Nimepiga marufuku safari zote za mke wangu msimu huu wa sikukuu

DeepPond

JF-Expert Member
Nov 18, 2017
40,490
99,252
Wakuu,

Usiku wa Juzi nilivorud nyumbani,

MKE wangu alinipokea kwa uchangamfu na bashasha kubwa Sana,nami baada ya Lile tukio la sintofahamu ya laini mpya hivi karibuni, nilishajiapiza sitopanic Wala kuonesha kuchukia au kumshuku ananicheat.

Pia Nishaahidi nitakua kawaida ili kuweza kupata nafas ya kumchunguza. Hivyo nami nikamchangamkia vizuri Kama yeye vile alivonichangamkia.

Kisha baada ya kula,nmeoga nmepanda zangu kitandani kulala, ghafla akaanza kuniuliza Kama leo nmeongea na mama yake mkubwa wa mkoani, nikamjibu hapana.

Akanambia "ma mkubwa yake anakumbushia lile suala lake la kwenda kula xmass mkoani kwake na watoto, tar 16 uloniahidi ntaenda Ndo kesho iyo mme wangu"

Nikamjibu, "nishasahau bhana, kumbe tar 16 ndo kesho, Basi sawa haina shida, jiandae, kesho jion ntakaporud utanikumbusha, sjabeba nauli yako leo, utaenda kesho kutwa asbh Basi MKE wangu" akasema "sawa mme wangu,asante" kanichum shavuni, tumelala vzur mpk kumekucha.

Ila punde TU nmeegesha kichwa, usingz unakuja afu kama unakata, Nikaanza kuiwazia sana hiyo safar ya Mke wangu uko mkoani kwa ma ake mkubwa, akili yangu inagoma kabisa kuikubali akilini mwangu.

Nikakumbuka Ni kweli ilishapangwa MDA mrefu Sana, ila nishaisahau (Zaid ya miez 2 ilopita,na siku inapangwa sikutilia maanani sana, ilkua ni Kwny story tu na ma mkubw, nilikubali kwa kuropoka TU, Sikua serious kivile "sawa ma mkubwa, tufanye basi tar 16 decemba uhakika atakuletea wajukuu wako uko,ule nao xmass" kisha nkaendeleana shughuli zangu.

Nkaendelea kuwaza,
"Sawa Ni kweli, kesho Ni tar 16 Kama nilivomuahidi mke wangu atasafiri, Ila inahusiana vp na hii laini mpya iloniletea sintofahamu leo mchana?"

Kitandani hapalaliki,
Kichwa kikazid kupata Moto,
"Usikute ana mtu wake uko mkoani keshamseti, alifufua laini yake kusudi wawasiliane kwamba anakuja uko, njemba ijiandae kumshughulikia ?"
Nikaona ebu nilale kwanza ntulize kichwa,

haya nnayowaza Ni mawazo ya wazimu kabisa,ntachanganyikiwa Sasa, kukishakucha ndo ntajua Nini sahii Cha kuamua,Hapa nakurupuka tu. Kiukweli nikajilazimisha sana mpk nikalala usngz.

Sasa Kumekucha Nmeamka alfajiri kuoga nijiandae kwenda dukani, nastuka MKE wangu hayupo kitandani na tayr keshapakia nguo zake Kwny mabegi na nayaona yamesimamishwa pembeni.

Ikanibd kumuita kwa saut, naskia anaitikia uko vyumba vya watoto. Ikanibd kumfata uko, nmefka namkuta anawavalisha watoto nguo, wengine wanajipaka mafuta.

Nkamuuliza vipi, unawavalisha watoto, unawapeleka wapi na alfajir yote Hii. Akasema "ile safar ya ma mkubw, nataka nifike mapema leo mme wangu?" Nkamuulza nauli umepata wapi, Akasema anayo akiba ya pesa za maziwa na maji alizitunza, nisipate shida kumpa nauli".

Nikamwambia "usikaidi maagizo yangu, nishasema utaenda kesho asbh,nmemaliza, usinijaribu" Kisha nikaondoka zangu kujiandaa ili kwenda zangu dukani.

Saa 4 asbh Niko dukan, namwona wife Yuko na watoto pamoja na mabegi, anasema "nmekuletea wanao wakuage, uwape Ela ya chocolate njiani, afu kingine mme wangu, mwenzio nmepata gar ya saa 7 mchana, Ni nzuri na luxury sana, haina, usumbufu wwt au unaionaje Hii kampuni?" Uku ananionyesha ticket ya bus.

Nikamkata jicho Kali sana, afu nikamwambia "usinijaribu, nishasema safar Ni kesho, kinachokufanya hasa unabishana na maamuz yangu Ni Nini?" Akasema , "Sasa mme wangu, ticket nishakata tangu jana, Ina maana Ela yangu ya nauli ndo ipotee?"

Ikanibd kurudi kuitizama Tena ile ticket alonipa, kweli imekatwa tar 15, Siku ya jana ambayo ndo imetokea ile sintofahamu ya laini mpya. Nikamuuliza wife "Ina maana baada ya kukata Hii ticket ndo ukakosea pia kunipigia kwny ile laini yako mpya sio?"

Akasema "hapana, hivi mme wangu mbona unapenda sana kuniwazia mabaya sana mimi? Mi sijawai na sitowaza kukusaliti hata Mara Moja mme wangu, ebu acha mawazo Ayo. Mi siwazii Ayo unayoyafikiria bhana"

Nikamjibu, "nishasema safar yako ni kesho asbh, usnipime wala kunijaribu akili yangu" Akaanza kunibembeleza Sana asafiri Siku iyo,nikakataa katakata haendi kokote.

Akasema, "sawa mi narud nyumbani, ila jua ujawatendea Haki wanao,pia umemkosea Sana ma mkubw, una ahadi za uongo Sana babaG" sikumjibu chochote,nkaendelea na mambo yangu.

Sasa sikujua alimwambia nini mama ake mkubwa, baadae nashangaa ma mkubw ananipigia, nmepokea ananihoji kwann nmemzuia MamaG asiondoke na ticket tayar keshakata,

nkamwambia ma mkubw "mwanao aliiandaa safar yake ya leo Bila kunishirikisha, hiyo ticket yake alokata Ni hasara yake,hainihusu mimi" nikaona Kama vile ma mkubwa kachukia na analalama sana.

Nikamsisitiza,
"Ma mkubw, ujue mimi ndo baba wa familia hii, popote anapokwenda napaswa kua na taarifa, akilazimisha kwenda popote na watoto wangu bila ridhaa yangu, ajue sitowatambua Tena hao anaowaita watoto wangu. Pia Akija mwenyew bila ridhaa yangu,atambue sitomtambua Tena Kama mke wangu. Na atakaempokea sitomuelewa kabisa. Naomba uheshimu maamuzi yangu ma mkubwa"

ma mkubw akasema "nmekuelewa baba angu, sawa ukijiskia utawaleta mwnyw basi Kama utak mkeo aje, ila mkwe wangu Sikua ana Nia mbaya kuwaita kula nao sikukuu, usiniwazie vibaya, labda ntawaroga wanao" . Nikamjibu "haina shida ma mkubw" Kisha nkakata simu na kuendelea na shughuli zangu.

Jion nmerud nyumban, nmeingia kuoga, nmetoka najifuta maji, Wife anaingia na kunishutumu sio vizur kumtuhumu ma mkubwa wake kwamba Ni mchawi,atawaroga wanao.

Nkamwambia "lazima awaze ivo maana umemwambia nmekuzuia ndio, ila wewe umemficha sababu halisi ya kukuzuia, nami sijamwambia sababu ya msingi kukuzuia Wewe usiende kwake. Kwaiyo Wala hata sijali ataniwazia nini, Hilo Ni jukumu lako wewe bintiye kumwelewesha mama ako"

Akasema " Basi sawa ntamwelewesha mimi mwnyw kesho nikifika uko" nikamjibu "sawa, niletee chakula Nile nilale" kweli baada ya chakula nmelala. Ila kitandani ila bado Moyo wangu Ni mzito Sana kuruhusu hii safar yake kwa mama mkubwa wake kesho yake.

Alfajr ya leo kumekucha naamshwa na mke wangu, Anaomba nimpatie nauli, MDA wa Safari yake ndo huu. Nikamjibu "Nmeshaghaili, safar yako haipo Tena"

Akauliza tatizo Nini, mbona Jana tushakubaliana alfajir leo naondoka?. Nikamjibu, "Nmeshaghaili sasa, hakuna Safari yoyote ile, na sitaki unihoji maswali yoyote yale" akasema "sawa,ila unachofanya sio halali mme wangu" .Sikumjibu, nikaamka nikaoga, nikavaa na Kwenda zangu kazini

Nmefika kazini salama, nmejaribu kufanya Kazi ila haziend vizur. Kila nikijaribu kuliwazia tukio la Juzi la laini mpya, Kisha Hii presha ya wife kulazimisha hii Safari, kiukweli Moyo wangu umekua mzito Sana kumruhusu mke wangu asafiri.

Pengine sijajua kama nakosea au vipi,
Ila nmedhamiria kabisa MKE wangu hatosafiri kwenda popote pale msimu huu wote wa sikukuu.

Nawasilisha wakuu
 
Kitandani hapalaliki,
Kichwa kikazid kupata Moto,
"Usikute ana mtu wake uko mkoani keshamseti, alifufua laini yake kusudi wawasiliane kwamba anakuja uko, njemba ijiandae kumshughulikia ?"
Nikaona ebu nilale kwanza ntulize kichwa, haya Ni mawazo ya wazimu kabisa, kukishakucha ntajua Nini sahii Cha kuamua. Kiukweli nikajilazimisha sana mpk nikalala.

Sasa Kumekucha Nmeamka alfajiri kuoga nijiandae kwenda dukani, nastuka MKE wangu hayupo kitandani na tayr keshapakia nguo zake Kwny mabegi yamesimamishwa pembeni, ikanibd kumuita kwa saut, naskia anaitikia uko vyumba vya watoto. Ikanibd kumfata, nmefka kwake namkuta anawavalisha watoto nguo.

Nkamuuliza vipi, unawavalisha watoto, unawapeleka wapi na alfajir yote Hii. Akasema "ile safar ya ma mkubw, nataka nifike mapema leo mme wangu?" Nkamuulza nauli umepata wapi, Akasema anayo akiba ya pesa za maziwa na maji alizitunza, nisipate shida kumpa nauli".

Nikamwambia "usikaidi maagizo yangu, nishasema utaenda kesho asbh,nmemaliza, usinijaribu" Kisha nikaondoka zangu kujiandaa ili kwenda zangu dukani.
Ngoja nikuulize swali kidogo mkuu.
Mna watoto wa ngapi,mkubwa ana umri gani na mdogo ana umri gani?
 
DeepPond Kosa lako unapanic sana sijaona sababu yoyote yakumkumbushia lile tuko, we muache asafiri then utakuwa unafanya uchunguzi wako wa chini chini na pia ikiwezekana unatenga siku unawastukiza bila Taarifa hapa utakuwa umefanya la maana ili ujue uhakika kwa unachowaza juu ya mke wako inaweza ikawa kweli anakuchiti au sio uchunguzi wako ndio utakupa majibu sahihi nazani hiyo safari kwa namna moja au nyingine inaweza kukupa mwanga.
 
DeepPond Kosa lako unapanic sana sijaona sababu yoyote yakumkumbushia lile tuko, we muache asafiri then utakuwa unafanya uchunguzi wako wa chini chini na pia ikiwezekana unatenga siku unawastukiza bila Taarifa hapa utakuwa umefanya la maana ili ujue uhakika kwa unachowaza juu ya mke wako inaweza ikawa kweli anakuchiti au sio uchunguzi wako ndio utakupa majibu sahihi nazani hiyo safari kwa namna moja au nyingine inaweza kukupa mwanga.
Sasa a ruhusu aende ili abaki na mawazo?
Akifanya uchunguzi Baada akagundua tendo lishatendeka unadhani itakuwaje.
Jamaa kaamua kuzuia mvua kwa Jani la mgomba
 
Sasa a ruhusu aende ili abaki na mawazo?
Akifanya uchunguzi Baada akagundua tendo lishatendeka unadhani itakuwaje.
Jamaa kaamua kuzuia mvua kwa Jani la mgomba
Kuna watu wanachukulia simple vitu Kama hivi, aisee inaumaje unamruhusu mkeo na akili yako tayar ishakwambia uko anakoenda ataenda kuliwa?

Ni Mara akaliwe nisijue, sio nimruhusu kabisa akaliwe
 
Unakosea sana kijana hapo mwanamke una muua Saikorojia yake yaani uyo mkeo anaenda kupunguza intimacy level juu yako

hata penzi atakupa kama baba au gaidi mbakaji na mean time huwez mzuia mwanamke ku date na mchepuko kwasab mchepuko by hu mda ndio huwa wana enjoy sana kwasb ndio comfortzone yake ilipo

wew mwanamke ina bidi una mcomand lakn mpe space yani una kosea Alpha male hawi hivo uki kaa vibaya unaweza lea watoto sio wako

mwanamke unapo mkera nirahis sana kuku cheat huyo kijana wa ng’ombe anaweza mpa nae au majiran wew si uko kazin kijana?

mwanamke ili akuheshimu lazma agundue kua unajiamin na yeye unamuamin hapo mnaenda sana

acha kumbana mwanamke and kama kosa ulisha solve unalileta mezan tena thats red flag kwa mwanamke

kama una nia ya kufanya uchunguzi izo signs unamuonesha huwez fanikisha kabsa kwasb 24hrs unawaza iko iko sehemu ya kuwekeza akili wew unaweka moyo huwez ona majibu sahihi Change your plan bro

Huo ni ukweli wanawake wengi wanaolewa kwasab ya kutimiza ndoto tu ya kua na mume lkn wengine Ex wao waliachana kwa aman means penzi lao lipo hai kwaio huwez zuia wao kuendelea

wanaume wenye wivu au kuwachunguza sana wanawake mahusiano yao huvunjika kaka badirika ukiendelea ndoa yako inaenda kua chungu sana


Rudia kusoma hii com
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom