Nipo njia panda....

vkeisy2006

JF-Expert Member
Mar 26, 2010
229
99
SIJUI nifanyeje.......

........he is ma men for more than 6 years.........................TUMEKUWA PAMOJA..........and kusema ukweli wa mungu mi mwanamke mvumilivu na ye mwenyewe anasema tulikua tunakorofishana sana lakini navumilia...ameshaniumiza sana navumilia..and one day nimemuuliza baba naona mda unaenda unamsimamo gani na mimi? akasema kama unaongea ndoa mimi sijaplan kuoa katika maisha yangu...nkamuuliza hujaplani kuoa au hujaplani kunioa mimi?akasem aye hajaplani kuoa.....

...ooooh nikajua labda ananitania maneno tuu mda unazidi kwenda....nau anakaa kwake....imagine mi nakaa home kule naenda tuu..jmamosi na juma2...lakini uwiiiii dah ni mwanaume mwenye manung'uniko sana and hapo i do everything..kodi nimempa half,mshara wangu ukiingia namnunulia nguo,viatu,chakula.na out namtoa na nauli y akazini nampa..... nkijua ukiingia wake itakua the same kwangu lakn..wake ukiingia....nimepata mshahara mdogo nimempa mama hivo sina hela siunajua wazazi wangu wamestaafu wadogo zangu shule ..hata ndani kwake sabuni tuu ya kuogea hanunui kilakitu mpaka mimi vyake makochi na kitanda tuu vingine vyote vyangu ama serious for this guys and am not stayin there......

JUZI KAJA HOME kwetu yani kwa wazazi wangu.... KANIKUTA NIKO NA RAFIKI ANGU yule friend akamuuliza vip shem ndoa lini yesu wangu alichomjibu ndo kinanifanya niandike hapa leo hii.....akamjibu rafiki ako hajakwambia mimi nimempa ukweli sioi..hvo akipata mwanmme huko mwenye nia aeende tuu mi simfichi kitu coz mi mzungu na he seemed serious anavyoongea hayo maneno....niliona aibu kwa kweli yule rafiki angu akasema mbele yak eeh mbona maneno makali mi nisingeweza kuvumilia...kaniuliza how can u? Kweli una moyo...RAFIKI ALIVYOONDOKA NIKAMUULIZA HIVI ULIMAANISHA YALE MANENO AKSEMa NOO NILISEMA TUU....sasa nkifikiria kashawahi niambia the same words si chini ya mara 3....

Nashindwa nifanyeje niendelee na maisha yangu au nifanyeje sio kama sitongozwi nakataa coz i know na mtu halafu mtu anakuvunja moyo hivi yani mi sijui nifanyeje coz tangu hiyo juzi am not in a gud condition coz nawaza those words.....na kila siku anvyorudia kwamab nikipata mtu niendee tuu nifanyeje guys...mimi jamani...
 
Dah!.............
HAPO MAMA umeingilia mlango wa kutokea!

nayahurumia sana maisha yako.........

huenda ukawa mu wa stresses 24/7......
 
shost umeshaambiwa ukweli hana mpango wa kuoa sasa labda kama nawe huna mpango wakuolewa kaa! lakini kama unawish kuja kuishi katika ndoa cku moja na may be kuwa na watoto, basi anza mbele mapema. Miaka 6 ni mingi sana, yaonyesha hana nia ya kuoa kweli au anampenzi mwingine.

nawewe kwanini unaamua kulipa kila kitu chake, maana huishi hapo au ni kwasababu unampenda sana? kuna wanaume hawapendi mwanamke anayejionyesha ana pesa.
 
HUWEZI KULIZIBA JUA NA UNGO!!!!!!!!!!!!!!!

Huyo sio wako.Mwombe Mungu akupe wako atakayethamini mapenzi yako.
Uvumilivu nao una LIMITS zake kumbuka.Usijejuta baadae.
Na isitoshe huyo anaye mwingine sema hujagundua tu,dalili ya mvua ni mawingu
 
Dada, leo sitaki kukuhukumu kwanini unalala na mtu ambaye hamjafunga naye ndoa, najua kwasababu umeumizwa kama unavyosema, so nikikupiga msumari nisije kukumaliza kabisa.

Nakupa pole kwa leo, mwombe Mungu akupe mwanaume wa kufunga naye ndoa, uingie kwenye ndoa ili upate heshima yako kama mwanamke, mme wako aje akuheshimu na kukuthamini hata mbele za watu, na watu wote wanaokujua pamoja na wazazi wako wajivunie kwa kuleta heshima nyumbani kwao, yaani heshima ya kuolewa kwa ndoa na kukaa na mme mmoja. kuishi na mtu mkifikiri mnachunguzana kwanza kwa miaka kama sita yote hiyo, mnaendelea kuvunja amri ya sita tu, ndi dhambi mbele za Mungu, waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu...Mungu anakupenda ndo maana bado uko hai leo....hivyo you have a second chance kuamua kufanya kitu kipya kitakachomfurahisha Mungu ktk maisha yako, hakuna haja ya kuendelea kumchukiza Mungu kwa matendo yetu.

hakuna mantiki kukaa na mtu asiye kuthamini...kuna ndoa zingine mme hataki hata kuongozana na mkewe...hivyo kama mtu hakuthamini mbele za watu mkiwa hamjaoana, mkiingia ndani, ukazaa na kuanza kukongoroka si ndo atasema maneno ya ajabu...kama mtu anakupenda lazima atajivunia hata mbele za watu, na atathamini uvimilivu ule unaompa...kwa mwanaume, wakati mwingine huwa ni vigumu kumwambia mtu kuwa "nakuacha, ", matendo tu yanaweza kueleza....

Sijui umependea nini kiasi cha kutoa hata nauli kwa mwanaume asiye mmeo, au wewe peke yako ndo unajibembeleza kwake yeye anadeka kwasababu labda kakuona wewe si mzuri sana hivyo utamfata tu kwasababu yeye hana shida na anaona wewe hautaolewa...mbona inaonyesha wewe ndo unajipeleka zaidi kwake na yeye hamaanishi...unampenda mtu asiyekupenda kwa dhati?, mtu asiyekupenda atakudunda mkiwa ndani hadi ukome kwasababu hakuthamini,....unatakiwa uwe na mtu atakaye kutetea wewe mbele za ndugu zake, mbele za marafiki zake, mwenye busara na atakayekufanya wewe ujisikie furaha kuolewa naye, sasa kama anamwambia rafiki yako kuwa ameshakwambia kuwa hatokuoa, busara gani hiyo....huyo kakuchoka halafu wewe ndo unajipendekeza....samahani kuongea hivi.
 
warembo mcwe mna hudumia ki hivyo kabla ya muda wake, mkifika kwenye ndoa c ndio mtaachiwa kila jukumu?
 
Pole mpenzi the guy seems not serious with you
It happens saa zingine unapata disappointments when you are are about to close the chapter
I suggest ukae naye chini mkiwa mmetulia umuulize if he is not into marriage with you its you life mnaongelea hapa pia
So muongee muelewane kwa mapana na marefu na kama jibu litakuwa ndo hivyo basi you try to move on with your life. Infact you will need a break to collect yourself again. Ndo maana saa zingine si vizuri sana kujiekea like over 90% on someone you are dating that you will get married no matter how long you have been together.

SHIT HAPPENS..................POLE
 
hivi unajua kwa wale walioko kwenye ndoa kama haujaokoka, mkiishi miaka miwili unaweza kumchoka mkeo au mmeo ukajuta kwamba kwanini umeoa?..sasa kama utakuwa unachovyachovya tuu kwa miaka sita, ni dhahiri kwamba ameshakuchoka, anahitaji kitu kipya na kwasababu hamjapigwa pingu, yuko free...kama unataka kuolewa usivue kufuli, ukivua tu, atakufanyia experiment na comparison mwishoni atatoa makisi za mtihani 10/100, sio fresh kama yule na yule..hivyo hata kama ataendelea kuwa na wewe anakuwa anafanya mahali pa kumalizia hamu tu, mipango ya kutafuta mwingine inakuwa inaendelea kimyakimya.

Hivi kama nikija kukutongoza, ukakubali, kidogo tu ukaja kwangu kupiga deki,mara kufua nguo na kufuli umeshatoa tayari, si nitajua wewe hauna msimamo jamani, nikija kukuoa kweli nikasafiri nitajua wewe si mrahisi?...jamani jamani, mnakaa na wanaume bila kuoa?....wadada walio tulia huwa hawataki kutoa kufuli hata ufanyeje kwasababu hawajui jamaa atawapa maksi gani kabla ya kuwabwaga....wanakataa kabisa kutoa kufuli na wanawaambia kama unanitaka njoo utoe posa kwa wazazi wangu ili wazazi pia waheshimike....ukifanya hivyo hata kama mwanaume atakuwa anang'ang'ania kutaka mapenzi, moyoni atakuwa anajivunia "lakini ametuliaaaa, si mrahisi, wanaume wengine si rahisi kumwingia huyu"...utapata upendo wa ajabu...

Ukiwa mrahisi kama mdada wa kwenye madanguro, atakushusha hadhi na utakuwa sawa tu na housegeli..tulieni wadada..
 
dada huyo mbona hakupendi,wala hakuna haja ya kutafakari mara mbili na anavyojifanya kukuambia maneno hayo then bdae anasema anakutania ni mnafiki,kama ana nia na ww na ili ujue anakudanganya ama vipi hebu mwambie ww umeamua kufanya maamuzi mengine unasitisha uhusiano uone atachukua hatua gani kama alikuwa anakutania atarudi kukubembeleza na kukueleza serious kuwa alikuwa anatania,bt km alimaanisha wala hataahangaika na ww.jaribu uone pole sana my dear
 
hivi unajua kwa wale walioko kwenye ndoa kama haujaokoka, mkiishi miaka miwili unaweza kumchoka mkeo au mmeo ukajuta kwamba kwanini umeoa?..sasa kama utakuwa unachovyachovya tuu kwa miaka sita, ni dhahiri kwamba ameshakuchoka, anahitaji kitu kipya na kwasababu hamjapigwa pingu, yuko free...kama unataka kuolewa usivue kufuli, ukivua tu, atakufanyia experiment na comparison mwishoni atatoa makisi za mtihani 10/100, sio fresh kama yule na yule..hivyo hata kama ataendelea kuwa na wewe anakuwa anafanya mahali pa kumalizia hamu tu, mipango ya kutafuta mwingine inakuwa inaendelea kimyakimya.

hivi kama nikija kukutongoza, ukakubali, kidogo tu ukaja kwangu kupiga deki,mara kufua nguo na kufuli umeshatoa tayari, si nitajua wewe hauna msimamo jamani, nikija kukuoa kweli nikasafiri nitajua wewe si mrahisi?...jamani jamani, mnakaa na wanaume bila kuoa?....wadada walio tulia huwa hawataki kutoa kufuli hata ufanyeje kwasababu hawajui jamaa atawapa maksi gani kabla ya kuwabwaga....wanakataa kabisa kutoa kufuli na wanawaambia kama unanitaka njoo utoe posa kwa wazazi wangu ili wazazi pia waheshimike....ukifanya hivyo hata kama mwanaume atakuwa anang'ang'ania kutaka mapenzi, moyoni atakuwa anajivunia "lakini ametuliaaaa, si mrahisi, wanaume wengine si rahisi kumwingia huyu"...utapata upendo wa ajabu...ukiwa mrahisi kama mdada wa kwenye madanguro, atakushusha hadhi na utakuwa sawa tu na housegeli..tulieni wadada..

hapo cjaelewa wokovu wa namna gani, mana imani nazo zinachanganya, ule wa kakobe/mama rwekatare?....kama ni huo wengine hatupo kwenye huo wokovu lakini tunasongesha na hizo ndoa.....hapo kwenye red heshima haitokani na kuvua kofuli, kama mtu anakuheshimu anakuheshimu tu mambo ya cjui ulimvulia kufuli kabla ya ndoa yalishapitwa na wakati, wengi humu walivua kabla ya hizo ndoa na bado wanaheshimika kwenye hizo hizo ndoa...mmoja wapo mie.
 
Shukuru mungu kakwambia kweli mamy ujipange upya maisha yako ..usiseme kama umepoteza muda hizo zote ni exprience za maisha .la sivyo ungeendelea kukaa nae muda mrefu sana bila kujua hatima yako
I am sorry for you Bi mdogo ...iko nafasi nyingine kwako
Ila usishangae kukuta jamaa kaoa ingawa yeye kakwambia hajaplan kuoa
 
Dah pole sana huyo jamaa hana taimu na ww inaonekana ana mtu mwingine ameshamzingua.ww chukua zako mapema ila atakuja kukukumbuka kwani umemfanyia mema sana.usilipe mema kwa ubaya ww muache kwa upole na unyenyekevu ww utakuja kuniambia siku moja.poleeeeeee!
 
Shukuru mungu kakwambia kweli mamy ujipange upya maisha yako ..usiseme kama umepoteza muda hizo zote ni exprience za maisha .la sivyo ungeendelea kukaa nae muda mrefu sana bila kujua hatima yako
I am sorry for you Bi mdogo ...iko nafasi nyingine kwako
Ila usishangae kukuta jamaa kaoa ingawa yeye kakwambia hajaplan kuoa


na ishu ni kwamba watu hawatakagi kuukubali ukweli kama huu, lakini huu ni ukweli mtupu...
 
Pole saana! imeniTOUCH sana hiyo... Miaka 6 sio mchezo halafu unajibiwa hivo.. Nahisi ana mtu mwingine ndio maana anajiamini na majibu hayo. Kula kona achana nae. Pole tena Mama.
 
kina dada jamani msipende kulazimisha mambo, nimesoma hiyo post nimegundua huyo dada alikuwa analazimisha mapenzi kwa huyo kaka maana anaweka wazi kuwa alikuwa anamnunulia kila kitu sasa hapo kuna nini zaidi ya kuhonga m/ume

jamani watoto wa kike hakuna m/ume mwenye akili za kiume anayependa kulelewa kimtindo huo, halafu utakuta labda yeye alikuwa hajajipanga kimaisha na huyo dada ameshayatoa hivyo anatumia uwezo wake kulazimisha ndoa, na labda kuna masimamango kutoka kwa huyo dada maana nimeona hapo anasema kuwa jamaa vyake ni kitanda na makochi vingine vyote kanunua yy sasa hayo ni masimango

huyo jamaa sio kwamba hataoa ila hajajipanga na style unayoishi naye na uwezo wake ameona akupotezee

Ushauri: Achana naye tafuta wa class yako, huyo hamtawezana kabisa kwani inaonyesha kuwa kwa sasa hakupendi nadhani kuna kitu nyuma ya pazia,
 
Pole! Huyo hakupendi kabisa. Tena anakudharau sana na anaona unambabaikia mno mnavomuhudumia kwa hili na lile. Na pengine huduma hizo ndizo zinamfanya aendelee kukuvumilia. Ila hakupendi. Mi naona hujachelewa sana. Piga moyo konde, uambie moyo wako kwamba: INATOSHA. Unataka aongee lugha gani ndipo uelewe a kuamini? Kesha ongea yote ya moyoni mwake huyo. Kaweka nukta. Uamuzi ni wako! Usipoteze muda, anza upya, usiogope.
 
Kiukweli stori yako inasisimua.

Kwanza pole kama ni kweli, pia bado hujachelewa badili msimamo wako usijirahisi tena kwake na ataona umuhimu wako kama hataki pia mbwage kwa kumwambia umepata mwingine hata kama hujapata afu utaona atakavyo changanyikiwa.
Kumsahau mtu ni rahisi sana hata wiki haipitii unaweza kusahau historia yake kabisa.
mfanyia sa hivi afu tuletee mrejesho wana JF.
Cheers..
 
Back
Top Bottom