Juzi niliingia duka la mhindi mmoja nikiwa natafuta kitu fulani. Nilishangaa kuona nguo za kijani nyigi zikiwa kwenye shelf, nilipouliza je anauza, aliniambia haziuziki, ila tunatoa bure kama nyongeza kwa mtu anayenunua kitu hapa. Nilijaribu kudadisi namna wavyozipata ikaonekana CCM huwalazimisha kuzinunua hizi nguo kama mchango kwa chama. Kinachotokea ni kwamba hazinunuliki hivyo huamua kuzigawa bure kwa anayetaka kama bakhishishi. Nilipata uhakika kwamba huyu muhindi alikuwa amelazimishwa kununua nguo hizo na si kwa mapenzi yake kwa chama.
Kitu kimoja ambacho kiko dhahiri nikwamba mtu akishakusaidia kwa fedha, umekuwa mtumwa kwake wala hutaweza kuyakataa matakwa yake. Wahindi ni watu wenye akili nyingi inapokuja kwenye swala la pesa,HATATOA HELA YAKE BURE BILA KURUDI!
Kuna jamaa yangu mmoja alinipa udaku wa uchaguzi wa 2005, aliniambia tajiri wa mabasi fulani yanayoenda dodoma, alichangia chama kwa mkataba kwamba angerudisha fedha yake kwa kuua usafiri wa train ya Dar mpaka dodoma ili mabasi yake yatumike. Nilijaribu kukumbuka na kweli kukawa na ukweli fulani ndani ya udaku huu. Nikweli kwa kipindi kirefu kulikuwa hamna usafiri wa train toka dar-dom. Inasemekana ulirejea mara baada ya jamaa kurudisha fedha yake na faida.
Kwangu mimi hii ni hujuma kwa wantanzania masikini, sijuwi kunahujuma ngapi za namna hii zilifanyika baada ya 2005 na ni ngapi zimepangwa kufanyika baada ya 2010.
NIAMINIVYO MIMI: KIONGOZI ANAYESHIRIKIANA NA MATAJIRI KUTAWALA HAWEZI KUPELEKA NCHI MASIKINI KAMA TANZANIA KWENYE MAISHA BORA! NI MAISHA BORA KWA KILA TAJIRI NA BORA MAISHA KWA KILA MASIKINI.
Kitu kimoja ambacho kiko dhahiri nikwamba mtu akishakusaidia kwa fedha, umekuwa mtumwa kwake wala hutaweza kuyakataa matakwa yake. Wahindi ni watu wenye akili nyingi inapokuja kwenye swala la pesa,HATATOA HELA YAKE BURE BILA KURUDI!
Kuna jamaa yangu mmoja alinipa udaku wa uchaguzi wa 2005, aliniambia tajiri wa mabasi fulani yanayoenda dodoma, alichangia chama kwa mkataba kwamba angerudisha fedha yake kwa kuua usafiri wa train ya Dar mpaka dodoma ili mabasi yake yatumike. Nilijaribu kukumbuka na kweli kukawa na ukweli fulani ndani ya udaku huu. Nikweli kwa kipindi kirefu kulikuwa hamna usafiri wa train toka dar-dom. Inasemekana ulirejea mara baada ya jamaa kurudisha fedha yake na faida.
Kwangu mimi hii ni hujuma kwa wantanzania masikini, sijuwi kunahujuma ngapi za namna hii zilifanyika baada ya 2005 na ni ngapi zimepangwa kufanyika baada ya 2010.
NIAMINIVYO MIMI: KIONGOZI ANAYESHIRIKIANA NA MATAJIRI KUTAWALA HAWEZI KUPELEKA NCHI MASIKINI KAMA TANZANIA KWENYE MAISHA BORA! NI MAISHA BORA KWA KILA TAJIRI NA BORA MAISHA KWA KILA MASIKINI.