Nilijua kaa la moto

Idd Ninga

JF-Expert Member
Nov 18, 2012
5,136
4,298
NIJUA KAA LA MOTO.





1)Ni jivu linatutisha,vipi tunadhani moto.
Ni figa lajisafisha,lije kutoa uoto.
Ten linajing'arisha,liwe mweupe uroto
Nijua kaa la moto,kumbe jivu la baridi





2)kumbe jivu la baridi,kimbizo mkong'oto.
Twachoka zake ahadi,zilo za maji ya moto.
Itakuwa baghidadi,hawezi kata ufito.
Nijua kaa la moto,kumbe ni picha ya kwanza.




3)kumbe ni picha ya kwanza,mtindo gongo la mboto.
Ama vituko vya mwanza,vichekesho kwake mboto.
Siyo kama livyoanza,limenza kushuka joto.
Nijua kaa la moto,kunbe picha ile ile




Shairi=NILIJUA KAA LA MOTO .
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arush.+255010160
iddyallyninga@gmail.com
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom