Nini kimemsababisha Membe kuzigeuka nchi nyingine kuhusiana na Nile Treaty?

MpendaTz

JF-Expert Member
May 15, 2009
2,185
884
Wana JF,
Magezeti yameandika habari kuhusu Waziri wetu wa Uhusiano wa kimataifa kuwageuka wenzake wa Rwanda, Congo, Burundi, Kenya, Ethiopia Uganda na Sudan Kusini kuhusu matumizi ya maji ya mto Nile.

Nchi hizi za Afrika ambazo ni maskini sana ziliazimia kuongeza matumizi ya maji ya mto huo ikiwa ni pamoja na kuzalisha umeme na kwa ajili ya umwagiliaji. Mfumo uliokuwa umewekwa na Waingerza miaka ya ishirini ulikuwa hauna maslahi kabisa kwa nchi ambazo mto huu umepitia.

Kwa kifupi ni sawa na kwamba mto ule unamilikiwa na Egypt. Kuna wakati hata waliwahi kutamka eti nchi itakayogusa maji yale itapigana nayo vita.

Tanzania ilikuwa kati ya nchi zilizokuwa mstari wa mbele kudai mfumo huo wa kibepari na kibaguzi ubadilishwe kwa maslahi ya mataifa yote ambamo mto huu umepitia. Cha kushangaza Mh. Membe (au tuseme Tanzania) hivi karibuni imezigeuka nchi zote zenye kudai matumizi zaidi ya mto huo eti kwamba anajali zaidi maslahi ya wa-Egypt.

Nashindwa kutafakari maana ya uamuzi huo. Najiuliza hivi huu ndiyo mwendo wa kuelekea uchaguzi mwakani?? Maana inasemekana aliliongelea hata Bungeni.

Ukitaka kuona mojawapo ya maandiko kuhusu jambo hilo soma The EastAfrican la June 22-27 2014.
===========================


HATUA ya Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, kutetea taifa la Misri katika mgogoro wa matumizi ya maji ya Mto Nile imewakera mawaziri wenzake kwa vile matamshi yake yanapingana na msimamo wa Baraza la Mawaziri, Raia Mwema limeambiwa.

Hivi karibuni, Membe alikaririwa katika vyombo vya habari akieleza kwamba Taifa la Misri linapaswa kutazamwa katika suala la matumizi ya maji ya Mto Nile kwa vile bila maji hayo, nchi hiyo itaumia zaidi.

Hata hivyo, msimamo huo wa Membe umepokewa kwa mshangao na mawaziri wenzake waliozungumza na gazeti hili na kusema kwamba anachokifanya ni kupingana na Baraza zima la Mawaziri.

"Sikiliza. Membe amekosea. Mambo yote ya maji, na hususan, masuala ya Mto Nile yako chini ya Waziri wa Maji. Hili nakwambia kwa uhakika kabisa. Membe si msemaji wa serikali kwenye mambo ya maji kama anavyotaka kuaminisha umma.

"Kimsingi, mambo yote anayofanya Waziri wa Maji kuhusu Mto Nile yamejadiliwa katika Baraza la Mawaziri na yameafikiwa. Hakuna tena waziri mmoja anayeweza kutengua," alisema mmoja wa mawaziri aliyezungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki ambaye kwa sababu za wazi kabisa tunahifadhi jina lake.

Membe na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Jumanne Maghembe, wameingia katika hali ya sintofahamu kuhusu suala hilo la Mto Nile, katika namna ambayo imewashangaza wafuatiliaji wa siasa za Tanzania katika eneo hilo.

Maghembe alisema Tanzania inakaribia kuridhia Mkataba wa Matumizi Endelevu ya Maji ya Mto Nile (Nile Basin Cooperative Framework Agreement-CFA) ifikapo Novemba mwaka huu, kauli ambayo ilipingwa na Membe aliyesema hilo halitatokea.

Maghembe alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha mawaziri wa nchi zilizo kwenye Bonde la Mto Nile kilichofanyika nchini Ethiopia na Membe ndiyo akaja kuikanusha.

"Mimi ndiye Waziri wa Mambo ya Nje na suala la Mto Nile liko chini yangu. Mimi ndiye ninayewasiliana na Rais kuhusu jambo hilo kila wakati na tayari nimemwambia mwenzangu (Maghembe) kwamba kwenye hili aende taratibu," Membe alinukuliwa na gazeti la The East African akitoa kauli hiyo.

Kauli hiyo ya Membe ndiyo inayodaiwa kuwaudhi mawaziri ambao wanaona kwamba Waziri huyo wa Mambo ya Nje ameshindwa kuonyesha heshima kwa mwenzake na kwa Baraza zima.

Mmoja wa mawaziri waandamizi wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete ameliambia Raia Mwema kwamba kupishana na Baraza la Mawaziri kwa sasa ni sawa na kupingana na misingi ya Taifa.

"Hili suala la Mto Nile lina historia ndefu. Tangu enzi za Mwalimu Nyerere msimamo wetu umekuwa kwamba tupewe haki zetu za kutumia maji hayo. Haya mambo ya kuionea huruma Misri hayapo.

"Ukitaka kuamini, subiri Mkutano wa Bunge wa Novemba mwaka huu, serikali itaridhia makubaliano hayo ya CFA kama ambavyo Maghembe aliwaambia mawaziri wenzake wa Maji," alisema.

Kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, wananchi wa nchi zilizo kwenye CFA wameonyesha mshangao wao kuhusu hatua ya sasa ya Tanzania wakati yenyewe ilikuwa miongoni mwa waanzilishi wa kwanza wa mchakato huo ulioanza Mei, 2010.

Serikali ya Ethiopia pamoja na wananchi wa Taifa ndiyo wanaoonekana kuwa wakali zaidi; wakihisi pengine Tanzania ‘imenunuliwa' na Misri inayodaiwa kufanya hujuma za kukwamisha mchakato huo kufanikiwa.

Ethiopia imezindua ujenzi wa bwawa kubwa kuliko yote barani Afrika la kuzalisha umeme kwa njia ya maji linalofahamika kwa jina la Grand Ethiopia Renaissance Dam (GERD) litakalokuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 6,000 za umeme. Bwawa hilo litakamilika mwaka 2017.

Misri inapinga ujenzi wa bwawa hilo kwa maelezo kwamba litatumia sehemu kubwa ya maji ya Mto Nile na hivyo kuathiri kiwango kinachokwenda katika Taifa hilo la Afrika Kaskazini.

Ethiopia inachangia asilimia 80 ya maji ya Mto Nile.

Wakati wa zama za ukoloni, mwaka 1929, Misri iliingia katika mkataba na Uingereza iliyokuwa bado na makoloni au ikiwa mdhamini wa baadhi ya nchi za Afrika, ulioipa nguvu na udhibiti wa maji ya mto huo mrefu kuliko yote duniani na wenye urefu wa takribani kilomita 6700.

Mojawapo ya vipengele vya mkataba huo, vinaipa Misri haki pekee ya kutumia maji kutoka katika Mto Nile wakati wa majira ya kiangazi na nchi nyingine zisitumie hadi majira hayo yamalizike.

Katika kile kinachofahamika kwa jina la The Nyerere Doctrine; ambao ulikuwa msimamo rasmi wa Tanzania wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere; "mikataba yote iliyoingiwa na wakoloni kwa niaba ya Taifa hili ni batili kwa vile hii haikuwa nchi yao."

CFA iliundwa kwa lengo la kuweka utaratibu mpya wa matumizi ya Mto Nile, kwa vile bila ya kuwepo kwa makubaliano mapya; maana yake yale yaliyokuwepo awali yanakuwa na msingi kisheria.

Nchi zinazounga mkono CFA ni pamoja na Tanzania, Rwanda, Uganda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Ethiopia na Sudan Kusini.

Sudan na Misri zinapinga makubaliano hayo kwa maelezo kwamba yatasababisha maji yanayokwenda kwenye nchi zao kupungua.

Mwaka huu, Waziri wa Mambo ya Nje ya Misri, Nabil Fahmy, alifanya ziara hapa nchini ambapo katika mazungumzo yake na Kikwete; alidai kwamba nchi yake ni kame na inapata wastani wa siku tatu tu za mvua kwa mwaka na hivyo wanategemea zaidi maji ya mto huo.

Aliyepata kuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Meles Zenawi, alipata kusema kwamba japo Misri inadai kwamba ina shida ya maji; inaongoza kwa matumizi mabaya ya nishati hiyo kwa njia ya mvuke unaotoka katika Bwawa la Aswan, umwagiliaji wa zaidi ya ekari milioni mbili za mchele katika eneo la Sinai na pia kuhudumia viwanja vingi vya mchezo wa gofu vilivyopo katika Taifa hilo.

Chanzo: Raia mwema

Mada zaidi kuhusu Mipaka ya Ziwa - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...umie-usomi-wetu-tusimame-kwenye-ukweli-2.html
 
Sidhani kama huu unaweza kuwa msimamo wa Membe na Tanzania...msimamo wa Tanzania kuhusu Nile upo wazi na hakuna wa kuubadilisha....lakini sometimes "dawa ya jeuri ni jeuri"........kidogo hii dawa inaweza kufanya Membe aseme hayo.......bila Tanzania kuna mambo hayaendi....sometimes tunahitaji kuwakumbusha "wajeuri" hilo.....

Uzalendo kwanza....
 
Tangu lini The East African ikaandika mazuri kuhusu Tanzania... Ni kweli Membe ana mapungufu yake pia, lakini hilo gazeti kwa miezi ya karibuni ni linatumika kuiponda Tanzania na kusifia nchi zingine za Africa Mashariki. Lipo tayari hata ku-spin habari ilimradi Tanzania ionekane hovyo..
 
Tangu lini The East African ikaandika mazuri kuhusu Tanzania... Ni kweli Membe ana mapungufu yake pia, lakini hilo gazeti kwa miezi ya karibuni ni linatumika kuiponda Tanzania na kusifia nchi zingine za Africa Mashariki. Lipo tayari hata ku-spin habari ilimradi Tanzania ionekane hovyo..

Lakini ningependa kufahamu kama kweli Mh. Membe aliligusia swala hili bungeni, na alisema nini haswa?
Ingekuwa vyema kufahamu hilo kwanza. La pili kama jambo si la kweli a limeandikwa na hili gazeti si wanao uwezo wa kukanusha na kulielezea lieleweke? Kwanini hakuna aliyekanusha?
I think there is something wrong here!
 
Jibu rahisi:

attachment.php

source: https://www.jamiiforums.com/international-forum/671682-nation-media-group-rwandan-connection.html
 
Tangu lini The East African ikaandika mazuri kuhusu Tanzania... Ni kweli Membe ana mapungufu yake pia, lakini hilo gazeti kwa miezi ya karibuni ni linatumika kuiponda Tanzania na kusifia nchi zingine za Africa Mashariki. Lipo tayari hata ku-spin habari ilimradi Tanzania ionekane hovyo..

Soma vizuri habari yenyewe badala ya kuishi kwa hisia. Membe binafsi kahojiwa katoa sababu za Tanzania kubadili msimamo. Sasa issue ni kama hata hapa nyumbani wadau walishirikishwa ktk msimamo huo mpya ambao umewastua jirani zetu!! Na sijui kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ndugu Edward Lowassa aliarifiwa kuhusu msimamo mpya kwasababu nafahamu jinsi gani alipambana kutetea msimamo wetu wa awali wakati huo akiwa Waziri wa Maji.
 
hivi ndivyo viongozi wetu wanavyotugeuka swali hili liliulizwa bungeni likajibiwa na naibu waziri kuwa msimamo wa Tanzania ni kuwa wamisri wanategemea mto nile tukizidisha matumizi wataathirika lakini ni membe huyo huyo aliyemshambulia Wenje kuwa hana uzalendo lakini yeye sio tu kakosa uzalendo bali pia ni msaliti
 
membe, wamisri ni noma, oooh. ona walivyowafanya aljezeera siku moja tu baada ya kupokea mshiko wa nguvu kutoka marekani
 
Lakini ningependa kufahamu kama kweli Mh. Membe aliligusia swala hili bungeni, na alisema nini haswa?
Ingekuwa vyema kufahamu hilo kwanza. La pili kama jambo si la kweli a limeandikwa na hili gazeti si wanao uwezo wa kukanusha na kulielezea lieleweke? Kwanini hakuna aliyekanusha?
I think there is something wrong here!
In short, ni kweli Mheshimiwa Membe amezungumzia suala hilo... lakini ukiangalia sana, tukiacha haya mengine, tone yake imesimama sana kwenye ubinadamu...

Hoja yake ni kwamba, Misri ni Mto Nile... pasipo na Mto Nile Misri is almost dead! Misri haina mvua za kutosha... Misri haina mito... Misri haina maziwa... uzima wa Misri unategemea kwa kiasi kikubwa sana, tena sana Mto Nile! Mathalani, In most areas, Egypt receives less than 80mm of precipitation na ni maeneo machache sana, especially yale ya Mediterranean, ndiyo yanayofikia angalau 200 mm annual average wakati Tanzania, ukichukua Dodoma ambayo ni moja ya maeneo kame kabisa, inapata average annual rainfall ya 500mm! Unlike Misri, nchi zingine zina alternatives... mathalani, Tanzania tuna mito na maziwa kila kona not mentioning enough annual rainfall. UKiangalia Uganda nao, wana mito na maziwa with enough annual rainfall probably than any other EA State. Sasa basi, hoja ya Membe (au ya wale wanaomshauri) ni kwamba, tukisema kila nchi iliyo kwenye Bonde la Mto Nile itumie maji yake kama inavyotaka, inaweza kuleta madhara makubwa sana kwa nchi kama Misri ambayo uhai wake unategemea Nile River kwa kiasi kikubwa!!! Hivyo basi, hoja ya Membe ni kwamba, mosi suala la Egypt kuwa na Exclusive Right ya kutumia Mto Nile hilo nalo halikubaliki... kila nchi mwanachama lazima awe na haki ya kutumia mto huo. Lakini pamoja na kwamba kila nchi iwe na haki hiyo, lakini pia tuwazingatie na wengine ambao hawana alternatives... God forbid, leo hii Mto Nile ukikauka, All EA Countries zitaendelea na maisha lakini Egypt balaha litakalotokea Egypt si dogo!
 
Tangu lini The East African ikaandika mazuri kuhusu Tanzania... Ni kweli Membe ana mapungufu yake pia, lakini hilo gazeti kwa miezi ya karibuni ni linatumika kuiponda Tanzania na kusifia nchi zingine za Africa Mashariki. Lipo tayari hata ku-spin habari ilimradi Tanzania ionekane hovyo..

Heshima kwako mpnz
 
In short, ni kweli Mheshimiwa Membe amezungumzia suala hilo... lakini ukiangalia sana, tukiacha haya mengine, tone yake imesimama sana kwenye ubinadamu...

Hoja yake ni kwamba, Misri ni Mto Nile... pasipo na Mto Nile Misri is almost dead! Misri haina mvua za kutosha... Misri haina mito... Misri haina maziwa... uzima wa Misri unategemea kwa kiasi kikubwa sana, tena sana Mto Nile! Mathalani, In most areas, Egypt receives less than 80mm of precipitation na ni maeneo machache sana, especially yale ya Mediterranean, ndiyo yanayofikia angalau 200 mm annual average wakati Tanzania, ukichukua Dodoma ambayo ni moja ya maeneo kame kabisa, inapata average annual rainfall ya 500mm! Unlike Misri, nchi zingine zina alternatives... mathalani, Tanzania tuna mito na maziwa kila kona not mentioning enough annual rainfall. UKiangalia Uganda nao, wana mito na maziwa with enough annual rainfall probably than any other EA State. Sasa basi, hoja ya Membe (au ya wale wanaomshauri) ni kwamba, tukisema kila nchi iliyo kwenye Bonde la Mto Nile itumie maji yake kama inavyotaka, inaweza kuleta madhara makubwa sana kwa nchi kama Misri ambayo uhai wake unategemea Nile River kwa kiasi kikubwa!!! Hivyo basi, hoja ya Membe ni kwamba, mosi suala la Egypt kuwa na Exclusive Right ya kutumia Mto Nile hilo nalo halikubaliki... kila nchi mwanachama lazima awe na haki ya kutumia mto huo. Lakini pamoja na kwamba kila nchi iwe na haki hiyo, lakini pia tuwazingatie na wengine ambao hawana alternatives... God forbid, leo hii Mto Nile ukikauka, All EA Countries zitaendelea na maisha lakini Egypt balaha litakalotokea Egypt si dogo!

..asante kwa kulileta suala hili hapa.

..kuna mgogoro unafukuta kuhusu mkataba wa matumizi ya mto Nile.

..kuna hali ya kugeukana ktk suala zima la mkataba wa matumizi ya maji ya mto Nile.

..hali hiyo imetokea baada ya Egypt kutuma wajumbe wake ktk nchi moja moja ambako mto Nile unapita.

..I wish Membe angeacha kabisa kulizungumzia suala hili. Kwasababu wakati mwingine huyu bwana akizungumza ndivyo anavyozidi kuharibu.

NB:

..Egypt walikataa kushiriki ktk vikao vilivyokuwa vikijadili kuhusu mkataba mpya wa matumizi ya mto Nile.
 
PAYING FOR GIANT NILE DAM ITSELF, ETHIOPIA THWARTS EGYPT BUT TAKES RISKS


Ethiopia's bold decision to pay for a huge dam itself has overturned generations of Egyptian control over the Nile's waters, and may help transform one of the world's poorest countries into a regional hydropower hub.

By spurning an offer from Cairo for help financing the project, Addis Ababa has ensured it controls the construction of the Renaissance Dam on a Nile tributary. The electricity it will generate – enough to power a giant rich-world city like New York – can be exported across a power-hungry region.
But the decision to fund the huge project itself also carries the risk of stifling private sector investment and restricting economic growth, and may jeopardise Ethiopia's dream of becoming a middle income country by 2025.

The dam is now a quarter built and Ethiopia says it will start producing its first 750 megawatts of electricity by the end of this year. In the sandy floor of the Guba valley, near the Sudanese border, engineers are laying compacted concrete to the foundations of the barrage that will tower 145 metres high and whose turbines will throw out 6,000 megawatts – more than any other hydropower project in Africa.

So far, Ethiopia has paid 27 billion birr ($1.5 billion) out of a total projected cost of 77 billion birr for the dam, which will create a lake 246 km (153 miles) long.

It is the biggest part of a massive programme of public spending on power, roads and railways in one of Africa's fastest growing economies. Ethiopia's output has risen at near double digit rates for a decade, luring investors from Sweden to China.

But economists warn that squeezing the private sector to pay for the public infrastructure could hurt future prospects. Growth is already showing signs of slowing.
Even so, Addis Ababa says the price is worth paying to guarantee Egypt has no veto over the dam, the centrepiece of a 25-year project to profit from East Africa's accelerating economic growth by exporting electricity across the region.
"We did not want this dam to suffer from external pressures, particularly with respect to financing," saidFekahmed Negash, a director within Ethiopia's Ministry of Water and Energy.

DIPLOMACY RECAST
Ethiopia's transformation from an economic disaster barely able to feed its people into an emerging regional leader capable of self-financing mega-projects has recast diplomacy over the Nile, northeast Africa's most important resource.

Egypt, which has claimed exclusive right to control the river's waters for generations, is fuming. Cairo worries the dam will reduce the flow on which it has depended for drinking water and irrigation for thousands of years.
It has demanded building be halted pending negotiations between the countries, and had offered to take on joint ownership of the project, an offer Addis Ababa dismissed.

Cairo no longer wields the same leverage it once did when upriver sub-Saharan countries were too poor to build such huge projects themselves.
Still, the dam's cost of more than $4 billion is roughly 12 percent of the annual output of Ethiopia, a steep price to pay for a country spurning outside help.

Ethiopia has resorted to measures like forcing banks that lend to private borrowers to lend the equivalent of 27 percent of their loan books to the government at a low return, effectively a tax on private lending.

Along with other projects, the dam is draining so much financing from the economy that private investors' access to credit and foreign exchange is being jeopardised, hurting growth, the International Monetary Fund says.

The IMF forecast in November that output growth would slow to 7.5 percent this fiscal year from 8.5 percent in 2011/12, and said the economy needed restructuring to encourage private sector investment now crowded out by huge public projects.

Ethiopia needs high growth to fulfil plans to lift its population out of deep poverty. Per capita income was still just $410 in 2012, the World Bank says.
The government disputes the view that lavish public spending is hurting overall economic performance, and forecasts a higher growth rate than the IMF.

Italy's biggest construction firm, Salini Impregilo , which is building the dam, says all payments have been made on time so far and it has no worries about Addis Ababa continuing to come up with the needed billions.
"We have full confidence in the government of Ethiopia," the firm said in an e-mail to Reuters.
And the dam is just the start for Ethiopia's ambition of becoming a regional power hub. A government plan seen by Reuters would see Africa's second most populous nation target installed capacity of 37,000 MW within 25 years – far more than the World Bank's estimate of just 28,000 MW for the entire current output of sub-Saharan Africa excluding South Africa.

More dams are being built and Prime Minister Hailemariam Desalegn is fast securing deals to sell power abroad.
In the Ministry of Energy, a building whose stark design is a throwback to when communists ran Ethiopia's economy into the ground, a poster maps Ethiopia's energy goals.

From a dot on the Nile, lines run north through Sudan and across the Sahara desert as far as Morocco while extending southwards to South Africa, linking Kenya, Rwanda, Tanzania and other power-hungry economies.
Djibouti, Kenya and Sudan already take 180 MW, which, though a small amount so far, is already changing the economics of electricity in the region, Ethiopian officials say.
"Before it started getting power from Ethiopia, Djibouti's tariff was 30 U.S. cents per kilowatt hour. We are selling to them at 6 cents," said Mekuria Lemma, corporate planning chief at Ethiopia's state-run power corporation,EEPCO.
Kenya has signed an agreement to buy about 400 MW. Rwanda too inked a deal in March to take 400 MW by 2018 and a similar arrangement with Tanzania is expected. Beyond Africa, talks are expected over supplying 900 MW to Yemen via an undersea cable.


NATIONAL SECURITY
As long as Ethiopia spurns outside funding, there seems to be little an angry Cairo can now do to stop the dam.
The sparkling streams at the foot of Ethiopia's Mount Gish spill into Lake Tana from where the Blue Nilemeanders gently towards Sudan's capital, Khartoum, where it joins the White Nile and flows north through Egyptand drains into the Mediterranean.

Among Cairo's worries is concern that years of filling the new dam's 74 billion cubic metre reservoir will temporarily cut the river's flow, and that surface water evaporation from the huge new lake will then reduce it permanently.
"Water problems even without this dam are sky high," said water expert Klaus Lanz in reference to Egypt's shortage.
Egypt leans on a 1959 treaty with Sudan which hands Cairo the lion's share of water. Some Egyptian politicians even urged military action last year against Ethiopia, raising concerns of a "water war".

The public political bluster has died down, but Egyptian officials still refer to safeguarding their nation's quota of the Nile's flow as a matter of national security.

In a government white paper, Cairo calls the construction of the dam a "violation" of international legal principles, in particular the duty to prevent harm to other riparian nations.

"We have no other resources," Egyptian foreign ministry spokesman Badr Abdelatty told Reuters. "So it's not a joke. We will not allow our national interests, our national security … to be endangered."

LIMITED OPTIONS
"We are still for cooperation, negotiation, but only serious negotiations, not to waste time," Abdellaty added.

But distracted by militant violence and political turmoil at home, Cairo appears to have few levers with which to force Addis Ababa to halt the project. Ethiopian officials say the dam could be completed as early as 2016.

Ethiopia denies Egypt will suffer and complains that its northern neighbour has flexed its political muscle to deter financiers from backing other Ethiopian power projects.

Fekahmed of the water ministry said Cairo had influenced a decision by China's Electric Power Equipment and Technology Co. to pull out of a $1 billion deal to connect the dam to the grid.
"The authorities in Egypt made a noise," Fekahmed said, adding that another Chinese group was now lined up to fund the high voltage lines. Egypt's Abdelatty did not comment on the specific case but confirmed that Cairowas trying to use its influence to push foreigners away from backing the project.

"We have contacts with everybody," said Abdelatty. "(The minister) raised it with Russia, with China, you name it."
In a diplomatic coup for Ethiopia, and a political blow to Egypt, the other major down river country, Sudan, has slowly warmed to the dam project and lifted its own earlier objections. Sudan may benefit from cheap power and irrigation water.

Egyptian Foreign Minister Nabil Fahmy told Sky News Arabic this month he rejected a military solution and dismissed referring the dispute to the International Court of Justice, which would require the agreement of both sides.

Instead, Egypt continues to push hard for further studies on the dam's design and impact on downstream countries. All the while, Ethiopia shows no sign of ordering the downing of tools.

"We will finish it whether they like it or not," said a senior Ethiopian official who requested anonymity. "But of course, we will continue negotiating in the meantime."

source: Paying for giant Nile Dam itself, Ethiopia thwarts Egypt but takes risks | Ethiopian Opinion
 
Labda kishapokea mshiko kutoka Misri. Uongozi wa Tanzania unanunulika.

Mkuu kuna mkataba uliingiwa toka Enzi za awamu ya kwanza baina ya Tanzania na Misri mbali na ile ya Mwingereza!!! Mpaka sasa fedha zote za kuchimba visima virefu zinatoka Misri! Wajanja wachache sana Serikalini wanalijua hili na mara nyingi huwa inaishia kwenye mifuko ya MAJIZI machache ya CCM!... Inasemekana kuwa Misri walitoa fedha nyingi sana kumchafua Lowassa kwani alikuwa anaonekana tishio sana kwa mipango yake kabambe ya matumizi ya maji ya ziwa Victoria! Sito shangaa kusikia kuwa Membe amevuta fedha za kumsaidia Kampeni kutoka Serikali ya Misri via USA!!! ... Soon Mambo mengi yatafunguka tu, suala la muda tu ...
 
RockSpider,

..Egypt wamepiga kampeni ili Ethiopia anyimwe fedha za ujenzi wa mradi wao wa umeme.

..sasa Ethiopia wamewazidi maarifa kwani wameamua kuwa watakamilisha mradi huo kwa fedha zao za ndani.

NB:

..Egypt wamemwaga misaada kwa Tanzania ndiyo maana unaona tumeanza kuyumba kimsimamo.

cc NasDaz
 
Last edited by a moderator:
In short, ni kweli Mheshimiwa Membe amezungumzia suala hilo... lakini ukiangalia sana, tukiacha haya mengine, tone yake imesimama sana kwenye ubinadamu...

Hoja yake ni kwamba, Misri ni Mto Nile... pasipo na Mto Nile Misri is almost dead! Misri haina mvua za kutosha... Misri haina mito... Misri haina maziwa... uzima wa Misri unategemea kwa kiasi kikubwa sana, tena sana Mto Nile! Mathalani, In most areas, Egypt receives less than 80mm of precipitation na ni maeneo machache sana, especially yale ya Mediterranean, ndiyo yanayofikia angalau 200 mm annual average wakati Tanzania, ukichukua Dodoma ambayo ni moja ya maeneo kame kabisa, inapata average annual rainfall ya 500mm! Unlike Misri, nchi zingine zina alternatives... mathalani, Tanzania tuna mito na maziwa kila kona not mentioning enough annual rainfall. UKiangalia Uganda nao, wana mito na maziwa with enough annual rainfall probably than any other EA State. Sasa basi, hoja ya Membe (au ya wale wanaomshauri) ni kwamba, tukisema kila nchi iliyo kwenye Bonde la Mto Nile itumie maji yake kama inavyotaka, inaweza kuleta madhara makubwa sana kwa nchi kama Misri ambayo uhai wake unategemea Nile River kwa kiasi kikubwa!!! Hivyo basi, hoja ya Membe ni kwamba, mosi suala la Egypt kuwa na Exclusive Right ya kutumia Mto Nile hilo nalo halikubaliki... kila nchi mwanachama lazima awe na haki ya kutumia mto huo. Lakini pamoja na kwamba kila nchi iwe na haki hiyo, lakini pia tuwazingatie na wengine ambao hawana alternatives... God forbid, leo hii Mto Nile ukikauka, All EA Countries zitaendelea na maisha lakini Egypt balaha litakalotokea Egypt si dogo!

Hili la ubinadamu vema kabisa,Tanzania sio kisiwa na ndio diplomasia ya juu, maanake ukienda kwa wenzetu wa misri ,huu mto utazania kuna almasi ndani au ndio uzima unapatikana hapo,hapa Mhe Membe naona kajitofautisha sana na na wanasiasa wenzake ndani na nje ya nchi,maanake wengine kwakutaka misifa wasinge angalia upande wa pili wa hili swala ambao niubinadamu,wao wangekomaa na msimamo usio na tija kwa sababu tu za umaarufu, nikisoma hii nakala nimejifunza kuhusu sawa na usawa yani equally and equity...Mh Membe si ulala tu uoteshwe haraka
 
Back
Top Bottom