FORTUNE JR
Member
- Mar 20, 2021
- 69
- 336
Wakuu habari zenu.
Naomba ushauri wenu ili nipate kuruka kiunzi hiki mbele yangu na Maisha ya endelee kama kawaida bila kumdhuru au kumuumiza yoyote na mimi pia kua salama
Wiki iliyopita nilipata taarifa Ex wang niliedumu nae takribani miaka 3 kwenye mahusiano yupo Taabani hospitali baada ya kujifungua maana alipoteza damu nyingi sana na kujifungua kwake kulikua Complicated kidogo hivo nikachukua mda wangu kwenda hospitali kumwona
Ni hivi Wakuu, kitu ninachoamini ni kwamba katika safari ya maisha ya mahusiano wengi wetu tuna yule mtu ambae ulikua nae kwenye mahusiano na mmepitia nae mengi yanayojenga kumbukumbu ambazo zinakua ni ngumu kufutika kiwepesi na huenda bado unatamani kuendelea nae kwenye safari ya mahusiano ila ndo vile tena ya dunia ni Mengi.
Kwa upande wangu mm ni huyu binti(Ex) ambaye namzungumzia hapa. Nilianza nae mahusiano Chuo masomoni, Alichukua nafasi kubwa sana kwenye maisha yangu kama Mshauri, Msaidizi, Mfariji na kifupi Chemistry yangu na yake zili match kwasababu alimudu madhaifu yangu na mm nlimudu yake na nikienda mbali zaidi nilimwona huyu binti kama Mama yangu wa pili kwasababu alizijua Mood zangu zote kama kuumwa, Huzuni hata kama nilizificha vipi kitu ambacho hata Dada zangu hawajawai kueleewa kiivo moods zangu. Hivyo naweza sema Huyu binti na Mamangu walinielewa sana(My strength and Weakness). Kifupi aliniheshimu na kunithamini sana na hakuona taabu kumweka bayana Mwanaume mwingine aliyemtaka kimapenzi kwamba anaye mimi inatosha.
Nimedumu na huyu binti takribani miaka mitatu na kifupi Sikupenda mwanamke mwingine zaidi ya kutamani tu tamaa za kawaida ambazo kila mwanaume kaumbiwa ila moyoni alijaa huyu binti.
Kilichonitenga na huyu binti baada ya miaka 3 ya mahusiano ni kwamba Alikua ana shoga yake mmoja Ambae nilikuwa na mazoea nae na kifupi tulizoeana kama mtu na shemeji yake na tuliishi kama familia kwakuwa alikuwa rafiki wa Mpenzi wangu, nashindwa kuielezea vizuri hii sehemu kwakuwa huwa inanifanya nijute kila nikikumbuka kifupi niliteleza na nilishindwa kukabiliana na Tamaa, nililala na shemeji yangu siku moja baada ya kupata nae Faragha.
Na ni kwamba mtu wangu aligundua na kuubaini ukweli wote kitu ambacho kilimfanya alie sana na kupatwa na hasira kwa namna nyingine naweza kusema hakuweza kuamini kama siku moja ningeweza kumfanyia kitu kama hicho na mbaya zaidi kwa rafiki yake mkubwa. Na katika hali hio hio ya hasira alimkubalia mwanaume mwingine ambaye alikuwa akimtaka kitambo tu na hakuwai kukata tamaa licha yakuwa mwanzo alikuwa ananiambia jamaa anamsumbua sana na hakati tamaa, safari hii jamaa alifanikiwa kukubaliwa baada ya mimi ya kuyakanyaga
Mwamba alienda nyumbani kwa binti akaonekana kwa wazazi wake na akatoa mahali na taratibu zote zikafwata hatimae mtoto akawekwa ndani na kufumba na kufumbua mwamba alivyokosa adabu na stara akamtundika na Mimba daaaa! 😢 Wakuu nilikosa raha,nilikua Mnyonge, usingizi ulinipaa na zaidi ya yote nilikosa Mwelekeo kwasababu katika kila nilichokifanya nilikua naona dhahiri kuna ki2 kinamiss, nikijaribu Mahusiano mengine ndo kwanza Moto unazidi kuwaka nivizinga kwa kwenda mbele, kuchitiwa kwa sana.
Nilianza kukubaliana na ukweli kwamba tayari nishapoteza moja ya nguzo yangu mhimu. Nilifuta namba za binti nikajiweka busy na maisha Mengine. Baada ya kama miezi 2 kupita bila mawasiliano na binti, siku moja nimekaa namba ngeni inanipigia kucheki kwa makini niya huyu Ex sabu niliikariri ikabidi kumsikiliza bidada ananung'unika Maisha yamemkua Mgumu, hana raha na maisha kiujumla na kachoka na hiyo ndoa na ndio kwanza ana miezi 2 tu anautafuta wa 3, lakini hana raha na huyo bwana na anaona wanapishana nae kwenye vingi yani hana Chemistry nae kabsa mbaya zaidi vijisenti vyake vinaishia kwenye bia kwaio imekua ni ngumu hata kwa bidada ku survive na ni mjamzito bidada kaenda mbali zaidi na kunilaumu kwamba mm ndo nimeua hatmi yake apa duniani haoni radha ya maisha tena. Binafsi iliniumiza lakini pia nilitoa ya moyoni kwamba nae alikurupuka sana hata kama sawa ni hasira zilimwendesha ila kujiingiza kwenye ndoa na m2 ambae hakupata mda wa kumfahamu vizuri.
Kuanzia siku hio niliendelea kuwasiliana na binti ila mara zote yeye ndo alinitafuta akiniomba ushauri na sometimes alidai hana hata hela ya kula bwana busy na bia kwaio nlikua na desturi ya kumsaidi kwakua mm nilikua na kazi hatakama sio ya moja kwa moja ila iliniingizia kipato na niliweza walau kuendesha maisha yangu kwaio nilikua namsaidia pia.
Kiukweli nilijua nafanya makosa kwanza kufanya mawisiliano nae na pia kumpa pesa ilihali ana mme wake ila kiukweli nilifanya toka moyoni ukizingatia ni binti ambae kiukweli ni ngumu kwangu kuona anapata shida na mimi naona kifupi hata iwe usiku wa manane ni lazima nitamsaidia tu kama nina uwezo wa kufanya ivo, ni yale maisha tuliyoyaishi kabla na hadi sasa huwa naona kabisa kuna milango ya maisha ingekua ngumu kufunguka kwangu pasina huyu binti ni kama (destiny helper) vile na ndomaana huwa nashindwa kukaa kimya pindi atakapo msaada. Ubaya ni kwamba utata unakuja ni kwamba ndoa ya binti ikaanza kuingia matatani kwasababu sometimes akigombana na Mumewe ananitaja kwa Bwana ake et mm nlikuwa nam handle ila sio yy mumewe. Wanaume wenzangu mnaweza elewa maumivu ya hii kitu.
Ushauri wenu nauhitaji hapa wakuu. Ni kwamba wiki iliyopita bidada mda wake wakujifungua ulifika ila haukua salama kidogo alimwaga damu nyingi sana hivo akazidiwa nilivyozipata hizi habari ikabidi niende kumwona kama rafiki. Kufika pale nikapata taarifa bidada anahitaji donation ya damu ili aludi kwenye utimamu wake, binti Group lake ni "AB" na mimi langu ni "O " wataalamu mtakua mmenipata hapo kwamba niko kwenye nafasi ya kufanya donation kwa binti na kikubwa kilicho ni push kufanya ivo ni kwamba binafsi huwaga na shida ya ugonjwa wa polycythemia au hypervolemia, huu ni ugonjwa wa mtu kuwa na damu nyingi sana mwili hali inayopelekea kuumwa na kichwa mara kwa mara na kupatwa na kizunguzungu hivyo binafsi huwa na utaratibu wa kwenda kufanya donation baada ya mda fulani kwaajili ya afya yangu pia binafsi. Ivo kwakua sikua nimefanya ilo zoezi kwa miezi kadhaa nikaona sio mbaya kwafaida yangu na kwa binti pia.
Nashukuru Mungu zoezi likaenda vizuri kwangu na kwa binti hadi aka recover. Utata unakuja baada ya binti ku recover mahaba yamezidi kwangu hali yakushindwa kujizuia hata kwa Mumewe na hivi ninavyoandika uzi huu wametengana Jamaa kamaindi na issue ya mm kumchangia damu mkewe ndo imemchefua zaidi na jamaa kaenda mbali zaidi kwa kunitisha kama kuna surprise yangu ambayo sitakaa niisahau.
Bidada ni kama vile anataka kunilazimishia mm ndo nimwoe vle na mm inanipa ukakasi io kwakua tayari ana mtoto na jamaa, kwaio najua italeta shida mbeleni ila jamaa anabifu na mimi ambalo so la kawaida na jamaa navoelewa anampenda sana binti ila binti ndo vile tena. Ushauri wenu wakuu naluka vipi iki kiunzi bila kumuumiza yoyote na maisha yaendele. Asanteni kwa time yenu.
Naomba ushauri wenu ili nipate kuruka kiunzi hiki mbele yangu na Maisha ya endelee kama kawaida bila kumdhuru au kumuumiza yoyote na mimi pia kua salama
Wiki iliyopita nilipata taarifa Ex wang niliedumu nae takribani miaka 3 kwenye mahusiano yupo Taabani hospitali baada ya kujifungua maana alipoteza damu nyingi sana na kujifungua kwake kulikua Complicated kidogo hivo nikachukua mda wangu kwenda hospitali kumwona
Ni hivi Wakuu, kitu ninachoamini ni kwamba katika safari ya maisha ya mahusiano wengi wetu tuna yule mtu ambae ulikua nae kwenye mahusiano na mmepitia nae mengi yanayojenga kumbukumbu ambazo zinakua ni ngumu kufutika kiwepesi na huenda bado unatamani kuendelea nae kwenye safari ya mahusiano ila ndo vile tena ya dunia ni Mengi.
Kwa upande wangu mm ni huyu binti(Ex) ambaye namzungumzia hapa. Nilianza nae mahusiano Chuo masomoni, Alichukua nafasi kubwa sana kwenye maisha yangu kama Mshauri, Msaidizi, Mfariji na kifupi Chemistry yangu na yake zili match kwasababu alimudu madhaifu yangu na mm nlimudu yake na nikienda mbali zaidi nilimwona huyu binti kama Mama yangu wa pili kwasababu alizijua Mood zangu zote kama kuumwa, Huzuni hata kama nilizificha vipi kitu ambacho hata Dada zangu hawajawai kueleewa kiivo moods zangu. Hivyo naweza sema Huyu binti na Mamangu walinielewa sana(My strength and Weakness). Kifupi aliniheshimu na kunithamini sana na hakuona taabu kumweka bayana Mwanaume mwingine aliyemtaka kimapenzi kwamba anaye mimi inatosha.
Nimedumu na huyu binti takribani miaka mitatu na kifupi Sikupenda mwanamke mwingine zaidi ya kutamani tu tamaa za kawaida ambazo kila mwanaume kaumbiwa ila moyoni alijaa huyu binti.
Kilichonitenga na huyu binti baada ya miaka 3 ya mahusiano ni kwamba Alikua ana shoga yake mmoja Ambae nilikuwa na mazoea nae na kifupi tulizoeana kama mtu na shemeji yake na tuliishi kama familia kwakuwa alikuwa rafiki wa Mpenzi wangu, nashindwa kuielezea vizuri hii sehemu kwakuwa huwa inanifanya nijute kila nikikumbuka kifupi niliteleza na nilishindwa kukabiliana na Tamaa, nililala na shemeji yangu siku moja baada ya kupata nae Faragha.
Na ni kwamba mtu wangu aligundua na kuubaini ukweli wote kitu ambacho kilimfanya alie sana na kupatwa na hasira kwa namna nyingine naweza kusema hakuweza kuamini kama siku moja ningeweza kumfanyia kitu kama hicho na mbaya zaidi kwa rafiki yake mkubwa. Na katika hali hio hio ya hasira alimkubalia mwanaume mwingine ambaye alikuwa akimtaka kitambo tu na hakuwai kukata tamaa licha yakuwa mwanzo alikuwa ananiambia jamaa anamsumbua sana na hakati tamaa, safari hii jamaa alifanikiwa kukubaliwa baada ya mimi ya kuyakanyaga
Mwamba alienda nyumbani kwa binti akaonekana kwa wazazi wake na akatoa mahali na taratibu zote zikafwata hatimae mtoto akawekwa ndani na kufumba na kufumbua mwamba alivyokosa adabu na stara akamtundika na Mimba daaaa! 😢 Wakuu nilikosa raha,nilikua Mnyonge, usingizi ulinipaa na zaidi ya yote nilikosa Mwelekeo kwasababu katika kila nilichokifanya nilikua naona dhahiri kuna ki2 kinamiss, nikijaribu Mahusiano mengine ndo kwanza Moto unazidi kuwaka nivizinga kwa kwenda mbele, kuchitiwa kwa sana.
Nilianza kukubaliana na ukweli kwamba tayari nishapoteza moja ya nguzo yangu mhimu. Nilifuta namba za binti nikajiweka busy na maisha Mengine. Baada ya kama miezi 2 kupita bila mawasiliano na binti, siku moja nimekaa namba ngeni inanipigia kucheki kwa makini niya huyu Ex sabu niliikariri ikabidi kumsikiliza bidada ananung'unika Maisha yamemkua Mgumu, hana raha na maisha kiujumla na kachoka na hiyo ndoa na ndio kwanza ana miezi 2 tu anautafuta wa 3, lakini hana raha na huyo bwana na anaona wanapishana nae kwenye vingi yani hana Chemistry nae kabsa mbaya zaidi vijisenti vyake vinaishia kwenye bia kwaio imekua ni ngumu hata kwa bidada ku survive na ni mjamzito bidada kaenda mbali zaidi na kunilaumu kwamba mm ndo nimeua hatmi yake apa duniani haoni radha ya maisha tena. Binafsi iliniumiza lakini pia nilitoa ya moyoni kwamba nae alikurupuka sana hata kama sawa ni hasira zilimwendesha ila kujiingiza kwenye ndoa na m2 ambae hakupata mda wa kumfahamu vizuri.
Kuanzia siku hio niliendelea kuwasiliana na binti ila mara zote yeye ndo alinitafuta akiniomba ushauri na sometimes alidai hana hata hela ya kula bwana busy na bia kwaio nlikua na desturi ya kumsaidi kwakua mm nilikua na kazi hatakama sio ya moja kwa moja ila iliniingizia kipato na niliweza walau kuendesha maisha yangu kwaio nilikua namsaidia pia.
Kiukweli nilijua nafanya makosa kwanza kufanya mawisiliano nae na pia kumpa pesa ilihali ana mme wake ila kiukweli nilifanya toka moyoni ukizingatia ni binti ambae kiukweli ni ngumu kwangu kuona anapata shida na mimi naona kifupi hata iwe usiku wa manane ni lazima nitamsaidia tu kama nina uwezo wa kufanya ivo, ni yale maisha tuliyoyaishi kabla na hadi sasa huwa naona kabisa kuna milango ya maisha ingekua ngumu kufunguka kwangu pasina huyu binti ni kama (destiny helper) vile na ndomaana huwa nashindwa kukaa kimya pindi atakapo msaada. Ubaya ni kwamba utata unakuja ni kwamba ndoa ya binti ikaanza kuingia matatani kwasababu sometimes akigombana na Mumewe ananitaja kwa Bwana ake et mm nlikuwa nam handle ila sio yy mumewe. Wanaume wenzangu mnaweza elewa maumivu ya hii kitu.
Ushauri wenu nauhitaji hapa wakuu. Ni kwamba wiki iliyopita bidada mda wake wakujifungua ulifika ila haukua salama kidogo alimwaga damu nyingi sana hivo akazidiwa nilivyozipata hizi habari ikabidi niende kumwona kama rafiki. Kufika pale nikapata taarifa bidada anahitaji donation ya damu ili aludi kwenye utimamu wake, binti Group lake ni "AB" na mimi langu ni "O " wataalamu mtakua mmenipata hapo kwamba niko kwenye nafasi ya kufanya donation kwa binti na kikubwa kilicho ni push kufanya ivo ni kwamba binafsi huwaga na shida ya ugonjwa wa polycythemia au hypervolemia, huu ni ugonjwa wa mtu kuwa na damu nyingi sana mwili hali inayopelekea kuumwa na kichwa mara kwa mara na kupatwa na kizunguzungu hivyo binafsi huwa na utaratibu wa kwenda kufanya donation baada ya mda fulani kwaajili ya afya yangu pia binafsi. Ivo kwakua sikua nimefanya ilo zoezi kwa miezi kadhaa nikaona sio mbaya kwafaida yangu na kwa binti pia.
Nashukuru Mungu zoezi likaenda vizuri kwangu na kwa binti hadi aka recover. Utata unakuja baada ya binti ku recover mahaba yamezidi kwangu hali yakushindwa kujizuia hata kwa Mumewe na hivi ninavyoandika uzi huu wametengana Jamaa kamaindi na issue ya mm kumchangia damu mkewe ndo imemchefua zaidi na jamaa kaenda mbali zaidi kwa kunitisha kama kuna surprise yangu ambayo sitakaa niisahau.
Bidada ni kama vile anataka kunilazimishia mm ndo nimwoe vle na mm inanipa ukakasi io kwakua tayari ana mtoto na jamaa, kwaio najua italeta shida mbeleni ila jamaa anabifu na mimi ambalo so la kawaida na jamaa navoelewa anampenda sana binti ila binti ndo vile tena. Ushauri wenu wakuu naluka vipi iki kiunzi bila kumuumiza yoyote na maisha yaendele. Asanteni kwa time yenu.