Nchi Kavu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 4,271
- 2,401
Yaani nimemtembelea rafiki yangu leo hom kwake kwa ishu za kimikakati. Sasa nikiwa pale nikamwona binti wa kazi. Aisee yuko mzuri. Sasa roho ya kumpenda (sijui kumtamani) ikaniingia. Mie bachela. Kila akipita namcheki kwa umakini na tathmini. Hana maringo, hajishaui. Uzalendo ukanishinda nikamjulisha mwenyeji kuwa nataka kumsoma akili huyu binti kupima ufahamu wake ili ikiwezekana awe mwandani. Jamaa akaniambia kama ni kwa wema utazungumza nae. Mtoto wa kisukuma, mrefu hivi. Maji ya kunde. Anavutia. Ni type ninayotaka. Nikawa najiuliza moyoni, je namhitaji? Elimu yake haitanipa mushkeli? Japo nimewazia kumuendeleza iwapo uzalendo utanishinda. Mi nina shahada. Napanga kumwambia jamaa amweleze ili nipate wasaa nae wa kutosha jmosi (si kingono) kumsoma na kuona upeo wake wa ufahamu na kama anaendelezeka maana siwezi kuwa nae kwa elimu yake. Nafsi nyingine inaniambia nipotezee tu na kumtafuta wa class yangu. Wenye maujuzi na mawazo kuhusu hili uwanja ni wenu