Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
Prof. Kabudi mtaalamu wa majadiliano kuwahi kutokea nchini akiongoza timu ya majadiliano kati ya Tanzania na kampuni ya Barrick juu ya mikataba ya madini na upigwaji Tanzania uliofanyiwa.
Ikafanywa tathmini kubwa na ya kina na kubaini kuwa kuna ukwepaji wa Kodi wa takribuni trilion 400 za kitanzania na kwa kiwango hicho kama angepewa kila mtanzania basi kila mtu angepata Noah mpya.
Kwa hakika ni kiwango kikubwa sana lakini Prof.Kabudi alikuja kukiri kwamba kutaja kiwango hicho ilikuwa ni mbinu ya majadiliano.
Yawezekana bila mbinu hiyo pasingekuwa na mabadiliko kwenye sheria ya madini kwa sababu hao mabepari wasingeona udanganyifu waliokuwa wanafanya.
Yawezekana bila mbinu hiyo tungeshtakiwa MIGA lakini hao mabepari wameshindwa kutushtaki kwa kuhofia tungedai fidia ya trilion 400.
Kupitia mbinu hiyo makubaliano na mkataba yakafanyika upya na Taifa kunufaika vya kutosha.
Twendeni mbele turudi nyuma Prof. kabudi ni akili kubwa mno, ni moja ya watu wenye mapenzi na uzalendo wa kweli kwa Taifa. Ni rasilimali adimu sana.
Ni wakati sasa Taifa tuzalishe wataalamu wengi wa majadiliano kama Prof.Kabudi ili waweke sawa masuala ya mikataba inayohusu unyonyaji huko mbeleni.
Ikafanywa tathmini kubwa na ya kina na kubaini kuwa kuna ukwepaji wa Kodi wa takribuni trilion 400 za kitanzania na kwa kiwango hicho kama angepewa kila mtanzania basi kila mtu angepata Noah mpya.
Kwa hakika ni kiwango kikubwa sana lakini Prof.Kabudi alikuja kukiri kwamba kutaja kiwango hicho ilikuwa ni mbinu ya majadiliano.
Yawezekana bila mbinu hiyo pasingekuwa na mabadiliko kwenye sheria ya madini kwa sababu hao mabepari wasingeona udanganyifu waliokuwa wanafanya.
Yawezekana bila mbinu hiyo tungeshtakiwa MIGA lakini hao mabepari wameshindwa kutushtaki kwa kuhofia tungedai fidia ya trilion 400.
Kupitia mbinu hiyo makubaliano na mkataba yakafanyika upya na Taifa kunufaika vya kutosha.
Twendeni mbele turudi nyuma Prof. kabudi ni akili kubwa mno, ni moja ya watu wenye mapenzi na uzalendo wa kweli kwa Taifa. Ni rasilimali adimu sana.
Ni wakati sasa Taifa tuzalishe wataalamu wengi wa majadiliano kama Prof.Kabudi ili waweke sawa masuala ya mikataba inayohusu unyonyaji huko mbeleni.