Alipokuwa akiongea na waandishi wa habari siku alipoita mikutano ya uchangiaji M4C ya CHADEMA kuwa ni usanii mtupu, Nape alieleza kuwa CHADEMA wamepanga kufanya vurugu ktk mkutano wao wa Morogoro. Hivi inawezena ukaandaa mkutano alafu ukapanga pia kujifanyia vurugu? Hakuna m2 mwenye akili timamu anayeweza kufanya ujinga kama huu isipokuwa kwa sasa ni ccm pekee ndio wanaweza kufanya ujinga huu ili kuvipaka matope vyama vingine. Walijaribu kuingilia mkutano wa CHADEMA Singida yakawakuta yaliyowakuta. Hivyo ninafikiri kuwa sasa wameamua kutumia policcm kuzima vuguvugu la mabadiliko (M4C). Aliyoyasema Nape yalikuwa na lengo tu la kuhalalisha upumbavu wao huu ili ionekane mbele ya wananchi kuwa ni CHADEMA ndio wanaoasisi vurugu hizi.
Mbinu hizi chafu za ccm zinadhihirisha kuwa kwa sasa ccm haiwezi tena kupambaNA na vyama vya upinzani kwa siasa za majukwaani kwani hawana sera zenye mvuto kwa wananchi. Hivyo basi lengo lao kubwa ni kuwatisha wananchi wasiwe wanahudhuria mikutano ya vyama vya upinzani zaidi ikiwa ni CHADEMA, bila kujua kuwa kufanya hivyo ndio kunazidi kukiimarisha CHADEMA na kujenga chuki dhidi ya serikali ya ccm.
Ninaomba Nape leo hii ajibu aseme kauli yake aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari ilikuwa na mantiki gani kama si alikuwa anawaandaa wananchi waelewe kuwa CHADEMA ni chama cha vurugu? Wamepiga santuri nyingi sana lakini watu hawakuzicheka (udini, ukabila, ukanda, ukatoliki na sasa vurugu) na kwa hili la sasa nadhani wanafikia mwisho wa kufikiri kwani huwa ni wavivu sana wa kufikiri.
Mbinu hizi chafu za ccm zinadhihirisha kuwa kwa sasa ccm haiwezi tena kupambaNA na vyama vya upinzani kwa siasa za majukwaani kwani hawana sera zenye mvuto kwa wananchi. Hivyo basi lengo lao kubwa ni kuwatisha wananchi wasiwe wanahudhuria mikutano ya vyama vya upinzani zaidi ikiwa ni CHADEMA, bila kujua kuwa kufanya hivyo ndio kunazidi kukiimarisha CHADEMA na kujenga chuki dhidi ya serikali ya ccm.
Ninaomba Nape leo hii ajibu aseme kauli yake aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari ilikuwa na mantiki gani kama si alikuwa anawaandaa wananchi waelewe kuwa CHADEMA ni chama cha vurugu? Wamepiga santuri nyingi sana lakini watu hawakuzicheka (udini, ukabila, ukanda, ukatoliki na sasa vurugu) na kwa hili la sasa nadhani wanafikia mwisho wa kufikiri kwani huwa ni wavivu sana wa kufikiri.