Nini husababisha watu kupata shoti kama ya umeme wanaposalimiana?

bCg

JF-Expert Member
Jan 16, 2014
385
689
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2004, miaka 19 imepita nikiwa nimehitimu kidato Cha nne, nilikwenda kumtembelea mjomba wagu.

Nikiwa nyumbani kwa mjomba mjini Tabora mtaa wa Isebya, siku hiyo mjomba alinichukua kwa lengo la kunizungusha sehemu mbalimbali mjini Tabora. Katika pitapita tuliingia katika baa moja (jina nimelisahau) kwa ajili ya kupata angalau soda.

Basi tulimkuta mhudumu (kwa umri nahisi alikuwa kwenye miaka 30 plus) wakasalimiana na mjomba kwa kushikana mikono, na baadaye ikafika zamu yangu. Ile namshika mkono tu nilihisi kupigwa na shoti ya umeme (kitendo cha kushikana ilikuwa kama vile nimeshika waya wenye umeme), ikanibidi kuutoa mkono harakaharaka na kwa nguvu na tukabaki tunashaangaana!

Wana JF hilo tukio mpaka leo sijawahi lisahahu, na kila huwa nikipata utulivu hilo tukio hunijia hakili, na huwa nawaza kuwa ilikuwa ni hali au kitu gani?

Najua humu tuna watu wa kila aina, tafadhali kwa yeyote mwenye ujuzi wa hali kama hiyo kisayansi au namna nyingine au kukutana na jambo kama hilo anaweza kunifahamisha.
 
Kuna dogo mmoja miaka ya 2017 alikuwa akishika kitu chochote kisicho cha umeme anapigwa shoti na hata ukimshika mkono mara moja moja alikuwa na shoti hatari,labda wataalamu waje watupe majibu.
 
Wanaposalimiana naomba marekebisho kwenye heading
 
Kuna uwezekano mkubwa moja kati yenu likuwa amegusa waya wa umeme au eneo alipokuwa palikua na unyevu nyevu ulipita kwenye njia ya umeme, kwaiyo mliposhikana mikono ndiyo umeme ukapata asi
 
labda kulikuwa na waya upo wazi na kuna unyevu, halafu mmoja kati yenu hakuvaa viatu au alivaa viatu vimelowa. Hapo mlipigwa na kiumeme kidogo sana, either chaja au taa. Mngekutana na mashine mngejua. NILIKUWA NAINSTAL A/C MAHALI IKWAWEPO LEAKAGE, NIKAMWAMBIA JAMAA ANIPE UDJUST CABLE. NILIKUWA PEKU. TULIPIGWA KITU HADI JAMAA ALIZIMIA. Umeme ni hatari.
 
Hii hali alinisimulia wife mwezi wapili ktk shughuli zake alikuja mteja wakati anamrudishia chenji wakagusana mikono basi ikamtokea hiyo shoti.
 
labda kulikuwa na waya upo wazi na kuna unyevu, halafu mmoja kati yenu hakuvaa viatu au alivaa viatu vimelowa. Hapo mlipigwa na kiumeme kidogo sana, either chaja au taa. Mngekutana na mashine mngejua. NILIKUWA NAINSTAL A/C MAHALI IKWAWEPO LEAKAGE, NIKAMWAMBIA JAMAA ANIPE UDJUST CABLE. NILIKUWA PEKU. TULIPIGWA KITU HADI JAMAA ALIZIMIA. Umeme ni hatari.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom