Nina mkosi wa kudhulumiwa

mwanga mweusi

JF-Expert Member
Dec 21, 2020
255
407
Hata sielewi kwanini inanitokea hivi. Nilifanya kazi kwa jamaa mmoja akanidhulumu Tsh. 470,000/-. Nikafanya kazi kwa mwingine akanidhulumu Tsh. 70,000/-, mwingine Tsh. 35,000/-, nikauziwa tofali mbovu za Tsh. 200,000/-.

Nikakodi shamba la kulima nimefika kulima nakuta kuna mtu kaanza kulipa pale kwangu anasema nipewe sehemu nyingine!

Mimi sijawahi kula cha mtu, napambana nipate haki yangu ila nadhulumiwa tu hadi nimekata tamaa kabisa!

Sijui hata uelekeo wa kwenda polisi, maana sijawahi kanyaga toka nizaliwe. Nataka niende kwa mganga japo napo sijawahi kanyaga. Sasa naona ugumu kuanza haya mambo ya polisi na wapi huko wakati hata sijui nikifika nasemaje!

Naomba mwenye njia ya kunisaidia anisaidie.
 
Hata sielewi kwanini inanitokea hivi.
Nilifanya kazi kwa jamaa mmoja akanidhulumu 470,000.
Nikafanya kazi kwa mwingine akanidhulumu 70,000
Mwingine 35,000
Nikauziwa tofali mbovu za 200k
Nikakodi shamba la kulima nimefika kulima nakuta kuna mtu kaanza kulipa palekwangu anasema nipewe sehemu nyingine

Mimi sijawai kula cha mtu napambana nipate haki yangu ila nadhulumiwa tu hadi nimekata tamaa kabisa .
sijui hata uelekeo wa kwenda polisi maana sijawai kanyaga toka nizaliwe nataka niende kwa mganga napo sijawai kanyaga sasa naona ugumu kuanza haya mambo ya polisi na wapi uko wakati hatasijui nikifika nasemaje naomba mwenye njia ya kunisaidia

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Jifunze kupambania haki yako, wote tumepitia hayo ila ni kufunga mkanda ili ulinde haki yako, watanzania wengi wakikukuta wewe boya utadhulumiwa tu.......mimi kwenye haki yangu niko tayari kufa na mtu.
 
Moja ya Mafunzo niliyopewa ni kuhakikisha sidhulumiwi hasa pesa nilizozitolea jasho nikiwa na umri Mdogo.
Nisisamehe.
Msamaha ni miaka hiyo angalau umefika miaka 50 huko.

Kudhulumiwa ukiwa kijana mdogo ni kujipa mapepo na roho ya kuonewa. Sio ajabu maisha yako yote yakawa hivyo.
 
You will be a victim... To many times!
If you lough when everyone seem to demand seriously treatment.

If you believe in someone else love and care what you have as his/her own

If you will be weak to everyone, ukiwa na Imani ya kutoa viashiria vya utu.

Unyenyekevu ni outdated principle of life
 
Ni mambo sijawahi kukutana nayo ktk harakati za utafutaji nakushauri kama kazi zako ni kugusa hapa gusa pale (namaanisha siyo kazi moja ni kazi mbalimbali) next time weka vigezo vyako ukipatana na mtu hakikisha kadiri unavyofanya kazi yake na wewe uwe unachukua kiasi cha pesa ktk makubaliano yenu.

Hii itakusaidia mpaka ukikaribia kumaliza unakuwa unadai kiasi kidogo cha pesa ambacho siyo rahisi mtu kuingia tamaa kukudhulumu shida inakuja umepatana kazi laki tano unachukua advance nauli 30K kwa utendaji wako wa haraka unamaliza baada ya siku mbili lazima tajiri aone kama anatupa hela.
 
Moja ya Mafunzo niliyopewa ni kuhakikisha sidhulumiwi hasa pesa nilizoziyolea jasho nikiwa na umri Mdogo.
Nisisamehe.
Msamaha ni miaka hiyo angalau umefika miaka 50 huko.

Kudhulumiwa ukiwa kijana mdogo ni kujipa mapepo na roho ya kuonewa. Sio ajabu maisha yako yote yakawa hivyo
Itabidi nipambinie

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Ni mambo sijawahi kukutana nayo ktk harakati za utafutaji nakushauri kama kazi zako ni kugusa hapa gusa pale (namaanisha siyo kazi moja ni kazi mbalimbali) next time weka vigezo vyako ukipatana na mtu hakikisha kadiri unavyofanya kazi yake na wewe uwe unachukua kiasi cha pesa ktk makubaliano yenu.

Hii itakusaidia mpaka ukikaribia kumaliza unakuwa unadai kiasi kidogo cha pesa ambacho siyo rahisi mtu kuingia tamaa kukudhulumu shida inakuja umepatana kazi laki tano unachukua advance nauli 30K kwa utendaji wako wa haraka unamaliza baada ya siku mbili lazima tajiri aone kama anatupa hela.
Na hiyo ndii sababu kubwa

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Mimi niliwahi kupiga kazi ngumu kisha jasho langu likapotea bure na kudhulimiwa bila hata senti moja , nikaamue niache tu hakuna namna deni langu litalipwa siku ya kiyama..

Nilifanya kazi mwezi mmoja na nusu jamaa akanidhulumisha laki 7 ivi...

laptop accessories yule mwamba 150,000 yangu mpaka Leo.

we Mzee wa makamo (50 years almost) niliekutumia elfu 20 kisa unadai gari Yako imepata hitilafu miezi mitatu iliopita nikusaidie hujalipa mpaka Leo ungejua navyoitafuta hela.

Ile kazi ya uviko na mliopita na hela zetu (150,000) fresh tu ....

Dogo hivyo viatu ulivyonidhulumu hiyo elfu 30 na Mpira wenyewe hutoboi shabbash ......

ndugu mtumishi , naww pia rafiki yangu Ile elfu 50 mpaka tusomeane Dua kweli ,miezi 4 sasa umejikausha ......😔

Ndugu Ile laki uliyosema unanirudishia soon Miaka mi 5 hii sasa ....

nk.

Namshukuru Mungu kwa wote mlionidhulumisha huwa sioni kilichopungua kwenye kile ninachopata hata kama ni kidogo. Ila mkae mkijua kama huko mbeleni kuna kulipana na bila shaka ipo , haki yangu mtailipa tu maana haki ya mtu haidhulumiwi.
 
Back
Top Bottom