Nini kamati kuu ya CHADEMA itaamua kesho kutwa?

KAMATI Kuu (CC) ya Chadema inakutana keshokutwa Ijumaa Dodoma kujadili pamoja na mambo mengine,

1. ripoti ya mgogoro ulioibuka kati ya madiwani wa chama hicho na CCM kuhusu Meya wa Jiji la Arusha
2. maadili ndani ya chama
3. kupokea taarifa ya utendaji wa chama na hali ya kisiasa ndani ya chama na nchini kwa jumla
4. ..........................
5. Mengineyo.........sakata la Shibuda?

Kauli ya Dr. Slaa

"Tuna ajenda mbalimbali katika kikao hicho cha Ijumaa wiki hii, kwanza ni kikao cha kawaida si maalumu, watu wasifikiri tunakaa kwa suala moja, lakini moja ya ajenda ni kujadili suala mgogoro wa Meya wa na Madiwani wa Arusha kwa mapana yake na kisha tutawapa taarifa,"

Alipoulizwa kama watajadili suala la Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda, Slaa alisema

"Hilo suala sinalo mezani kwangu, hivyo hatuwezi kujadili kitu tusichonacho, ila Katiba iko wazi, kuna mamlaka husika ya nidhamu, kamati ya wabunge wa Chadema ndiyo hasa inashughulika na suala hilo, kwanza si sisi, likiletwa kwangu sawa, ila kabla sina cha kusema," alisisitiza Dk Slaa.

Magwanda kwa kuiga bana, eti na wao wanafanyia kikao Dodoma !
 
CHADEMA ni waoga wa kuchukua maamuzi mazito, wataendelea tu kuwakumbatia Zito na Shibuda ingawa ndiyo wanaoongoza kuharibu chama. Hivi kwanini hamchukui ujasiri wa CCM?
a MAGAMBA MNA UJASIRI GANI? HUO WA ROSTAM KUJIVUA GAMBA? KM MNA UJASIRI KWELI MPELEKENI KORTINI KWA UFISADI WAKE BASI. KUDADADEKI WE.
 
Heee!!!!! Kazi ya CDM ni hii saa nashanga kwamba hakuna komplihensivu ratiba? Slaa jivue gamba ama tupe ratiba ya maandamano ya miaka mitano.
Eti 'komplihensivu magamba' CCM bana utawajua tu kwa gutter politics zao LOL!
 
Jadilini pia jimbo la Igunga, na Sababu zilizopelekea hali ya sintofahamu kati ya machinga katika Jiji la Mwanza na Polisi.

 
KAMATI Kuu (CC) ya Chadema inakutana keshokutwa Ijumaa Dodoma kujadili pamoja na mambo mengine,

Alipoulizwa kama watajadili suala la Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda, Slaa alisema

“Hilo suala sinalo mezani kwangu, hivyo hatuwezi kujadili kitu tusichonacho, ila Katiba iko wazi, kuna mamlaka husika ya nidhamu, kamati ya wabunge wa Chadema ndiyo hasa inashughulika na suala hilo, kwanza si sisi, likiletwa kwangu sawa, ila kabla sina cha kusema,” alisisitiza Dk Slaa.

Hapa ndo ninapo ukubali utaratibu mzuri wa chadema. Si kila mtu anaibuna na kuongea ovyo. Ameweka wazi kuna utaratibu. Ingekuwa CCM, nape kesha sema lake, sijui nani vyote vinapingana
 
CDM msifanye makosa kadri mnavyomchekea nyani ndivyo anavyomaliza mahindi flash out Shibuda immediately and start afresh.
 
Hapa ndo ninapo ukubali utaratibu mzuri wa chadema. Si kila mtu anaibuna na kuongea ovyo. Ameweka wazi kuna utaratibu. Ingekuwa CCM, nape kesha sema lake, sijui nani vyote vinapingana
Nape sasa is everything nasikia ameanza kuhoji uadilifu wa Mwenyekiti siku si nyingi atampa siku 90 wait&see.
 
Jadilini pia Jimbo la Igunga na machafuko yaliyotokea Mwanza kati ya machinga na polisi, yawezekana kulikuwa na mkono wa Serikali kuchafua hali ya hewa Mwanza iliyokuwa imetulia kwa muda mrefu.
 
Chief Mkwawa;Nawatakia kila kheri kwenye mkutano wenu. Sisitizeni maadili ya viongozi, hekima na uvumilivu. Imarisheni kitengo cha habari na kuweni na msemaji makini wa chama sio swala la kila mtu kuropoka. Jifunzeni ku-debate mada nzito kabla ya kuzimwaga kwenye jamii. Elwesheni wabunge wapya jinsi ya kufanya kazi. Hadhi ya kiongozi ni pamoja na kuwa kioo cha jamii, elimisheni maana ya kuwa na nidhamu ndani na nje ya chama kwani matendo ya kiongozi yanaathiri uongozi wake na taasisi husika nje na ndani.Jitahidi kuelewa kazi kubwa ni kukuza chama kuliko kugombania vyeo, ugomvi wa vyeo mnaweza kukosa wote, kwani ugomvi unadhoofisha chama. Watambueni wasaliti mapema na muwe wakweli kuwaambia asubuhi msisubiri usiku.Hakikisheni mnaweka mkakati wa kutompa mtu nafasi ya kugombea nafasi yeyote ya chama , ubunge au udiwani kama hana walau miaka miwili ndani ya chama, hii itasaidia kupunguza mamluki kutoka nje wenye tamaa ya pay check badala ya kuhudumia watu. Jitahidi kuelewana ndani, na kama mna tofauti tafutine jinsi ya kuzitatua ndani. kauli zenu zinazoufisha chama hasa kauli hasi na za ugomvi. wekeni rekodi za matukio na matamshi, matendo na uwajibikaji wa kila kiongozi, diwani, na mbunge wa chama ili kuweza kumtathimini pale anapotaka kukwea cheo ndani ya chama asije sema anaonewa.Jengeni chama kwa nia ya kumkomboa mtanzania sio kufikisha nia za ubinafsi, cheo, au utajiri wa mtu. Nawatakia mkutano mwema na muwe na afya na hekima ya kuwatumikia watanzania ambao wengi wao ni masikini na wanawategemea ninyi kuwatetea.Ni mimiChief Mkwawa wa Kalenga.I wish hizi ziwe hadidu za rejea za huo mkutano wa CC ya cdm!
 
Nini kimejiri kwenye kikao maana hili ndilo la maana sasa zaidi ya historia za RA.
 
Jana Ijumaa Kamati kuu ya Chadema ilitegemewa kukaa kikao chake cha kawaida kule Dodoma

Kuna mwenye taarifa zozote kama kilifanyika na kama kilifanyika ajenda zake zilikuwa zipi.

kikao kimekuja na ufumbuzi gani hasa uchaguzi wa Meya na mgogoro wa madiwani wa Arusha.

Asanteni.
 
KAMATI Kuu (CC) ya Chadema inakutana keshokutwa Ijumaa Dodoma kujadili pamoja na mambo mengine,

1. ripoti ya mgogoro ulioibuka kati ya madiwani wa chama hicho na CCM kuhusu Meya wa Jiji la Arusha
2. maadili ndani ya chama
3. kupokea taarifa ya utendaji wa chama na hali ya kisiasa ndani ya chama na nchini kwa jumla
4. ..........................
5. Mengineyo.........sakata la Shibuda?

Kauli ya Dr. Slaa

“Tuna ajenda mbalimbali katika kikao hicho cha Ijumaa wiki hii, kwanza ni kikao cha kawaida si maalumu, watu wasifikiri tunakaa kwa suala moja, lakini moja ya ajenda ni kujadili suala mgogoro wa Meya wa na Madiwani wa Arusha kwa mapana yake na kisha tutawapa taarifa,”

Alipoulizwa kama watajadili suala la Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda, Slaa alisema

“Hilo suala sinalo mezani kwangu, hivyo hatuwezi kujadili kitu tusichonacho, ila Katiba iko wazi, kuna mamlaka husika ya nidhamu, kamati ya wabunge wa Chadema ndiyo hasa inashughulika na suala hilo, kwanza si sisi, likiletwa kwangu sawa, ila kabla sina cha kusema,” alisisitiza Dk Slaa.
Asante mkuu kwa tariifa nzuri...CDM ni chama makini kinachojiandaa kuchukua nchi 2015 hivyo mashushu kama Shibuda laziima wafyekwe sasa hivi ili tukichukua nchi tusiwe na vilaza watakao turudisha nyuma...we believe in CDM and we can rule for more than another 30 years hivyo ni lazima tubakie na watu wenye fikra za maendeleo tu na si kudai ongezeko la posho.
 
Asante mkuu kwa tariifa nzuri...CDM ni chama makini kinachojiandaa kuchukua nchi 2015 hivyo mashushu kama Shibuda laziima wafyekwe sasa hivi ili tukichukua nchi tusiwe na vilaza watakao turudisha nyuma...we believe in CDM and we can rule for more than another 30 years hivyo ni lazima tubakie na watu wenye fikra za maendeleo tu na si kudai ongezeko la posho.


chadema naomba tusiendelee kufanya makosa yanayoepukika
swala la shibuda ni uongozi wa chadema kulaumiwa
lile swala la kutoa maamuzi limulikwe upya!
 
Suala la shibuda na Uchaguzi mdogo wa igunga ni moja ya agenda za kikao. Ushauri wangu: SHIBUDA APEWE ONYO LA MWISHO, AKIFANYA UPUUZI TENA AFUKUZWE JUMLA!
 
Back
Top Bottom