanaume huyo alikuwa amesimama Bi Fatma ambaye uso wake ulikuwa umejeruhiwa. Ni wazi alikuwa amepata majeraha hayo toka kwenye mikono ya Raisi baada ya ukaidi.

“Kone!” Raisi aliita. Kone hakuitika, zaidi alimtaka aweke silaha chini na kuisukumizia kwake kwa kutuma mguu.

“Naomba tuyamalize, Kone,” Raisi alinguruma. “Hatuna haja ya kufikia hatua hii.”
“Kama usingetaka yafikie hapa, basi usingenifanya uliyonifanya,” Kone akajibu kwa sauti ya msisitizo. Alisogelea bunduki ya Raisi akaiokota na kuiweka kibindoni.
“Nilijituma sana kutimiza kazi zako. Sikujali uhai wangu kwa kuamini kufanikiwa kwako ndiyo kufanikiwa kwa nchi yangu. Kumbe nilikosea. Wakati nahangaika usiku na mchana, basi nawe ukawa unahangaika vivyo hivyo kuharibu furaha yangu.”
“Sio hivyo unavyofikiri Kone,” Raisi alijitetea. Kabla hajaendelea, Kone akampa ishara ya kumtaka aufunge mdomowe, alafu akamwambia maneno machache:
“Sali sala yako maana nakumaliza.”

Raisi alijiona kama mtoto mbele ya simba mwenye njaa, hakuwa na wa kumuokoa. Mwili wake ulitetemeka kwa hofu ya kifo, ndani tu ya hiyo punde alikuwa amelowa jasho mgongoni. Pumzi yake ilikuwa inaenda upesi kadiri ya mapigo yake ya moyo.

“Tafadhali usiniue, Kone. Nitakupa hata nusu ya mali zangu ila unibakizie tu uhai wangu.”
“Nitaamini vipi?”
Kone aliapa.
“Hapahapa nitakupatia pesa, dola za kimarekani, za kutosha. Naomba tu unipatie simu yangu.”

Kone alitabasamu tabasamu la kando.

“Unaniona mjinga enh?”
“Basi kama hauamini, ichukue wewe hiyo simu mimi nitakuelekeza,” Raisi alinena akitia huruma. Kone alimtazama Fatma, mwanamke huyo akampatia simu ya Raisi aliyoifungua baada ya Raisi kumpatia nywila, ilikuwa mwaka wake wa kuzaliwa.

Kwa maelekeo ya Raisi, Kone alifanikiwa kuhamisha kiasi chote cha pesa kilichokuwemo kwenye mfuko benki wa Raisi, akaumwagia kwake. Baada ya hapo, Kone alimtaka Raisi aeleze miradi yake yote ya siri aliyonayo, Raisi akatii amri. Alimweleza mwanaume huyo ya kwamba ana nyumba nyingi alizozijenga huko nchi za magharibi ambazo yupo tayari kumpatia baadhi.

Kone aliona hiyo ni fursa. Kwa namna moja aliona nyumba hizo zaweza kumsaidia kumpatia hifadhi pale atakapokuwa anatafutwa baada ya kummaliza huyu adui yake. Ndio. Hakuwa na malengo ya kumwacha hai. Alijua kabisa akifanya hivyo, atakuja kujutia sana huko mbeleni. Raisi hatokuwa radhi kumwachia aishi ingali anajua siri zake, ni lazima atataka kumnyamazisha. Lakini juu ya yote kuonyesha umwamba wake.

Baada ya Kone kuyapata yale aliyokuwa anayahitaji, alifyatua risasi yake kulenga paji la uso la Raisi. Asiombe hata maji, Raisi akadondoka chini kama mzigo. Alikuwa maiti tayari.

Haraka Kone na Bi Fatma walitoka ndani wakakwea kwenye gari na kutimkia kwa mama yake Fatma. Ulikuwa ni usiku mzito na hali ya hewa ilikuwa tulivu. Lami iliwachukulia kama dakika kumi na tano tu kufika walipokuwa wanaelekea. Kutokuwepo kwa foleni, na mwendo mkali wa Kone ulifanikisha hilo.

Ngo! Ngo! Ngo! Ngo! Kone aligonga geti. Ni mwenyewe ndiye alishuka toka kwenye gari akimwacha Fatma ndani. Aliligonga geti kwanguvu kiasi kwamba hakuwa na haja ya kuligonga tena ili wenyeji wasikie.

“Kone, vipi muda huu?” ilikuwa sauti ya mamaye Fatma. Ilikuwa imejaa usingizi ndaniye.
“Naomba watoto. Upesi tafadhali,” Kone aliamuru. Sura yake ilikuwa imejikunja. Dhahiri hakutaka kurudia ujumbe wake mara mbili.
“Kuna nini?” usingizi ulimuisha mama Fatma. Alipata wasiwasi. Kuna jambo halikuwa sawa.
“Nawaomba watoto kwa sasa, tutaongea mengine baadae.”
“Wamelala.”
“Waamshe,” Kone aliagiza. “Mama naomba ufanye upesi!”

Mama Fatma aliingia ndani akatoka na watoto wawili wa Kone baada ya dakika zisizozidi nane. Kone aliwaamuru watotowe wapande gari upesi wakati yeye akimuaga mama Fatma.

“Kone, nini kinaendelea? – Fatma yupo wapi?” Mama Fatma alipaliwa na hofu. Kone hakumpatia majibu zaidi ya kumuaga na kumpa ahadi atamueleza yote siku za mbeleni. Alirudi kwenye gari akatimka.

Kwa usiku mzima, gari lilitembea juu ya lami. Mpaka unafikia wakati ambao jua linakaribia kuchomoza, akawa amefika mpakani mwa Sierra Leone. Alizama nchini humo akaendelea na safari iliyoenda kukomea kwenye hoteli ya hadhi ya kati, akachukua vyumba viwili hapo kwa ajili ya mapumziko.

Hapo alikuwa salama, moyo wake ulimwambia hivyo. Nchi ya Guinea na Sierra Leone ni wahasimu, tena wakubwa. Alijua fika akiwamo ndani ya nchi ya Sierra Leone, hakuna mtu yeyote atakayetishia uhai wake, wala kuhangaika kumtafuta. Akiwa juu ya kitanda aliwaza na kuwaza, mwishowe usingizi ukampitia. Fatma alikuwa tayari yu usingizini, pia na watoto.



***


Habari kubwa ilishika anga, Raisi ameuawa. Habari hii ilikuwa ni zaidi ya kushtua kwa wananchi wa Guinea. Hata yule ambaye hana hulka ya kusikiliza redio, kutazama video, ama kusoma magazeti, hakuikosa.

Lakini habari hii ilijawa na utata. Wapi Raisi alipouawa? Alikuwa anafanya nini huko? Alikuwa na nani? Maswali haya yaligonga vichwa vya watu. Walinzi waliokuwa wanamlinda Raisi ndio walikuwa watu pekee wenye majibu mazuri, ila kwa muda huo wote walikuwa hospitalini wakiuguza majeraha. Ni ajabu kabisa walikuwa wazima.

Na hapa ndipo panapoweka wazi kwanini Kone alikuwa amewalenga walinzi hao kwenye eneo moja tu la mwili, kando ya shina la shingo. Ni ajabu kusema alifanya jambo hili kwa bahati mbaya, lah! Pengine hakutaka kuwamaliza watu wasio na hatia mbele ya macho yake.

Wakati kila chombo cha habari kikisema jambo linalolijua, Kone akiwa mlengwa mkubwa wa mauaji hayo, mke wa Raisi anaibuka na kufanya mambo kuwa makubwa zaidi. Mwanamke huyo aliyekuwa kwao kwa muda wote huo, anavuta vyombo vya habari kwa maneno yake makali na mdomo uliokosa staha. Tuhuma zake kali juu ya marehemu zinawafanya watu kubaki midomo wazi.

“Kone alikuwa ananisaliti kwa kutembea na mke wa Kone, mmoja wa watumishi wake wakubwa. Kwasababu ya mwanamke huyo, alisahau kabisa kukaa ikulu akahamia kwenye makazi yake ya siri nisiyoyajua. Hakuwa anaonana na mimi kwa njia yoyote ile zaidi ya kuwasiliana tu kwa njia ya simu. Alikuwa ananipiga mara kwa mara, nikachoshwa na kuondoka nyumbani.”

Raisi aliuawa kwasababu ya hawara? Tena mke wa mtu? Mke wa mfanyakazi wake! Sasa vyombo vya habari vikachafuka mpaka huko mitandaoni, huku televisheni ya taifa ikiwa ndiyo chombo pekee kilichoifumbia macho habari hiyo kana kwamba hakijasikia wala kuona chochote.

Kadiri muda ulivyokuwa unasonga, salamu za rambirambi zikawa zinatumwa toka nchi za nje, na mipango ya msiba ikaanza kuainishwa vilevile uratibu wa kiutawala.

Ikiwa harakati hizo zinaendelea, Talib alikuja mbele ya hadhira akitumia chombo cha habari cha taifa, mada kuu mezani ikiwa ni salamu za rambirambi kwa kifo cha Raisi wa Guinea. Maelfu ya watu walitega masikio yao kusikiliza ni nini Talib ataongea juu ya kifo cha kushtukiza cha Raisi huyo aliyekuwa hawaivi naye chungu kimoja.

Maji makubwa pamoja na glasi yake vilikuwa vimekaa juu ya meza. Kwenye kiti kikubwa cheusi, cha starehe, alijaa Talib aliyekuwa tayari ameshaveshwa kidaka sauti. Mwanaume huyo alikuwa amevalia sare ya jeshi iliyokuwa imebandikwa kila aina ya cheo ulimwenguni.

Alikunywa kwanza mafundo mawili ya maji kisha akatabasamu akiweka chupa yake kando.

“Ni siku njema tena nakuja mbele ya hadhira ya wananchi wangu, na hata dunia nzima. Siku hii imekuwa njema si tu kwasababu Mungu ametupa fursa ya kuamka salama, bali pia ametupa ahueni kwa kumuondoa mmojawapo wa watu ambao walikuwa mzigo hapa ulimwenguni.”

Kuongea tu maneno hayo kukatoa taswira halisi kwa yale yote aliyoyadhamiria kuyatema siku hiyo – chuki, dhihaka na shutuma. Hotuba yake yote alikalia kumsema Raisi wa Guinea kwa kumuita jirani mnafiki, mhalifu na pia mwizi wa wake za watu, utadhani ya kwamba yeye alikuwa amedondoshwa toka mbinguni siku hiyo.

Alipohakikisha hajabakiza lolote kifuani mwake, alihitimisha kwa kusema:

“Mungu akulaze unapostahili. Na ashukuriwe kwa kutupunguzia tatizo mojawapo duniani.”

Alikunywa tena fundo moja la maji kabla ya runinga kuzima.



**



Kutokana na msiba mkubwa wa Raisi wa Guinea, safari ya wanadiplomasia toka Ughaibuni kwenda Liberia, kukutana na Al Saed, ilisitishwa ghafla na kupangwa siku mbili baadae. Al Saed alipanga kwenda kuhudhuria msiba huo hivyo asingalikuwapo kuwapokea wageni.

Pasipo kukawia, taarifa hiyo inamfikia Mr. X, na basi mipango ikabidi itenguliwe kuendana na mandhari husika. Mr. X aliwapigia simu watu wake aliowatuma kwa ajili ya kazi, akawaelekeza namna ya kufanya.

“Mtumie siku hizo kusoma mazingira yenu ya kazi, kugawana majukumu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa.”

Agizo hilo la Mr. X lilitiliwa maanani. Pasipo kupoteza muda kazi ya kupekua eneo la tukio inaanza. Miongoni mwa wanaume wale watano, anatoka majira ya jioni kwenda uwanja wa ndege. Alikuwa amevalia suruali ya kadeti rangi ya kaki na tisheti rangi ya maziwa. Uso wake ulikuwa mtulivu, ila macho yake yakiwa kazini kuyasoma mazingira vema.

Alizunguka maeneo kadha wa kadha ya uwanja ndege. Alichukua muda wake kuketi kwenye moja ya benchi nje ya uwanja wa ndege, akaendelea na zoezi lake la kupekua mazingira. Baada ya kutosheka na alichokipata akatoka eneo hilo kufuata barabara ya lami, pale uwanjani alipoteza kama lisaa limoja.

Alisimamisha taksi moja, akakwea na kuondoka. Ila nyuma yake kuna gari likawa linamfuatilia.



***
 
*Njia nyembamba -- 15*



*Mtunzi: SteveMollel*











Baada ya muda mchache Kone alikuwa nyumbani kwake. Mikono na nguo yake vilikuwa vina mabaki ya damu. Alionana na kusalimia na mlinzi kisha akaingia ndani upesi. Ilimchukua dakika tano tu kumaliza kilichomuingiza ndani, akatoka. Alikuwa amevalia nguo safi, mkononi akibebelea funguo ya gari na bunduki ndogo.

Aliwasha gari baada ya kumuachia mlinzi maagizo kadhaa, kwamba hataonekana kwa muda, ila lazima atarudi. Kwa muda wote huo ambao hatakuwapo, basi atazame nyumba maana anamwamini.

Aliondoa gari lake mpaka sheli alipojaza mafuta kujaza kibubu cha gari. Alipotoka hapo akaenda kwenye kiotomotela, akatoa pesa za kumtosha. Sasa akawa tayari kufanya kazi yake mujarabu. Kazi aliyopata kuitandaza kichwani.

Sasa huu ulikuwa ni muda wake kuonyesha na kuyatumia mafunzo yake ya jeshi, na hata karate aliyowahi kuyapata huko nyuma. Maisha yake yalichezewa vya kutosha na sasa moyo wake ulisema basi.

Alijikuta anakunja lips zake. Macho yake yalikuwa njiani lakini akili haikuonekana pale. Macho yake yalikuwa mekundu na machungu. Mishipa ya damu ilijichora kwenye mikono yake kana kwamba barabara. Damu ilikuwa inazunguka mwilini kumpatia joto. Mwili wake ulipokea mapokeo toka ubongoni juu ya shughuli iliyo mbele yake.

“Mungu atanisamehe,” alijikuta anasema mwenyewe. Alikuwa sasa anakaribia jengo mbadala la Raisi. Alipaki gari lake mbali kidogo na jengo hilo kabla hajakaa humo kusoma eneo lake la tukio. Alihitaji dakika tatu tu kutimiza kazi yake hiyo.

Kulikuwa tulivu sana. Mbele ya geti kulikuwapo na wanaume wawili aliowaona wamebebelea bunduki. Walikuwa wamevalia sare za jeshi, warefu. Kwa ukimya uliokuwepo na umakini wake aliweza kusikia hatua zao wakiwa wanatembea kwenda huku na huko.

Kone alivesha mdomo wa bunduki yake kiwamba cha kumezea sauti, kiwamba hiki alikitoa kwenye kadroo kadogo ndani ya gari, kisha akaichomeka bunduki yake nyuma ya kiuno na kushuka garini kujongea jengo lengwa. Alipopiga hatua kadhaa tu, tayari walinzi wale, wanajeshi, wakawa wameshamrushia macho. Kuwaondoa mashaka, alitengua mwendo wake kuigiza mlevi.

Hapo akahitaji tena kama dakika moja na nusu kukaribia mahali alipoweza kufanya jambo. Kama angeendelea kusogea zaidi, ni wazi walinzi wale wangemfuata ama kumtia kwenye rada za ushambuliaji. Haraka mno alichomoa bunduki yake akawafyatua walinzi. Ajabu ni kwamba wote aliwalenga eneo moja, karibia na shina la shingo. Wakadondoka chini na kuwa kimya.

Alisogea mpaka getini akajaribu kuufungua mlango mdogo, ulikuwa wazi. Aliingia ndani kwa haraka, akaufuata mlango wa kuingia ndani ya jengo. Huo ulikuwa umefungwa. Aliuvunja kwa kuupiga teke. Sauti hiyo ikamshtua Raisi aliyekuwa amelala kitandani, kandokando na Bi Fatma.

Alijaribu kutumisha masikio yake kama atasikia jambo, hakuambulia kitu. Aliamka akavuta droo ya kitanda na kutoa silaha, bunduki ndogo, kisha akafuata mlango wa chumba na kuufungua. Alishika korido akienenda katika njia ya tahadhari. Alipaza sauti yake kuuliza:

“Nani? – kuna mtu ndani?” Hakukuwa na majibu. Ghafla alisikia sauti ya kitu cha glasi kuvunjika, moyo ukapiga fundo. Alisimamisha bunduki yake akiangaza. Alisogeza miguu yake taratibu kwenda sebuleni. Alifika pasipo kuona kitu. Aliita walinzi wake, hakuna aliyeitika.

Walinzi wote walikuwa wapo chini wakivuja damu – wa nje na ndani. Kama Raisi angetoka ndani ya sebule kwenda nje, mlangoni tu angekutana na mwili wa mlinzi wa ndani ambaye aliuawa punde tu baada ya Kone kuuvunja mlango. Na basi kama angelimalizia kutoka getini, angeliiona mingine.

Haya yalikuwa makazi ya siri ya Raisi. Si bure ni kama sehemu yake ya kufanyia maovu. Hakutaka kabisa sehemu hii ijulikane na hivyo ndio maana sehemu hiyo ulinzi wake ulikuwa kawaida sana, pia Raisi kutumia kwake magari ya kawaida kuingilia na kutokea ndani ya jengo hili, yote haya yalikuwa jitihada tu za kufanya eneo hilo lisitiliwe shaka.

Sasa leo mambo haya yalikuwa yanamgeukia.

Akili yake pevu ilimfanya ajione yupo hatarini na hawezi tena kujificha humo ndani kama kweli anahitaji uhai. Macho yakiwa yamemtoka, moyo unakita, alikimbia kurudi chumbani mwake apate kupiga simu ya msaada haraka. Alifungua mlango akazama ndani, macho kwa macho akakutana na Kone!

Mifupa yake ya magoti ililia kah-kah! Baridi kali lilimpitia kwanzia kichwani mpaka kwenye ncha ya vidole vya miguu upesi.

Mdomo wa bunduki ya Kone ulikuwa unamtazama. Sura ya Kone haikuwa na masikhara hata kidogo. Pembeni ya mwanaume huyo alikuwa amesimama Bi Fatma ambaye uso wake ulikuwa umejeruhiwa. Ni wazi alikuwa amepata majeraha hayo toka kwenye mikono ya Raisi baada ya ukaidi.

“Kone!” Raisi aliita. Kone hakuitika, zaidi alimtaka aweke silaha chini na kuisukumizia kwake kwa kutuma mguu.

“Naomba tuyamalize, Kone,” Raisi alinguruma. “Hatuna haja ya kufikia hatua hii.”
“Kama usingetaka yafikie hapa, basi usingenifanya uliyonifanya,” Kone akajibu kwa sauti ya msisitizo. Alisogelea bunduki ya Raisi akaiokota na kuiweka kibindoni.
“Nilijituma sana kutimiza kazi zako. Sikujali uhai wangu kwa kuamini kufanikiwa kwako ndiyo kufanikiwa kwa nchi yangu. Kumbe nilikosea. Wakati nahangaika usiku na mchana, basi nawe ukawa unahangaika vivyo hivyo kuharibu furaha yangu.”
“Sio hivyo unavyofikiri Kone,” Raisi alijitetea. Kabla hajaendelea, Kone akampa ishara ya kumtaka aufunge mdomowe, alafu akamwambia maneno machache:
“Sali sala yako maana nakumaliza.”

Raisi alijiona kama mtoto mbele ya simba mwenye njaa, hakuwa na wa kumuokoa. Mwili wake ulitetemeka kwa hofu ya kifo, ndani tu ya hiyo punde alikuwa amelowa jasho mgongoni. Pumzi yake ilikuwa inaenda upesi kadiri ya mapigo yake ya moyo.

“Tafadhali usiniue, Kone. Nitakupa hata nusu ya mali zangu ila unibakizie tu uhai wangu.”
“Nitaamini vipi?”
Kone aliapa.
“Hapahapa nitakupatia pesa, dola za kimarekani, za kutosha. Naomba tu unipatie simu yangu.”

Kone alitabasamu tabasamu la kando.

“Unaniona mjinga enh?”
“Basi kama hauamini, ichukue wewe hiyo simu mimi nitakuelekeza,” Raisi alinena akitia huruma. Kone alimtazama Fatma, mwanamke huyo akampatia simu ya Raisi aliyoifungua baada ya Raisi kumpatia nywila, ilikuwa mwaka wake wa kuzaliwa.

Kwa maelekeo ya Raisi, Kone alifanikiwa kuhamisha kiasi chote cha pesa kilichokuwemo kwenye mfuko benki wa Raisi, akaumwagia kwake. Baada ya hapo, Kone alimtaka Raisi aeleze miradi yake yote ya siri aliyonayo, Raisi akatii amri. Alimweleza mwanaume huyo ya kwamba ana nyumba nyingi alizozijenga huko nchi za magharibi ambazo yupo tayari kumpatia baadhi.

Kone aliona hiyo ni fursa. Kwa namna moja aliona nyumba hizo zaweza kumsaidia kumpatia hifadhi pale atakapokuwa anatafutwa baada ya kummaliza huyu adui yake. Ndio. Hakuwa na malengo ya kumwacha hai. Alijua kabisa akifanya hivyo, atakuja kujutia sana huko mbeleni. Raisi hatokuwa radhi kumwachia aishi ingali anajua siri zake, ni lazima atataka kumnyamazisha. Lakini juu ya yote kuonyesha umwamba wake.

Baada ya Kone kuyapata yale aliyokuwa anayahitaji, alifyatua risasi yake kulenga paji la uso la Raisi. Asiombe hata maji, Raisi akadondoka chini kama mzigo. Alikuwa maiti tayari.

Haraka Kone na Bi Fatma walitoka ndani wakakwea kwenye gari na kutimkia kwa mama yake Fatma. Ulikuwa ni usiku mzito na hali ya hewa ilikuwa tulivu. Lami iliwachukulia kama dakika kumi na tano tu kufika walipokuwa wanaelekea. Kutokuwepo kwa foleni, na mwendo mkali wa Kone ulifanikisha hilo.

Ngo! Ngo! Ngo! Ngo! Kone aligonga geti. Ni mwenyewe ndiye alishuka toka kwenye gari akimwacha Fatma ndani. Aliligonga geti kwanguvu kiasi kwamba hakuwa na haja ya kuligonga tena ili wenyeji wasikie.

“Kone, vipi muda huu?” ilikuwa sauti ya mamaye Fatma. Ilikuwa imejaa usingizi ndaniye.
“Naomba watoto. Upesi tafadhali,” Kone aliamuru. Sura yake ilikuwa imejikunja. Dhahiri hakutaka kurudia ujumbe wake mara mbili.
“Kuna nini?” usingizi ulimuisha mama Fatma. Alipata wasiwasi. Kuna jambo halikuwa sawa.
“Nawaomba watoto kwa sasa, tutaongea mengine baadae.”
“Wamelala.”
“Waamshe,” Kone aliagiza. “Mama naomba ufanye upesi!”

Mama Fatma aliingia ndani akatoka na watoto wawili wa Kone baada ya dakika zisizozidi nane. Kone aliwaamuru watotowe wapande gari upesi wakati yeye akimuaga mama Fatma.

“Kone, nini kinaendelea? – Fatma yupo wapi?” Mama Fatma alipaliwa na hofu. Kone hakumpatia majibu zaidi ya kumuaga na kumpa ahadi atamueleza yote siku za mbeleni. Alirudi kwenye gari akatimka.

Kwa usiku mzima, gari lilitembea juu ya lami. Mpaka unafikia wakati ambao jua linakaribia kuchomoza, akawa amefika mpakani mwa Sierra Leone. Alizama nchini humo akaendelea na safari iliyoenda kukomea kwenye hoteli ya hadhi ya kati, akachukua vyumba viwili hapo kwa ajili ya mapumziko.

Hapo alikuwa salama, moyo wake ulimwambia hivyo. Nchi ya Guinea na Sierra Leone ni wahasimu, tena wakubwa. Alijua fika akiwamo ndani ya nchi ya Sierra Leone, hakuna mtu yeyote atakayetishia uhai wake, wala kuhangaika kumtafuta. Akiwa juu ya kitanda aliwaza na kuwaza, mwishowe usingizi ukampitia. Fatma alikuwa tayari yu usingizini, pia na watoto.



***


Habari kubwa ilishika anga, Raisi ameuawa. Habari hii ilikuwa ni zaidi ya kushtua kwa wananchi wa Guinea. Hata yule ambaye hana hulka ya kusikiliza redio, kutazama video, ama kusoma magazeti, hakuikosa.

Lakini habari hii ilijawa na utata. Wapi Raisi alipouawa? Alikuwa anafanya nini huko? Alikuwa na nani? Maswali haya yaligonga vichwa vya watu. Walinzi waliokuwa wanamlinda Raisi ndio walikuwa watu pekee wenye majibu mazuri, ila kwa muda huo wote walikuwa hospitalini wakiuguza majeraha. Ni ajabu kabisa walikuwa wazima.

Na hapa ndipo panapoweka wazi kwanini Kone alikuwa amewalenga walinzi hao kwenye eneo moja tu la mwili, kando ya shina la shingo. Ni ajabu kusema alifanya jambo hili kwa bahati mbaya, lah! Pengine hakutaka kuwamaliza watu wasio na hatia mbele ya macho yake.

Wakati kila chombo cha habari kikisema jambo linalolijua, Kone akiwa mlengwa mkubwa wa mauaji hayo, mke wa Raisi anaibuka na kufanya mambo kuwa makubwa zaidi. Mwanamke huyo aliyekuwa kwao kwa muda wote huo, anavuta vyombo vya habari kwa maneno yake makali na mdomo uliokosa staha. Tuhuma zake kali juu ya marehemu zinawafanya watu kubaki midomo wazi.

“Kone alikuwa ananisaliti kwa kutembea na mke wa Kone, mmoja wa watumishi wake wakubwa. Kwasababu ya mwanamke huyo, alisahau kabisa kukaa ikulu akahamia kwenye makazi yake ya siri nisiyoyajua. Hakuwa anaonana na mimi kwa njia yoyote ile zaidi ya kuwasiliana tu kwa njia ya simu. Alikuwa ananipiga mara kwa mara, nikachoshwa na kuondoka nyumbani.”

Raisi aliuawa kwasababu ya hawara? Tena mke wa mtu? Mke wa mfanyakazi wake! Sasa vyombo vya habari vikachafuka mpaka huko mitandaoni, huku televisheni ya taifa ikiwa ndiyo chombo pekee kilichoifumbia macho habari hiyo kana kwamba hakijasikia wala kuona chochote.

Kadiri muda ulivyokuwa unasonga, salamu za rambirambi zikawa zinatumwa toka nchi za nje, na mipango ya msiba ikaanza kuainishwa vilevile uratibu wa kiutawala.

Ikiwa harakati hizo zinaendelea, Talib alikuja mbele ya hadhira akitumia chombo cha habari cha taifa, mada kuu mezani ikiwa ni salamu za rambirambi kwa kifo cha Raisi wa Guinea. Maelfu ya watu walitega masikio yao kusikiliza ni nini Talib ataongea juu ya kifo cha kushtukiza cha Raisi huyo aliyekuwa hawaivi naye chungu kimoja.

Maji makubwa pamoja na glasi yake vilikuwa vimekaa juu ya meza. Kwenye kiti kikubwa cheusi, cha starehe, alijaa Talib aliyekuwa tayari ameshaveshwa kidaka sauti. Mwanaume huyo alikuwa amevalia sare ya jeshi iliyokuwa imebandikwa kila aina ya cheo ulimwenguni.

Alikunywa kwanza mafundo mawili ya maji kisha akatabasamu akiweka chupa yake kando.

“Ni siku njema tena nakuja mbele ya hadhira ya wananchi wangu, na hata dunia nzima. Siku hii imekuwa njema si tu kwasababu Mungu ametupa fursa ya kuamka salama, bali pia ametupa ahueni kwa kumuondoa mmojawapo wa watu ambao walikuwa mzigo hapa ulimwenguni.”

Kuongea tu maneno hayo kukatoa taswira halisi kwa yale yote aliyoyadhamiria kuyatema siku hiyo – chuki, dhihaka na shutuma. Hotuba yake yote alikalia kumsema Raisi wa Guinea kwa kumuita jirani mnafiki, mhalifu na pia mwizi wa wake za watu, utadhani ya kwamba yeye alikuwa amedondoshwa toka mbinguni siku hiyo.

Alipohakikisha hajabakiza lolote kifuani mwake, alihitimisha kwa kusema:

“Mungu akulaze unapostahili. Na ashukuriwe kwa kutupunguzia tatizo mojawapo duniani.”

Alikunywa tena fundo moja la maji kabla ya runinga kuzima.



**



Kutokana na msiba mkubwa wa Raisi wa Guinea, safari ya wanadiplomasia toka Ughaibuni kwenda Liberia, kukutana na Al Saed, ilisitishwa ghafla na kupangwa siku mbili baadae. Al Saed alipanga kwenda kuhudhuria msiba huo hivyo asingalikuwapo kuwapokea wageni.

Pasipo kukawia, taarifa hiyo inamfikia Mr. X, na basi mipango ikabidi itenguliwe kuendana na mandhari husika. Mr. X aliwapigia simu watu wake aliowatuma kwa ajili ya kazi, akawaelekeza namna ya kufanya.

“Mtumie siku hizo kusoma mazingira yenu ya kazi, kugawana majukumu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa.”

Agizo hilo la Mr. X lilitiliwa maanani. Pasipo kupoteza muda kazi ya kupekua eneo la tukio inaanza. Miongoni mwa wanaume wale watano, anatoka majira ya jioni kwenda uwanja wa ndege. Alikuwa amevalia suruali ya kadeti rangi ya kaki na tisheti rangi ya maziwa. Uso wake ulikuwa mtulivu, ila macho yake yakiwa kazini kuyasoma mazingira vema.

Alizunguka maeneo kadha wa kadha ya uwanja ndege. Alichukua muda wake kuketi kwenye moja ya benchi nje ya uwanja wa ndege, akaendelea na zoezi lake la kupekua mazingira. Baada ya kutosheka na alichokipata akatoka eneo hilo kufuata barabara ya lami, pale uwanjani alipoteza kama lisaa limoja.

Alisimamisha taksi moja, akakwea na kuondoka. Ila nyuma yake kuna gari likawa linamfuatilia.



***
Mbona umerudia mkuu
 
*Njia nyembamba -- 16*


*Mtunzi: SteveMollel*







Baada ya kama nusu saa, kutokana na foleni za hapa na pale, mwanaume huyo anashuka mbele ya jengo moja la ghorofa tatu lililokaliwa na maduka mengi kwenye sakafu yake ya chini. Anatazama kushoto na kulia kisha anapenya kwenye uchochoro mmoja unaomtokeza karibia na mapokezi, anapojitambulisha na kuingia zake ndani.

Ni chumba kikubwa chenye kitanda kipana, juuye wakiwa wamelala wanaume wanne waliovalia nguo nyepesi nyepesi, mathalani bukta na kaushi, huku mmoja tu akiwa kifua wazi: kifua chake kilikuwa kama ubao kikiwa kimejazwa na nywele lukuki. Wote walitazama mlangoni wakati mwenzao akiingia na kuurudishia mlango upesi.

“Kila kitu kipo kwenye mstari,” alisema mwanaume yule aliyetoka nje akiketi kitandani. Alieleza yote kinaganaga akiufafanua uwanja wa ndege kana kwamba upo kichwani mwake, ama kana kwamba alikuwa mhandisi aliyeujenga. Alitumia karatasi akichora kusadifu macho na akili yake. Alipoweka kituo, wenzake wakampongeza.

“Kazi yako kabambe, sasa tumebakiza tonge moja tu kumaliza chakula chetu,” alisema mwanaume mmoja mwenye sauti nzito, kisha akaanza kuainisha ‘tonge’ hilo moja lililobaki.

“Inabidi sasa tujue njia zote ziingiazo na zitokazo; fupi na ndefu; nyoofu na zilizopinda.”

Karatasi nyingine ikachafuliwa kwa kujazwa mipango. Macho ya kila mmoja wao mule ndani yalitazama karatasi hiyo kwa umakini kana kwamba wanafunzi wafanyao mtihani uliovuja. Zoezi hilo lilipokoma akateuliwa mtu wa kuitenda, naye hakuwa mwingine bali yule aliyekuwa kifua wazi, twaweza kumuita kifua ubao.

“Uwe macho muda wote,” alipewa angalizo. “Hakikisha unakuwa mwenyewe na hakuna mtu anayekufuatilia. Na pia kumbuka kutunza kumbukumbu vema.”

Wanaume hawa hawana desturi ya kurekodi mambo yao vitabuni, hilo lingeweza kupelekea wakatiliwa shaka na watu na hatimaye kukamatwa. Macho yao na ubongo wao ndivyo vitu pekee wanavyovitumia. Wakiwa kwenye eneo la kazi basi macho yataachwa yafanye kazi na huku ubongo ukitunza kila jambo muhimu.

Mpaka usiku unaenda hawakuwa wameteta kingine isipokuwa tu baadhi yao kuwasiliana na familia zao. Ila hakuna aliyesema ni kazi gani anafanya kwa muda huo, wala yupo eneo gani. Aidha walihofia kudukuliwa na kudakwa kwa taarifa zao.




***



Asubuhi na mapema ya saa kumi na moja, mlango unafunguliwa anatoka kifua ubao. Alikuwa amevalia suruali nyeusi inayombana, tisheti nyekundu na koti la ngozi rangi ya kaki, miguuni moka. Anatazama kando na kando akiurudishia mlango. Anatoka kwa mwendo wa haraka mpaka mapokezi anapoaga na kisha kuendea barabara.

Macho ya mwanaume huyu yanarandaranda kwa kasi mno. Anatazama huku na kule. Akiwa kwenye gari kuelekea uwanja wa ndege, basi anatumia mwanya wa madirisha vilivyo kwa kuangaza njia ndogo zinazochipuka na pana zinazoingia. Anafanya zoezi hilo kwa ustadi sana kiasi kwamba hata jirani yake hakugundua hilo. Kuhangaika kwake kwa macho hakukuhusiana na shingo kabisa.

Ila kuna jambo alitakiwa alifahamu. Mwanaume huyu alikuwa anafuatiliwa. Tangu pale alipotoka ndani ya jengo waliloweka makazi, kuna mwanaume, aliyekuwa amevalia kofia mithili ya turubai na jezi za michezo, alimuweka kwenye rada zake. Hali ya mwanaume huyu mfuatiliaji kuwapo eneo hilo kwa muda wa saa kumi na moja, kulitoa namna mbili: aidha alikuwepo hapo tangu jana usiku, yani amelala hapo, au amewahi sana kuja kukaa hapo.

Aliipanda daladala tofauti na ya mlengwa wake. Alikaa eneo zuri garini la kumuwezesha kuona gari la mbele yake, na hata pale ikitokea mlengwa wake akishuka. Macho yake hayakubandika kwenye gari alitazamalo mpaka wanafika uwanja wa ndege ambapo mlengwa wake alishuka. Naye akashuka. Alivua kofia yake akaiacha garini.

Kifua ubao alitazama kushoto na kulia. Alianza kutembea kuingia uwanja wa ndege, ila asiyeketi, akawa anazungukazunguka huku na kule. Alichambua barabara zote za karibu. Kama haitoshi, akafuatilia barabara moja baada ya nyingine, tena kwa kutumia miguu. Mpaka anamaliza zoezi lake hilo, alikuwa amezunguka kwa wastani wa kama kilomita tatu toka uwanjani kuelekea kila upande. Ilimtosha.

Mwanaume aliyekuwa anamfuatilia naye hakuwa nyuma. Alimpa nafasi mlengwa wake kwa umbali mkubwa. Ila si tu hilo, kuna njia nyingine alikuwa anafanya. Mwanaume huyu alibadili nguo yake ya juu mara mbili, hatufahamu alitolea wapi ila kwa njia moja ama nyingine, tena kubwa ilimsaidia kumuepusha dhidi ya kugundulikana.

Kifua ubao alipanda daladala akarudi kwenye makazi yake. Alikuwa mwangalifu kweli ila hakufua dafu. Alifika chumbani ikiwa ni majira ya mchana ya saa nane, wenzake wakafanya mpango wa chakula. Wakiwa wanakula, maongezi yakaendelea kuchukua nafasi. Maongezi ya mipango yao.

Kifua ubao alieleza kila alichokinukuu. Alikuwa mwepesi sana kukumbuka mambo kedekede pasipo kukosea. Alizielezea barabara kana kwamba anaziona kwenye televisheni, lakini pia mwishoni akatoa ushauri ni barabara ipi itumike kuchoropokea toka uwanjani. Barabara fupi zaidi kutoka nje ya jiji, na yenye upungufu wa msongamano vikiwa vigezo vilivyotumika.

Sasa mipango ilikuwa kamili, kilichokuwa kinangojewa ni utekelezaji tu. Kifua ubao alikabidhiwa zoezi la uendeshaji gari, wakati wengine wakibakia na jukumu la kurusha risasi kwa wanadiplomasia.

“Asubuhi tutakodi taksi, tutamteka dereva na kulitumia. Tukipata taksi itakuwa rahisi sana kwenye parking lakini pia kupunguza mashaka juu yetu. Dereva atatushusha mbali kidogo na uwanja wa ndege kisha tutatembea mpaka huko uwanjani. Tukishafanya tukio, tutakutana na taksi, mahali tulipopanga, na kutimka.”

Walielewana wakajipumzisha kukusanya nguvu za kesho.




***



Usiku ukiwa unasogea sasa, wanaume sita waliovalia sare za jeshi wakiwa wamebebelea bunduki, wanajongea karibu na hoteli iliyowatunza wanamgambo watano wa AMAA. Wanajeshi hawa wanawasiliana kwa ishara. Wanafika uwanja wa mapokezi na kujitambulisha kisha wanajigawa, watatu wakienda kushoto na wengine kulia.

Wanafanya matendo yao kwa ukimya na ustadi. Hakuna hata mtu yeyote ndani ya vyumba aliyefahamu juu ya ugeni huo. Wanatembea kwa kunyata mpaka mlangoni mwa chumba kinachowahifadhi watumishi wa mr. X, hapo wanatazamana na kupeana ishara ya kuhesabu vidole – moja, mbili, tatu! Mara mlango unavunjwa, wanazama ndani.

Wanamgambo wa AMAA walishtuka mno. Hawakuwa na namna yoyote ya kupambana, walishachelewa. Walikuwa tayari wamezingirwa na midomo ya bunduki ikiwatazama. Walinyoosha mikono yao juu kusalimu amri. Waliamriwa wapige magoti chini, wakatii, wakafungwa pingu na kuamriwa walale chini.

Baada ya muda mfupi, yalifika magari mawili ya jeshi. Mateka wakaswekwa ndani na kutimka, huo ukawa mwisho wa misheni ya kuua wanadiplomasia. Ila yanabakia maswali: kazi hii maridadi aliifanya nani? Mtu huyu hakuwa mwingine, bali Al Saed. Ila kwa muda gani? Aliwaza nini?
Kichwa cha mwanaume huyo kilishachambua na kubainisha mambo kadhaa ndani ya mwamvuli wake wa utawala. Alijua kabisa kuna watu asiotakiwa kuwaamini, na hili halikuhitaji ufanisi wa hali juu kulitambua, bali jicho tu la karibu kwenye kazi zilizofanywa karibuni. Mazingira ya kazi hizo yalionyesha wazi kuna mtu kwenye meza yake anampatia chakula adui, mr.X, kiasi cha kumpa kiburi.

Hilo lilikuwa mosi, pili: alishajua fika taarifa za ujio wa wanadiplomasia toka ughaibuni zitakuwa zimemfikia mr. X na kwa namna moja ama nyingine atataka ama kujaribu kufanya jambo. Alikuwa na uhakika na hili kwa asilimia zote maana aliitisha kikao cha usalama ikulu kwa ajili ya kujipanga. Na ndani ya kikao walikuwepo wale wote aliowashirikisha hata kwenye mipango ya awali.

Ila ambacho hawakujua ni kwamba, Al Saed aliendesha kikao kingine binafsi baada ya kile. Hiki cha pili akiwa na watu wawili tu anaowaamini. Watu hao wakiwa ni wanajeshi wa kawaida, wasio na cheo chochote ndani ya jeshi. Walipanga namna ya kufanya, tena kwa usiri.

“Wote wanajua wageni wanakuja mtondogoo, ila ukweli ni kwamba wanakuja kesho. Nimeshaongea nao, mtaenda kuwapokea kama watu wa kawaida na kuwapeleka mahali nilipowaelekeza. Kisha baada ya hapo kazi yenu itakuwa kutazama uwanja wa ndege kwa macho makubwa. Hakikisheni maeneo yote ya kungojea wageni, na pia rekodi za kamera zinatazamwa kuwapata wahalifu.”

Ratiba hiyo ya wageni haikuingiliwa hata na msiba wa Raisi wa Guinea. Wakati Al Saed anaenda msibani, wageni walikuwa tayari wameshawasili na kuweka makazi yao kwenye hoteli moja kubwa ndani ya jiji. Walishawasiliana na Al Saed akawapa miadi ya kuteta baada ya kurejea toka msibani.

Mr. X alizidiwa kete. Na sasa tayari watu wake walikuwa kwenye mikono ya Al Saed, mahali pasipo julikana.




***



Kwenye chumba chenye giza totoro, mara taa inawashwa na watu watano waliokalia kwenye viti wakiwa wamefungwa mikono, miguu na kufunikwa vichwa, wanaonekana. Mara punde wanatokea wanaume watatu waliovalia sare za jeshi, wanawasogelea wanaume hao watano na kuwavua mifuko iliyowafunika vichwa.

“Karibuni,” alisema mwanajeshi mmoja akitabasamu. Wenzake walikuwa wamenyamaza wakiwa nyuma yake.

“Najua mnajua kwanini mpo hapa, kwahiyo tusipoteze muda. Hatuna haja ya kuumizana wala kutoana ngeu.”

Mwanajeshi huyo aliuliza taarifa za kikundi cha AMAA, na pia juu ya kiongozi wao; wapi walipo, wapo wangapi, wana itikadi na malengo gani. Bahati mbaya, hakuna yeyote aliyekuwa tayari kujibu swali lolote. Walikula yamini kutosema, afadhali tu wakauawa.

Ilibidi sasa mbinu ya kutafuta majibu ibadilishwe, wanajeshi wakatumia nguvu na njia ya maumivu. Waliwatesa mno mateka wao mpaka pale walipohakikisha watu hao wamelowana damu na kujazwa majeraha. Walikuwa hoi kwa kipigo kizito, lakini bado hamna aliyekuwa tayari kusema lolote.

“Tuue, hatutasema kitu,” alisema kifua ubao akicheua damu.

“Sawa, ngoja tuone,” akadakia mwanajeshi kiongozi akiwa na uso wa mauaji. Alimtazama mwenzake akampa ishara kwa kichwa, mwenzake akatoka ndani, baada ya muda akarejea akiwa amebebelea simu mkononi.

“Sasa basi kama uhai wenu hamuuonei huruma, vipi wa familia zenu?”

Hakuna aliyejibu.

“Hatutahangika na nyie tena, bali wake na watoto zenu. Na kama mnadhani hatujui walipo basi mnakosea sana.”

Mwasiliano ya wanamgambo hao wa AMAA yalikuwa yamedukuliwa, ikabainika kuna ambao waliwasiliana na watu wao wa karibu muda si mrefu. Namba hizo ziliangazwa na kutoholewa taarifa muhimu. Walijaribu pia na kutafuta taarifa za Mr. X, zoezi likashindikana. Laini yake ya simu haikuwa kwenye mfumo wa mawasiliano kabisa. Laiti kama wangelipata, wasingelikuwa na haja ya kusumbuana na mateka wale.

“Sasa basi ni jukumu lako kuamua. Aidha unatupa tunachotaka, ama tukamalizane na familia na watu wenu?” Kauli hiyo ilikuja baada ya mwanajeshi huyo muongeaji kusema kwa uwazi ni wapi familia hizo aziongelezo zilipo. Na bahati njema au mbaya, yote aliyosema yalikuwa yana kweli ndani yake.

Hakuna mfuasi yeyote wa AMAA aliyejibu, wala kusema jambo. Walitazamana kwa macho ya dosari kisha wakaendelea kufunga midomo yao wakiutunza ukweli vifuani.

“Sawa kama mmeamua hivyo,” alisema mwanajeshi. “Tutawaletea vichwa vya wapenzi wenu hapa.”

Baada ya kusema hivyo, alitazamana na wenzake wakapeana ishara ya kutoka. Ila kabla hawajafika mlangoni, mara wanaitwa.

“Nitasema, tafadhali msiue familia yangu!” Alikuwa mwanaume mmoja kando na kifua ubao. Alijawa na shaka. Wenzake walimtazama kana kwamba wanataka kumtoa roho.

“Abdul, unataka kufanya nini?” Aliropoka kifua ubao. “Unataka kufanya nini Abdul? Unakumbuka kiapo chako!” alifoka.

“Hakuna kitu kikubwa kama familia yangu,” akajibu mwanaume huyo, Abdul. Mara akapunguza sauti, ananong’oneza:
“Mke wangu ana mimba. Siwezi nikaruhusu yeye na mwanangu wapoteze uhai.”



***




☆Steve
 
Back
Top Bottom