Nimeacha kuishabikia Arsenal

Mbona umechelewa sana? Mi nlishaihama mda mrefu,maisha yenyewe mafupi tena magumu kwelikweli halafu timu ikuongezee presha utafurahia wapi maisha na huna ugakika wa kwenda peponi? Hamia timu yenye kukupa raha..penda vizuri
 
Hongera sana Ngongo umefanya uamuzi wa maana karibu sana Old Trafold,karibu klub yenye mafanikio,karibu ukutana na kocha mwenye mafanikio,karibu upate rahaaaaaaaaaaaa.
 
karibu sana mkuu Ngongo, MAN U chama kubwa...Arsenal kweli presha za kumwaga si unawaona kina Wacha1, AW, BAK, Quesst, Viper n.k.

1st lady wa ManU@JF, Belinda!!!!!!
 
karibu sana mkuu Ngongo, MAN U chama kubwa...Arsenal kweli presha za kumwaga si unawaona kina Wacha1, AW, BAK, Quesst, Viper n.k.

1st lady wa ManU@JF, Belinda!!!!!!

Groly hunter au ni shabiki wa Manure ana ditch around chezea kuhama timu wewe
 
Mimi ni mshabiki wa Liverpool

kuishabikia Arsenal ni sawa tu na kuishabikia Totenham
wao wanatafuta 'the fourth place' kila mwaka
 
Hongera kwa uvumilivu hata hivyo umevumilia sana, umechelewa kuachana na ushabiki wa arsenal.
Baada ya kuacha kuishabikia arsenal, sina timu ninayoishabikia Uingereza. Bahati nzuri kwa spain nilikuwa naipenda Barca., kwa italy nilikuwa naipenda AC Milan ya kina Ruud Gullit, Marco Van Basten, na Frank Rijkaard. So far, ndio timu ninazoendelea kuzishabikia.
 
Wakuu nimeamua kwa hiyari yangu na pasipo kulazimishwa na mtu yoyote kuitosa club ya Arsenal.Nina sababu nyingi za kuitosa The Gunners.

[1] Kukwepa magonjwa ya moyo.

[2] Imeshindwa kutwaa kikombe chochote kwa muda mrefu sana.

[3] Arsenal imekuwa gulio la kuuza wachezaji wake mahiri kwa Club nyingine

Baada ya kutafakari kwa kinaa na bila kushawishiwa au kulazimishwa na mtu au kikundi chochote nimeamua kujiunga na Club ya Manchester United yenye kutumia uwanja Old Trafold.Zipo sababu kibao lakini nitazitaja chache.

[1] Manchester United inaongozwa na manager mwenye mafanikio makubwa kuliko makocha wote wa UK.

[2] Manchester United imechukua ubingwa wa ligi kuu ya UK mara 19,timu inayoikaribia ni Liverpool pekee yake imechukua ubingwa mar 18 tu.

[3] Manchester United inakaribia kuweka rekodi mpya kwa kuchukua ubingwa mara 20,mpaka leo hii inaongoza ligi kwa tofauti ya point 12.

[4] Ukiishabikia Mancheter United uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo na kisukari ni mdogo sana.Kila wakati una kuwa ni mtu wa kucheka na kufurahia maisha duniani.

[5] Mwaka 1999 iliweka historia kwa kuchukua vikombe vitatu.Ubingwa wa ulaya.ubingwa wa Uk na Kombe la ligi.

[6] Mashabiki wa Manchester United ni wakarimu,wapole na wenye kujua kuchambua soka.Sifa hizo zinanihakikishia kwamba nitapokelewa vizuri.

Wapenzi wa Arsenal mtanisamehe sana kuhama club ni jambo la kawaida kwa mashabiki kama ilivyo kawaida kwa wachezaji.Siwezi kuendelea kusononeka hapa duniania kisa kupenda Club mbovu.

Nakala: Wacha1 Idimi Belo Steve Dii Mphamvu Dark City gfsonwin The Boss BAK Rejao Viper mfarisayo MwafrikaHalisi Kibunango Maxence Melo EMT Balantanda JMUshi Mwita Maranya .....

:biggrin1: karibu sana kwenye chama chetu hapa huwezi kupata pressure za maisha hata siku na sisi ni wakarimu welevu na wapenda amani kama ulivosema mwenyewe hapo juu....nimeshakutayarishia kadi yako ya uanachama na naomba uje na Viper Richard MwafrikaHalisi Wacha1 kashengo na wengineo ambao kucha wanakosa usingizi kwa sababu ya policies za kijinga arsene wenger na ivan gazidis wanazofanya....WELCOME TO OLD TRAFFORD....BEST CLUB IN THE WORLD AND MOST SUCCESSFULL IN ENGLAND
 
Last edited by a moderator:
Suala la mtu kuhama kushabikia from timu moja hadi nyingine kwa kweli mi haliniingii akilini and I get puzzed how can one dare to do that...!
Si kwamba sisi mashabiki wa Simba tunapenda mwenendo wa timu yetu, lakini tulianza kushabikia tukiwa na sababu tofautitofauti ambazo leo hii mtu akwambie hamia Yanga eti kwa sababu inamwenendo mzuri kwenye VPL sijui kama utaweza.
Vilevile, siamini kama inawezekana mtu uliyependa kushabikia say Arsenal, leo hii unaweza kwa urahisi kabisa Man U, au Totenham...! Siamini, labda kama ungesajiliwa kuchezea from one team to another lakini siyo kushabikia.
Ninachokiamini mimi ni kuwa: Ni rahisi kuacha upenzi wa chama cha Siasa ukahamia kingine (kwa sababu nyingi tu), au kuacha kumpenda demu uliye naye ukampenda mwingine lakini si rahisi kuhama kushabikia club yeyote ukahamia nyingine eti kisa inashinda sana...!

hakuna kisichowezekana chini ya jua. Yani kuhama timu iwe ishu?
 
Wakuu nimeamua kwa hiyari yangu na pasipo kulazimishwa na mtu yoyote kuitosa club ya Arsenal.Nina sababu nyingi za kuitosa The Gunners.

[1] Kukwepa magonjwa ya moyo.

[2] Imeshindwa kutwaa kikombe chochote kwa muda mrefu sana.

[3] Arsenal imekuwa gulio la kuuza wachezaji wake mahiri kwa Club nyingine

Baada ya kutafakari kwa kinaa na bila kushawishiwa au kulazimishwa na mtu au kikundi chochote nimeamua kujiunga na Club ya Manchester United yenye kutumia uwanja Old Trafold.Zipo sababu kibao lakini nitazitaja chache.

[1] Manchester United inaongozwa na manager mwenye mafanikio makubwa kuliko makocha wote wa UK.

[2] Manchester United imechukua ubingwa wa ligi kuu ya UK mara 19,timu inayoikaribia ni Liverpool pekee yake imechukua ubingwa mar 18 tu.

[3] Manchester United inakaribia kuweka rekodi mpya kwa kuchukua ubingwa mara 20,mpaka leo hii inaongoza ligi kwa tofauti ya point 12.

[4] Ukiishabikia Mancheter United uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo na kisukari ni mdogo sana.Kila wakati una kuwa ni mtu wa kucheka na kufurahia maisha duniani.

[5] Mwaka 1999 iliweka historia kwa kuchukua vikombe vitatu.Ubingwa wa ulaya.ubingwa wa Uk na Kombe la ligi.

[6] Mashabiki wa Manchester United ni wakarimu,wapole na wenye kujua kuchambua soka.Sifa hizo zinanihakikishia kwamba nitapokelewa vizuri.

Wapenzi wa Arsenal mtanisamehe sana kuhama club ni jambo la kawaida kwa mashabiki kama ilivyo kawaida kwa wachezaji.Siwezi kuendelea kusononeka hapa duniania kisa kupenda Club mbovu.

Nakala: Wacha1 Idimi Belo Steve Dii Mphamvu Dark City gfsonwin The Boss BAK Rejao Viper mfarisayo MwafrikaHalisi Kibunango Maxence Melo EMT Balantanda JMUshi Mwita Maranya .....

Mwandiko wako wenyewe unaonyesha hukuwahi kushabikia arsenal bwana. Kama kweli ulikuwa mshabiki wa Arsenal naomba ujibu hili. Ina maana miaka ijayo Manchester United wakija kuwa kama Liverpool au Nottingham Forrest utawakimbia? Mashabiki kama wewe hamfai hata siku moja. Mpira sio kama ndondi unapoweza kuhama toka bondia mmoja hadi mwingine. Kuna michezo mingi ya kufuatilia na kushabikia jaribu huo wa ndondi, draft, mdako, makida makida nk.
 
mm niko na chama langu liverpool na kamwe sintohama
Piga ua garagaza,hata nifungwe goli 10 nitabaki I will never walk alone
 
Hatua nzuri, lakini niko na swali kidogo.

Unapataje magonjwa ya moyo kwa timu za Ulaya, kilomita elfu kadhaa kutoka nyumbani kwako? Wakati mwingine wanawake huwa wanashangaa tunavyopigizana makelele na wengine hata kufikia kurushiana mangumi kwa mechi za Ulaya.

Athari za muda mrefu ni pamoja na kuporomoka kwa michezo yetu. Kama makocha, wachezaji, washabiki na wadau wote wako bize kujadili mustakabali wa timu za Ulaya ambazo ni kifurushi kingine cha ukoloni mamboleo, unadhani michezo yetu itapanda lini ili tulingane na hao munaowashobokea?

Hatuwezi kuamka japo kidogo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom