Nilishaeleza kwanini hatupaswi kuona ni kosa kwa Tanzania kukopa fedha za miradi kutoka nje, kwa kuwa tusipokopa athari zake ni hizi hapa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Watanzania wengi hawaelewi kwamba suala la kutekeleza miradi mikubwa nchini kwa kutumia fedha yetu ya ndani sio suala la kujivunia wala kujisifia hata kidogo. limetuletea maumivu makali katika karibu kila sehemu ya uchumi, hasa wakati wa Magufuli.

Miradi ya Magufuli aliyojivunia kutumia fedha za ndani ni kutia ndani ununuzi ndege, Reli ya SGR, Umeme wa Stiegler, daraja la baharini, Uwanja wa Chato, kuhamia Dodoma, nk.

Tanzania ni nchi masikini, sasa jiulize ikiwa fedha za miradi mikubwa kama hii sehemu yake kubwa ni fedha za ndani, fedha hizo zitatoka wapi? Katika nchi zote ambazo hazina vyanzo vikubwa vya fedha kama mafuta, miradi mikubwa kama hii hutekelezwa kwa fedha za mikopo ya nje na ndani.

Ili kupata fedha za ndani kwa wingi, Magufuli alifanya yafuatayo hapa chini, hatua ambazo zilituumiza sana. Ni kweli kuna mambo yanayotuumiza Samia ameyarithi toka kwa Magufuli, lakini si kwa kiwango kile cha wakati wa Magufuli.
  1. Wananchi na biashara zao kubanwa kodi kwa kila namna, kiasi kwamba hata biashara nyingine kufa kutokana na mzigo wa kodi
  2. Kutafuta vyanzo visivyo rasmi vya fedha kama vitambulisho vya wamamchinga ili kuongeza pato la serikali
  3. Kuanzisha kodi ya miamala ya simu kama Mpesa na vifurushi
  4. Kuanzisha kodi za kuchukua fedha ATM za benki
  5. Kutoa agizo kwa polisi kwamba wafanye kila namna kukusanya fedha kutoka kwa wananchi kwa njia ya faini za barabarani
  6. Kubana nyongeza za mishahara ya wafanyakazi serikalini na maruurupu mengine ya wafanya kazi ili fedha ziende kwenye kutekeleza miradi mikubwa
  7. Kuondoa sherehe za kitaifa hata za matukio muhimu katika historia ya nchi
  8. Kupunguza kwa kiasi kikubwa bajeti za maendeleo ya serikali za mitaa - hii ni kutia ndani bajeti za miradi midogo midogo katika miji na majiji kiasi kwamba kunakuwa na athari mbaya ya mzunguko wa fedha na kila mtu anaanza kulia hali mbaya
  9. Kubana mikopo ya elimu ya juu ya wanafunzi, kwa mfano kusema wale waliosoma shule fulani hawastahili mikopo
  10. Kubana misaada ya Watanzania walioathirika na majanga kama matetemeko na kupunguza bajeti ya majanga ya kitaifa na hata kuwaambia wananchi wakipatwa na majanga watajijua
  11. Kutopunguza bei ya mafuta hata pale ambapo bei ya mafuta katika soko la dunia imeshuka kwa kiwango kikubwa ili sehemu kubwa ya faida katika biashara ya mafuta ya magari ilirudi serikalini
  12. Kubana safari za kikazi za wafanyakazi kwa kisingizio cha kubaki kazini ili kuwajibika
  13. Kubambikia kesi za uhujumu uchumi wafanya biashara wakubwa na kuwaambia kwamba wakitaka wasifungwe basi inabidi watoe malipo ya "makubaliano" ambapo ni kama kusema waihonge serikali
  14. Kunyang'anga mamlaka ya Bunge kupanga matumizi ya fedha za serikali na kuiweka chini ya uamuzi wa raisi
  15. Kupandisha ushuru wa bidhaa zinazoagizwa na wananchi toka nje kama magari kwa kisingizio cha "price uplift" ili fedha zaidi ziingie serikalini
  16. Nk, nk, nk

Hivyo basi, Watanzania tunapaswa kuamka na kutambua kwamba, unapokopa leo, ukalipa baadae, unalipa wakati uchumi wako umekua kutokana na mkopo uliochukua, na maumivu ya kurejesha mkopo taratibu yanakuwa si makubwa ukilinganisha na kama ungewakamua wananchi fedha za ndani.

Kwa hiyo si vibaya kwa Samia kukopa ili kutekeleza miradi mikubwa kwa manufaa ya maendeleo ya taifa. Kama kuna lawama tunapaswa kumtupia raisi Samia ni pale atakapokuwa akikopa kwa ajili ya matumizi ya kawaida (recurrent expenditure) na sio matumizi ya miradi yenye kuinua uchumi (capital expenditure).
 
Tatizo sio kukopa tatizo pesa zinakopwa, na hizi za ndani nazo hazionekani mtaani kwa hiyo faida ya kukopa haionekani ili hizi za ndani zizunguke nazo hazionekanina hali inakua ngumu
 
Tatizo sio kukopa tatizo pesa zinakopwa, na hizi za ndani nazo hazionekani mtaani kwa hiyo faida ya kukopa haionekani ili hizi za ndani zizunguke nazo hazionekanina hali inakua ngumu
Mkuu, ukikopa kwa ajili ya capital expenditure sio rahisi kuona fedha mitaani, ila ukikopa kwa ajili ya recurrent expenditure, jambo ambalo sio zuri, utaiona fedha mitaani, lakini baadae utapata maumivu sana.

Kukopa kwa ajili ya recurrent expenditure kunaleta athari kubwa ya inflation, na unaweza kujikuta inafikia unanunua fungu la nyanya kwa elfu kumi.
 
Kukopa hakukwepeki, hata magufuli alikopa Sana, sema kuna baadhi ya wanasiasa wanapenda kupotosha Sana.
 
Kukopa hakukwepeki, hata magufuli alikopa Sana, sema kuna baadhi ya wanasiasa wanapenda kupotosha Sana.
Kama ni hivyo basi Magufuli alikuwa hajui ku-balance kati ya kukopa na kukamua wananchi fedha za ndani, hasa ukizingatia hizo athari nilizoweka hapo juu, ambazo mara nyingi ni kichocheo cha aidha nchi kupinduliwa kijeshi au chama cha upinzani kuchukua utawala ikiwa kuna uchaguzi huru.

Ukiweka athari hizo juu lazima ukandamieze demokrasia na hata kuua wapinzani, kuweka watu wako (yes men au psychophants) kama mkuu wa jeshi, TISS, Polisi wizara ya fedha na sehemu nyeti, na ndicho Magufuli alifanya. Huwezi asilani kuwa na athari kama hizo halafu ukawa na uhuru katika uchaguzi mkuu - chama chako kitaondolewa tu madarakani, kirahisi kama kumsukuma mlevi.
 
Bado tunakopesheka mazee, acheni kutisha watu.


Screenshot_20221230-115947_Twitter.jpg
 
FYI: Watu hawakatai nchi kukopa. Huu ni uposhaji. Watu wanakataa nchi kukopa wakati viongozi hawachukuwa hatua yoyote kubana matumizi ya kifahari na ufisadi uliotamalaki kila kina. Kwa kifupi fedha zinazokopwa zinatumika vibaya.

Kabla hatujakopa ilitakiwa tuondoa matumizi yote ya kifahari, tukomeshe ufisadi na ufujaji wa fedha uliojaa kila kona ya nchi, na kupunguza viongozi wengi wasio na umuhimu eg tupunguze wingi wa wabunge, viongozi wa kuteuliwa nk.
 
FYI: Watu hawakatai nchi kukopa. Huu ni uposhaji. Watu wanakataa nchi kukopa wakati viongozi hawachukuwa hatua yoyote kubana matumizi ya kifahari na ufisadi uliotamalaki kila kina. Kwa kifupi fedha zinazokopwa zinatumika vibaya. Kabla hatujakopa ilitakiwa tuondoa matumizi yote ya kifahari, tukomeshe ufisadi na ufujaji wa fedha uliojaa kila kona ya nchi, na kupunguza viongozi wengi wasio na umuhimu eg tupunguze wingi wa wabunge, viongozi wa kuteuliwa nk.
Mkuu, naungana nawe kwamba ikiwa Samia ataruhusu hali ambapo tunakopa halafu fedha tulizokopa zinafanyiwa ufisadi, basi hata mie nitakuwa wa kwamza kuokota jiwe ili nimpige. Lakini kukopa na ufisadi ni mambo mawili tofauti. Lawama nyingi zimeelekezwa kwa Samia kwenye suala la kukopa. Kina Ndugai hawakusema nchi itapigwa mnada kwa sababu ya ufisadi wa fedha za mikopo bali kwa sababu ya kukopa.

Na ni kweli Samia hajawa makini sana kwenye kudhibiti ufisadi unaoendelea kukua kila siku tangu kifo cha Magufuli. Pamoja na ubaya wote na matumizi ya hovyo ya Magufuli kwenye fedha za serikali, aliweza kuweka hofu ya kufanya ufisadi nchini, ambapo chini ya Samia hofu hiyo inatoweka taratibu.

Samia anahitaji kuwa mkali kwenye ufisadi, watu wamemsoma na kuona hana ukali katika sehemu hii. Sijawahi kumsikia Samia anakemea ufisadi kwa nguvu zote au kuchukua hatua na kutangaza hadharani kuwawajibisha watu kwa sababu ya ufisadi. Sijui kama anaogopa au na yeye yuko compromised, yaani kaambiwa ukitumwagia ugali wetu tutamwaga mboga
 
Kama ni hivyo basi Magufuli alikuwa hajui ku-balance kati ya kukopa na kukamua wananchi fedha za ndani, hasa ukizingatia hizo athari nilizoweka hapo juu...
Suala la kukopa wananchi wanaliona halina impact, Kwa sababu kinachokopwa kinaimbwa Sana kwenye media kuliko kinacholipwa! Kwa mfano Mkopo wa ndani na nje inaweza kuwa imekopwa jumla tilioni sita lkn inayokwenda kutumika ni tilioni 1(either for recurrent or development expenditure or both) lkn tilioni 5 zinarudi Kulipa deni la nyuma, so wananchi nyimbo za tilioni 6 Fresh loan zinakaa masikioni kuliko inshu ya tilioni 5 zinazoenda Kulipa deni, pengine nashauri wizara iwe inatoa vipeperushi kuwaelimisha wananchi mfumo wa get fresh loan, pay old debts ili maswali ya mikopo imeenda kufanya kazi gani au ina faida gani! Yapungue
 
Bado tunakopesheka mazee, acheni kutisha watuView attachment 2479608
Hizi data bwana mara nyingine hazitoi taswira halisi - true situation on the ground. Kwa mfano, DRC kuwa na rati ya 14.66% ni kama kusema wahisani waone kwamba DRC inakopesheka zaidi ya Kenya, lakini si kweli.

Unapaswa kuelewa kwamba DRC kuwa na ratio ndogo ni kwa sababu hakuna anaeikopesha kwa kuwa risk za kuikopesha ziko juu mno. Kwa hiyo interpretation unayofanya hapa kwamba Tanzania tukope zaidi kwa sababu ratio yetu ipo chini zaidi ya Kenya sio kweli. Tunapaswa kukopa, lakini sio kwa vigezo kama hivi vyenye kupotosha
 
Nilitaka kuunga mkono hoja yako kiujumla wake, lakini niliposoma aya ya mwisho, na maneno yaliyokolezwa na wino wa bluu, nikajua huko 'serious' na uliyoandika hapa..

Wewe ni chawa tu kama chawa wengine wapuuzi.

Samia siyo wa kwanza kukopa. Na licha ya hivyo, hujui kuwa kishaamua kukimbia kukopa, sasa hivi anasukuma PPP mbele, ili upigaji ushamiri zaidi; lakini wewe kama chawa hujui hilo, na utakapojua mara moja utageuka na kuleta hekaya za kusifu upigaji huo mpya atakaouanza.

Lakini najua kwa akili za uchawa, utadhani napinga kutumia njia ya PPP kutimiza baadhi ya miradi; kwa sababu umepofushwa na uchawa huoni udhaifu wa utekelezaji huo bila ya kuwa na mifumo imara za usimamiaji wake ili kulinufaisha taifa, kazi asiyoiweza kabisa Samia.
 
Suala la kukopa wananchi wanaliona halina impact, Kwa sababu kinachokopwa kinaimbwa Sana kwenye media kuliko kinacholipwa! Kwa mfano Mkopo wa ndani na nje inaweza kuwa imekopwa jumla tilioni sita lkn inayokwenda kutumika ni tilioni 1(either for recurrent or development expenditure or both) lkn tilioni 5 zinarudi Kulipa deni la nyuma, so wananchi nyimbo za tilioni 6 Fresh loan zinakaa masikioni kuliko inshu ya tilioni 5 zinazoenda Kulipa deni, pengine nashauri wizara iwe inatoa vipeperushi kuwaelimisha wananchi mfumo wa get fresh loan pay old debts ili maswali ya mikopo imeenda kufanya kazi gani au ina faida gani!
Hapana Mkuu, hatukopi ili kulipa madeni. Tunakopa kwa ajili ya capital au development expenditure ili kujiongezea uwezo wa national revenue ili tuwe na uwezo zaidi wa kuongeza pato la taifa na in turn kuongeza uwezo wa kulipa madeni ya nyuma kutokana na increased national revenue
 
Mkuu, naungana nawe kwamba ikiwa Samia ataruhusu hali ambapo tunakopa halafu fedha tulizokopa zinafanyiwa ufisadi, basi hata mie nitakuwa wa kwamza kuokota jiwe ili nimpige. Lakini kukopa na ufisadi ni mambo mawili tofauti...
Kwahiyo kama tumekubaliana tukope kadri tunavyoweza sasa suala la ufisadi nani anatakiwa kulishughulikia ili kile tunachokopa kitumike vizuri kuleta maendeleo ya nchi na wananchi mmoja mmoja??
 
Nilitaka kuunga mkono hoja yako kiujumla wake, lakini niliposoma aya ya mwisho, na maneno yaliyokolezwa na wino wa bluu, nikajua huko 'serious' na uliyoandika hapa....
Sijaona point yeyote ya maana uliyoongea, naona kelele za mlevi tu asieelewa mambo wala kujua aseme nini kwenye hii thread. Kwa hiyo nakusamehe bure, hujui unenalo

Na kwa taarifa yako, hayo maneno ya blue sio sehemu ya hii thread, ni signature yangu. Unaonekana huelewi mambo mengi tu
 
Kwahiyo kama tumekubaliana tukope kadri tunavyoweza sasa suala la ufisadi nani anatakiwa kulishughulikia ili kile tunachokopa kitumike vizuri kuleta maendeleo ya nchi na wananchi mmoja mmoja??
Ni serikali chini ya Samia. Hilo halihitaji PhD kulijibu. Na kama nilivyosema, naunga mkono Samia kukopa, bali namkosoa kwa nguvu zote kwamba hajawa mkali kwenye suala la ufisadi. Anahitaji kutuonyesha kwa vitendo kuwa havumilii ufisadi ambao tunashuhudia ukikua kila siku
 
Sijaona point yeyote ya maana uliyoongea, naona kelele za mlevi tu asieelewa mambo wala kujua aseme nini kwenye hii thread. Kwa hiyo nakusamehe bure, hujui unenalo
Kwani unadhani nilitegemea kuwa "utaona pointi", kwa upofu ulionao katika akili unaosababishwa na sifa ya kuwa chawa?
 
Ni serikali chini ya Samia. Hilo halihitaji PhD kulijibu. Na kama nilivyosema, naunga mkono Samia kukopa, bali namkosoa kwa nguvu zote kwamba hajawa mkali kwenye suala la ufisadi. Anahitaji kutuonyesha kwa vitendo kuwa havumilii ufisadi ambao tunashuhudia ukikua kila siku
Sawa nimekuelewa point yako ni kua hutaki watu waikosoe serikali kwa kuvuna mikopo kila uchao! Ila bado nina swali vp hii mikopo tunayokopa je haina madhara kabisa hapo baadae ikiwa haitatumika kwa uwekezaji unaotakiwa?
 
Kwani unadhani nilitegemea kuwa "utaona pointi", kwa upofu ulionao katika akili unaosababishwa na sifa ya kuwa chawa?
Tatizo lako wewe ni kwamba huelewi maana ya signature ya JF member, ukakurupuka kujibu signature ukidhani ni sehemu ya thread.

Hata hivyo, akili yako ya kuelewafilosofia iko chini sana, la sivyo ungeielewa hiyo signature, kwa sababu iko factual. Niambie, kuna tatizo gani katika kusema "Changamoto kubwa sana inayoyakabili mataifa masikini duniani na kufanya washindwe kuendelea ni nyingi ya akili ndogo kupewa mamlaka makubwa, kwa njia ya kura au kuteuliwa" Hiyo ni philosophical statement. Kasome shule uelewe na kuondoa ujinga.
 
Tatizo lako wewe ni kwamba huelewi maana ya signature ya JF member, ukakurupuka kujibu signature ukidhani ni sehemu ya thread.

Hata hivyo, akili yako ya kuelewafilosofia iko chini sana, la sivyo ungeielewa hiyo signature, kwa sababu iko factual. Niambie, kuna tatizo gani katika kusema "Changamoto kubwa sana inayoyakabili mataifa masikini duniani na kufanya washindwe kuendelea ni nyingi ya akili ndogo kupewa mamlaka makubwa, kwa njia ya kura au kuteuliwa" Hiyo ni philosophical statement. Kasome shule uelewe na kuondoa ujinga.
Kama huoni 'contradiction' ya signature hiyo na uliyoandika kumhusu unayemsifia hapa, basi wewe utakuwa ni mmoja wa hao wenye akili ndogo sana.
 
Sawa nimekuelewa point yako ni kua hutaki watu waikosoe serikali kwa kuvuna mikopo kila uchao! Ila bado nina swali vp hii mikopo tunayokopa je haina madhara kabisa hapo baadae ikiwa haitatumika kwa uwekezaji unaotakiw
 
Back
Top Bottom