Ninayahusisha mauaji ya Morogoro na Iringa na CCM kutokana na kauli ya Nape Nnauye

Mercyless

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
655
131
Alipokuwa akiongea na waandishi wa habari siku alipoita mikutano ya uchangiaji M4C ya CHADEMA kuwa ni usanii mtupu, Nape alieleza kuwa CHADEMA wamepanga kufanya vurugu ktk mkutano wao wa Morogoro. Hivi inawezena ukaandaa mkutano alafu ukapanga pia kujifanyia vurugu? Hakuna m2 mwenye akili timamu anayeweza kufanya ujinga kama huu isipokuwa kwa sasa ni ccm pekee ndio wanaweza kufanya ujinga huu ili kuvipaka matope vyama vingine. Walijaribu kuingilia mkutano wa CHADEMA Singida yakawakuta yaliyowakuta. Hivyo ninafikiri kuwa sasa wameamua kutumia policcm kuzima vuguvugu la mabadiliko (M4C). Aliyoyasema Nape yalikuwa na lengo tu la kuhalalisha upumbavu wao huu ili ionekane mbele ya wananchi kuwa ni CHADEMA ndio wanaoasisi vurugu hizi.

Mbinu hizi chafu za ccm zinadhihirisha kuwa kwa sasa ccm haiwezi tena kupambaNA na vyama vya upinzani kwa siasa za majukwaani kwani hawana sera zenye mvuto kwa wananchi. Hivyo basi lengo lao kubwa ni kuwatisha wananchi wasiwe wanahudhuria mikutano ya vyama vya upinzani zaidi ikiwa ni CHADEMA, bila kujua kuwa kufanya hivyo ndio kunazidi kukiimarisha CHADEMA na kujenga chuki dhidi ya serikali ya ccm.

Ninaomba Nape leo hii ajibu aseme kauli yake aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari ilikuwa na mantiki gani kama si alikuwa anawaandaa wananchi waelewe kuwa CHADEMA ni chama cha vurugu? Wamepiga santuri nyingi sana lakini watu hawakuzicheka (udini, ukabila, ukanda, ukatoliki na sasa vurugu) na kwa hili la sasa nadhani wanafikia mwisho wa kufikiri kwani huwa ni wavivu sana wa kufikiri.
 
Nape anajua kinachoendelea kwani aliwataadhalisha wananchi wasiende mikutano ya CHADEMA kwa kuwa kutakuwa na vurugu.Pia navyojua akili ya Mwigulu na Lusinde bila shaka wao ndio waliotoa ushauri wa huu mkakati wa mauaji unaondelea
 
Ameshasema CDM kitasambaratika!!!!!
CDM haiwezi kusambaratika kwa mbinu za kijinga namna hiyo. Kumbukeni zile picha za vita ya Rwanda mlizotembea nazo 2005 hamkuthubutu kuja nazo 2010kwani wananchi walishajua nia ni kuwaogopesha .Kwa sas wananchi wana uelewa mpana na tumeshawashtukia .POLENI SANA
 
Nape ameshacove nafasi ya Yahya Hussein.anapaswa kuhojiwa kwa kauli yake iyo pengine anawajua wapanga hujuma..angekuwa mnyika katoa kauli ile leo 2ngekuwa tunaimba nyimbo za kumtoa segerea.
 
Back
Top Bottom