Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
Leo nimeshuhudia kitu ambacho kwa miaka mingi nilikuwa nasimuliwa tu. Mbunge wa jimbo la Tunduru kusini-Eng. Ramo Makani(CCM) ambaye alikuwa "mwenyekiti kamati ya Jairo" anafanya mkutano wake sasa. Cha ajabu mkutano umefurika akinamama, watoto na wazee, na vijana wachache sana. Malori ya kubeba mchanga yanaendelea kusomba akina mama kupeleka eneo la mkutano (maarufu kama baraza la IDI) muda huu hapa mjini Tunduru. Kubwa zaidi leo ni sherehe ya vijana wakodisha pikipiki(boda boda) kwani pikipiki karibu mia mbili zimenyweshwa mafuta na CHAMA CHA MAPINDUZI huku wakipewa pesa (10,000) kila dereva pikipiki.................MHESHIMIWA KAPIGWA SWALI "kwa nini tangu 31 octoba mwaka jana hajaja?". Mheshimiwa kajitetea kuwa haina haja ya kuja ila yeye atakaa Dar es salaam tu anahangaika mawizarani kutafuta "MISAADA". Sijui misaada gani.