G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
"Mheshimiwa Spika kwanza naomba kuunga hoja mkono kabla sijasahau. Mheshimiwa spika; naona upinzani wamefikia pabaya, wanaikashifu serikali sikivu ya CCM. Chama kimefanya mengi sana, maendeleo makubwa tumepata, shule za msingi, sekondari na vyuo viko vingi leo, barabara za lami, umeme nchi nzima mpaka vijijini maji aslimia 70 tayari na hizo 30 zitakamilishwa ifikapo mwaka 2015 kama ilani yetu tukufu ya CCM inavyoelekeza, lakini CHADEMA wanakebehi. Naipongeza sana serikali ya chama cha Mapinduzi kutuletea maendeleo lukuki.Na naomba wananchi wawapuuze CHADEMA kwa kitendo chao cha kuichonganisha serikali tukufu ya CCM na watanzania.
Mheshimiwa...Spika, nikiendelea mbele naomba nielezee kwa kifupi matatizo madogomadogo yaliyo katika jimbo langu. Kule hatuna shule ya sekondari katika kata sita, maji ni ndoto, tunategemea mvua. Shule zilizopo hazina ubora wala walimu wa kutosha. Rais alikuja sasa ni miaka sita akatuahidi umeme lakini mpaka leo hakuna lolote. Barabara ni mbovu hazipitiki. Nauliza ni lini serikali híi (ya CCM) ITATUSIKIA NA KUTULETEA MAENDELEO?
Mheshiiwa spika naunga tena mkono hoja mia kwa mia"
pwa pwa pwa pwa...
Mheshimiwa...Spika, nikiendelea mbele naomba nielezee kwa kifupi matatizo madogomadogo yaliyo katika jimbo langu. Kule hatuna shule ya sekondari katika kata sita, maji ni ndoto, tunategemea mvua. Shule zilizopo hazina ubora wala walimu wa kutosha. Rais alikuja sasa ni miaka sita akatuahidi umeme lakini mpaka leo hakuna lolote. Barabara ni mbovu hazipitiki. Nauliza ni lini serikali híi (ya CCM) ITATUSIKIA NA KUTULETEA MAENDELEO?
Mheshiiwa spika naunga tena mkono hoja mia kwa mia"
pwa pwa pwa pwa...