MWENDAPOLE1
Member
- Dec 8, 2011
- 26
- 1
Hapa chuon kwetu kuna mama anafanya kazi ktk ofisin fulani ,na nmekuwa classrep kwa muda toka nikiwa first year mpaka sasa second year,kinachonishangaza ni huyu mama anayefanya kazi kwenye hii ofisi ye kila akiniita anapenda tuongelee mambo ya mapenz kwa kunidodosa kama mimi nina mchumba au laah,kwa kuwa nilkiuwa namuheshimu nilishndwa kumwambia kwamba ninaye ,ila siku zilivozid kwenda siku moja natoka maeneo ya mwenge naelekea ghetto kwangu nlishangazwa sana mara baada ya kuonana naye,pale pale akaniuliza ninaenda wapi nami nikamjibu naelekea kwangu ,akaniomba kama naelekea ghetto kwangu si mbaya kama yeye akinipa lift,kwa kuwa nlkuwa nashida nilikubali.tulipoanza safari kwenda kwangu ktk ktk ya maongezi aliniambia kwamba ananipenda sana,nlishangaaa sana kusikia maneno kama hayo hsa ukizingatia ni mama mtu mzima ma watoto, jaman wana jf wenzangu hebu naombeni mnipe ushauri nimkubalie ombi lake? Pili kuna tetesi kuwa mme wake alikufa kwa ukimwi miaka mitatu iliyopita hichi nacho ndo kinaniogopesha sana! Nikikataa sijui chuo akiniona au tukionana itakuwaje? Nmefikiria sana nmeshndwa kupata jibu sahihi hivyo nawaomba wanajf wenzangu mnisaidie nifanye nini?