Nipo Moshi kikazi, mbona utitiri wa shule kila kona ninayopita?

Kuna uzi mmoja tumezungumzia sana hili na kueleza kama unavyosema.

Ndugu yetu Mkandara akasema shule hizo zinajengwa na serikali kwa upendeleo.
Nadhani unaweza kuzungumza naye sasa maana wewe ni shahidi umeyaona kwa macho

Uzi ukihitajika tutauweka hapa

Naomba kuuona huo uzi eeh
 
Last edited by a moderator:
Kata Niliyopa Ina Vijiji 4 Na Ina Shule Mnasoziita Za Kata Si Tunaziita Na Za Vijiji Zipo 3 Na Privet Ipo 1
Na Simejengwa Kwa Nguvu Ya Wanachi
Ila Humwezi Kulinganisha Uchumi Wa Huku Na Sehem Nyingine
Maana Huku Tunategemea Ndiz Na Kahawa Na Raia Wengi Wapo Mijin Na Wanawatumia Wazaz Wao Pesa Kwa Ajili Ya Kusomeshea Na Kuchangia Shughuli Za Maendeleo Pia Pesa Ya Mfuko Wa Elim Jimbo Unatumika Ipasavyo Maana Sie Tunaongozwa Na Cdm Mb
 
Ha ha haaa.... Ume mshambulia Zio vikali sana, ila cha kuongezea wakati sehemu nyingine za Tanzania zikilia na uhaba wa bidhaa za viwandani miaka ya 1980's watu wa Kilimanjaro walikuwa wanazipata kwa urahisi via magendo tokea Kenya, na kipindi hicho wengine wakikomaa kulima maindi na kuuza kilo Tsh. 55 kahawa kilo moja ilikuwa inauzwa Tsh 1000. Na Mungu akiwabariki wote wakavuna gunia 20 nadhani mkulima wa maindi atapata pesa kidogo saaana kuliko yule wa kahawa. Na cha ziada wengine wakifuata maji makilomita sisi tulikuwa tuna maji safi kwenye mifereji yetu iliyo chimbwa na babu zetu miaka ya 1890's.

Miaka ya 50 babu yangu alikuwa ana ngano, kahawa kwenda Kenya na kuimport bidhaa nyingine kuja Dar es Salaam. Alikuwa na plantations za kufa mtu za ngano na mashamba.
Babu yangu mwingine alikuwa na boda za mpunga kule kahe. Alikuwa analeta Dar.
Sijui mikoa mingine walikuwa wanafanyaje.
 
hivi mkoa wa Kilimanjaro una wabunge wa ccm wangapi na upinzani wangapi? madiwani wa ccm wangapi na wa upinzani wangapi? hizi data nafikiri ndio zitatuonyesha kwamvba wanachagua ccm au upinzani.

Ina Majimbo 9
Majimbo Yaliyopo Uchagani Ni 6
Ccm2 Na Cdm 3 Tlp1
Upareni 3 Na Yote Na Ccm
Majimbo Ya Uchagani Ni
Rombo Cdm
Vunjo Tlp
Moshi Vijijin Ccm
Moshi Mjin Cdm
Hai Cdm
Siha Ccm
 
bado nipo Moshi vijijini..
lengo langu katika huu Uzi ni kushea kile nilichokiona na kujifunza huku ugenini .naomba nisieleweke vibaya najua siwezi wafurahisha wote wala kuwaudhi wote.
MAJENGO: karibu nyumba zote za kuishi ni za block yaani matofali ya sement na zilizo ezekwa na bati tens almost no Msauzi.
tulikua tumeweka hema kwenye eneo la nyumba ya Mwenyekiti wa kitongoji alakini Leo kaja mzee mmoja akatupeleka kwenye nyumba ya wanae( kutokana na Maelezo yake) nikua hiyo nyumba ni ya wanae huwa wanakuja kila mwisho wa mwaka..akasisitiza kua ni usafi tu huwa unafanyika kila kukicha.
kwakweli imetusaidia sana kwani baridi huku ni Kali sana.kwa Mara ya kwanza toka nimefika hapa usiku wa kuamkia Leo ndio nimelala usingizi fofo bada ya kua nimelala ndani na halo ya hewa sio baridi.
hawa ndugu zetu wachaga bado wanaheshimu mila kwani japo kuna nyumba ya kisasa pembeni lazima nyumba ya bati ya kizamani IPO.
nimeiliza kwanini sio ya majani wakaniambia kwao majani no chakula cha mifugo toka enzi na nikufuru kuezekea kwani mifugo ni sehemu ya mila hivyo watakua wamevunja miiko.
hawa jamaa kweli ni shidah kama wasemavyo watoto wa mjini.
ntendelea na stori zaidi hapo keshokutwa.
 
Huko wameweza bila ccm, Wachaga walishafuta uchafu wa ccm, ndio maana unaona mambo yanakwenda

Za kwako changanya na za kupewa..., aminia sana wachagga! Kazi kwa wale wote wanaoona muda wa mabadiliko bado hajawadia! Poleni sana kwa kuendelea kapoteza muda!! Tumia kura yako vyema na tuonane tena Oktoba.
 
isingekuwa wizi hao jamaa wangekuwa kama sie wengine tu.

Vipi nyie wengine mmeshindwa kuiba na Wachagga walikuibia nini labda?na kama unaiba halafu unafanya maendeleo huo wizi ni mzuri sana na kingine unasema isingekuwa Wizi wangekuwa kama nyie unataka kuniambia Wachagga wote walikuwa wanafanya kazi Serikalini maana kule Moshi karibu watu wote wana maisha mazuri/kipato cha kati.
 
aisee nilikuwa sijasikia hii.. Hii ni habari njema zaidi

mkuu jiandae, tumeshamaliza kukarabati zile nyumba za ibada kwa sasa ndo tumehamia huko.....kila kata tumejiwekea alengo tuwe na chuo cha ufundi......tulianza kwa kuwataarifu watia nia wote wa ubunge...lengo lilikuwa mtu kipita asije sema hajui...wachungaji na watawa wote pia walishataarifiwa....michango ikianza aliyesikia na amaye hajasikia nikushiriki kwa nia moja.....lengo ni kuwasaidia vijana wetu......tulianza na kirua.....kilema...marangu....mbatia na lyatonga walishiriki....effective tutaanza baada ya kumaliza miradi ya barabara kwanza
 
Ila tatizo naona kama huu mji unakuwa bila mipangilio kuna habari nilizisikia ila sikiamini chanzo chake kwamba kuna mtaalamu wa kizungu aliwahi kusema mji wa moshi ukijengwa kwa ustadi na mipangilio mizuri unaweza kuwa mji mzuri kuliko yote Afrika Mashariki kama sio Afrika

Hlf wakuu siku hizi mbona namba 1 ya usafi tumepotea?
 
Kama hujui Historia ya wachagga kaa kimya mkuu..

Vijiji vya Uchaggani vilijengwa na Serikali ya Uchagga ikishirikiana na KNCU.. Ulikuwa ukiuza kahama kwa chama kuna percent inakatwa inapelekwa kwenye kuimarisha miundombinu, kujenga shule, zahanati, kusomesha wanafunzi na huduma zingine za kijamii. Badala ya Serikali kuona hivyo wakafanya juu chini kuiua KNCU na hizo kazi zake zote wanazofanya..

Baada ya KNCU kukosa nguvu, ndiyo wananchi wakaanza kuchangishana wenyewe na kuendeleza yale yaliyokuwa yanafanywa na serikali waliyokuwa wanaiamini na si serikali ya TANU+CCM.

Mbowe+CDM+Ukawa kwa ujumla wanakataa wananchi ambao wanaishi maisha magumu kuchangishwa michango ovyo angali madini yanamalizwa, gesi inaelekea kuuzwa, bado kodi wanalipa, na deni la taifa kuongezeka kila kukicha. hayo yote bado mnataka muwabane wananchi wa hali ya chini?? Watu wanaiba mabilioni, wengine wanasema million 10 ni pesa ya mboga bado mnataka mchangishe watu??

Haya pitia hiyo attachment uone harakati zilianza lini..
View attachment 275644


Kuna baadhi ya watu neno Kncu ni msamiati kwao hasa wale mikoa yao hailimi kahawa, ila kwa ufupi kahawa ni zao lenye faida kubwa kwani kilo moja la kahawa ni bei juu sana na mti wa kahawa huweza kudumu kwa miaka mingi. Hivyo hii iliwasaidia na hadi sasa inasaidia kuwapatia wakulima wa zao hili kipato cha uhakika na ikumbukwe soko la kahawa ni la uhakika na la kudumu tofauti na la mahindi n.k

Kncu ilianzishwa na wakoloni kama mbinu ya kukusanya na kununua kahawa toka wakulima na kuitumia kuwasambazia pembejeo na ndivyo ilivyo hadi sasa serikali imeurithi utamaduni huo jambo ambako ni neema kwa wakulima wa kahawa toka Klm na Bukoba na pembejeo kubwa wanayotoa sana madawa tu

Pia kuhusu maendeleo yamechangiwa na wananchi mwenyewe na pia kwa hamasa kubwa na maendeleo wakoloni waliyotuachia kwani uzuri wa mandhari na hali ya hewa iliwavutia kuishi huku na kuanzisha Miradi ya kimaendeleo

Huyu ndugu atakuwa kaona shule za juzi juzi tu za private na za kata ila huko kijijini ndani ndani kuna shule kongwe na nzuri hadi ma swimming pool yapo mfano Umbwe sec, lyamungo, Weruweru, Ashira Girls, Machame sec hizi baadhi zilitaifishwa na serikali toka kwenye mikono ya dini Rc, + maseminari kibao zilizoachwa na mkoloni
 
Ni Mara yangu ya kwanza kuja Moshi Vijijini,nipo kikazi huku nikiwa mtumishi wa Serikali nimeshazunguka vijiji vinne sasa mandhari na hali ya hewa ni nzuri sana na wenyeji ni wakarimu pia.

Naona kila Kijiji kuna shule ya sekondari nzuri tu kama sio moja ni mbili au tatu kabisa wenyeji wananiambia ni kila Kata na imejengwa kwa nguvu za wananchi na baadhi kwa kushirikiana na mashirika ya dini.

Hii nimeipenda sana kumbe ndio maana kila Sector Serikalini hukosi Mchaga hata mmoja kweli inavutia na nimejifunza kitu kutoka kwenye vinywa vya watu.

Tembea uone tembea ujifunze

Mkuu huko hizo shule zilijengwa miaka mingi sana.
Hata ule uhamasishaji wa kujengwa shule za kata wao haukuwahusu kabisa maana tayari wanashule za kutosha kwa kila kata wengi walichagua tu ipi iwe ya kata.
Kama sasa hivi tunahangaika kujenga maabara utekelezaji wa agizo la Rais JK.
Huko ulikopita umekuta wanajenga maabara kwa kila shule? Hawajengi wanazo toka miaka mingi.
 
Mi babu yangu miaka ya 1950's alikua anazunguka akifanya biashara mpaka Mombasa. Na huwezi amini alifanikiwa mpaka kununua lorry miaka hiyo na mpaka leo machuma yake yapo kama ukumbusho.

Na watoto zake wengine alisomesha private schools miaka hiyo Uganda.

Mi nawasifu wazee wetu wa kichaga maana walituwekea background nzuri sana. Dini, elimu, kutafuta pesa.
 
Ila tatizo naona kama huu mji unakuwa bila mipangilio kuna habari nilizisikia ila sikiamini chanzo chake kwamba kuna mtaalamu wa kizungu aliwahi kusema mji wa moshi ukijengwa kwa ustadi na mipangilio mizuri unaweza kuwa mji mzuri kuliko yote Afrika Mashariki kama sio Afrika

Hlf wakuu siku hizi mbona namba 1 ya usafi tumepotea?

Swala la kupotea kwenye usafi hii imesababishwa na rushwa na uonevu wa wahusika wanaosimamia usafi. Jamaa ni waonevu sana na wapo after money hawafanyi kazi yao ipasavyo kama alivyokuwa Mkurugenzi Mama Kinabo.
 
Back
Top Bottom