Nimevutiwa na house girl

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Sep 11, 2010
4,271
2,401
Yaani nimemtembelea rafiki yangu leo hom kwake kwa ishu za kimikakati. Sasa nikiwa pale nikamwona binti wa kazi. Aisee yuko mzuri. Sasa roho ya kumpenda (sijui kumtamani) ikaniingia. Mie bachela. Kila akipita namcheki kwa umakini na tathmini. Hana maringo, hajishaui. Uzalendo ukanishinda nikamjulisha mwenyeji kuwa nataka kumsoma akili huyu binti kupima ufahamu wake ili ikiwezekana awe mwandani. Jamaa akaniambia kama ni kwa wema utazungumza nae. Mtoto wa kisukuma, mrefu hivi. Maji ya kunde. Anavutia. Ni type ninayotaka. Nikawa najiuliza moyoni, je namhitaji? Elimu yake haitanipa mushkeli? Japo nimewazia kumuendeleza iwapo uzalendo utanishinda. Mi nina shahada. Napanga kumwambia jamaa amweleze ili nipate wasaa nae wa kutosha jmosi (si kingono) kumsoma na kuona upeo wake wa ufahamu na kama anaendelezeka maana siwezi kuwa nae kwa elimu yake. Nafsi nyingine inaniambia nipotezee tu na kumtafuta wa class yangu. Wenye maujuzi na mawazo kuhusu hili uwanja ni wenu
 
ukishakuwa na uhakika kama umempenda au umemtamani rudi tukushauri
senkyu fo nau
 
Mi nina shahada. Napanga kumwambia jamaa amweleze ili nipate wasaa nae wa kutosha jmosi (si kingono) kumsoma na kuona upeo wake wa ufahamu na kama anaendelezeka maana siwezi kuwa nae kwa elimu yake. Nafsi nyingine inaniambia nipotezee tu na kumtafuta wa class yangu. NANI KAKWAMBIA MAPENZI YANAENDANA NA CLASS?BABA YAKO NA MAM YAKO WAKO CLASS MOJA?HIYO ELIMU YAKO HAIJAKUSAIDIA KI2.NYAMBAF:mmph::mmph::mmph::mmph:
 
I think unataka ku m abuse, achana nae, ushamuona sio wa class yako utakuja kumnyanyasa at the end, tuachie sisi hao wa class yetu bana.:biggrin1:

( Mzee kama umempenda wewe ongea nae then ukiaona anaelimika , fanya mambo umuendeleze, ila..... usije kumnyanyasa kwa hali uliyomkuta nayo sasa, mpende kama mwanamke na umpe heshima yake!)
 
Mapenzi hayana CLASS kama kwenye ndege!! Si ajabu akawa bora zaidi kimaisha, Na akawa MSAADA mkubwa sana kwako! kuliko mwenye SHAHADA kama wewe! kumbuka, MAFAHALI WAWILI.................
 
Nashangaa natukanwa humu. Ni kweli kwa elimu yake tutapishana mitazamo. Ndio maana nikazungumzia ajenda ya kumuendeleza.
 
jamani mapenzi hayana usomi,hao wasomi mara nyingi hujifanya kujua sana,kama kweli umempenda wewe mwenyewe ukitaka kumuendeleza,utamuendeleza tu.lakini uwe serious nae,ma house girl wengine huwa wana akili za kusoma na za maisha,isipokuwa hali zao za maisha ndio zinawafanya wawe house girl,na ila kama unampenda usije ukasikiliza ya watu wa nje,maana ukuwaambia huyu ni house girl wa fulani,watakuona wa ajabu kumpenda house girl.Kwa ninavyoelewa,moyo ukipenda,huwa unapenda.Hauangalii sura,rangi,kabila na mengineyo.Cha muhimu,kabla hujaingia kichwa kichwa ni vizuri kumtambua zaidi yule unaempenda.maana unaweza ukampenda mtu,kumbe yeye hana mapenzi na wewe kabisaaaaaaaa,akaishia kukuchuna tu.Good luck
 
Katika maisha yako umekutana na wa aina hiyo wangapi?Kama ni wengi je uliwa treat vipi?
Kama huyo ndo wa kwanza nakushauri upate nafasi uongee naye ili ujiridhishe kama anaweza kuwa mwandani wako,then take time kumsoma na umpe nafasi akusome wewe pia.Baada ya muda kama kweli mmezaliwa muishi pamoja,mambo yanajiset automatikali,Ila mimi ninawasiwasi inawezekana hizo ni tamaa tu,take time utagundua.
 
jamani mapenzi hayana usomi,hao wasomi mara nyingi hujifanya kujua sana,kama kweli umempenda wewe mwenyewe ukitaka kumuendeleza,utamuendeleza tu.lakini uwe serious nae,ma house girl wengine huwa wana akili za kusoma na za maisha,isipokuwa hali zao za maisha ndio zinawafanya wawe house girl,na ila kama unampenda usije ukasikiliza ya watu wa nje,maana ukuwaambia huyu ni house girl wa fulani,watakuona wa ajabu kumpenda house girl.Kwa ninavyoelewa,moyo ukipenda,huwa unapenda.Hauangalii sura,rangi,kabila na mengineyo.Cha muhimu,kabla hujaingia kichwa kichwa ni vizuri kumtambua zaidi yule unaempenda.maana unaweza ukampenda mtu,kumbe yeye hana mapenzi na wewe kabisaaaaaaaa,akaishia kukuchuna tu.Good luck

nimekusoma ndugu.
 
Katika maisha yako umekutana na wa aina hiyo wangapi?Kama ni wengi je uliwa treat vipi?
Kama huyo ndo wa kwanza nakushauri upate nafasi uongee naye ili ujiridhishe kama anaweza kuwa mwandani wako,then take time kumsoma na umpe nafasi akusome wewe pia.Baada ya muda kama kweli mmezaliwa muishi pamoja,mambo yanajiset automatikali,Ila mimi ninawasiwasi inawezekana hizo ni tamaa tu,take time utagundua.

kiukweli nimekutana nao kadhaa kama yeye. Ndio maana nasema sijui kama ni mapenzi au vipi na ndio maana nataka muda nae.
 
Nashangaa natukanwa humu. Ni kweli kwa elimu yake tutapishana mitazamo. Ndio maana nikazungumzia ajenda ya kumuendeleza.

Kumuendeleza inawezekana. Siku nilipo-graduate pale mlimani kuna best yangu mmoja ali-graduate siku ileile kozi moja na mamake mzazi, sociology. Yule mama alituambia alipoolewa alikuwa na elimu ya darasa la saba. Huyu best yangu alipozaliwa, mamake alikuwa mfagizi pale hospitali ya Muhimbili. Sasa hivi maza anayo masters kapatia Marekani na ni lecturer and PhD candidate. Don't you ever underestimate what determination can bring.
 
Kumuendeleza inawezekana. Siku nilipo-graduate pale mlimani kuna best yangu mmoja ali-graduate siku ileile kozi moja na mamake mzazi, sociology. Yule mama alituambia alipoolewa alikuwa na elimu ya darasa la saba. Huyu best yangu alipozaliwa, mamake alikuwa mfagizi pale hospitali ya Muhimbili. Sasa hivi maza anayo masters kapatia Marekani na ni lecturer and PhD candidate. Don't you ever underestimate what determination can bring.

thats a fascinating story man. I will work on details
 
thats a fascinating story man. I will work on details

a true story, ilitokana sana na support ya mumewe maana huyo dingi ni profesa siku hizi, lakini obviously miaka hiyo alipooa inawezekana alikuwa na first degree tu, but akamsapoti mkewe hadi hapo.
 
Mapenzi hayana macho kama uko serious take time kumsoma usimweleze wazi wazi kuwa unataka kumuoa ataficha makucha yake. Data zingine za huyo msichana utazipata kupitia kwa huyo rafiki yako kwa kuwa sijui amekaa naye muda gani lakini hata kama atakuwa ameshakaa muda mfupi rafiki yako atakuwa ameshaanza kumjua tabia zake. Ukisharidhika na kumjua vizuri ndipo unaweza kueleza ajenda yako na katika kipindi hicho mtakuwa mmeshafahamiana vizuri. Kitu kingine ujue unaingia kuuza sera sasa sera zako zinaweza kukubalika au kukataliwa yule naye ni binadamu ana utashi wake na maamuzi yake hivyo anaweza kukubali au kukukataa. Cha muhimu kama kweli uko serious uingie kwa staha mchunguze na kisha fikisha ujumbe wako. Kama akikuona uko serious na unamstahi uwezekano wa kufanikiwa kumuoa upo. Lakini ukiingia na mapomp yako ya kisomi na kumuona ah huyu ni housegirl umeula wa chuya atakushtukia na huenda asikukubalie. Habari ndiyo hiyo.
 
Mtoto wa kisukuma, mrefu hivi. Maji ya kunde. Anavutia. Ni type ninayotaka. Nikawa najiuliza moyoni, je namhitaji? Elimu yake haitanipa mushkeli? Japo nimewazia kumuendeleza iwapo uzalendo utanishinda. Mi nina shahada.

Sisi hatuwezi kukushauri la maana kwa sababu taarifa zako hatuna ila umetupa za huyo binti tu........Acha uchoyo tuelezee zaidi.. una miaka mingapi na huyo binti ana umri gani. Wewe umekulia wapi...............na dini zenu zinasemaje.............hayo ni maswali mepesi lakini huwezi kujua........Wazazi wa pande mbili watayaona haya maswali nyeti sana.............Halafu kosa kubwa unafikiri ni wewe tu mwenye uamuzi unajuaje yeye anafikiria nini?

Au unafikiri kwa kuwa ni "Housegirl" basi atabebwa na yeyote mwenye ujasiri wa kusema "I love you?'

Be serious than that my friend and show some maturity.........Best wishes, all the same.................
 
Mapenzi hayana macho kama uko serious take time kumsoma usimweleze wazi wazi kuwa unataka kumuoa ataficha makucha yake. Data zingine za huyo msichana utazipata kupitia kwa huyo rafiki yako kwa kuwa sijui amekaa naye muda gani lakini hata kama atakuwa ameshakaa muda mfupi rafiki yako atakuwa ameshaanza kumjua tabia zake. Ukisharidhika na kumjua vizuri ndipo unaweza kueleza ajenda yako na katika kipindi hicho mtakuwa mmeshafahamiana vizuri. Kitu kingine ujue unaingia kuuza sera sasa sera zako zinaweza kukubalika au kukataliwa yule naye ni binadamu ana utashi wake na maamuzi yake hivyo anaweza kukubali au kukukataa. Cha muhimu kama kweli uko serious uingie kwa staha mchunguze na kisha fikisha ujumbe wako. Kama akikuona uko serious na unamstahi uwezekano wa kufanikiwa kumuoa upo. Lakini ukiingia na mapomp yako ya kisomi na kumuona ah huyu ni housegirl umeula wa chuya atakushtukia na huenda asikukubalie. Habari ndiyo hiyo.

na chaji inakata. Jamaa kaishi nae miaka 3 so atakuwa anamjua vizuri. Pia ingekuwa ni kudunga tu mbona msingeniona humu?
 
Back
Top Bottom