Bin Shaib
JF-Expert Member
- Aug 1, 2019
- 1,315
- 1,186
Wakuu habari za jf Bwana Yesu asifiwe, assaalam alykum wapendwa,, niwaombe tuzidi kuliombea taifa letu liwe na uchaguzi wa amani.
Bila kupoteza muda niingie kunako maada,, siku za nyuma nilileta kesi ya huyu binti humu aliyekuwa akinitishia tuachane na ni kama mara mbili amewahi nitishia tuachane, basi tunaachana baada ya siku anakuja kuniomba msamaha kwa alicho fanya.
Sasa tumeendelea na mapenzi yetu muda mrefu, kwa sasa yapata miaka 2 na ushee lakini hatujawahi kufanya mapenzi, kila nikimwabia anasema hadi nimuweke ndani yaami nimuoe,nimekaa nae kwa muda huo wote nimevumilia mashart yake,
Yeye kuhusu mizinga au vizawadi labda hadi nimpe mwenyewe kwa kupenda, kwakweli nimemchunguza ni kama binti ambaye ana mapenzi ya kweli kwa mabinti wote ambao nimekuwa nao na nilio wachunguza.
Na nimekuwa nikimwambia nahitaji nikakutamblishe kwa wazazi wangu yaani yupo radhi.
Kasheshe hii hapa.
Kuna binti hapa mtaani ambae ni kama rafiki yangu, timekuwa tukipiga nae story nyingi tu,lakini kwa huyu mpenzi wangu imekuwa kasheshe ananambia kuwa huyu rafiki ni mtu wangu na ninatembea nae kimapenzi,, nimejaribu kumuuaminisha lakini haelewi anazidi kunikazia tu kuwa nisikatae huyo ni mpenzi wangu.
Alianzisha dharau na maringo hadi nikahisi kashapata mtu mwingine maana unaweza kumwita lakini asiitikie na heshima kama mwanzo imeshuka sana, ananidharau.
Na ikafikia hatua nikamwambia we niweke wazi tu kama hunihitaji katika maisha yako,, anasema labda mimi nimuache ila siyo yeye.
Uzalendo ulinishinda wa kuvumilia zile dharau nikaamua kumtamukia,, "it's over "kila mtu ajue hamsini zake ,,alitoka kwa kasi nilipo mtamkia hivo nikawa nimeenda zangu.
Nimemuacha lakini naona ni binti mwenye msimamo na ambae naona harubuniwi kirahisi,, anafaa kuwa wife yupo tofauti sana na mabinti wengine ambao ukitaka kuweka ndani, labda hizo dharau alizileta alipo hisi nina mtu.
Na tulipo achana siku ya pili nilisikia maneno kwa jujuu kutoka kwa mke wa anko wangu kuwa binti anataka aombewe msamaha juu yangu ili turudiane..
Ushauri wakuu juu ya huyu binti vipi nifanye uamzi gani. Wakati huo nisha mtema?
Maana moyo unanituma kuwa huyu binti yupo vizuri japo kuna changamoto..
Bila kupoteza muda niingie kunako maada,, siku za nyuma nilileta kesi ya huyu binti humu aliyekuwa akinitishia tuachane na ni kama mara mbili amewahi nitishia tuachane, basi tunaachana baada ya siku anakuja kuniomba msamaha kwa alicho fanya.
Sasa tumeendelea na mapenzi yetu muda mrefu, kwa sasa yapata miaka 2 na ushee lakini hatujawahi kufanya mapenzi, kila nikimwabia anasema hadi nimuweke ndani yaami nimuoe,nimekaa nae kwa muda huo wote nimevumilia mashart yake,
Yeye kuhusu mizinga au vizawadi labda hadi nimpe mwenyewe kwa kupenda, kwakweli nimemchunguza ni kama binti ambaye ana mapenzi ya kweli kwa mabinti wote ambao nimekuwa nao na nilio wachunguza.
Na nimekuwa nikimwambia nahitaji nikakutamblishe kwa wazazi wangu yaani yupo radhi.
Kasheshe hii hapa.
Kuna binti hapa mtaani ambae ni kama rafiki yangu, timekuwa tukipiga nae story nyingi tu,lakini kwa huyu mpenzi wangu imekuwa kasheshe ananambia kuwa huyu rafiki ni mtu wangu na ninatembea nae kimapenzi,, nimejaribu kumuuaminisha lakini haelewi anazidi kunikazia tu kuwa nisikatae huyo ni mpenzi wangu.
Alianzisha dharau na maringo hadi nikahisi kashapata mtu mwingine maana unaweza kumwita lakini asiitikie na heshima kama mwanzo imeshuka sana, ananidharau.
Na ikafikia hatua nikamwambia we niweke wazi tu kama hunihitaji katika maisha yako,, anasema labda mimi nimuache ila siyo yeye.
Uzalendo ulinishinda wa kuvumilia zile dharau nikaamua kumtamukia,, "it's over "kila mtu ajue hamsini zake ,,alitoka kwa kasi nilipo mtamkia hivo nikawa nimeenda zangu.
Nimemuacha lakini naona ni binti mwenye msimamo na ambae naona harubuniwi kirahisi,, anafaa kuwa wife yupo tofauti sana na mabinti wengine ambao ukitaka kuweka ndani, labda hizo dharau alizileta alipo hisi nina mtu.
Na tulipo achana siku ya pili nilisikia maneno kwa jujuu kutoka kwa mke wa anko wangu kuwa binti anataka aombewe msamaha juu yangu ili turudiane..
Ushauri wakuu juu ya huyu binti vipi nifanye uamzi gani. Wakati huo nisha mtema?
Maana moyo unanituma kuwa huyu binti yupo vizuri japo kuna changamoto..