Ama kwa hakika wakati tulio nao ni rahisi zaidi kuingo'a CCM na serikali yake kuliko wakati wowote mwingine uliopita.Kuna kila sababu na uwezo wa kufanya hivyo kipindi hiki ambacho tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Binafsi huwa sipendelei kuviita vyama vingine vya siasa (mbali ya CCM) kama ni vya upinzani bali ni vyama vya USHINDANI. Vyama vyote vya siasa vinashindana kupata ridhaa ya wananchi ili viweze kuongoza nchi sio kupingana. Na hili la kuviita vyama vingine kuwa ni vya upinzani, ni moja ya sumu mbaya ambayo CCM huwa inaimwaga kwa wananchi wengi ambao wako vijijini na kujenga taswira kwao kwamba ni vyama vya kihaini, kigomvi, kidini na vinavyoweza kuleta madhara katika nchi - hivyo basi waviogope na wavikatae.
Kwa hili hiyo basi tuviite vyama vya USHINDANI, tofauti yake na CCM ni kwamba CCM kilishinda uchaguzi (kama hila au laa sote tunajua jibu lake) - period.
Nini kifanyike:
Kwa vile CCM imeshindwa ku-deliver na wala haielekei kubadilika, vyama vya USHINDANI vina nafasi kubwa ya kuutumia mwanya huu pamoja na madudu mengine anuai ambayo yametokana na CCM na serikali yake. Ni wakati muafaka vyama hivi vya USHINDANI sio tu kutangaza sera za chama chao, waende mbele zaidi wakati wanajinadi wawaambie wananchi watazilindaje sera zao baada ya kupewa ridhaa ya kuongoza (sio kutawala). Hata wanaotaka kupindua nchi huwa tayari wameshapanga rais pamoja baraza la mawaziri. Kama wanavyokuwa na inayoitwa "Bajeti ya Upinzani" basi wakati wanatangaza sera ni vizuri pia wasema bila kuficha kwamba baraza lao litafanya nini:
1. Tuanze na katiba ambayo inaonekana ina mapungufu na viraka vingi, waseme kwamba tutasimamia mabadiliko ya katiba ili yaweze kukidhi haja za watanzania kwa kizazi kilichopo na kijacho bila kujali ni kwa manufaa ya chama gani cha siasa.
2. Tutabana matumizi ya serikali ili mapato yanayowanufaisha wateule wachache yaweze kwenda kwenye maeneo yanayonufaisha wengi - how?
- tutapunguza baraza la mawaziri
- tutaondoa vyeo vilivyojazana na kufanya "duplication" of duties. Hakuna sababu kwenye mkoa kuwa na msururu wa viongozi, mkuu wa mkoa, RAS, meya wa mkoa (jiji), mkuu wa wilaya, DAS, mameya wa wilaya,nk wakati huo huo kukiwa na halmashauri za jiji na wilaya na madiwani kibao -WHY? Halmashauri ya miji na wilaya zikiongozwa na madiwani na mameya ambao wamechaguliwa na wananchi wanatosha kabisa kuleta maendeleo katika maeneo yao husika wakishirikiana na wabunge wao waliowachagua.
- tutapunguza mishahara na marupurupu makubwa (kama alivyosema ndugu Slaa) ya wabunge na mawaziri ili iweze kuendana na hali halisi ya mtanzania ( kwahili nandani wengi hawatagombea ubunge, kwani sasa ni dili inayolipa kuliko zote).Ikibidi tutapunguza viti vya ubunge kwani pia ni vingi bila ya uwiano wa uchumi.
- Magari yote ya anasa (VX, GS, BMW) tutayapiga mnada na kununua magari yananoendana na uchumi wetu, km Suzuki.
3. Viporo vyote ambavyo hajafanyiwa kazi sisi tutavinyia - VIPI?
- Madudu yote ya EPA, Meremeta,Kagoda, Richmond, rada,nyumba za serikali zilizouzwa,nk tutafufua upya bila kuacha jiwe moja kiligeuza na kila aliyehusika atachukuliwa hatua stahiki hata kama alikwisha staafu au kujiuzulu, hii ni pamoja na wale wote ambao kesi zao za kisanii ziko mahakamani.
4. Kwavile watakuwa wameshapanga baraza lao la mawaziri ni vizuri wakawaambia wananchi kila wizara itafanya nini, km:
-Wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga taifa( kama watakuwa nayo), wawaambie wananchi kuwa kwa hali halisi ya dunia ilivyo hivi sasa, hatuhitaji jeshi kubwa ambalo ni mzigo kwa taifa. Majirani wetu wote sasa hivi wanajitawala na wala hatuna mpango wa kupigana nao hivyo basi tunahitaji jeshi dogo lenye vifaa vya kisasa na sanasana ni jeshi ambalo litakuwa linatusaidia wakati wa vipindi vya maafa kama kule Kilosa au Same (tender za hovyo hovyo zitapungua kama sio kwisha kabisa).
- wataalam ambao wako jeshini kama wahandisi, mabwana shamba, madakitari,nk, watashirikishwa kwenye wizara zingine kama miundo mbinu, kilimo, afya,nk ili waweze kuongeza tija kwenye taifa.
5. Wizara ya madini na nishati:
- wawaambie wananchi kuwa wataipitia upya mikataba yote kati ya serikali na makampuni yote yanayochimba madini yetu na kwa kushirikiana na wataalam na wadau wote kuhakikisha kwamba tunanufaika nayo na sio tutaachiwa mashimo.
- wawaambie wananchi wataipitia upya mikataba ya IPTL, SONGAS, DOWANS na mjomba wake Richmond na kuirekebisha ili imsaidie mwananchi na pale ambapo kuna uchafu ulifanywa, mhusika atachukuliwa hatua stahiki.
- wawaambie wananchi kwamba warudisha mazungumzo ya kufua umeme kutoka Stieglers Gorge ili kukamiliana tatizo sugu la umeme nchini.
6. Wizara ya elimu:
- wawaambie wananchi kwavile tumepunguza gharama nyingi serikalini niwazi kwamba sasa tutakuwa na uwezo wa kuwa na shule bora zenye kutoa elimu bora na sio bora elimu. Vitabu, madawati, maabara, walimu wanaolipwa vizuri na kufanya kazi katika mazingira mazuri vitapatikana.
- wawaambie wananchi ni jinsi gani wataitunza na kuilinda mitihani ili isiibwe na kwa namna gani itawashughulikia wale wote watakaobainika kuiiba au kujipatia vyeti bandia kwa mustakabala wa heshima ya elimu yetu.
Wana jamvi nimejaribu kuweka angalau wizara chache na dondoo chache lakini nia ni kwamba kila wizara sasa hivi ina madudu, kwahiyo hivi vyama vya USHINDANI viseme kwa kila wizara itafanya nini - hii ndio serikali (pamoja na sera zao).
Tusaidiane kuainisha nini kifanyike kwa kila wizara kwa nia ya kuing'oa CCM.
Naomba kuwasilisha.
Moringe wote ni wamasai lakini sio kila mmasai ni Moringe
Binafsi huwa sipendelei kuviita vyama vingine vya siasa (mbali ya CCM) kama ni vya upinzani bali ni vyama vya USHINDANI. Vyama vyote vya siasa vinashindana kupata ridhaa ya wananchi ili viweze kuongoza nchi sio kupingana. Na hili la kuviita vyama vingine kuwa ni vya upinzani, ni moja ya sumu mbaya ambayo CCM huwa inaimwaga kwa wananchi wengi ambao wako vijijini na kujenga taswira kwao kwamba ni vyama vya kihaini, kigomvi, kidini na vinavyoweza kuleta madhara katika nchi - hivyo basi waviogope na wavikatae.
Kwa hili hiyo basi tuviite vyama vya USHINDANI, tofauti yake na CCM ni kwamba CCM kilishinda uchaguzi (kama hila au laa sote tunajua jibu lake) - period.
Nini kifanyike:
Kwa vile CCM imeshindwa ku-deliver na wala haielekei kubadilika, vyama vya USHINDANI vina nafasi kubwa ya kuutumia mwanya huu pamoja na madudu mengine anuai ambayo yametokana na CCM na serikali yake. Ni wakati muafaka vyama hivi vya USHINDANI sio tu kutangaza sera za chama chao, waende mbele zaidi wakati wanajinadi wawaambie wananchi watazilindaje sera zao baada ya kupewa ridhaa ya kuongoza (sio kutawala). Hata wanaotaka kupindua nchi huwa tayari wameshapanga rais pamoja baraza la mawaziri. Kama wanavyokuwa na inayoitwa "Bajeti ya Upinzani" basi wakati wanatangaza sera ni vizuri pia wasema bila kuficha kwamba baraza lao litafanya nini:
1. Tuanze na katiba ambayo inaonekana ina mapungufu na viraka vingi, waseme kwamba tutasimamia mabadiliko ya katiba ili yaweze kukidhi haja za watanzania kwa kizazi kilichopo na kijacho bila kujali ni kwa manufaa ya chama gani cha siasa.
2. Tutabana matumizi ya serikali ili mapato yanayowanufaisha wateule wachache yaweze kwenda kwenye maeneo yanayonufaisha wengi - how?
- tutapunguza baraza la mawaziri
- tutaondoa vyeo vilivyojazana na kufanya "duplication" of duties. Hakuna sababu kwenye mkoa kuwa na msururu wa viongozi, mkuu wa mkoa, RAS, meya wa mkoa (jiji), mkuu wa wilaya, DAS, mameya wa wilaya,nk wakati huo huo kukiwa na halmashauri za jiji na wilaya na madiwani kibao -WHY? Halmashauri ya miji na wilaya zikiongozwa na madiwani na mameya ambao wamechaguliwa na wananchi wanatosha kabisa kuleta maendeleo katika maeneo yao husika wakishirikiana na wabunge wao waliowachagua.
- tutapunguza mishahara na marupurupu makubwa (kama alivyosema ndugu Slaa) ya wabunge na mawaziri ili iweze kuendana na hali halisi ya mtanzania ( kwahili nandani wengi hawatagombea ubunge, kwani sasa ni dili inayolipa kuliko zote).Ikibidi tutapunguza viti vya ubunge kwani pia ni vingi bila ya uwiano wa uchumi.
- Magari yote ya anasa (VX, GS, BMW) tutayapiga mnada na kununua magari yananoendana na uchumi wetu, km Suzuki.
3. Viporo vyote ambavyo hajafanyiwa kazi sisi tutavinyia - VIPI?
- Madudu yote ya EPA, Meremeta,Kagoda, Richmond, rada,nyumba za serikali zilizouzwa,nk tutafufua upya bila kuacha jiwe moja kiligeuza na kila aliyehusika atachukuliwa hatua stahiki hata kama alikwisha staafu au kujiuzulu, hii ni pamoja na wale wote ambao kesi zao za kisanii ziko mahakamani.
4. Kwavile watakuwa wameshapanga baraza lao la mawaziri ni vizuri wakawaambia wananchi kila wizara itafanya nini, km:
-Wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga taifa( kama watakuwa nayo), wawaambie wananchi kuwa kwa hali halisi ya dunia ilivyo hivi sasa, hatuhitaji jeshi kubwa ambalo ni mzigo kwa taifa. Majirani wetu wote sasa hivi wanajitawala na wala hatuna mpango wa kupigana nao hivyo basi tunahitaji jeshi dogo lenye vifaa vya kisasa na sanasana ni jeshi ambalo litakuwa linatusaidia wakati wa vipindi vya maafa kama kule Kilosa au Same (tender za hovyo hovyo zitapungua kama sio kwisha kabisa).
- wataalam ambao wako jeshini kama wahandisi, mabwana shamba, madakitari,nk, watashirikishwa kwenye wizara zingine kama miundo mbinu, kilimo, afya,nk ili waweze kuongeza tija kwenye taifa.
5. Wizara ya madini na nishati:
- wawaambie wananchi kuwa wataipitia upya mikataba yote kati ya serikali na makampuni yote yanayochimba madini yetu na kwa kushirikiana na wataalam na wadau wote kuhakikisha kwamba tunanufaika nayo na sio tutaachiwa mashimo.
- wawaambie wananchi wataipitia upya mikataba ya IPTL, SONGAS, DOWANS na mjomba wake Richmond na kuirekebisha ili imsaidie mwananchi na pale ambapo kuna uchafu ulifanywa, mhusika atachukuliwa hatua stahiki.
- wawaambie wananchi kwamba warudisha mazungumzo ya kufua umeme kutoka Stieglers Gorge ili kukamiliana tatizo sugu la umeme nchini.
6. Wizara ya elimu:
- wawaambie wananchi kwavile tumepunguza gharama nyingi serikalini niwazi kwamba sasa tutakuwa na uwezo wa kuwa na shule bora zenye kutoa elimu bora na sio bora elimu. Vitabu, madawati, maabara, walimu wanaolipwa vizuri na kufanya kazi katika mazingira mazuri vitapatikana.
- wawaambie wananchi ni jinsi gani wataitunza na kuilinda mitihani ili isiibwe na kwa namna gani itawashughulikia wale wote watakaobainika kuiiba au kujipatia vyeti bandia kwa mustakabala wa heshima ya elimu yetu.
Wana jamvi nimejaribu kuweka angalau wizara chache na dondoo chache lakini nia ni kwamba kila wizara sasa hivi ina madudu, kwahiyo hivi vyama vya USHINDANI viseme kwa kila wizara itafanya nini - hii ndio serikali (pamoja na sera zao).
Tusaidiane kuainisha nini kifanyike kwa kila wizara kwa nia ya kuing'oa CCM.
Naomba kuwasilisha.
Moringe wote ni wamasai lakini sio kila mmasai ni Moringe