Nilipotabiri Ujio wa Kocha Olivieira Simba SC na ikatokea na Kushauri yafuatayo nilikuwa namaanisha

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
57,115
110,509
Nilisisitiza mno kama siyo sana kuwa Kocha Mpya Simba SC Roberto Olivieira akitua Simba SC aje na Watu wake anaowaamini na kamwe asiendelee na Hawa akina Mgunda, Matola na Meneja Rweymamu aliowakuta GENTAMYCINE nilimaanisha na kuna Hatari niliiona na leo imejidhihiri.

Nawaombeni rejeeni marejeo ya Picha za Azam Tv wakati Mbeya City wamesawazisha Goli la Kwanza na lile la Pili kisha kwa Umakini kabisa tizameni Body Language ya Kocha Msaidizi Mgunda na Meneja Rweymamu kisha mtanielewa vyema.

Kocha Msaidizi Juma Mgunda alikuwa anajifanya Kuumia Magoli kurejea ( Kusawazishwa ) huku anajificha Mdomo na anatizamana na Meneja Rweymamu na baadhi ya Watu wa Benchi la Ufundi na Kumcheka Kimoyomoyo Kocha Mkuu Roberto Olivieira kitu ambacho Kwangu ni very Unprofessional na kimenilazimisha nianze Kumdharau Kocha Msaidizi Mgunda.

Na ili Kuzuga / Kutuzuga kila Simba SC ilipokuwa ikipata Magoli yake Kocha Msaidizi Mgunda Kinafiki kabisa alikuwa anajifanya anaamka na Kushangilia kwa Nguvu ( Kihisia ) huku akikongeana Mikono na Kocha Mkuu Olivieira.

Uongozi wa Simba SC mmefanya Kosa Kubwa sana Kumleta Fundi na Mtaalam Roberto Olivieira kama Kocha Mkuu na kumuachia hawa Waswahili na Wapika Majungu Wenzetu akina Kocha Msaidizi Mgunda na Meneja Rweymamu.

Ile Shangilia yake ya Kihisia Kali Kocha Mkuu wa Simba SC Roberto Olivieira baada ya Mchezaji Pape Ousmane Sakho Kufunga Goli zuri la Tatu ilikuwa na maana Kubwa na kuna Jibu alikuwa akilitoa Kwetu Mashabki na hasa kwa Benchi lake la Ufundi alilonalo ambalo huenda akawa ameshalisoma na kuhisi kuwa amezungwa na Wanafiki wanaovalia Ngozi ya Kondoo huku wakijifanya Wanamchekea na Kumpenda wakati kumbe Wanafurahia Kufeli Kwake Kimbinu (kutokana na Ugeni wake) na Wanamchukia kutokana na Uzungu wake wakiamini kuwa kaja Kuwaharibia na hawatofaidika tena na Simba SC.
 
Majungu yako tu , kijicho kipo dunia nzima so ni vitu vya kawaida tu hivyo as long as timu imeshinda mengine ni stori za kuungaunga

Mgunda alisimama akamwuliza Saidoo kwa nini Mbeya city wako pungufu afu wao wanawaachia wacheze mpira? Je hapo utasema Mgunda alikuwa hana uchungu wa kuona timu imezidiwa uwezo hadi useme alifurahia Simba kufungwa?
 
Tupe scenario nzima hiyo hujuma inafanyikaje. Maana kuna wakati ulikuwa unasema kina Bocco, Kyombo na Kibu wanapangwa kwa sababu ya ushkaji, kaja kocha kawapenda. Anawapanga, kimya!

Sakho kafunga goli, je hakuwa kwenye mpango huo wa hujuma? Je Saido na magoli yake? Kwa nini hakupiga penalti nje?

Mimi niliona wachezaji wa akiba ndiyo wameziba midomo wananong'onezana kama wanacheka, ndiyo nilijiuliza wanacheka nini wakati mambo bado magumu.
 
Mgunda alimpiga misumari yule muegypt mpaka akafukuzwa pale Coastal.

Bora Simba wangembakiza tu Suleiman Matola ameshazoea kufanya kazi na hawa makocha wakigeni bila majungu na unafiki.
Kwa taarifa yako Mgunda ni afadhali, la Matola ni Hatari zaidi ya Kirusi cha Kimeta na hafai wala hatufai pia Simba SC kama Kocha Msaidizi.
 
Mpira ni mchezo wa wazi.

Robert kipindi Cha kwanza mfumo wake ulifanya zipigwe popo tu.

Ndio maana Kibu akaonekana anafaa sana kwenye mfumo huo kuliko Chama.

Kipindi Cha pili Simba ili ingia na approach yake ya siku zote wanapokuwa kwa Mkapa pasi fupi fupi halafu nyingi.

Hapo ndipo watazamaji wakaanza kuuliza kwanini Chama atolewe awekwe Kibu.

Asingebadili mfumo hata hizo goli tatu asingeweza kuzilinda?
 
Siyo busara kubadilisha bench lote la ufundi mara moja na siyo hekima kubadilisha mfumo mara moja.
-Kocha ni vema kuendelea la Wasaidizi wa bench la ufundi katika kipindi cha mpito,ili kufahamu vema falsafsa ya klabu au timu, ubora na mapungufu ya timu nk.
-Baada ya kutolewa Chama Ni dhahiri kuna baadhi ya wachezaji na wapenzi wa SIMBA walivurugwa kwa kutolewa playmaker wao mapema.
-Chama ana jicho kuona na pua ya kunusa fursa.
-Chama ndiyo alitoa assist ya goli la Saido,
-Kuna mchezaji akiwa kiwanjani, walinzi hupeana majukumu ya kumchunga na huwa analindwa na wachezaji wawili,kumdhibiti,lakini akipata fursa anaitumia,kukuadhibu/kusababisha goli/assist (Mayele au Chama).
-Kocha Mkuu alipaswa kushauriana na Wasaidizi wake , ndiyo maana ya teamwork ,sidhani kama alishauriana Wasaidizi wake.
-Huwa tunaona hata timu kubwa huko Ulaya,Kuna utamaduni wa Kocha Mkuu kushauriana na technical bench lake kabla ya kufanya uamuzi.
Yote kwa yote,tunawakia uongozi, mashibiki na wachezaji wa SIMBA kuwa na mshikamano na kuacha kunyosheana vidole.





Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Nilisisitiza mno kama siyo sana kuwa Kocha Mpya Simba SC Roberto Olivieira akitua Simba SC aje na Watu wake anaowaamini na kamwe asiendelee na Hawa akina Mgunda, Matola na Meneja Rweymamu aliowakuta GENTAMYCINE nilimaanisha na kuna Hatari niliiona na leo imejidhihiri.

Nawaombeni rejeeni marejeo ya Picha za Azam Tv wakati Mbeya City wamesawazisha Goli la Kwanza na lile la Pili kisha kwa Umakini kabisa tizameni Body Language ya Kocha Msaidizi Mgunda na Meneja Rweymamu kisha mtanielewa vyema.

Kocha Msaidizi Juma Mgunda alikuwa anajifanya Kuumia Magoli kurejea ( Kusawazishwa ) huku anajificha Mdomo na anatizamana na Meneja Rweymamu na baadhi ya Watu wa Benchi la Ufundi na Kumcheka Kimoyomoyo Kocha Mkuu Roberto Olivieira kitu ambacho Kwangu ni very Unprofessional na kimenilazimisha nianze Kumdharau Kocha Msaidizi Mgunda.

Na ili Kuzuga / Kutuzuga kila Simba SC ilipokuwa ikipata Magoli yake Kocha Msaidizi Mgunda Kinafiki kabisa alikuwa anajifanya anaamka na Kushangilia kwa Nguvu ( Kihisia ) huku akikongeana Mikono na Kocha Mkuu Olivieira.

Uongozi wa Simba SC mmefanya Kosa Kubwa sana Kumleta Fundi na Mtaalam Roberto Olivieira kama Kocha Mkuu na kumuachia hawa Waswahili na Wapika Majungu Wenzetu akina Kocha Msaidizi Mgunda na Meneja Rweymamu.

Ile Shangilia yake ya Kihisia Kali Kocha Mkuu wa Simba SC Roberto Olivieira baada ya Mchezaji Pape Ousmane Sakho Kufunga Goli zuri la Tatu ilikuwa na maana Kubwa na kuna Jibu alikuwa akilitoa Kwetu Mashabki na hasa kwa Benchi lake la Ufundi alilonalo ambalo huenda akawa ameshalisoma na kuhisi kuwa amezungwa na Wanafiki wanaovalia Ngozi ya Kondoo huku wakijifanya Wanamchekea na Kumpenda wakati kumbe Wanafurahia Kufeli Kwake Kimbinu (kutokana na Ugeni wake) na Wanamchukia kutokana na Uzungu wake wakiamini kuwa kaja Kuwaharibia na hawatofaidika tena na Simba SC.
Mzembe mmoja!
 
Mimi kama kutaka Mgunda aondoke Simba, basi nataka aondoke nikiamini kwamba ni kocha mkubwa kwa level ya klabu zetu nyingine kwenye ligi yetu, hastahili kuitwa kocha msaidizi kwa experience yake kwenye ligi yetu, anatakiwa atafute timu nyingine akawe kocha mkuu..

Mgunda kwa umri wake, naona anastahili heshima ya kuwa kocha mkuu sehemu nyingine.
 
Ni mapema sana kumuhukumu kocha kwa mechi moja. Lakini kwa kuwa mpira ni mchezo wa wazi tuwe wakweli tu kuna kosa moja kubwa la wazi kabisa kocha alilifanya kwenye mchezo wa jana na kwa yeyote anaojua mpira atakuwa ameliona. Narudia tena nazungumzia mchezo wa jana tu huku mbele ya safari huenda akajirekebisha na timu ikafanya vizuri.

Kosa kubwa alianza na washambuliaji wawili ambao wote wote walikuwa wamesimama tu hakuna mwenyewe uwezo kati yao wa kushuka kidogo chini kuchukua mpira kucheza "one two" au kupunguza angalau wachezaji wawili watatu wa Mbeya City au hata kutembea na mpira walau mita tano kuelekea lango la adui. Matokeo yake timu iligawanyika katikati ya uwanja Mbeya City wakaliteka dimba la katii. Kiasi mtu aliyefika kuangalia kipindi cha pili mwishoni ilikuwa si rahisi kwake kujua kuwa Mbeya City walikuwa pungufu uwanjani. Kwa maana nyingine iwapo huyo kocha ataendelea na mfumo huo akikutana na timu yenye viungo imara naona kabisa Simba itaenda kukutana na dhahama ya kapu la magoli.
 
Back
Top Bottom