Siyane
Member
- Dec 26, 2010
- 46
- 9
Nilikutana na huyu binti kwa mara ya kwanza ndani ya basi moja maarufu lifanyalo safari zake kati ya Dar na Morogoro. Tulikaa nae siti zilizopakana, na sikuongea nae kwa takribani nusu saa nzima ya safari. Baadae akawa amepitiwa na usingizi na kunilalia kwa kuniegemea. Kama ilivyo kawaida ya wanaume walio wengi sikuthubutu kumkatiza usingizi wake kwa kumwamsha asiniegemee. Nilivumilia na robo saa baadae basi likapiga tuta akaamuka na kuniomba radhi kwa kuniegemea. Nilitabasamu nikamwambia usijali na hapo ndio ukawa mwanzo wa maongezi yetu yaliyo pelekea kufahamiana na hadi kubadilishana mawasiliano. Tumetokea kuwa marafiki wakubwa sana sijawahi kuona. Hadi watu walio wengi wanadai nina mahusiano nae ya kingono kwa jinsi nilivyo karibu nae.
Ilikuwa ni mwezi uliopita siku ya boxing day alinipa mwaliko maalumu kumtembelea katika chumba chake anachoishi. Hii haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda kumtembelea na hata yeye alishawahi kunitembelea kwangu mara kadhaa. Kwa kweli kama ni zile sifa za uzuri zinazovuma mitaani naona zote anazo. Ninachokiona cha zaidi kwake ni ile sifa ya kumcha Mungu sana. Nilifika mida ya saa kumi jioni, nikabisha hodi bila kuitikiwa. Kwa kuwa mlango ulikuwa umeachama kidogo yapata uwazi wa sentimeta kumi hivi nilijua hayuko mbali yupo karibu tu. Lakini msukumo mkubwa ulioibuka mshindi ni ule ulionituma kuchungulia kwa kuongeza kidogo upenyo wa uwazi wa mlango. Baada ya kuufungua mlango mboni zangu za macho zikatua katika mwili wake uliositiriwa na kanga moja tu. Alikuwa amelala kifudifudi na ilionekana kama alikuwa amesinzia fofofo.
Nililazimika kumwita mpaka mara nne ndipo akastuka, akanikaribisha, nikaingia na kuketi. Tulibadilishana mawazo, tukaangalia music katika screen, tukacheka, nikala, nikanywa na ilipofika saa moja jioni nilimuaga. Alinisihi nimsubiri aoge ili anitoe kidogo maana nae alikuwa anataka kutoka jioni hiyo. Alikwenda kuoga na aliporejea na kanga yake moja hiyo hiyo nilitaka kumpisha ili avae lakini alikataa na kuvaa nikiwa ndani humohumo. Baadae akaniambia anataka anifanyie surprise lakini sharti nifumbe macho kwanza. Nilitii sharti kwa kuwa nilipatwa shauku ya kuiona surprise yenyewe. Baada ya dakika kama moja akaniambia nigeukie upande wa kitanda ndipo nifumbue macho, nami nikafanya hivyo. Sikuelewa elewa baada ya kufumbua macho kwa juu ya kitanda niliona vitu ambavyo sikutarajia kabisa kuviona. Nilikuta ametapakaza kitanda kizima vipakti vya mipira ya kiume. Nilipogeuka ili kumuuliza kulikoni nilijuta kugeuka. Nilikuta amevua nguo zake zote yupo mtupu kama alivyozaliwa.
Damu yangu ilichemka, akili ikawa sio yangu tena maana kwa kweli maungo yake hadharani yana sifa nzuri mno sijawahi kuona. Damu ilitembea mpaka kwa mwana wa pale kati akakasirika na kuamka. Ghafla iliniijia sura ya mchumba wangu ambaye ninae kwa miaka miwili sasa na mwezi wa kumi mwaka huu tunatarajia kufunga ndoa. Nikamwambia simuelewi mambo anayofanya, wakati huo nikiwa nimetizama pembeni. Tulijibizana huku akiniongelesha kwa sauti ya mahaba na hata akadhubutu kunifuata kwa nyuma na kunigusa gusa. Ili kuepusha mengi niliamua kumuaga huku nikielekea usawa wa mlango pasipo kuinua kichwa kumtazama. Nikakishika kitasa cha mlango na kukinyongea chini huku nikiuvuta mlango kwa ndani. Haukufunguka nikajua amefunga na kuutoa ufunguo. Kuikata stori iwe fupi, ilibidi niwe mpore busara ikatawala zaidi mpaka mdada huyu akaamua kuvaa nguo zake na mambo yakarudi kawaida. Akanisindikiza mpaka nikapanda daladala nae akarudi kwake.
Toka siku hiyo hakomi kunipigia simu na kunitumia meseji za kimahaba. Bahati mbaya mchumba wangu anasoma mwaka wa tatu na wa mwisho chuo kikuu Dododma nami nipo ninaishi Dar es salaam hivyo inakuwa vigumu hata kumchunia rafiki yangu huyu au kuwa na hofu na meseji zake anazonitumia. Toka tukio hili litokee nimekuwa mbali kidogo nae lakini yeye amezidi kuwa karibu sana. Kitu kimoja kikubwa ninachokihusudu toka kwake ni sifa ya urembo pamoja na kujichunga lakini nashangaa kwa nini mimi ananifanyia hivyo. Kuna watu wenye pesa wengi sana huwa wanamfukuzia na hajawahi kumkubalia mtu hata mmoja kati yao na kila kukicha idadi ya wanao ongezeka kwenye list ya wanaomtokea inaongezeka tu. Mda wote wa urafiki wetu sikuwahi kumuona na boy friend tofauti na mimi, na amekuwa akipenda sana kuwa nami na ndio kisa cha watu kusema nina mahusiano nae.
Ndugu zangu wapendwa hayo ndiyo yanayonisibu kwa wakati huu. Nimekamatika njia panda, watu wengi sana wanamtaka tena watu wazito kabisa na maarufu lakini hawajampata lakini kwangu mimi amekuja yeye mwenyewe! Sasa kila siku najiuliza sijui nimshughulikie? au sijui vipi? Naombeni ushauri wenu wana jamii forum wenzangu.
Aksanteni sana.
Ilikuwa ni mwezi uliopita siku ya boxing day alinipa mwaliko maalumu kumtembelea katika chumba chake anachoishi. Hii haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda kumtembelea na hata yeye alishawahi kunitembelea kwangu mara kadhaa. Kwa kweli kama ni zile sifa za uzuri zinazovuma mitaani naona zote anazo. Ninachokiona cha zaidi kwake ni ile sifa ya kumcha Mungu sana. Nilifika mida ya saa kumi jioni, nikabisha hodi bila kuitikiwa. Kwa kuwa mlango ulikuwa umeachama kidogo yapata uwazi wa sentimeta kumi hivi nilijua hayuko mbali yupo karibu tu. Lakini msukumo mkubwa ulioibuka mshindi ni ule ulionituma kuchungulia kwa kuongeza kidogo upenyo wa uwazi wa mlango. Baada ya kuufungua mlango mboni zangu za macho zikatua katika mwili wake uliositiriwa na kanga moja tu. Alikuwa amelala kifudifudi na ilionekana kama alikuwa amesinzia fofofo.
Nililazimika kumwita mpaka mara nne ndipo akastuka, akanikaribisha, nikaingia na kuketi. Tulibadilishana mawazo, tukaangalia music katika screen, tukacheka, nikala, nikanywa na ilipofika saa moja jioni nilimuaga. Alinisihi nimsubiri aoge ili anitoe kidogo maana nae alikuwa anataka kutoka jioni hiyo. Alikwenda kuoga na aliporejea na kanga yake moja hiyo hiyo nilitaka kumpisha ili avae lakini alikataa na kuvaa nikiwa ndani humohumo. Baadae akaniambia anataka anifanyie surprise lakini sharti nifumbe macho kwanza. Nilitii sharti kwa kuwa nilipatwa shauku ya kuiona surprise yenyewe. Baada ya dakika kama moja akaniambia nigeukie upande wa kitanda ndipo nifumbue macho, nami nikafanya hivyo. Sikuelewa elewa baada ya kufumbua macho kwa juu ya kitanda niliona vitu ambavyo sikutarajia kabisa kuviona. Nilikuta ametapakaza kitanda kizima vipakti vya mipira ya kiume. Nilipogeuka ili kumuuliza kulikoni nilijuta kugeuka. Nilikuta amevua nguo zake zote yupo mtupu kama alivyozaliwa.
Damu yangu ilichemka, akili ikawa sio yangu tena maana kwa kweli maungo yake hadharani yana sifa nzuri mno sijawahi kuona. Damu ilitembea mpaka kwa mwana wa pale kati akakasirika na kuamka. Ghafla iliniijia sura ya mchumba wangu ambaye ninae kwa miaka miwili sasa na mwezi wa kumi mwaka huu tunatarajia kufunga ndoa. Nikamwambia simuelewi mambo anayofanya, wakati huo nikiwa nimetizama pembeni. Tulijibizana huku akiniongelesha kwa sauti ya mahaba na hata akadhubutu kunifuata kwa nyuma na kunigusa gusa. Ili kuepusha mengi niliamua kumuaga huku nikielekea usawa wa mlango pasipo kuinua kichwa kumtazama. Nikakishika kitasa cha mlango na kukinyongea chini huku nikiuvuta mlango kwa ndani. Haukufunguka nikajua amefunga na kuutoa ufunguo. Kuikata stori iwe fupi, ilibidi niwe mpore busara ikatawala zaidi mpaka mdada huyu akaamua kuvaa nguo zake na mambo yakarudi kawaida. Akanisindikiza mpaka nikapanda daladala nae akarudi kwake.
Toka siku hiyo hakomi kunipigia simu na kunitumia meseji za kimahaba. Bahati mbaya mchumba wangu anasoma mwaka wa tatu na wa mwisho chuo kikuu Dododma nami nipo ninaishi Dar es salaam hivyo inakuwa vigumu hata kumchunia rafiki yangu huyu au kuwa na hofu na meseji zake anazonitumia. Toka tukio hili litokee nimekuwa mbali kidogo nae lakini yeye amezidi kuwa karibu sana. Kitu kimoja kikubwa ninachokihusudu toka kwake ni sifa ya urembo pamoja na kujichunga lakini nashangaa kwa nini mimi ananifanyia hivyo. Kuna watu wenye pesa wengi sana huwa wanamfukuzia na hajawahi kumkubalia mtu hata mmoja kati yao na kila kukicha idadi ya wanao ongezeka kwenye list ya wanaomtokea inaongezeka tu. Mda wote wa urafiki wetu sikuwahi kumuona na boy friend tofauti na mimi, na amekuwa akipenda sana kuwa nami na ndio kisa cha watu kusema nina mahusiano nae.
Ndugu zangu wapendwa hayo ndiyo yanayonisibu kwa wakati huu. Nimekamatika njia panda, watu wengi sana wanamtaka tena watu wazito kabisa na maarufu lakini hawajampata lakini kwangu mimi amekuja yeye mwenyewe! Sasa kila siku najiuliza sijui nimshughulikie? au sijui vipi? Naombeni ushauri wenu wana jamii forum wenzangu.
Aksanteni sana.