Nimechaguliwa kinyume cha sheria - Naibu Meya mteule Arusha

Si KWELI KIVUYO HAWEZI SEMA HIVYO ANANJAA KALI NAMJUA,HUU NI UZUSHI
Samahani SoP siko kwenye group la kuleta vitu vya uzushi kama wewe umezoea vitu kama hivyo si wote tunaofanya hivyo havinisaidii kitu.

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=12633

HabariLeo

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), amedai kipigo alichokipata kutoka kwa Jeshi la Polisi mkoani hapa, wakiongozwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Arusha (OCD), Zuberi Mombeji, ni matokeo aliyotarajia kutoka kwa Jeshi hilo siku nyingi, lakini hatarudi
nyuma kudai haki za msingi na yuko tayari kufa.

................................................................................

Kwa upande wake, Kivuyo akizungumza kwa simu, alisema Chadema wamepagawa na hawajui wanaloongea kwani kwenda kwake katika ukumbi na CCM kumchagua, sio kwamba amesaliti chama hicho.

Kivuyo alisema kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.

Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.

''Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa?" alisema Diwani huyo wa Sokoni One.
 
Hivi huyo diwani wa TLP aligombea? Alijieleza wakati wa uchaguzi? Alipochaguliwa akijua ilikuwa kinyume cha kanuni, je alikubali uchaguzi huo?

Hapo ndipo nami na shangaa!!!!!
Kama aliyajua hayo yote alitakiwa kupinga pale pale na kuwaambia wajumbe wote walimpigiua kura kuwa hapo tumekosea! na ndicho chanzo cha vurugu wewe wajua kabisa haki haija tendeka wewe wasema hawa CDM wanaleta vurugu kivipi? kweli haki haijatendeka kweli vurugu isitokeee????

Mlisha wahi ona wapi kikao cha kumpitisha mayor kinakuwa na OCD ndani ya ukumbi???kwa mujibu wa kikao kama wajumbe hawajaafikiana kikao kinahairishwa na kinakua next time. Na kumbukeni Mbunge ana Immunity yake haruhusiwi kukamatu kama vile walivyo mfanyia Lema. Nadhani watu huwa hawajui sheria ya kukamata na kukamatwa Police wetu wakisha tumwa na wakubwa basi wao ni kuja kufanya just follow orders siku sheria ikichukua mkondo wake Police hiyo kazi wataiacha mara moja maana nao watakuwa wanashitakiwa kwa kuvunja mashariti ya kukukamata.

 
diwani wa kata ya sokoni kupitia tlp, michael kivuyo amesema meya wa jiji la arusha gaudence lyimo wa ccm pamoja na yeye wamechaguliwa kinyume na kanuni ila kinachopaswa kufanywa na chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.

'meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa chadema wanalia nini? sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa?" alisema diwani huyo wa sokoni one.

Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.

Kifungu cha 8(3) kinaeleza bayana kuwa uchaguzi utafanyika kwa wajumbe (madiwani) kufika theluthi mbili na hilo ndilo tatizo kwa ccm wako 17 pamoja na diwani wa tlp, lakini sheria inakinzana na hilo na ili uchaguzi ufanyike lazima kuwe na wajumbe zaidi ya 21

habari leo:

Erinaceous Depone
 
HabariLeo
MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), amedai kipigo alichokipata kutoka kwa Jeshi la Polisi mkoani hapa, wakiongozwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Arusha (OCD), Zuberi Mombeji, ni matokeo aliyotarajia kutoka kwa Jeshi hilo siku nyingi, lakini hatarudi
nyuma kudai haki za msingi na yuko tayari kufa.

.................................................. ..............................

Analolisema hapo juu ni kweli jamaa hataniii kwa jinsi nilivyo mwona yuko kwa lolote lile, Police wawe makini wasipo angalia Murder case itawahusu au The Hague itawafuata au Human Rights watakuwa milangoni mwao hayo yote yanarecordiwa na yanawekwa.
Kwa upande wake, Kivuyo akizungumza kwa simu, alisema Chadema wamepagawa na hawajui wanaloongea kwani kwenda kwake katika ukumbi na CCM kumchagua, sio kwamba amesaliti chama hicho.

Wamepagawa nini ???? au Police ndio walipagawaaa, Hivi hao police walitokea wapi mpaka kuingia ndani ya ukumbi ulisha wahi onawapi Police wanaruhusiwa kuingia ukumbini? Nadhani Kivuyo alipaswa jua la kuongea kabla ya kulopoka kwa vyombo vya habari
Kivuyo alisema kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.

Kivuyo alisema alisemaaaa hii kweli Kivuyo kama unajua siasa usinge tamka kuwaambia CDM wangelifanya nini hapo inaashiria fika wewe ulijuwa fika ni kitu gani kilikuwa kimepangwa, kwanini nasema hivyo kama ulikuwa wazijua taratibu kwanini pale ukumbini uliruhusiwa kuingia? na ukachukua jukumu la kwenda directly kwa lema kumkamata kwani usi ombe utulivyu kwanza na ukauliza hizo taratibu zao zikoje na fujo zinatokea wapi na ndipo baada ya maelekezo ndio uwakamate wahusika maana umeharibu mari nyingi za serikali kwanini umetumia mafuta na kupeleka magari pale wakati watu waliokuwepo ni wachache sana ambao wasinge weza leta fujo, pili askali wako walikuwa wakirusha mabomu ya machozi mahali amabako hakuna ghasia yaani akili za police zilizokuwa zikitumika pale ni kufuata order basi

Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.
Kanuni gani ziko wazi kama walikuwa wanazijua kanuni kwanini police waliitwa pale inamaana waliokuwa wanazijua kanuni ni kuwa waliashiria kuzi vunja na kuzihamishai kuwa CDM wanaleta fujo sasa unapo taka kuleta mfano wa kipofu nadhani wewe ndie kipofu unae ona kumbe hujui kama unaona
''Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa?" alisema Diwani huyo wa Sokoni One.

Na wewe diwani wa sokoni wani kama kweli ulijua umechaguliwa kinyume na sheria na utaratibu ulipaswa kugomea hicho cheo walicho kupa, kama kweli wewe ni mwana democrasia hukupaswa kuungana mkono nao kwani ulukiuka sheria na taratibu zote za uchaguzi kwani huko ndani walikushikia panga au mtutu ukubali hicho cheo??
 
Wale wanaodai CDM walikataa ushirikiano na vyama vingine, si wakweli kwa sehemu fulani. Nijuavyo, CDM wana ushirikiano na vyama vingine katika ngazi za jimbo na kata. Hapa Arusha, katika kata ya Sokoni, CDM hawakuweka mgombea udiwani ili kuwachia Kivuyo wa TLP. Ushindi wake ulitokana na CDM kuwachia nafasi hiyo. Kwa hili alilofanya baada ya kukutana JK kwa siri, limemmaliza kisiasa na hata kiuhai! Msiniquote.
 
Wale wanaodai CDM walikataa ushirikiano na vyama vingine, si wakweli kwa sehemu fulani. Nijuavyo, CDM wana ushirikiano na vyama vingine katika ngazi za jimbo na kata. Hapa Arusha, katika kata ya Sokoni, CDM hawakuweka mgombea udiwani ili kuwachia Kivuyo wa TLP. Ushindi wake ulitokana na CDM kuwachia nafasi hiyo. Kwa hili alilofanya baada ya kukutana JK kwa siri, limemmaliza kisiasa na hata kiuhai! Msiniquote.
Kwenye red unauhakika na unayosema, kama ni kweli Kikwete analitakia nini taifa si kabakiza miaka yake minne awe historia, hata Mwinyi alikuwa rais lakini leo ni kama historia tu.
 
Diwani wa Kata ya Sokoni kupitia TLP, Michael Kivuyo amesema Meya wa jiji la Arusha Gaudence Lyimo wa CCM pamoja na yeye wamechaguliwa kinyume na kanuni ila kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.

‘Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa?” alisema Diwani huyo wa Sokoni One.

Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.

Kifungu cha 8(3) kinaeleza bayana kuwa uchaguzi utafanyika kwa wajumbe (madiwani) kufika theluthi mbili na hilo ndilo tatizo kwa CCM wako 17 pamoja na diwani wa TLP, lakini sheria inakinzana na hilo na ili uchaguzi ufanyike lazima kuwe na wajumbe zaidi ya 21

Habari Leo:



Thanks Luteni, that is what I expected it.
Nitafute baadaye upate moja moto.
Ninatabia ya kutokusoma magazeti ya ccm, lakini kwa hili nawapa shav.
 
Kituko cha mwaka!! Yaani katika madiwani mbumbu!!!.... huyo ni zaidi ya mno!!!!... Sasa ndo nini??? Ina maana yeye wakati anaingia kwenye mchakato alikua hajui kanuni na taratibu???? Amekuja kuzijua baada ya kusoma magazeti!!!! Duh!!! Hao waliomchagua huyo!!! Nawapa pole....
 
Nakupa hii karo ya shule na ukaile vitumbua kama hamisi alivyokula aliyopewa na babaye. Mtoto mjinga ataelewa baba yake anamsisitizia aile ile karo.Lakini mwelevu atatambua vinginevyo.
 
Nakupa hii karo ya shule na ukaile vitumbua kama hamisi alivyokula aliyopewa na babaye. Mtoto mjinga ataelewa baba yake anamsisitizia aile ile karo.Lakini mwelevu atatambua vinginevyo.

Hahahahahahhhh
 
Kuna sarakasi nyingine kuzielewa lazima uwe umesoma chuo alichosomea Mzee Kingunge.

Kivuyo kanasa kwenye mtego wa CCM na sasa anahaha kujinasua. Kama amelishwa kitu bora aseme ili awaumbue CCM na heshima yake itapanda mara dufu.
Nionavyo mimi diwani wa TLP alijua atakuwa naibu mayor kwani wote CCM na CDM walihitaji kura yake ili kumpata Mayor. CDM waende nae taratibu pengine bado kuna tumaini kama kweli kanuni ya uchaguzi ndivyo ilivyo. Kwa makosa kama haya kuna uhalali gani wa mkurugenzi wa jiji la Arusha kuendelea na wadhifa huo.
 
Nakupa hii karo ya shule na ukaile vitumbua kama hamisi alivyokula aliyopewa na babaye. Mtoto mjinga ataelewa baba yake anamsisitizia aile ile karo.Lakini mwelevu atatambua vinginevyo.

God bless your dad for having you as a child.
 
Hii nayo kubwa kuliko, anawashauri CDM wasivunje sheria wakati yeye anaendelea kuzivunja tena kasema hata kipofu anajua nimevunja kanuni.

Mungu ni mkubwa kaleta tukio hili ili kutuonyesha jinsi CCM wanalivyo waroho wa madaraka na jinsi JK alivyoingia ikulu kwa mabavu.

Kweli CCM hawana aibu.
 
Diwani wa Kata ya Sokoni kupitia TLP, Michael Kivuyo amesema Meya wa jiji la Arusha Gaudence Lyimo wa CCM pamoja na yeye wamechaguliwa kinyume na kanuni ila kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.

‘Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa?” alisema Diwani huyo wa Sokoni One.

Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.

Kifungu cha 8(3) kinaeleza bayana kuwa uchaguzi utafanyika kwa wajumbe (madiwani) kufika theluthi mbili na hilo ndilo tatizo kwa CCM wako 17 pamoja na diwani wa TLP, lakini sheria inakinzana na hilo na ili uchaguzi ufanyike lazima kuwe na wajumbe zaidi ya 21

Habari Leo:

Gazeti la Uhuru la leo linadai ya kuwa hiyo kauli ya huyu Meya limeifanya CCM-Halmashauri imweke kiti moto
 
Diwani wa Kata ya Sokoni kupitia TLP, Michael Kivuyo amesema Meya wa jiji la Arusha Gaudence Lyimo wa CCM pamoja na yeye wamechaguliwa kinyume na kanuni ila kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kufuata taratibu za kisheria na sio kuleta vurugu na kutuhumiana kwani huo sio wakati muafaka kwa sasa.

‘Meya amechaguliwa kinyume na kanuni na hata mimi nimechaguliwa kinyume na kanuni sasa Chadema wanalia nini? Sheria si ziko wazi, mahakama zipo kwa ajili ya watu wafuate taratibu kudai haki zao za msingi na sio kulaumu watu eti nimenunuliwa?” alisema Diwani huyo wa Sokoni One.

Alisema kanuni ziko wazi na hata kipofu anajua hilo na kinachopaswa kufanywa na Chadema ni kwenda katika vyombo vya sheria na sio kuleta vurugu na kupayuka ovyo barabarani.

Kifungu cha 8(3) kinaeleza bayana kuwa uchaguzi utafanyika kwa wajumbe (madiwani) kufika theluthi mbili na hilo ndilo tatizo kwa CCM wako 17 pamoja na diwani wa TLP, lakini sheria inakinzana na hilo na ili uchaguzi ufanyike lazima kuwe na wajumbe zaidi ya 21

Habari Leo:

Nimechaguliwa kinyume cha sheria! Sawa Michael Kivuyo umesema tumekuelewa! sasa pia tunataka CCM nao watoe tamko kama hilo lako tujue kama ni kweli nao pia wanaCCM waseme MEYA AMECHAGULIWA KINYUME CHA SHERIA!!!
 
Back
Top Bottom